Msemaji wa JWTZ kuteuliwa kwenye NEC ya CCM, hii imekaaje?

Joined
Sep 29, 2016
Posts
34
Reaction score
84
NI UKIUKWAJI WA KATIBA AU MAJINA YAMEFANANA KATI YA MSEMAJI WA JWTZ NA HUYU MTEULE WA NEC YA CCM?
JPM JITOKEZE KUUELEZEA UMMA KUHUSU UTATA HUU.​

Msemaji wa JWTZ ni Kanali Ngemela Lubinga.

Katibu Mteule wa NEC ya CCM Siasa na Uhusiano wa Kimataifa ni Kanali Ngemela Eslom Lubinga.

Katiba ya Jamhuri 1977 inasema :-

SURA YA TISA
MAJESHI YA ULINZI

Ibara ya 147.

Ibara ndogo ya (3),
Itakuwa ni marufuku kwa mwanajeshi yeyote kujiunga na chama chohote cha siasa, isipokuwa tu kama atakuwa na haki ya kupiga kura iliyotajwa katika ibara ya 5 ya Katiba hii.

Ibara ndogo ya (4),
Kwa madhumuni ya ibara hii, "mwanajeshi" maana yake ni askari aliyeajiriwa kwa masharti ya muda au ya kudumu katika Jeshi la Ulinzi, Jeshi la Polisi, Jeshi la Magereza au Jeshi la Kujenga Taifa.

----------
 
Mtukufu wetu yuko juu ya kila kitu na hata akiamua kusema watz wote ni vilaza tutampigia makofi na kushangilia
Siku unayoteuliwa unaacha jeshi huwi mwanajeshi na unashika madaraka siku hiyo hiyo kama ambavyo lowasa alivyofanya.Siku alipoteuliwa na CHADEMA kuwa mgombea siku hiyo hiyo aliacha CCM na kuwa mgombea uraisi
 
Siku unayoteuliwa unaacha jeshi huwi mwanajeshi na unashika madaraka siku hiyo hiyo kama ambavyo lowasa alivyofanya.Siku alipoteuliwa na CHADEMA kuwa mgombea siku hiyo hiyo aliacha CCM na kuwa mgombea uraisi



Hoja si uteuzi wake tu,alianza lini kuwa mwanachama wa Chama cha mapinduzi huku akiwa mwanajeshi?
 
Siku unayoteuliwa unaacha jeshi huwi mwanajeshi na unashika madaraka siku hiyo hiyo kama ambavyo lowasa alivyofanya.Siku alipoteuliwa na CHADEMA kuwa mgombea siku hiyo hiyo aliacha CCM na kuwa mgombea uraisi
Swali ni kuhusu uteuzi bro, kwa sababu mtu hawezi kuteuliwa tena kwenye nafasi kama ya msemaji kama sio mwanachama wa muda mrefu
 
Siku unayoteuliwa unaacha jeshi huwi mwanajeshi na unashika madaraka siku hiyo hiyo kama ambavyo lowasa alivyofanya.Siku alipoteuliwa na CHADEMA kuwa mgombea siku hiyo hiyo aliacha CCM na kuwa mgombea uraisi
kama kaacha,mbona haitwi "mstaafu" au atumie jina lisilo na asili ya jeshI,atumie majina yake tu?

halafu hii ya kurundika wanajeshi,je ikitokea ccm imeshindwa kwenye uchaguzi,hawa wanajeshi wataelewa? au wanachonganishwa na wananchi?
 
Siku unayoteuliwa unaacha jeshi huwi mwanajeshi na unashika madaraka siku hiyo hiyo kama ambavyo lowasa alivyofanya.Siku alipoteuliwa na CHADEMA kuwa mgombea siku hiyo hiyo aliacha CCM na kuwa mgombea uraisi
Sawa lkn hii ni picha kuwa wakati alipokua jeshini alikua ni mwanachama wa ccm. Haiwezekani kuwa wamemchukua MTU wasiomjua. Ndio maana tunasema vyombo vyetu vya usalama sio huruma na haviko tayari kuona ccm ikishindwa ndio maana hutumia mbinu yote hata za wizi kuleta ushindi kwa ccm
 
Lowasa walipomchukua CHADEMA walimjua siku nyingi? Mbona aliingia tu na kupewa ugombea uraisi wakati hajawahi kuwa kiongozi wa tawi la chadema
 
Trend ya Magufuli na wanajeshi inaashiria maandalizi fulani. Huwezi kujua kwa hakika ni nini ila sio mambo mema.

Vijana wa ccm wanaoshabikia haya huku wakiwa na ndoto za kufanya siasa ndani ya demokrasia wajitafakari sana.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…