Msaada: Nyoka Mkali anazunguka Mazingira ya Nyumbani

Msaada: Nyoka Mkali anazunguka Mazingira ya Nyumbani

Inawezekana paka alileta ubabe akazidiwa na kukimbia baadae alisahau alirudi kulala na paka walivyo wavivu, mwamba akamgonga akiwa usingizini.


Nyoka baada ya huo ugomvi akaamua kubeba kinyongo dhidi ya huyo paka huyu nyoka wa kawaida kweli mama? Akamvizia hadi usingizini?
 
Chukua paketi za chumvi mwaga sehemu zote zenye maua na kwenye mabanda hutaona nyoka kwenye eneo lako
 
Mnatoboa kwenye kifuniko cha mdomo au pembeni ya chupa?
Sisi tulitaka yakae muda mrefu tulitoboa juu ya mfuniko.Jirani yetu alikuwa na ukuta kila mara aliuwa nyoka sisi aahh wala hawakusogea eneo letu sbb ya ile harufu
 
Raia wote hamna vyombo vya moto? Na mnakaa vijijini? Huyo msako wa siku moja tu risasi ya shingo mnaachana nae
 
Ofisi ya mali asili wanatoa hiyo kadhia haraka sana kama kutafuna biskuti..Asante
 
Raia wote hamna vyombo vya moto?na mnakaa vijijini?huyo msako wa siku moja tu risasi ya shingo mnaachana nae
Huyo nyoka wa kumlenga kwa bunduki anakua kafa au?

Hili swala lilijadiliwa bungeni juu ya koboko kuzidi maeneo ya Tabora na waziri Nyalandu akasema bunduki siyo option na hata logic tu inakuonyesha bunduki siyo option.
 
Inawezekana analala kwako halaf anaenda kutafuta chakula kwa jirani halafu nyie mnaenda kumtafuta kwa jiran wakat huo kasharudi kwako
Kwa kifupi kazi unayo
 
ni maeneo gani huko ili tujue aina ya nyoka??!!ukishajua ni aina gani ya nyoka na tabia zake itakuwa rahisi kumnasa.
kingine huwez kuchoma kila siku chupa za plastic cjui pilipili au kumwaga vitunguu maji sababu atakimbia then atarudi hali ikitulia!
taja eneo ulipo nikwambie ni aina gani hiyo ya nyoka wanapatikana hapo haswa wenye sumu!!
je ameweza kumeza kuku?au paka?
usije ukamuua bure kumbe alikuwa anasaidia kukupunguzia panya humo ndani!
inaonyesha toka dunia imeumbwa binadamu ameua nyoka mara 5000 kuliko nyoka kuua binadamu hata mmoja..
Mimi naonaga kwangu wa aina tatu wa kwanza ni wa kijani warefu na wa pili ni weusi wafupi pia na wa tatu ni silver flani hivi wanarangi kama tofali au cement nipo dar goba
 
Huyo nyoka wa kumlenga kwa bunduki anakua kafa au?

Hili swala lilijadiliwa bungeni juu ya koboko kuzidi maeneo ya Tabora na waziri Nyalandu akasema bunduki siyo option na hata logic tu inakuonyesha bunduki siyo option.
Nyoka mmoja anawashinda watu 1000? Nishalala na nyoka kifutu na akaondoka mwenyewe,
huyo wenu atakua kashadhuriwa.
Otherwise ni wapole sana na wao wenyewe wanaogopa binadamu.
 
😂😂😂😂😂Kwa hiyo RUKHSA ya kuua nyoka ni kwa maccm tu! 🤣🤣🤣
Kigwangala alimgonga Twiga na akafa kule Mdori Manyara, lakini hakujitafuta ili apelekwa mahakamani.
 
Nilisikia maua maua mengi huita nyoka. Kuna mafuta sijui ni machafu nasikia ukiwmwaga nyoka hukimbia. Ajaribu kumwaga kuzunguka mpaka wa eneo lake.
 
Kuna vingi vya kuviconsider hapo.

Afya ya mtu. Umri. Eneo la mwili lililogongwa n.k.

Kuna kesi ya mwanamke aliyeng'atwa na black mamba zaidi ya wawili na bado akapona. Na black mamba mmoja anagonga zaidi ya mara moja so zaidi ya wawili wanagonga mara nyingi nyingi na mwanamke aliishi.
Huyo hakuwa koboko, atakuwa alijuwa nyoka mwingine asiye na sumu. Koboko hawezi kung'ata bila kuweka sumu, hana uwezo wa kuzuia sumu akigonga. Tifauti na nyoka wengine ambao wanaweza kukupiga "dry bite" kama anajua wewe sio chakula chake na pia humuwindi ili kumuua.
 
Tafuteni oil chafu mwageni kuzunguka nyumba na sehemu mnazohisi ni rahisi wadudu hatari kuwepo...hakuna mdudu atayebaki hapo hata sisimizi..
 
Jana usiku Kama saa 6 nimeishiwa bando nilikuwa nafuatilia live fainali ya Europa Sasa kufika hatua za penati bqndo likaisha ikabidi nitoke nikaulizie matokeo Sasa ile narudi nikaona paka wawili Kama wanapigana na kimtindo palikuwa Giza.


Ile nakaribia nikagundua hawapigani Kama wanacheza na kitu ikanibidi nipakaribie kuangalia vzr wanacheza na kitu gani

Ase kumbe nyoka walikuwa wanacheza nae huku wakimpiga makofi na kuruka sasa wkt nimewasha tochi ya simu kumulika niangalie vzr wale paka wakakimbia na ndio walikuwa kizuizi wa yule nyoka

Ikanibidi nichukue jukumu la kuokota mawe na kumpiga yule nyoka ,Sasa kwenye ile nyumba kwa dirishani nasikia vijana mabishoo wa chuo bila Shaka wale wanabishana kuhusu mpira ,nikawa nawaita waje kusaidia maana yule nyoka alikuwa anataka kuingia kwenye tobo pale kwao walivyo wajinga wakawa wananiona chizi sijui wakakaa kimya na kuacha kubishana nikaendelea kuwaita wakajikausha


Nikajisemea kwanza sio kwangu najihangaisha bure wacha aingie ndani kwao watajijua wenyewe na ubisho wao,nikazima tochi nikasepa zangu, na nyoka alikuwa mrefu kweli


Paka wanasaidia ase nimegundua Jana night
 
Nyoka mmoja anawashinda watu 1000,?nishalala na nyoka kifutu na akaondoka mwenyewe,
huyo wenu atakua kashadhuriwa.
Otherwise ni wapole sana na wao wenyewe wanaogopa bin adam.
Kifutu (puff adder) siyo aggressive unless uwachokoze au umkanyage
 
Huyo hakuwa koboko, atakuwa alijuwa nyoka mwingine asiye na sumu. Koboko hawezi kung'ata bila kuweka sumu, hana uwezo wa kuzuia sumu akigonga. Tifauti na nyoka wengine ambao wanaweza kukupiga "dry bite" kama anajua wewe sio chakula chake na pia humuwindi ili kumuua.
Nyoka gani mwingine anafanya multiple bites? Afrika, Kenya?
 
Back
Top Bottom