Msaada wenu wakuu, nateketea ndani kwa ndani

Msaada wenu wakuu, nateketea ndani kwa ndani

Kama ulizaa naye na unampemda kwa nini ulioa mwingine? Shuba miti.

Na unafikiri yeye anajisikiaje, umri wake unaendelea ku songa, wewe una mshikilia tu. Huyo si fala na siku si nyingi.atakuletea kadi ya mchango.
 
Kila siku tunasema apa kuwa ukioa single mama hakikisha narudia tena hakikisha umeona kaburi la mme wake
 
MDA si mrefu Hapa nmetoka kuzinguana na mchepuko wangu mamaJ.

Mida ya saa 9 Tulkua tunachat,
Uchovu wa kutoka kazin Baada ya kufka home nikapitiwa na usngz.

Nikaja kustuka ni saa 12 mbio mbio nikaenda kuchek WORLD CUP bar mechi ishafk dkk ya 17.

MDA wote wa mechi Niko live in play natandaza mikeka na kukagua mikeka yangu inavochanika roho iko juu juu MDA wote.

Baada ya mechi ikabd nimchek tupige stories, ghafla mwanamke kaanza kujitia ujuaji mbuzi na kuleta kisirani mbuzi.

Ikabd nimuwakie mbovu mbovu mpk kaamua kuzima sim yake mwnyw.

View attachment 2451284View attachment 2451285View attachment 2451287

Sent using Jamii Forums mobile app
Mkuu ww ni mwamba kweli kweli kama Mpabe me huwa nakukubali sana japo sikujui
 
MDA si mrefu Hapa nmetoka kuzinguana na mchepuko wangu mamaJ.

Mida ya saa 9 Tulkua tunachat,
Uchovu wa kutoka kazin Baada ya kufka home nikapitiwa na usngz.

Nikaja kustuka ni saa 12 mbio mbio nikaenda kuchek WORLD CUP bar mechi ishafk dkk ya 17.

MDA wote wa mechi Niko live in play natandaza mikeka na kukagua mikeka yangu inavochanika roho iko juu juu MDA wote.

Baada ya mechi ikabd nimchek tupige stories, ghafla mwanamke kaanza kujitia ujuaji mbuzi na kuleta kisirani mbuzi.

Ikabd nimuwakie mbovu mbovu mpk kaamua kuzima sim yake mwnyw.

View attachment 2451284View attachment 2451285View attachment 2451287

Sent using Jamii Forums mobile app
Masikini mamaj na bado alivyozwazwa atakupa kipapwizo..khaa
 
Miaka 6 mbona kidogo

Mimi nina pasua kichwa wangu mwaka wa 20 huu ni stop-start-stop-start.

Pasua kichwa kweli lkn tumeshindwa kuachana, sometimes hatuongei hata mwaka lkn somehow badae tatizo linatokea namsaidia kutatua tunarudiana tena, then tutaachana tena
Unatafuta ukimwi
 
Utoto unakusumbua. Ukikua utajitambua.

Hata haujui maana ya mke na mzazi mwenzia!!?
Halafu mzazi mwenza wa mazingira unayotueleza!!
Mzinifu wewe. Acha uzinzi.
Mkuu sijakuelewa
Utoto unakusumbua. Ukikua utajitambua.

Hata haujui maana ya mke na mzazi mwenzia!!?
Halafu mzazi mwenza wa mazingira unayotueleza!!
Mzinifu wewe. Acha uzinzi.
Mkuu sijakuelewa hata kidogo Sasa hapo mie uzinifu wangu uko wapi. Na huo utoto umeupima Kwa namna Gani?
 
Ukishaona unaanza kuomba ushauri sjui unataka kujua kama anakupenda au hakupendi

Basi jua haupendwi na deep inside you know it. Ila unatafuta comfort zone hapa kuukataa uhalisia, na una expect watu tukwambie kuwa bibie anakupenda ili usuuzike nafsi. Ila unajua kabisa hauna chako

By the way ungekua unapendwa kweli usingekuja kuleta uzi hapa
 
Anakupenda, ila weee ndo unafanya mambo kua magumu.

Huyo keshajua unamke, hivo yupo nawewe kama Mzazi mwenzako.


Wewe naye badala ya kumchukulia kama Mzazi mwenzako, wee unanichukulia kama Mke.

Inaonekana siku akikuambia ,naolewa, UTAKUFA EEHH.


