Msaada wenu wakuu, nateketea ndani kwa ndani

Msaada wenu wakuu, nateketea ndani kwa ndani

Daaah mpaka nakuonea huruma jamaa, natamani nikuazime hizi akili na moyo wangu atleast ungeyashinda hayo.

Kama hapa tu kwenye maandishi uanonyesha kulialia hivi juu ya mwanamke (hadi naona aibu kusoma) huko ndani vipi mkuu? Usikute ukishawahi kumpigia magoti, labda ukamwambia hauwezi kuishi bila yeye, ukampigia simu ukilia na kuomba akurudie, ukamwambia akikuacha utajiua...hapo huwezi kujenga mahusiano ukiwa legelege hivi mkuu.


BE A MAN, japo kwa mazingira ya story yako ni ngumu ila ukiweza utakuwa umeishinda vita kubwa sana.
 
Msaada wenu wakuu, nateketea ndani kwa ndani.

Binafsi breakup nilishashindwa kuizoea, huwa inaleta maumivu haijalishi ni breakup ya ngapi.

Nisiwachoshe sana acha niende moja kwa moja kwenye tatizo langu.

Mimi nina mke na watoto wawili na mke wangu lakini pia kuna mzazi mwenzangu ambaye nilishashindwa kumuacha kabisa licha ya matukio anayonipiga kila baada ya muda. Huyu mzazi mwenzangu ndio ninayemleta hapa kwenu. Nimekuwa naye yapata miaka 6 sasa na mtoto wetu ana miaka 4.

Acha tu niwe muwazi ili kama ni kupata msaada niweze kupata maana najua humu JF kuna watu wenye busara ambao wanaweza kutoa ushauri wa kujenga. Kiukweli huyu mzazi mwenzangu nampenda sana yaani mno hata yeye analijua hilo japo huwa haishi kujikasirisha na kujisemesha kuwa simpendi bali namtumia tu.

Ukweli uliopo ndani ya moyo wangu nampenda sana kiasi kwamba huwa nashawishika nimuoe mke wa pili japo dini yetu hairuhusu. Lakini huwa nashawishika kujilipua tu nimuoe hivyohivyo kwa namna yoyote itakayowezekana.

Sasa huyu mzazi mwenzangu hatujawahi kuwa na stable relationship kwa muda mrefu. Furaha yetu imedumu sana labda mwezi mmoja lakini throughout ya mahusiano yetu ni migogoro tu, hakuna amani kabisa.

Tunaweza kukaa kwa amani na kufurahia mahusiano lakini the next thing utakuta unaibuka mtafaruku japo mtafaruku nao huwa haudumu. Mnaweza kuzinguana asubuhi lakini kufikia mchana mmeyamaliza na kuanza kucheka tena.

Au mnaweza kuzinguana leo ikadumu hadi wiki, anaomba msamaha namsamehe yanaisha. Hii ndio imekuwa routine yetu ya mahusiano kwa muda wote huu wa miaka 6. Kuna kipindi tulikuwa tunachuniana hadi miezi 3 lakini baadae tena tunatafutana, tunarudiana na penzi linaanza upya.

Lakini tangia July 2021 hadi hivi jana (Jumamosi) tulikuwa hatujagombana hadi ile kuachana kama ilivyokuwa inafanyika miaka ya nyuma ambapo tulikuwa tunagombana na kuchuniana hadi miezi 3, 2,1 and weeks. Ingawa hii mikwaruzano ya mara kwa mara na kuchuniana kwa wiki au siku kadhaa bado ipo kama nilivyoeleza hapo juu.

Sasa kilichotokea jana nahisi tunaenda kubreakup forever au kwa muda mrefu tena kabla hatujarudiana. Kama nilivyosema hapo awali, huyu mwanamke nampenda sana, hii break up inanitafuna ndani kwa ndani, sipati usingizi, japo dakika hii ninapoandika hapa maumivu yamepungua ukilinganisha na jana au usiku wa kuamkia leo.

Natamani kuachana naye moja kwa moja lakini nahisi siwezi, labda yeye aamue kuniacha moja kwa moja. Ila mimi nahisi siku akinipigia tu simu nitatepeta.

Ugomvi wetu huwa unasababishwa na tabia zake. Kwa kweli mimi kama mwanaume kuna tabia huwa sizipendi kuziona kwa mwanamke ninayempenda. Huyu mwanamke anapenda sana mpira, ni mshabiki wa simba. Yaani ni kama mwendawazimu linapokuja swala la mpira.

Kuna muda nilihack account yake ya instagram nilikuta ana wa-dm wachezaji kama vile anajitongozesha. Nilikuta miconversation kama vile anajitongozesha kwa wachezaji, yaani yeye ndio ana-initiate conversation. Mimeseji kibao, wachezaji tofautitofauti, anagawa namba bila hata kuombwa.

