kikoozi
JF-Expert Member
- Jun 24, 2015
- 2,094
- 3,108
Habari za uzima ndugu zangu, poleni sana na miangaiko ya hapa na pale, Mimi ni kijana mwenye miaka 37 kwa sasa elimu yangu ni degree, kama mnakumbuka nilishawai kuja na uzi wa baba yangu mzazi wa kunizaa kunitimua nyumbani kisa eti mimi ni mwanachama wa chama cha mapinduzi kisa cha kunifukuza ni kumshawishi yeye nae ajiunge kwenye chama cha mapinduzi (CCM)
Baada ya kunitaka niondoke kwake nilimuomba anirudishie pesa yangu niliokuwa nimemuazima kipindi nasoma chuo shilingi laki 7, aligoma kunipa mwanzoni ila baadae nilienda kwa mwenyekiti wa serikali za mtaa ili kuendelea kupigania haki yangu
Baba aliitwa serikali za mtaa, na alikubali kutoa pesa yangu kwa sharti moja tu, kama atanipa pesa yangu nisije kuonekana pale nyumbani, niame kabisa na nisije kukanyaga, mbaya zaidi alitoa maneno makali kabisa ya kusema kuwa niende kwa hao ccm ambao wananipa kiburi wakanipe nyumba ya kukaa (wakati anaongea maneno ayo mbele ya mwenyekiti wa serikali za mtaa ambaye ni mwenyekiti pia wa serikali za mtaa) nilisikitika sana wakuu.
Baada ya siku 6 baba alinipatia pesa yangu yote laki 7, siku hiyo hiyo nikaondoka nyumbani na kwenda kupanga chumba cha umeme pamoja na kununua godoro niakaanza maisha ya kubangaiza tangu mwaka jana,
Tatizo linaanzia hapa
Kodi yangu ilikuwa inamalizika mwezi wa nne tarehe 30, na sehemu tulipokuwa tunafanya kazi kama kibarua nilipunguzwa na kiwanda baada ya kuona uzalishaji umepungua kutokana na hili janga la corona, kwa hiyo tangu mwezi wa 3 nipo tu nyumbani sina kazi wala kibarua, baba mwenye nyumba alinieleza mapema kama naendelea na chumba au basi atafute mpangaji mwingine, nilimueleza kuwa atafute tu mpangaji maana sina pesa hata senti,
Mwisho wa mwezi uliopita nikatakiwa kuondoka pale nilipokuwa nakaa, nikampigia simu mzee wangu kumwelewesha kuwa pale ni kwetu natakaiwa kurudi kama mtoto maana sina pa kwenda, baba alipokea simu na baada ya kujua ni mimi akakata simu, Mimi nikabeba vitu vyangu nikaenda navyo palepale nyumbani, nimeshangaa sana mzee ananizuia nisiingie nyumbani. baba yangu mzazi amediliki kuniambia mimi sio mwanae mimi ni kibaka tu
Mpaka imefikia hatua ya kumweka mtu mlangoni ahakikishe kuwa hakuna mtu ambaye afahamiki kuingia pale ndani nikiwemo mimi, nilienda kwa mwenyekiti wa serikali za mtaa jana, akaniambia pale ni nyumbani na mzazi hapaswi kumfukuza mtoto katika kipindi kama hiki cha janga ili zito,
Mwenyekiti akaniambia ili huyu mzee asirudie iki kitendo cha kunifukuza inatakiwa niende kwenye ngazi ya kata, leo nimeenda kwenye kata na kuwaeleza mkasa mzima nimeshangaa sana yaani viongozi wa kata wanasema mimi inawezekana sina akili timamu, hapo akili ikanijia moja kwa moja mzee ameshatoa hongo kwenye ngazi ya kata ili nisiipate haki yangu kama mtoto, nimepanga kesho kwenda kwenye ngazi ya juu zaidi ya kuipigania haki yagu kama mtoto nirejee nikae pale nyumbani mpaka ili gonjwa litakapopita, kitu kingine naona kabisa hata kwenye ulithi kuna hati hati nikadhurumiwa na huyu baba,
Naombeni ushauri wenu wakuu.
