Msaada wa haraka kwenye tatizo hili la kiafya/ Ulozi

Msaada wa haraka kwenye tatizo hili la kiafya/ Ulozi

Sa 7 mchana

JF-Expert Member
Joined
Dec 30, 2018
Posts
5,214
Reaction score
10,276
Let me cut the bullshit and hit the point.

Leo nimepokea simu kutoka nyumbani, Napewa taarifa kuwa mdogo wangu wakiume amepata matatizo anapoteza fahamu.
Tatizo limeanza siku chache zilizopita( yani ijumaa ya tarehe 04.02.2022). Kijana aliondoka asubuhi sana kwenda shule, mashuhuda wanasema aliwahi sana siku hiyo isivyokawaida yake maana Kijana aliondoka sa kumi na Moja (11) alfajiri.
Mdogo wangu njiani alikutana na wenzie wawili na kufanya msafara uwe wa wanafunzi wa tatu.

Watatu hao walijongea mpaka shuleni. Baada ya kukaa kwa muda kidogo, dogo aliwaacha wenzie kuelekea chooni. Ila uko chooni dogo alikaa sana mpaka wenzie wakashuku kuwa kunakitu hakipo sawa, ikabidi waenda kumuangalia. Kufika uko dogo wakamkuta amedondoka chini hajitambui na ni kama amenyooka hivi.
Hivyo wakafanya utaratibu wa kumpeleka hospitali ila huko hakubahatika kupata nafuu wala kugundulika anatatizo lolote la kiafya ilihali dogo alikua bado hajitambui na amegangamara.

Siku hiyo hiyo ya Ijumaa ikabidi dogo apelekwe kwenye maombi kanisani.
Maombi yalifanya kuanza sa tatu asubuhi mpaka sa kumi na mbili jioni dogo akazinduka.

Jumamosi ya jana dogo siku nzima aliitumia kanisani (sabato). Ila kimbembe leo tena Jumapili, naambiwa dogo ameamka sa 11 alfajiri anajiandaa kuelekea shule, shuhuda dada wa kazi. Kumuuona vile akaenda kumshitua faza hausi. Dogo alivyokua "busted" pale pale kazima tena.

Duh ikawa ni noma sana, maombi yalifanyika na nyimbo, dogo akawa sawa. Dogo akaulizwa anakumbuka nini alivyoviona ama kuviishi muda mchache iliyopita. Dogo anasema alikua malaloni wanaofanya mazishi, anaulizwa mazishi ya nani hasemi.

Muda wa chakula cha mchana umefika dogo anasema ameshiba, eti ameshakula, anaulizwa umekula nini anasema kala nyama masibani. Watu duh!!!!

SASA NIMEKUJA KWAKO WANA JAMII FORUM.
Nakukaribisha utoe mchango wako wa mawazo ilituweze kumuundolea adha hii mdogo wetu mana hali ni mbaya japo siku ni chache. Ila pale anapokua amepoteza fahamu pia haja zote mdogo na kubwa hutoka bila kujizuia.

Ulishawahi kusikia kesi kama hii?
Je, mtu aliekubwa na hali hii alitibiwaje?

Am open kupokea kila aina ya tiba utakayoipendekeza iwe hospitali, ya kiimani au asili.

MCHANGO WAKE NI MUHIMU SANA KWA MDOGO WETU
 
Mkuu mimi ni Muislamu wacha nikueleze situation yko kwa mafundisho ya dini yetu

Chooni ni Sehemu wanayokaa mashetani na majini mabaya kwaio sisi tukiingia chooni tunasoma Dua ili kujikinga na hayo madudu

Huyo mdogo wako.kapatwa na hali iyo na wengine hutokea wakapigwa makofi mpk kufa mna hao majini wa huko chooni ni wabaya

Mm ninae mtu ambae anafanya visomo hivo na atakusaidia kma ukitaka nipm

N.b. Nipo kwa nia ya kukusaidia wala sio wizi
 
Keep on praying!, Hivyo ni vifungo vya shetani, hayo ni mapepo, mpeleke kanisani( kamati ya maombi) tafuta kanisa la wasabato lililokaribu watafanya maombi, hakuna kitu hapo
Inabidi tuweke kambi kanisani
 
Hongereni mdogo wako ana nafsi nzito, ilitakiwa palepale chooni shuleni awe amevuta, au amepoteza fahamu moja kwa moja..

