Msemaji wa JWTZ kuteuliwa kwenye NEC ya CCM, hii imekaaje?

Msemaji wa JWTZ kuteuliwa kwenye NEC ya CCM, hii imekaaje?

Watu wanafanya usajiri wakijiandaa kugomea matokeo 2020!
 
Wacha tu aendelee kuwaonjesha hawa jamaa utamu wa madaraka ya kisiasa siku wanamtoa hapo ndio ataelewa
 
Sio lazima awe alikuwa mwanachama.Aweza kuwa kaanza jana hiyo hiyo kila kitu kina tarehe ya kuanza





Hiyo ni "argument" ya kitoto mno,serikali iliyojipambanua kuwa itateua makada wa Chama chake katika nafasi za uongozi ili waweze kutekeleza ilani ya uchaguzi,itaanzaje kumteua mtu ambaye hana historia ndani ya Chama kuwa kiongozi katika Chama?

Akishindwa kutekeleza ilani,misingi na kanuni za Chama utamwajibishaje?Teuzi hizi za wakuu wa vyombo vya ulinzi na usalama ndani ya Chama na serikali ni kielelezo cha namna vyombo hivyo vinavyotumika kisiasa kwa madhumuni ya kukibeba Chama tawala.Chama kilichopoteza mvuto,sasa kimeamua kujiegesha kwenye"kwapa" la vyombo ya usalama ili kipate nguvu za kijeshi.

Hivi huyo mteule si ndiye yule aliyetuambia kuwa wamemchukua mwandishi aliyeripoti kuibiwa kwa kifaru cha jeshi na kwamba yupo kambini "anasurubiwa" ili akibahatika kutoka akawahadithie wenzake?

Tukifikia mahali tukaamua kuiweka kando katiba yetu na katiba ya vyombo vyetu vya ulinzi,tukaanza kuajiri na kuteua "wababe wa kivita" katika sehemu nyeti za uongozi wa Chama na serikali,taratibu tunaanza kuliondoa Taifa letu kwenye demokrasia tunayoihubiri.

Kina Nkurunzinza walioamua kung'ang'ania madaraka kwa kujiongezea mihula ya uongozi kinyume na katiba,walifanya hivyo baada ya kuona wana uungwaji mkono wa "jeshi lililoiasi katiba".Uasi huu wa katiba ufanywao na vyombo vyetu unamaana gani kama si maandalizi ya watu kuja kung'ang'ania madarakani huko tuendako?Au haya ndiyo yanayopelekea hadi jf ambayo ndiyo platform pekee iliyobaki tutumiayo kuihoji serikali baada ya magazeti,redio na TV kusalimu amri mbele ya dola na sasa wanaanza kumuwinda mkurugenzi wetu wa jf?

Tuendako ni Mungu tu ajuwaye,Yeye ndiye mweye uwezo wa kuichunguza mioyo yetu,Mungu wa Mbinguni Atuepushe na hili,amen.
 
Siku unayoteuliwa unaacha jeshi huwi mwanajeshi na unashika madaraka siku hiyo hiyo kama ambavyo lowasa alivyofanya.Siku alipoteuliwa na CHADEMA kuwa mgombea siku hiyo hiyo aliacha CCM na kuwa mgombea uraisi
Rudi kasome katiba vzr acha kupotosha umma
 
Watu kama hao wako tiyari kuilinda ccm uwe madakani miaka nenda rudi!
 
Lowasa walipomchukua CHADEMA walimjua siku nyingi? Mbona aliingia tu na kupewa ugombea uraisi wakati hajawahi kuwa kiongozi wa tawi la chadema
jadili hoja, wewe unaleta propaganda. Lowassa hapa wapi na wapi? RPC anastaafu leo kesho anachukua fomu kugombea nafasi ya siasa ndani ya CCM, alikuwa mwanachama tangu lini?
 
Ukitaka kuitawala nchi vizuri.kuna sahani moja na jeshi.
 
Siku unayoteuliwa unaacha jeshi huwi mwanajeshi na unashika madaraka siku hiyo hiyo kama ambavyo lowasa alivyofanya.Siku alipoteuliwa na CHADEMA kuwa mgombea siku hiyo hiyo aliacha CCM na kuwa mgombea uraisi
Safi sana ndugu, umemjibu sawasawa mleta mada.
 
Hiyo ni "argument" ya kitoto mno,serikali iliyojipambanua kuwa itateua makada wa Chama chake katika nafasi za uongozi ili waweze kutekeleza ilani ya uchaguzi,itaanzaje kumteua mtu ambaye hana historia ndani ya Chama kuwa kiongozi katika Chama?