Wachezaji wa Simba, Mtibwa, Namungo yaani kama wote. Ukimwuliza kwa nini anafanya hivi yeye anachukulia poa tu. Anakuambia yeye anachat nao tu wala hawatongozi, anasema maisha ya mtandaoni ni fake hivyo hizo chattings hazina maana yoyote ile bali ni fake life ya maisha ya mitandaoni.

Nilimwambia sipendi hiyo tabia inanikwaza yeye akawa anasisitiza hayo ni mambo ya mtandaoni hayana maana yoyote, anadai yeye ni mtu mzima anajielewa hivyo niache wivu wa kipumbavu, dah! Kwa hiyo hii ilikuwa moja ya sababu ya makwaruzano yetu maana niliendelea kuwa na access ya account yake zaidi ya miezi mitano kama sio sita ila baadae akaja kunilog out nikawa siwezi tena kuona kinachoendelea huko.

Kitu kingine ambacho sipendi ni kuikuta simu yake iko busy mara kwa mara. Ni mara chache sana siku inaweza kupita ukampigia usikute simu inatumika. Mie huwa namwuliza mbona wewe simu yako haiwezi ikapita siku nisiikute ikiwa busy?

Hii tabia hadi leo hii haijabadirika, na hii ni moja ya sababu za ugomvi wetu. Ila wakuu nisiwafiche nafsi huwa inaniambia nimezaa na malaya, ila naomba mniambie kama fikira zangu labda sio za kweli. Halafu mwanamke mwezi huu ndio katimiza miaka 25, nilianza naye mahusiano akiwa na miaka 19.

Miezi michache iliyopita nilibahatika kupata ajira serikalini na nikapelekwa mkoa ambao sio mbali na Dar. Huwa mara moja kwa mwezi siku za weekend naenda Dar kuiona familia na kuonana na mzazi mwenzangu. Na yeye mzazi mwenzangu huwa anakuja mara moja kwa mwezi huku nilipo, hivyo huwa tunaonana mara mbili kwa mwezi (Yeye anakuja mara moja na mimi naenda mara moja).

Nilipopangiwa huku yeye ndio alifanya manunuzi ya vitu vya ndani. Nilimtumia hela akaenda Kariakoo akaninunulia vitu vya ndani kama friji, vyombo n.k na kuzisafirisha kwa kutumia transpoter.

Hii point haina maana yoyote ila ninachotaka kukiwasilisha kwenu ni kwamba yeye ndio mnunuzi wa vitu vya ndani japo mie ndio mtoa hela hivyo inatufanya tujihisi huku ndio kwake. Yeye ndio huwa anakuja huku, mke wangu hajawahi kuja huku.

Na hii yote nilitaka kumjenga kisaikolojia kwamba huku ni kwake. Infact nilishamwambia huku ni kwako, Dar ni kwa mwenzio maana huwa nashawishika kumuoa kama nilivyotangulia kusema hapo awali.

Tatizo kubwa lililopelekea tubreak up this time around ni hili swala la yeye kuja huku. Huwa akija huku anafika jioni, analala na kesho yake mchana anarudi Dar. Basically huwa hakai hata siku. Anakuwepo usiku mmoja tu na hiyo asubuhi hadi mchana.

Wiki mbili zilizopita nilikuwepo Dar hivyo Jumapili ya leo ilikuwa zamu yake kuja. Toka nirudi kutoka Dar hadi jana tulikuwa hatuna mawasiliano mzuri na mimi nilikuwa nahisi kwa hali hii anaweza asije. Mimi nilimwambia nimechoka kukubembeleza na kuwa mtumwa wa mahusiano, usipokuja tunaachana.

Yeye akawa anasisitiza atakuja japo dalili zilikuwa zinaonyesha hawezi kuja. Na wiki zote hizi mbili tulikuwa na mtafaruku mkubwa sana ambao tulikuwa tunatoleana kauli za kuachana na kubaki kuwa kama wazazi tu.

Kweli kama nilivyotegemea leo hakuja kama tulivyopanga, anadai amechoka kuwa mtumwa wa mapenzi. Na mimi nimemwambia basi tuachane tu maana hata mimi nimechoka. Haya yote yametokea jana Jumamosi.

Sasa wakuu kama nilivyowaambia hapo awali, nateketea ndani kwa ndani japo kwa sasa najihisi maumivu yamepungua ukilinganisha na jana ila kila nikimkumbuka moyo unakuwa kama unataka kuchomoka.

Natamani haya mahusiano yaishe maana ni mateso sana kuwa kwenye mahusiano na mwanamke usiyemuamini ila natamani arudi tu tuendelee kuwa pamoja tulee mtoto wetu licha ya haya mateso anayonipitisha.

