kitu nanyonga mwenyewe
wala simwamini pusha,
hukawii kuuziwa ngano
ukaambiwa cha iran,
ganja navuta,
unga nabwia,
kwanja naruka,
unga wa kushea sindano
mi sijidungi,
hujui wamedunga wangapi mda uliopita
mabuti ya kijeshi uyaone mafupi mepesi//
yaani kama vile 'simple' toka nduki toka 'race'//
kama risasi ya bunduki au jeti/
no kunyuti no kuketi/
wape nafasi wakushuti kama Malcolm X//
usikubali kubaki uwe pimbi upewe kesi//
ikibidi jitose ndani ya dimbwi la kinyesi//
sio suala la uoga kuogopa ukunguru..\\
ila bora kulogwa kuliko kukosa uhuru\\
wapi sheikh Mponda wapi Jenerali Komba/
sirikali sera kali cheza mbali na wajomba/
kimbia,
mitihani imevuja nyie hamjasikia?//
ya nini kusoma huku elimu inanunuliwa//
kimbia,
nchi imeshauzwa hii hamna kusikilizia//
TANESCO,Madini hadi Air Tanzania//
watoto wa uswazi hawana matumaini/
ndoto za ujambazi sababu ya umasikini/
matapeli wenye shahada kila hatua tatu//
makahaba wa miaka kumi na tatu//
maskani kama msitu vicheche na machatu//
usipite pekupeku bila kuvaa viatu//
aaaaah!kimbiaa ♫♫♫
Lyrical And Natural Gifted African(L.A.N.G.A).
MUNGU AMLAZE MAHALI PEMA LANGA KILEO.............