Akishindwa kutekeleza ilani,misingi na kanuni za Chama utamwajibishaje?Teuzi hizi za wakuu wa vyombo vya ulinzi na usalama ndani ya Chama na serikali ni kielelezo cha namna vyombo hivyo vinavyotumika kisiasa kwa madhumuni ya kukibeba Chama tawala.Chama kilichopoteza mvuto,sasa kimeamua kujiegesha kwenye"kwapa" la vyombo ya usalama ili kipate nguvu za kijeshi.

Hivi huyo mteule ni ndiye yule aliyetuambia kuwa wamemchukua mwandishi aliyeripoti kuibiwa kwa kifaru cha jeshi na kwamba yupo kambini anasurubiwa ili akibahatika kutoka akawahadithie wenzake?"

Tukifikia mahali tikaamua kuiweka kando katiba yetu na katiba ya vyombo vyetu vya ulinzi,tukaanza kuajili na kuteua "wababe wa kivita" katika sehemu nyeti za uongozi wa Chama na serikali,taratibu tunaanza kuliondoa Taifa letu kwenye demokrasia tunayoihubiri.

Kina Nkurunzinza walioamua kung'ang'ania madaraka kwa kujiongezea mihula ya uongozi kinyume na katiba,walifanya hivyo baada ya kuona wana uungwaji mkono wa "jeshi lililoiasi katiba".Uasi huu wa katiba ufanywao na vyombo vyetu unamaana gani kama si maandalizi ya watu kuja kung'ang'ania madarakani huko tuendako?Au haya ndiyo yanayopelekea hadi jf ambayo ndiyo platform pekee iliyobaki tutumiayo kuihoji serikali baada ya magazeti,redio na TV kusalimu amri mbele ya dola na sasa wanaanza kumuwinda mkurugenzi wetu wa jf?

Tuendako ni Mungu tu ajuwaye,Yeye ndiye mweye uwezo wa kuichunguza mioyo yetu,Mungu wa Mbinguni Atuepushe na hili,amen.

Mkuu, unaweza ukawa na hoja lakini unasahau ukweli kwamba ndani ya CCM kuna wanajeshi.

1. Luteni kanali Abdulrahman Kinana

2. Kapteni George Mkuchika

3. Luteni Kanali Jakaya Kikwete

4. Kapteni John Zefania Chiligati

Na wengine wengi tu, sembuse huyu kanali Lubinga?

Kanali Lubinga alitoka jeshini akaenda kuwa DC Mlele Mkoani Katavi na baadae jeshi likamhitaji kuwa mkurugenzi wake wa habari na mahusiano (eneo ambalo ana utaalam nalo).

Hawa ni watu ambao ambao unaweza kusema kwamba wanacheza mpira kama "box to box midfielders" na ndicho kilichomsukuma JPM kumteua kuziba nafasi ya mama Migiro khasa lugha ya mawasiliano jamaa ametulia.
 
Nimegundua si kosa lako, tatizo lako unataka kuonyesha wana JF kuwa unajua lakini hujui chochote. Acha tukukumbushe-wakati tukiwa na chama kimoja asilmia kubwa ya wafanya kazi wote na wafanyabiashara walikuwa wanachama wa ccm, majeshi yote walikuwa wanachama wa ccm na siasa ilifundishwa hadi majeshini, na ndo maana tokea nyakati hizo wanajeshi waliteuliwa katika nyadhifa mbalimbali mfano-Mh. Jakaya Kikwete, Mh.Kinana na wengine wengi-si ajabu hicho kinachofanyika




Nilishasema hapa mara nyingi,na leo nasema tena- ni fedheha sana kuwa kiongozi wa ngazi yoyote ya Taifa letu ikiwa uongozi wako unatokana na kuchaguliwa na wanaCCM.Hebu angalia nukuu ya katiba yetu hapo juu kwenye huu Uzi halafu uniambie huyo mteule alianza lini kuwa mwanachama wa CCM hadi kuwa na sifa za kuteuliwa kuwa kiongozi ndani ya Chama?

Naanza kumuelewa yule mgombea aliyeinadi Elimu kuwa ingekuwa agenda yake namba 1,2 na 3 kama angepata ridhaa ya kuiongoza nchi,kama wewe ndiyo jamii ya watu mnaowachagua CCM,basi CCM ipo hapo ilipo kwa kuchaguliwa na watu wasiojielewa kabisa.
 