Relax, mchukulie kama Mzazi mwenzio, energy yako ,wekeza Kwa mkeo, huyu Mzazi mwenzio muishi kama Mzazi mwenzio tu .
mkuu umemwambia ukweli mchungu sana..asome hapa
 
Anakupenda, ila weee ndo unafanya mambo kua magumu.

Huyo keshajua unamke, hivo yupo nawewe kama Mzazi mwenzako.


Wewe naye badala ya kumchukulia kama Mzazi mwenzako, wee unanichukulia kama Mke.

Inaonekana siku akikuambia ,naolewa, UTAKUFA EEHH.


Relax, mchukulie kama Mzazi mwenzio, energy yako ,wekeza Kwa mkeo, huyu Mzazi mwenzio muishi kama Mzazi mwenzio tu .
kumbe sio tu kwenye kula kimasihara hata kwenye ushauri upo vyema mkuu[emoji23][emoji23][emoji23]
 
Uko mkoan una mpz dar utatesek san
Una block mtu bado unachat nae
Mwanamke hapendw sikuhz wew n kumjal tuu ili uwez kumuendesha
 
Natamani haya mahusiano yaishe maana ni mateso sana kuwa kwenye mahusiano na mwanamke usiyemuamini ila natamani arudi tu tuendelee kuwa pamoja tulee mtoto wetu licha ya haya mateso anayonipitisha.
 
Msaada wenu wakuu, nateketea ndani kwa ndani.

Binafsi breakup nilishashindwa kuizoea, huwa inaleta maumivu haijalishi ni breakup ya ngapi.

Nisiwachoshe sana acha niende moja kwa moja kwenye tatizo langu.

Mimi nina mke na watoto wawili na mke wangu lakini pia kuna mzazi mwenzangu ambaye nilishashindwa kumuacha kabisa licha ya matukio anayonipiga kila baada ya muda. Huyu mzazi mwenzangu ndio ninayemleta hapa kwenu. Nimekuwa naye yapata miaka 6 sasa na mtoto wetu ana miaka 4.

Acha tu niwe muwazi ili kama ni kupata msaada niweze kupata maana najua humu JF kuna watu wenye busara ambao wanaweza kutoa ushauri wa kujenga. Kiukweli huyu mzazi mwenzangu nampenda sana yaani mno hata yeye analijua hilo japo huwa haishi kujikasirisha na kujisemesha kuwa simpendi bali namtumia tu.

Ukweli uliopo ndani ya moyo wangu nampenda sana kiasi kwamba huwa nashawishika nimuoe mke wa pili japo dini yetu hairuhusu. Lakini huwa nashawishika kujilipua tu nimuoe hivyohivyo kwa namna yoyote itakayowezekana.

Sasa huyu mzazi mwenzangu hatujawahi kuwa na stable relationship kwa muda mrefu. Furaha yetu imedumu sana labda mwezi mmoja lakini throughout ya mahusiano yetu ni migogoro tu, hakuna amani kabisa.

Tunaweza kukaa kwa amani na kufurahia mahusiano lakini the next thing utakuta unaibuka mtafaruku japo mtafaruku nao huwa haudumu. Mnaweza kuzinguana asubuhi lakini kufikia mchana mmeyamaliza na kuanza kucheka tena.

Au mnaweza kuzinguana leo ikadumu hadi wiki, anaomba msamaha namsamehe yanaisha. Hii ndio imekuwa routine yetu ya mahusiano kwa muda wote huu wa miaka 6. Kuna kipindi tulikuwa tunachuniana hadi miezi 3 lakini baadae tena tunatafutana, tunarudiana na penzi linaanza upya.

Lakini tangia July 2021 hadi hivi jana (Jumamosi) tulikuwa hatujagombana hadi ile kuachana kama ilivyokuwa inafanyika miaka ya nyuma ambapo tulikuwa tunagombana na kuchuniana hadi miezi 3, 2,1 and weeks. Ingawa hii mikwaruzano ya mara kwa mara na kuchuniana kwa wiki au siku kadhaa bado ipo kama nilivyoeleza hapo juu.

Sasa kilichotokea jana nahisi tunaenda kubreakup forever au kwa muda mrefu tena kabla hatujarudiana. Kama nilivyosema hapo awali, huyu mwanamke nampenda sana, hii break up inanitafuna ndani kwa ndani, sipati usingizi, japo dakika hii ninapoandika hapa maumivu yamepungua ukilinganisha na jana au usiku wa kuamkia leo.

