Msanii Ray C azidiwa na Madawa ya Kulevya; asaidiwa na Polisi

Msanii Ray C azidiwa na Madawa ya Kulevya; asaidiwa na Polisi

dawa pekee ni kukaa sehemu ambayo atakuwa hapati madawa, iwe jela au popote pale
 
Unga sio kama pombe au sigara au kujichua mana ukiwa addicted na unga ni kama kuna kishetani kwa ndani ya moyo kila saa kinataka urudi kwaiyo kutibiwa ni moja ila inabidi na mazingira au style ya maisha ibadilike uwe associated na watu wa dini sana hii itasaidia ila uwezi kuacha afu marafiki wale wale, tusimuhukum bali tumsaidie
Anahitaji msaada wa hali na mali.ni khatari sana hii mkuu.
 
Kuna lundo la mateja linahitaji msaada achana na Ray C ambae hataki msaada ashaamua maisha yake.
Nadhani huelewi maana halisi ya 'addiction'. Mtu ambaye yupo addicted hayo mawazo kama yako inakuwa magumu kuyapata. Anaweza akawa ana nia lakini nia pekee itafeli. Hawa watu wanahitaji msaada ili watoke kwenye mtego wa addiction. Wanahitaji uangalizi wa hali ya juu, mwenyewe hawezi.
Na njia kuu ya kuwasaidia watu kama Ray C na mateja wengine ni kupambana na wafanyabiashara wakubwa wa madawa ya kulevya pamoja na wasambazaji wao.
 
DUH kweli yanaenda kasi alikuwa anamtafuta CHID BENZ amasaidie kuacha unga leo yy ndio kapotea mazima wkt Chid ka recover!
 
mkuu Serikali haiko siriasi kuhusu hili suala je sisi tufanyaje?
 
Wote hata hao waliotumbukia kwenye janga la mihadarati ni wakuomba Mola awasaidie.
ndiyo wote ni wakuombewa lakini ukipata msaada wakutoka huko ulipo siyo vyema kurudia tena japo tunajua binadamu ni viumbe dhaifu lakini isiwe sababu
 
Daaaaah..inasikitisha sana kwakweli...inauma zaidi pale ninapofikiria kuwa tutamsaidiaje mtu huyu tukiwa kama individual au taasisi flani....ilihali mtu huyu huyu alishapata msaada kutoka ikulu kabisaaaa yaaan raisi wa nchi kabisaaaa..but alishindwa.....tumuombee tuuu hamna namna.
 
M ntaanza NA maombi...kwavideo niloona tunakazi mbelekubwa kumkomboa kubwasana lakini tusikate yatamaa..wenye instagram mnaweza search globapublishers AMA obbytheng mtamwona anavyochopolewa NA poliisi usiku mawindoni
hasaidiki huyu mwanamke shenzi zake
 
Msanii wa muziki Rehema Chalamila aka Ray C usiku wa jana alikamatwa na jeshi la polisi maeneo ya Kinondoni Manyanya almaarufu ‘Kinondoni kwa Mpemba’ jijini Dar es salaam baada ya kupiga makelele barabarani akidai anataka kutekwa.

Ray C akiwa kwenye gari la polisi



=================
More:

Hali ya kiafya ya mwanamuziki mkongwe Rehema Chalamila ‘Ray C, imeonesha kuwa tata kutokana na kile kinachodaiwa kuwa ni matumizi ya madawa ya kulevya jambo lililoleta sintofahamu baada ya video inayozunguka mitandaoni ikionyesha akichukuliwa na Polisi huku akisema kuwa wanamteka.

Habari zinadai kuwa mama yake mzazi amekuwa akikesha kumtafuta mrembo huyo kutokana na kuzama kwenye vijiwe vya mateja wa madawa hayo na kushindwa kuonekana nyumbani kwani kwa siku kadhaa na watu kujitokeza kumsaidia bila mafanikio.

Sambamba na hilo siku za hivi karibuni mwanamuziki Jay Dee, alionekana kuwa naye karibu na kudai kuwa Ray C, anahitaji marafiki wazuri na watu wavumilivu kuweza kumsaidia kwani kumlaumu pekee hakuwezi kumjenga bali ni kumzidi kumharibu kisaikolojia.

Mmoja wa wasanii wa Bongo Movie, Esha Buheti, kupitia mtandao wa kijamii ameweza kueleza jinsi gani alivyoguswa baada ya kumuoa Ray C akiwa chini ya ulinzi wa polisi akiwa hajitambui na kuongea maneno yasiyoeleweka na kudai kuwa awali alijua mrembo huyo anasingiziwa tuu.

Ameandika “Nashindwa hata niongee nini jamani, Ray C leo Kinondoni umenitoa machozi, jamani tufanye kitu tumsaidie Ray C, I mean it jamani siku zote nlikuwa najua anaonewa ila nilichokishuhudia leo nimeumia kutoka moyoni amedhalilika mwanamke mwenzetu, jamani tufanyeje?”

Akaendelea “Nilikua na Kabula, Kinondono kwa wapemba tumefuata chips mara tukasikia mtu anasema me Ray C nataka kuvua nguo, nikajua utani kushuka ni Ray C anasema nishikeni kuna watu wanataka kuniteka, alikuwa na nguvu sana watu kumshika akaanza kuongea vitu havieleweki, akaanza kutafuta kisu ajichome, watu walimzuia sana walishindwa akaanza kugaragara kwenye matope akipiga kelele,”

“Kiukweli nilijikuta nalia mara ikaja gari ya polisi ikambeba ila kwa tabu sana alikua akipiga kelele jamani nisaidieni msiniache kiukweli mpaka Ray C anaondoka na ile gari ya polisi sikujua anapelekwa wapi alikuwa kama mtu alopata kichaa, YARRAB TUNAMSAIDIAJE RAYC?”.



Nguvu hizi naona tungezitumia Zaidi kushinikiza serkali ipambane na waingiza na wauzaji wa hayo madawa ya kuelevya. Hili ni tatizo la jamii kwa ujumla. Hautumii lakini tunao mitaani na twajua wanafanya nini. Wala unga wakamwatwe wawaulizwe wananunua wapi, wakikamatwa wanauza watapeleka kwa wauzaji chanzo. Tz hatupo serious na kupambana na hili janga. Hakuna hasiyejua madhara ya dawa za kulevya. Inakuwaje nguvu zisielekekezwe kupambana na biashara hii.
Kama kweli tunapinga dawa kulevya wala madawa ni waalifu na wapo wazi wakamatwe wachukuliwe hatua na waonyeshe walipozitoa na waliowapa wakamatwe pia mwisho atapatikana papa
 
mtu anakula starehe zake nyie mnalia lia [emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
 
unafiki tu wengi wajita wanahuruma kweli kisa anajina lakini kuna mateja wangapi mtaani,kunavijana wangapi wame blind future zao sababu ya haya madudu,jamii haichukui hatua serikali haichukui hatua ..ndo ivyo mchuma janga hula na wakwao
 
Back
Top Bottom