Naomba niwafundisheni jambo wana JF, msipende kutumia vyoo vya public sehemu yoyote.. Na pia mnapoingia chooni tangulizeni mguu wa kushoto na pia sema 'Mungu naomba nilinde'....

Msipokuwa serious hatofika tarehe4 ya mwezi ujao , yani hatomaliza mwezi tangu hilo tatizo limpate..
 
mkuu mimi ni Muislamu wacha nikueleze situation yko kwa mafundisho ya dini yetu

Chooni ni Sehemu wanayokaa mashetani na majini mabaya kwaio sisi tukiingia chooni tunasoma Dua ili kujikinga na hayo madudu

Huyo mdogo wako.kapatwa na hali iyo na wengine hutokea wakapigwa makofi mpk kufa mna hao majini wa huko chooni ni wabaya

Mm ninae mtu ambae anafanya visomo hivo na atakusaidia kma ukitaka nipm

N.b. Nipo kwa nia ya kukusaidia wala sio wizi
Visomo ni bure au
 
Hongereni mdogo wako ana nafsi nzito, ilitakiwa palepale chooni shuleni awe amevuta, au amepoteza fahamu moja kwa moja..

Naomba niwafundisheni jambo wana JF, msipende kutumia vyoo vya public sehemu yoyote.. Na pia mnapoingia chooni tangulizeni mguu wa kushoto na pia sema 'Mungu naomba nilinde'....

Msipokuwa serious hatofika tarehe4 ya mwezi ujao , yani hatomaliza mwezi tangu hilo tatizo limpate..
Mbona umetutisha mkuu? Japo yana ukweli ndani yake ... ngoja nitoe ushuhuda kidogo

Mimi naishi hapa dar ila kuna siku usiku niliamka kwwda haja ndogo nlipo fika toilet baada ya kumaliza haja nlipata kizungu zungu cha gafla
Mwili wote uka toka jasho

Nlijitahidi kutoka nje japo kwa tabu sana nikajikongoja hadi mlangoni nlipo pigwa na upepo kidogo nikajiskia afadhali ikanibidi nikae chini kwanza notafakari hali iliyo nipata ilinichukua kama dk 10 ivi ndo nkawa sawa ndipo nikaingia ndani

Mpaka Leo cjajua ile hali ilisababishwa na nini
Na kwenda toilet usiku ilikoma
 
Hhahaa mi sipingani na imani yeyote lkn pia ngoja nitoe maelezo kitaaluma,kulingana na maelezo yako!

Inaoneka mdg wako amepata kifafa(juvenile onset Epilepsy) ni ugonjwa ambao una sababu zake nyingi tu lkn inahitajika history ambayo itakua imejitosheleza kujua chanzo chake.

….anyway fika hospital ya karibu utapatiwa tiba,usipuuzie unaomia hapo ni ubongo!!
Sikati Dua na maombi lkn pia zingatia sana ushauri wa kitaalam dogo atakaa fresh na masomo yanaendelea
 
Mbona umetutisha mkuu? Japo yana ukweli ndani yake ... ngoja nitoe ushuhuda kidogo

Mimi naishi hapa dar ila kuna siku usiku niliamka kwwda haja ndogo nlipo fika toilet baada ya kumaliza haja nlipata kizungu zungu cha gafla
Mwili wote uka toka jasho

Nlijitahidi kutoka nje japo kwa tabu sana nikajikongoja hadi mlangoni nlipo pigwa na upepo kidogo nikajiskia afadhali ikanibidi nikae chini kwanza notafakari hali iliyo nipata ilinichukua kama dk 10 ivi ndo nkawa sawa ndipo nikaingia ndani

Mpaka Leo cjajua ile hali ilisababishwa na nini
Na kwenda toilet usiku ilikoma

Hii hutokea kwa watu wengi tu na Jibu ni rahisi sana
Ukiamka ghafla kutoka usingizini mara nyingi pressure hushuka ghafla kwa sababu ya change in position kitaalam tunaina postrual hypotension….
Ushauri ukiamka kaa kidogo kitandani kabla ya kusimama!
 
Back
Top Bottom