Natamani kuachana naye moja kwa moja lakini nahisi siwezi, labda yeye aamue kuniacha moja kwa moja. Ila mimi nahisi siku akinipigia tu simu nitatepeta.

Ugomvi wetu huwa unasababishwa na tabia zake. Kwa kweli mimi kama mwanaume kuna tabia huwa sizipendi kuziona kwa mwanamke ninayempenda. Huyu mwanamke anapenda sana mpira, ni mshabiki wa simba. Yaani ni kama mwendawazimu linapokuja swala la mpira.

Kuna muda nilihack account yake ya instagram nilikuta ana wa-dm wachezaji kama vile anajitongozesha. Nilikuta miconversation kama vile anajitongozesha kwa wachezaji, yaani yeye ndio ana-initiate conversation. Mimeseji kibao, wachezaji tofautitofauti, anagawa namba bila hata kuombwa.

Wachezaji wa Simba, Mtibwa, Namungo yaani kama wote. Ukimwuliza kwa nini anafanya hivi yeye anachukulia poa tu. Anakuambia yeye anachat nao tu wala hawatongozi, anasema maisha ya mtandaoni ni fake hivyo hizo chattings hazina maana yoyote ile bali ni fake life ya maisha ya mitandaoni.

Nilimwambia sipendi hiyo tabia inanikwaza yeye akawa anasisitiza hayo ni mambo ya mtandaoni hayana maana yoyote, anadai yeye ni mtu mzima anajielewa hivyo niache wivu wa kipumbavu, dah! Kwa hiyo hii ilikuwa moja ya sababu ya makwaruzano yetu maana niliendelea kuwa na access ya account yake zaidi ya miezi mitano kama sio sita ila baadae akaja kunilog out nikawa siwezi tena kuona kinachoendelea huko.

Kitu kingine ambacho sipendi ni kuikuta simu yake iko busy mara kwa mara. Ni mara chache sana siku inaweza kupita ukampigia usikute simu inatumika. Mie huwa namwuliza mbona wewe simu yako haiwezi ikapita siku nisiikute ikiwa busy?

Hii tabia hadi leo hii haijabadirika, na hii ni moja ya sababu za ugomvi wetu. Ila wakuu nisiwafiche nafsi huwa inaniambia nimezaa na malaya, ila naomba mniambie kama fikira zangu labda sio za kweli. Halafu mwanamke mwezi huu ndio katimiza miaka 25, nilianza naye mahusiano akiwa na miaka 19.

Miezi michache iliyopita nilibahatika kupata ajira serikalini na nikapelekwa mkoa ambao sio mbali na Dar. Huwa mara moja kwa mwezi siku za weekend naenda Dar kuiona familia na kuonana na mzazi mwenzangu. Na yeye mzazi mwenzangu huwa anakuja mara moja kwa mwezi huku nilipo, hivyo huwa tunaonana mara mbili kwa mwezi (Yeye anakuja mara moja na mimi naenda mara moja).

Nilipopangiwa huku yeye ndio alifanya manunuzi ya vitu vya ndani. Nilimtumia hela akaenda Kariakoo akaninunulia vitu vya ndani kama friji, vyombo n.k na kuzisafirisha kwa kutumia transpoter.

Hii point haina maana yoyote ila ninachotaka kukiwasilisha kwenu ni kwamba yeye ndio mnunuzi wa vitu vya ndani japo mie ndio mtoa hela hivyo inatufanya tujihisi huku ndio kwake. Yeye ndio huwa anakuja huku, mke wangu hajawahi kuja huku.

Na hii yote nilitaka kumjenga kisaikolojia kwamba huku ni kwake. Infact nilishamwambia huku ni kwako, Dar ni kwa mwenzio maana huwa nashawishika kumuoa kama nilivyotangulia kusema hapo awali.

Tatizo kubwa lililopelekea tubreak up this time around ni hili swala la yeye kuja huku. Huwa akija huku anafika jioni, analala na kesho yake mchana anarudi Dar. Basically huwa hakai hata siku. Anakuwepo usiku mmoja tu na hiyo asubuhi hadi mchana.

Wiki mbili zilizopita nilikuwepo Dar hivyo Jumapili ya leo ilikuwa zamu yake kuja. Toka nirudi kutoka Dar hadi jana tulikuwa hatuna mawasiliano mzuri na mimi nilikuwa nahisi kwa hali hii anaweza asije. Mimi nilimwambia nimechoka kukubembeleza na kuwa mtumwa wa mahusiano, usipokuja tunaachana.