Pamoja na ushauri wenu nataka kujua, kwa mtazamo wenu huyu mwanamke ananipenda kweli, au miaka yote sita naforce mapenzi. Mara nyingi tu akinizingua sana huwa namblock hata wiki lakini atapiga simu na kuomba msamaha, atatumia maneno yote mazuri ya kubembeleza ili nimsamehe.

Na mie huwa namblock tu ili kumwonyesha kuwa naweza kuishi bila yeye ila huwa sina dhamira ya dhati ya kumuacha. Kwa hiyo akinibembeleza siku 3 mfululizo kwa msg na simu namua-unblock na maisha yanaendelea.

Kuna watu wataanza kuuliza kama mtu umemblock atawezaje kukupigia na kukutumia msg? Jibu ni kwamba kuna sehemu unaenda na kukuta msg za namba uliyoiblock, Samsung namba uliyoiblock ikipiga huwa inaonyesha pale kwenye call register.
Kuwa masicular bwana acha kulilia penzi mwanaume mwenzangu, hiyo ni kazi ya wanawake.

Piga moyo konde, endelea na life jingine na ufocus kwa mkeo.

Kama ameshindwa kufuata unayotaka afuate utakaaje nae? Yanu eti upo tayari kukaa nae licha ya mateso anayokupatia?

Kwenye mahusiano wewe kama mwanaume unatakiwa kuwa kiongozi kisha mwanamke afuate maoni yako au kukushauri pale unapoenda mrama, sasa kama unataka kuuza uanaume wako kisha penzi utaishi ukiteseka miaka yote.
IMG_20221219_121842.jpg
IMG_20221219_121910.jpg
 
Ahhh sijasoma mpaka mwisho ila huyo mchepuko ana mambo mengi kumzidi hata mama j wa Mzee DeepPond ni kama amekufanya wewe ni kibatari ( taa ndogo za zamani zinazotumia mafuta ya taa) anakuwasha na kukuzima muda wowote atakao.

Kuwa kifikra kuzaasio sababu em Kaa kwa kutulia muache utaumia lakin utapona na maisha yataendelea,, sio vyema mwanaume kuwa kama ndezi buana
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]

Huo msitari wa mwisho umenichekesha sana[emoji23].
 
Mbona naona kama umeshikwa akili hivi au labda dish limeyumba?

Una mke wa ndoa, na una mwanamke uliyezaa naye mtoto kabla ya yule wa ndoa...

Lakini akili yako inapelekeshwa na huyo uliyezaa naye na mmejiachia kama wanandoa vile...

Shubamittti
Hana akili huyo achana nae aendeshwe Kuna siku atapata akili
 
itoshe kusema kwa kipande hichi kwangu ingekua ni talaka tosha View attachment 2451329
Hapo Hakuna Mwanaume Kuna mvulana na mjinga.

Then watu Kama Hawa baadae wanakuja kuomba ushauri,huwa nawajibu simple tuu kwamba huna akili ngoja unyooshwe Hadi akili zikae sawa..

Kiufupi sijawahi sumbuliwa Wala kubabaishwa na mwanamke,Nina uwezo wa kupiga chini mwanamke yeyote na nikikata shauri sijawahi Rudi nyuma kwa sababu Sina dhiki ya K Wala furaha yangu haiko kwenye K.
 
Pole sana mkuu,
Kwa uelewa wangu wewe ndio tatizo namba 1
2 je mkeo anajua haya?
3 mchepuko wako anajua km upo na mke si ndio?
Tujiulize mimi na wewe swali hili
Je unapokua na mkeo mchepuko hua yupo na nan?
Hivi unadhan yeye ni mjinga?
Kichwan kwake ameshavua upendo amebakiza uzazi mwenza!
Tarajia maamuzi yoyote kutoka kwa mzazi mwenzako kwasababu huna chakumzuia


Kinachokutesa wewe ni mazoea na sio upendo
Wekeza nguvu maamuzi na mawazo yako kwa mkeo na familia
Huyo mchepuko sio issue tena






Bythewayndiomaanasitakikuowasinglemother
 
Shida kubwa ambayo ni mbaya niliyoiona kwako ni EFFEMINATE CHARACTER, na hii itakutesa sana mkuu. Kwa lugha nyingine tunasema wewe ni SIMP.

Kwenye mahusiano yoyote yale unapoonyesha kuwa unampenda sana mwanamke na kwamba eti "hauwezi kuishi bila yeye" basi anguko lako linatabirika kabisa hata kama huko nyuma mlipendana kiasi gani.

Sikia wewe ni mwanaume huwezi kukaa ukasumbuliwa na kipampa ambaye ushamzalisha kabisa, focus na mambo yako mengine ya kimaisha ukiruhusu stress zikutawale utashindwa kutafuta hela na hata siku moja huyo mwanamke wako hatakuja kujutia kuachana na wewe kutokana na hiyo hali mbaya ya maisha uliyonayo.