Niende ngazi gani au nitumie njia gani huyu mzee asininyanyase kwenye nyumba nikiwa kama mtoto wake?
Na pia kama itatokea mirathi niwepo pasipo kupunjwa?
Baada ya kunitaka niondoke kwake nilimuomba anirudishie pesa yangu niliokuwa nimemuazima kipindi nasoma chuo shilingi laki 7, aligoma kunipa mwanzoni ila baadae nilienda kwa mwenyekiti wa serikali za mtaa ili kuendelea kupigania haki yangu
Baba aliitwa serikali za mtaa, na alikubali kutoa pesa yangu kwa sharti moja tu, kama atanipa pesa yangu nisije kuonekana pale nyumbani, niame kabisa na nisije kukanyaga, mbaya zaidi alitoa maneno makali kabisa ya kusema kuwa niende kwa hao ccm ambao wananipa kiburi wakanipe nyumba ya kukaa (wakati anaongea maneno ayo mbele ya mwenyekiti wa serikali za mtaa ambaye ni mwenyekiti pia wa serikali za mtaa) nilisikitika sana wakuu.
Baada ya siku 6 baba alinipatia pesa yangu yote laki 7, siku hiyo hiyo nikaondoka nyumbani na kwenda kupanga chumba cha umeme pamoja na kununua godoro niakaanza maisha ya kubangaiza tangu mwaka jana,
Tatizo linaanzia hapa
Kodi yangu ilikuwa inamalizika mwezi wa nne tarehe 30, na sehemu tulipokuwa tunafanya kazi kama kibarua nilipunguzwa na kiwanda baada ya kuona uzalishaji umepungua kutokana na hili janga la corona, kwa hiyo tangu mwezi wa 3 nipo tu nyumbani sina kazi wala kibarua, baba mwenye nyumba alinieleza mapema kama naendelea na chumba au basi atafute mpangaji mwingine, nilimueleza kuwa atafute tu mpangaji maana sina pesa hata senti,
Mwisho wa mwezi uliopita nikatakiwa kuondoka pale nilipokuwa nakaa, nikampigia simu mzee wangu kumwelewesha kuwa pale ni kwetu natakaiwa kurudi kama mtoto maana sina pa kwenda, baba alipokea simu na baada ya kujua ni mimi akakata simu, Mimi nikabeba vitu vyangu nikaenda navyo palepale nyumbani, nimeshangaa sana mzee ananizuia nisiingie nyumbani. baba yangu mzazi amediliki kuniambia mimi sio mwanae mimi ni kibaka tu
Mpaka imefikia hatua ya kumweka mtu mlangoni ahakikishe kuwa hakuna mtu ambaye afahamiki kuingia pale ndani nikiwemo mimi, nilienda kwa mwenyekiti wa serikali za mtaa jana, akaniambia pale ni nyumbani na mzazi hapaswi kumfukuza mtoto katika kipindi kama hiki cha janga ili zito,
Mwenyekiti akaniambia ili huyu mzee asirudie iki kitendo cha kunifukuza inatakiwa niende kwenye ngazi ya kata, leo nimeenda kwenye kata na kuwaeleza mkasa mzima nimeshangaa sana yaani viongozi wa kata wanasema mimi inawezekana sina akili timamu, hapo akili ikanijia moja kwa moja mzee ameshatoa hongo kwenye ngazi ya kata ili nisiipate haki yangu kama mtoto, nimepanga kesho kwenda kwenye ngazi ya juu zaidi ya kuipigania haki yagu kama mtoto nirejee nikae pale nyumbani mpaka ili gonjwa litakapopita, kitu kingine naona kabisa hata kwenye ulithi kuna hati hati nikadhurumiwa na huyu baba,
Naombeni ushauri wenu wakuu.
Niende ngazi gani au nitumie njia gani huyu mzee asininyanyase kwenye nyumba nikiwa kama mtoto wake?
Na pia kama itatokea mirathi niwepo pasipo kupunjwa?