Uchaguzi 2020 Msajili amwandikia barua Maalim Seif akimtaka ajieleze kwanini kapanda jukwaa moja na Tundu Lissu kule Kilimanjaro!

Uchaguzi 2020 Msajili amwandikia barua Maalim Seif akimtaka ajieleze kwanini kapanda jukwaa moja na Tundu Lissu kule Kilimanjaro!

Unafikiri kuna sheria yoyote, basi? Ni uonevu tu wa mchana kweupe. Watu wameamua kufanya udhalimu kwa ajili ya vyeo, mchana kweupe bila aibu.
Mbona leo Mrema kapanda Jukwaa moja na MAGUFULI huko kilimanjaro? kama ana ubavu amwandikie na Magufuli sasa....hivyo visheria vyao vya kipumbavu walivyowatungia wapinzani mwisho ni tarehe 28 by any means
 
Msajili wa vyama vya siasa amemtaka mwenyekiti wa ACT wazalendo maalim Seif ajieleze kwanini alisafiri hadi Kilimanjaro na kupanda jukwaa moja na Tundu Lisu wa Chadema kumpigia kampeni.

Kiongozi wa chama Zitto Kabwe amesema wanatarajia na mwenyekiti wa TLP mzee Mrema atajieleza pia.

Maendeleo hayana vyama!
Wewe kidogo una akili!! nahii ni kwasabu mapenzi yako yapo, kwenye mabadiliko ya kweli!! Sasa umeona wenzio walivyokabizi akili zao kwa mwenyekiti!! Msajili wa vyama unakuwa mjinga Kama vile hajasoma!
Ukienda CCM. haka Kama una phd! unakuwa kijinga tu!! sijui CCM Kuna nn??
 
katiba ya CCM na ya TLP hazitamki kuwa ukimuunga mkono mgombea mwingine unaachishwa uanachama ni katiba ya ACT wazalendo ndio inatamka hivyo .Hivyo Zitto KAJIVUA uanachama na Maalim SEIF kajivua uanachama kwa mujibu wa katiba yao
kifungu hicho hapo

1603287846900.png
 
Hahaha awaulize ZEC, kwanini walimfungia?!

Maalim Seif had free time, he decided to visit a friend, who happened to be campaigning in Kilimanjaro.

Mbona hakumuandikia Magufuli
alipokuwa pamoja na Dr.Mahera?!
 
Msajili wa vyama vya siasa amemtaka mwenyekiti wa ACT wazalendo maalim Seif ajieleze kwanini alisafiri hadi Kilimanjaro na kupanda jukwaa moja na Tundu Lisu wa Chadema kumpigia kampeni.

Kiongozi wa chama Zitto Kabwe amesema wanatarajia na mwenyekiti wa TLP mzee Mrema atajieleza pia.

Maendeleo hayana vyama!
Mrema ni mgombea wa chama gani?
 
Katiba ya Tanzania inatoa uhuru

https://www.tanzania.go.tz/egov_upl... JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA YA MWAKA.pdf

Ibara za 18 20 na 21 zinatoa uhuru wa maoni, uhuru wa mtu kushirikiana na wengine na uhuru wa mtu kushiriki shughuli za umma.

Haki ya Uhuru wa Mawazo
Uhuru wa Maoni Sheria ya 1984 Na.15 ib.6

18.-(1) Bila ya kuathiri sheria za nchi, kila mtu yuko huru kuwa na maoni yoyote na kutoa nje mawazo yake, na kutafuta, kupokea na kutoa habari na dhana zozote kupitia chombo chochote bila ya kujali mipaka ya nchi, na pia ana uhuru wa mawasiliano yake kutoingiliwa kati. (2) Kila raia anayo haki ya kupewa taarifa wakati wote kuhusu matukio mbalimbali nchini na duniani kote ambayo ni muhimu kwa maisha na shughuli za wananchi, na pia juu ya masuala muhimu kwa jamii.

Uhuru wa mtu kushirikiana na wengine Sheria ya 1984 Na.14 ib.6

20.-(1) Kila mtu anastahili kuwa huru, bila ya kuathiri sheria za nchi, kukutana na watu wengine kwa hiari yake na kwa amani, kuchanganyika na kushirikiana na watu wengine, kutoa mawazo hadharani, na hasa zaidi kuanzisha au kujiunga na vyama au mashirika yaliyoanzishwa kwa madhumuni ya kuhifadhi au kuendeleza imani au maslahi yake au maslahi mengineyo. (2) Bila ya kujali masharti ya ibara ndogo ya (1) haitakuwa halali kwa chombo chochote cha siasa kuandikishwa ambacho kutokana na Katiba au sera yake- (a) kinakusudia kukuza au kupigania maslahi ya- (i) imani au kundi lolote la dini; (ii) kundi lolote la kikabila pahala watu watokeapo, rangi au jinsia; (iii) eneo fulani tu katika sehemu yoyote ya Jamhuri ya Muungano; (b) kinapigania kuvunjwa kwa Jamhuri ya Muungano: (c) kinakubali au kupigania matumizi ya nguvu au mapambano kama njia za kufikia malengo yake ya kisiasa; (d) kinapigania au kinakusudia kuendesha shughuli zake za kisiasa katika sehemu moja tu ya Jamhuri ya Muungano; (e) hakiruhusu uongozi wake kuchaguliwa kwa vipindi na kwa njia za kidemokrasia. (3) Bunge laweza kutunga sheria inayoweka masharti yatakayohakikisha kuwa vyama vya siasa vinazingatia mipaka na vigezo vilivyowekwa na masharti ya ibara ndogo ya (2) kuhusu uhuru na haki ya watu kushirikiana na kujumuika. (4) Bila ya kuathiri sheria za nchi zinazohusika ni marufuku kwa mtu yeyote kulazimishwa kujiunga na chama chochote au shirika lolote, au kwa chama chochote au cha siasa kukataliwa kusajiliwa kwa sababu tu ya itikadi au falsafa.

Uhuru wa kushiriki shughuli za umma Sheria ya 1984 Na.15 ib.6 Sheria ya 1994 Na.34 ya ib.4

21.-(1) Bila ya kuathiri masharti ya ibara ya 5, ya 39 na ya 67 ya Katiba hii na ya sheria za nchi kuhusiana na masharti ya kuchagua na kuchaguliwa, au kuteua na kuteuliwa kushiriki katika shughuli za utawala wa nchi, kila raia wa Jamhuri ya Muungano anayo haki ya kushiriki katika shughuli za utawala wa nchi, ama moja kwa moja au kwa kupitia wawakilishi waliochaguliwa na wananchi kwa hiari yao, kwa kuzingatia utaratibu uliowekwa na sheria au kwa mujibu wa sheria.

(2) Kila raia anayo haki na uhuru wa kushiriki kwa ukamilifu katika kufikia uamuzi juu ya mambo yanayomhusu yeye, maisha yake au yanayolihusu Taifa.
 
Hii ni vita. Upinzani wanatakiwa wawe makini na mitego ya aina hii kwani wanaelewa fika jinsi wanavyowindwa
ni kuzingatia za vyama vyao ACT wazalendo hairuhusu mgombea au mwanachama kumuunga mkono mgombea wa chama kingine akifanya hivyo anakuwa kajivua uananchama

1603288020292.png
 
Back
Top Bottom