Msanii gani maarufu umewahi kuonana naye live mkaongea mawili matatu

Msanii gani maarufu umewahi kuonana naye live mkaongea mawili matatu

Hv bado iko active hii pub
Siku hizi imechoka sana tu. Watu wa maeneo haya siku hizi huwa tunakunywa Papii churo, kuna bar nyingine ipo nyuma ya Mwanamboka NBC ya zamani, Matema aka C PARK nk. Hata hizi bar za kuanzia Studio kuelekea Mwananyamala A asilimia kubwa zimechoka.
 
Nina ofisi ya photoshoot pande flani town wasanii kibao wa bongomovie,gospel na bongoflavour mpaka tulishawazoea hasa madem. Tena hadi wale wauzaji wakubwa bongo wanakuja, kuna jamaa yangu wa mkoa siku alikuja kunitembelea akamkuta dem mmoja basi yule dem alivoondoka jamaa akashangaa sana kumuona akanambia ni dem ananuonaga tu insta ni maarufu sana akanionesha akaunti ya huyo dem aisee utasema dem anaishi marekani na anafollowers zaidi ya milioni.
Ila zamani nilikutana na shilole kwenye atm na sikumtambua akawa ananiuliza kadi yake inazingua ilikua ya benki nyingine. Jamaa yangu ndo akanambia ulikua unaongea nini na shilole ndo nikagundua. Matonya nae alikua mshkaji sana pindi nafanya kazi benki nilimsaidia kujaza account opening form na hata slips nilikua namsaidia kujaza coz kuandika kwake ilikua ni shida sana,so kama anakuja benki ilikua lazima anipigie simu. Akaunti yake haikuwa haba mpaka nikawa najiuliza ndo badae nikajaga kuskia kumbe ngada
 
mm wasanii wa bongo wengi nimeshakutana nao na story za hapa na pale...ila msanii mkubwa wa nje niliyepiga nae story ni chris tucker ni comedian huyu wa usa huko Hollywood..alikuja tz, arusha miaka hiyo 2008 ilikuwa ngorongoro huko ...sema dah akiongea uambulii kitu ile lafudhi ya ndani..
 
Stamina nshawahi kuishi naye nyumba moja ya kupanga tegeta mitaa ya kibo complex ...jamaa hana makuu kabisa ...thou nlishahamaga pale
 
Me nilikutana na Inspector Harun bar moja inaitwa Micasa Ubungo alikuwa na mwanangu mmoja meza moja nikaenda kumpa hi, nikamkumbusha story za team Juma Nature na team Inspector enzi hizo napiga shule Moshi huko. Watu tulikuwa tunapigana hadi ngumi ukiamza huo ubishi, mm nilikuwa team Inspector alifurahi sana nikawaachia bia mbili mbili nikasepa. Banana Zoro pia alikuwa akija pale kuimba na band yake akitukuta counter lazima atoe hi kwa wote. KR Mura nilishawahi kuamulia ugomvi na mwanangu mmoja hivi walizinguana akaanza kusema mm ni msanii. Msafiri Diof enzi za Twanga alikuwa kila akinikuta pale Saniro Sinza anataka bia, dah kitambo sana.
 
Mie nakutana sana na mchekeshaji Mkwere ninajenga Kimara (nyumba ya kupangisha) jirani na kwake. Uwa tunapiga sana story . Prof. J pia mshikaji tunaongea nae, Afande Sele mwanangu mno na kuna msanii mmoja wa kike maarufu nilishapita nae kinyumba enzi zangu
Basi umetisha kamanda haswa huo mstari wa mwisho ni balaa
 
Mbona wengi sana


Drake alikuwa pale mabibo sokon ananunua nyanya

Lil wayne, maeneo ya keko ananunua cha arusha, (tulipeana HI kwa mbali) ananielewa sana


Mondi kwenye mitumba tandale, alikuja kuniomba chechi ya elfu kumi

Chris brown tumekutana sinza pale, alikuwa ameleta nguo mpya za "mr breezy"


Rihana Coco Beach kila siku yupo pale nampitaga nikiwa nafanya mazoezi
 
Nina ofisi ya photoshoot pande flani town wasanii kibao wa bongomovie,gospel na bongoflavour mpaka tulishawazoea hasa madem. Tena hadi wale wauzaji wakubwa bongo wanakuja, kuna jamaa yangu wa mkoa siku alikuja kunitembelea akamkuta dem mmoja basi yule dem alivoondoka jamaa akashangaa sana kumuona akanambia ni dem ananuonaga tu insta ni maarufu sana akanionesha akaunti ya huyo dem aisee utasema dem anaishi marekani na anafollowers zaidi ya milioni.
Ila zamani nilikutana na shilole kwenye atm na sikumtambua akawa ananiuliza kadi yake inazingua ilikua ya benki nyingine. Jamaa yangu ndo akanambia ulikua unaongea nini na shilole ndo nikagundua. Matonya nae alikua mshkaji sana pindi nafanya kazi benki nilimsaidia kujaza account opening form na hata slips nilikua namsaidia kujaza coz kuandika kwake ilikua ni shida sana,so kama anakuja benki ilikua lazima anipigie simu. Akaunti yake haikuwa haba mpaka nikawa najiuliza ndo badae nikajaga kuskia kumbe ngada
Kudadeki tellers mnachungulia sana salio la watu
 
diamond platnumz maeno ya sinza vatcan..alipokua anataka kuwapangishia dancers wake..hiyo nyumba alokua anaitaka..ipo jirani na ninapoishi.. jamaa anaongea haraka haraka mno[emoji23][emoji23]

pia bwana Juma Mchopanga (JAY MOE) ni jirani yangu..huwa tunapiga sana stori kijiweni kwa mkenya[emoji28][emoji28]
 
diamond platnumz maeno ya sinza vatcan..alipokua anataka kuwapangishia dancers wake..hiyo nyumba alokua anaitaka..ipo jirani na ninapoishi.. jamaa anaongea haraka haraka mno[emoji23][emoji23]

pia bwana Juma Mchopanga (JAY MOE) ni jirani yangu..huwa tunapiga sana stori kijiweni kwa mkenya[emoji28][emoji28]
Mkenya ni yule jamaa mfupi mwenye kipara.... Au nimechanganya madawa???
 
Back
Top Bottom