Ondoa huo mtazamano wa ONEITS linapokuja swala la wamawake, wapo wengi mno wazuri na wenye tabia nzuri tu sema ndo hivyo umeshakosea tayari.
[emoji1541][emoji1541][emoji1541][emoji1541]

NB; Kosa kubwa ulilowahi kufanya ni kuingia haraka kwenye mahusiano mengine baada ya wewe kuachana na mzazi mwenzako, matokeo yake ukachukua mwanamke mwingine usiyempenda, ungetulia ukaachana na mapenzi kabisa naamini ungekuja kupata mwanamke unayempenda kiasi cha kumsahau huyo mjinga.View attachment 2451681
Mwenye maskio na asikie

Sent using Jamii Forums mobile app
 
kweli unammudu[emoji28][emoji28][emoji28]
Huwa Anapenda kujizima Sana data yule,

Na niliwahi kumwambia Kama Kuna mganga kakupa limbwata ndo analijaribu Basi kakutapeli, bado nna akili zangu timamu.

Usinifanyie vitu ambavyo vinadhalilisha utu wangu ukadhan ntakuchekea kisa nakupenda au nahofu ntaachwa.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Huwa Anapenda kujizima Sana data yule,

Na niliwahi kumwambia Kama Kuna mganga kakupa limbwata ndo analijaribu Basi kakutapeli, bado nna akili zangu timamu.

Usinifanyie vitu ambavyo vinadhalilisha utu wangu ukadhan ntakuchekea kisa nakupenda au nahofu ntaachwa.

Sent using Jamii Forums mobile app
[emoji28][emoji28][emoji28]kajifunza kwakweli ni vizuri unamkumbusha nafasi yake hapa ndowengi wanapofeli mpk mchepuka anajiona mke
 
[emoji28][emoji28][emoji28]kajifunza kwakweli ni vizuri unamkumbusha nafasi yake hapa ndowengi wanapofeli mpk mchepuka anajiona mke
Sahii kabisa,

Yaan mtu anajiona mungu mtu wako
Anataka aabudiwe hatak kuskia excuse yyt akishapanga Jambo lake.

Hii Ni tabia ya kumanipulate akili yako na ikiendelea hivi Kuna siku atakwambia ua wazazi/mke/watoto wako ukishindwa tuachane.



Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ahhh sijasoma mpaka mwisho ila huyo mchepuko ana mambo mengi kumzidi hata mama j wa Mzee DeepPond ni kama amekufanya wewe ni kibatari ( taa ndogo za zamani zinazotumia mafuta ya taa) anakuwasha na kukuzima muda wowote atakao.

Kuwa kifikra kuzaasio sababu em Kaa kwa kutulia muache utaumia lakin utapona na maisha yataendelea,, sio vyema mwanaume kuwa kama ndezi buana
Utoto unakusumbua. Ukikua utajitambua.

Hata haujui maana ya mke na mzazi mwenzia!!?
Halafu mzazi mwenza wa mazingira unayotueleza!!
Mzinifu wewe. Acha uzinzi.
 
Kwa mujibu wa tafiti za kiroho inathibitishwa kuwa asilimia 75 ya wakazi wa hapa duniani hawana nafsi. Ikumbukwe binadamu anakamilishwa na vitu vitatu ambavyo ni mwili, nafsi na roho. Nikisema tafiti za kiroho namanisha wenye uwezo wa kuona vitu wanaona jinsi demons au mapepo wanavyoruka kutoka ndani ya mtu mmoja na kwenda kwa mtu mwingine.

Chanzo cha binadamu/ watu kukosa nafsi ni moja ni kuzaliwa ukiwa hivyo ukiwa huna nafsi hii inaitwa glitch in the matrix na mbili ni kuuza nafsi ili uweze kutumika kama chombo (vessel/portal) na viumbe wa daraja la chini kama vijini. Mtu mwenye vijini au anayepandisha kijini huyo hana nafsi wala nguvu yoyote ya kiroho na muda wote huwa na hisia kama upepo unaingia mwilini mwake.

Kukosa nafsi kwa lugha rahisi naweza kutoa mfano wa kifaa kama Computer. Bila kuwekwa Operating system computer haiwezi kufanya kazi kwamfano huo ni kwamba ili uweze kutumia vizuri computer ni lazima uwe na Windows bila hiyo windows inakuwa computer ambaye haija kamilika.

Watoto wengi waliozaliwa kuanzia miaka ya 2000 (millennials) wengi wao hawana nafsi ni kama Bots tuu. Maisha yao ni vanity and greedy hawana uwezo wa kuchambua hoja au uwelewa wa kuwa na malengo katika maisha yao. Hawana malengo isipokuwa wachache sana ambao wamebahatika kuzaliwa wakiwa kamili.
Noma sana!
 
Back
Top Bottom