Msekwa aongoza mjadala wa Katiba Mpya na Tanzania tunayoitaka

Msekwa aongoza mjadala wa Katiba Mpya na Tanzania tunayoitaka

Msekwa: nimejifunza umuhimu wa katiba mpya iwashirikishe wananchi......msekwa anataka watu watenganishe watekelezaji na katiba.......anamaanisha uongozi /viongozi wakiwa wabaya tatizo ni wao sio katiba
 
Godbless Lema........eti mlituua Arusha kwenye maandamano.
 
huyu mzee anajicontradict kila wakati mara akubali katiba mara aseme haina tatizo tatizo ni watekelezaji. Wkati watu wanataka katiba iweke kibano kwa hawa watakao kiuka maadili.
 
Niliyoyapata kwenye mdahalo ni kuwa wananchi wanataka katiba inayoendana na wakati huu-msekwa
 
huyu mzee hafai kuwa mtoa mada maana hanamtiririko mzuri anapoongea anabore tu.
 
Hivi kwanini ccm hawajaenda kwenye mjadala kumpa tafu mzee wao?
 
Mijadala juu ya katiba ni bora itenganishwe na mitizamo ya vyama!
 
msekwa nasema ni lazima tuainishe katiba yetu inataka iondoe mapungufu gani.........katiba yote sio mabaya, lazima watu waaainishe mapungufu ya sasa.......ha!ha!ha!ha!ha! anasema hajaweka msimamo leo kaja kusikiliza.....nadhani ile kauli ya kuwa wastaafu kwa wema kuliko kustaafia the heague..
 
wanawind up na kipindi kimekwisha...huu mdahalo wa leo haueleweki, ila inatia moyo moto wa katika unazidi kuwaka
 
Lema kamaliza tunataka katiba mpya

Lkn cjamkubali kivile hajaweza kujipanga katika kuwasilisha hoja ya nguvu yaani uwezo wake nadhani anahitaji semina au darasa la namna ya kusend msg katika hadhira tofauti amezungumza kama anaongea na masela wa unga ltd
 
huyu mzee kajitahidi kwa kiasi chake maana kuitetea sisi em sio kazi rahisi jamani! Lakini anaposema katiba haina tatizo ila watendaji inabidi nicheke tu! Hilo ni tatizo la kwanza. Katiba makini sio kwamba tu inaweka vyombo madarakani, bali inaviwajibisha vinapokiuka kazi na wajibu wao. Sasa kama katiba hii haina meno, then tutengeneze nyingine yenye meno ya kuwang'ata wote wasio waadilifu!

Kwa sasa naishia hapa!
 
TUache Ushabiki wa Vyama: Nadhani hawa ndio wazee waliokuwa wanakilinda chama wakati CCM ikiwa yenye Nguvu, ila hawakuwaandaa vijana wao kuwa na uwezo kama wao wa ku-deal na hoja motot bila kulipua moto zaidi yaani ni wataalamu wa kupooza hoja za moto. Ila nimependa pia tofauti na vimeo kama akina Makamba, yeye anaafiki udhaifu wa chama chake, anaushika na utovu wa nidhamu akisistiza kutokuwepo kwa maadili ndani ya chama chake, nawajua mamluki wa CCM waliomuuliza swali la maadili nadhani walimtaka mzee akiokoe chama kwa kusisitiza tatizo sio chama ila ni utovu wa nidhamu. NIMEPENDA HOJA YA mhusika mmojawapo aliposisitiza kuwa Mfumo (ambao ni katiba) usipokuwa imara unatoa mwanya kwa kutokuwepo kwa maadili na kutokuwepo mfumo wa kuwawajibisha wahusika. Sidhani kama maoni aliyotoa ni ya chama chake.

Sipati picha kilaza Makamba atakavyoropoka kesho maana duh! Ya leo ni oposite na wajinga wengi waliomo ndani ya CCM.

NIMEPENDA Zito Kabwe alivyotumia vizuri mbinu za Propaganda kwa kumuingiza kingi mzee na akauvaa.... nilicheka sikuweza kuvumilia mzee akauvua U-CCM na kuanza kubwabwaja maana angebaki kwenye U-CCM angetuboa zaidi maana si angeng'ngania vimsimamo viozo vya vilaza na mafisadi wenzao... ila ubaya alishindwa kumaintain hiyo ya kujivua maana yawezekana kabisa aliagizwa ... vijana wamemchakachua mpaka akaingia chaka saaafi sana vijana wa People's Power... naifagilia CCM kama chama ila nawachukia wooote waliomo ndani yake kwa sasa maana ni waozo wa kila aina name it wajinga wazembe wezi mafisadi wanafiki nisaidieni kumalizia jamani.....

Big up vijana wa Pople's Power leteni mabadiliko wakati ndio huu wa kuandika Historia Msifanye fujo waacheni wafanye wao halafu sijui watajificha wapi masikini....
 
heri yangu mie niliamua kwenda sinema nimemkuta ndo anamalizia kujiumauma. Ila alikuwa na kila dalili za pressure kupanda
 
Back
Top Bottom