Yeye akawa anasisitiza atakuja japo dalili zilikuwa zinaonyesha hawezi kuja. Na wiki zote hizi mbili tulikuwa na mtafaruku mkubwa sana ambao tulikuwa tunatoleana kauli za kuachana na kubaki kuwa kama wazazi tu.

Kweli kama nilivyotegemea leo hakuja kama tulivyopanga, anadai amechoka kuwa mtumwa wa mapenzi. Na mimi nimemwambia basi tuachane tu maana hata mimi nimechoka. Haya yote yametokea jana Jumamosi.

Sasa wakuu kama nilivyowaambia hapo awali, nateketea ndani kwa ndani japo kwa sasa najihisi maumivu yamepungua ukilinganisha na jana ila kila nikimkumbuka moyo unakuwa kama unataka kuchomoka.

Natamani haya mahusiano yaishe maana ni mateso sana kuwa kwenye mahusiano na mwanamke usiyemuamini ila natamani arudi tu tuendelee kuwa pamoja tulee mtoto wetu licha ya haya mateso anayonipitisha.

Pamoja na ushauri wenu nataka kujua, kwa mtazamo wenu huyu mwanamke ananipenda kweli, au miaka yote sita naforce mapenzi. Mara nyingi tu akinizingua sana huwa namblock hata wiki lakini atapiga simu na kuomba msamaha, atatumia maneno yote mazuri ya kubembeleza ili nimsamehe.

Na mie huwa namblock tu ili kumwonyesha kuwa naweza kuishi bila yeye ila huwa sina dhamira ya dhati ya kumuacha. Kwa hiyo akinibembeleza siku 3 mfululizo kwa msg na simu namua-unblock na maisha yanaendelea.

Kuna watu wataanza kuuliza kama mtu umemblock atawezaje kukupigia na kukutumia msg? Jibu ni kwamba kuna sehemu unaenda na kukuta msg za namba uliyoiblock, Samsung namba uliyoiblock ikipiga huwa inaonyesha pale kwenye call register.
Umeandika mno na ww khaaaa
 
Leo tarehe 21/12/2022 saa 6:04 usiku nimesoma uzi wa kipumbavu sana ulioandikwa na Mfia nchi. Nakushauri fanya jambo lolote litakalosababisha tukuite "Mfia nchi" ile yenye uhalisia kwasababu unachofanya ni upumbavu.
 
Kwa mujibu wa tafiti za kiroho inathibitishwa kuwa asilimia 75 ya wakazi wa hapa duniani hawana nafsi. Ikumbukwe binadamu anakamilishwa na vitu vitatu ambavyo ni mwili, nafsi na roho. Nikisema tafiti za kiroho namanisha wenye uwezo wa kuona vitu wanaona jinsi demons au mapepo wanavyoruka kutoka ndani ya mtu mmoja na kwenda kwa mtu mwingine.

Chanzo cha binadamu/ watu kukosa nafsi ni moja ni kuzaliwa ukiwa hivyo ukiwa huna nafsi hii inaitwa glitch in the matrix na mbili ni kuuza nafsi ili uweze kutumika kama chombo (vessel/portal) na viumbe wa daraja la chini kama vijini. Mtu mwenye vijini au anayepandisha kijini huyo hana nafsi wala nguvu yoyote ya kiroho na muda wote huwa na hisia kama upepo unaingia mwilini mwake.

Kukosa nafsi kwa lugha rahisi naweza kutoa mfano wa kifaa kama Computer. Bila kuwekwa Operating system computer haiwezi kufanya kazi kwamfano huo ni kwamba ili uweze kutumia vizuri computer ni lazima uwe na Windows bila hiyo windows inakuwa computer ambaye haija kamilika.

Watoto wengi waliozaliwa kuanzia miaka ya 2000 (millennials) wengi wao hawana nafsi ni kama Bots tuu. Maisha yao ni vanity and greedy hawana uwezo wa kuchambua hoja au uwelewa wa kuwa na malengo katika maisha yao. Hawana malengo isipokuwa wachache sana ambao wamebahatika kuzaliwa wakiwa kamili.
Mshana Jr ..njoo sema jambo apa
 
Na huyo mtoto unae sema umezaa naye chunguza huenda sio wako.Malaya hafugiki kama kunguru vile, huwezi mfuga
 
Back
Top Bottom