Siku unayoteuliwa unaacha jeshi huwi mwanajeshi na unashika madaraka siku hiyo hiyo kama ambavyo lowasa alivyofanya.Siku alipoteuliwa na CHADEMA kuwa mgombea siku hiyo hiyo aliacha CCM na kuwa mgombea uraisi
Hujajibu swali bado. Hoja kuu ni kwamba je alikuwa mwanachama wa CCM wakati angali mwanajeshi? La sivyo isingepatikaka base ya kumteua kwasababu kuwa mwanachama wa CCM ndio base kuu ya kuchaguliwa au kuteuliwa kwenye nafasi mbalimbali za kichama.
 
Nimehoji juzi kuhusu vyombo vya usalama, Polisi, magereza, JWTZ,Pale kwenye sherehe za uhuru kuimba kwaya ambayo ukiisikiliza maudhui yake ni kama kwaya ya Chama cha mapinduzi, nikauliza hii inaashiria nini?
 
Hujajibu swali bado. Hoja kuu ni kwamba je alikuwa mwanachama wa CCM wakati angali mwanajeshi? La sivyo isingepatikaka base ya kumteua kwasababu kuwa mwanachama wa CCM ndio base kuu ya kuchaguliwa au kuteuliwa kwenye nafasi mbalimbali za kichama.

Kwani mkuu, unafahamu ni lini Kanali Ngemela alikuwa mwanajeshi?

Jaribu kujiuliza kwanini amekuwa akihamahama kutoka uraiani (alipokuwa mkuu wa wilaya) na baadae kuombwa kurudi JWTZ Upanga.

Ukipata majibu ndiyo utaelewa kwanini raisi JPM hajakiuka katiba kwa kufanya uteuzi wa kanali Ngemela.
 
Mkuu, unaweza ukawa na hoja lakini unasahau ukweli kwamba ndani ya CCM kuna wanajeshi.

1. Luteni kanali Abdulrahman Kinana

2. Kapteni George Mkuchika

3. Luteni Kanali Jakaya Kikwete

4. Kapteni John Zefania Chiligati

Na wengine wengi tu, sembuse huyu kanali Lubinga?

Kanali Lubinga alitoka jeshini akaenda kuwa DC Mlele Mkoani Katavi na baadae jeshi likamhitaji kuwa mkurugenzi wake wa habari na mahusiano (eneo ambalo ana utaalam nalo).

Hawa ni watu ambao ambao unaweza kusema kwamba wanacheza mpira kama "box to box midfielders" na ndicho kilichomsukuma JPM kumteua kuziba nafasi ya mama Migiro khasa lugha ya mawasiliano jamaa ametulia.




Hoja yangu si uwepo wa majenerali na maluteni ndani ya chama,hoja ni je,walianza lini kuwa wanachama wa CCM?Mwaka jana Taifa lilipigwa na butwaa baada ya kumshuhudia aliyekuwa jaji Mh.Augustine Ramadhani akichukuwa fomu kuwania kuteuliwa kuwa mgombea wa urais kupitia CCM,orodha ni ndefu,wapo wakina Tibaigana na wengine wengi waliostaafu lakini ndani ya muda mfupi tuliwaona wakijitosa kwenye siasa kupitia CCM,hoja ni je,lini walianza harakati zao za kisiasa hadi kuamua kujiingiza katika kuwania uongozi?Au walikiuka viapo na katiba za vyombo vyao na ile ya nchi inayowakataza wao kuwa wanachama wa Chama cha siasa?
 
Katiba inasema mwanajeshi haruhusiwi.Ina maana nikiacha hata dakika hii,dakika ya pili inayofuata mimi sio mwanajeshi naweza chukua kadi ya chama chochote cha siasa na nikateuliwa kushika cheo chochote cha kisiasa na hakuna katiba iliyovunjwa.Swala la kuwa sina uzoefu kwenye chama huo ni umbeya.Wao walionipa cheo kama wananiamini tatizo liko wapi.Katiba haijavunjwa na hao wamenipa cheo kwa mapenzi yao hamna shida.
Umesikia tamko au yeye mwenye kuacha uanajeshi?
Halafu unaposema uzoefu, najua unajua kuwa mtu huyo hakutakiwa kuwa mwanachama wa chama chochote akiwa mwanajeshi...
 
NI UKIUKWAJI WA KATIBA AU MAJINA YAMEFANANA KATI YA MSEMAJI WA JWTZ NA HUYU MTEULE WA NEC YA CCM?
JPM JITOKEZE KUUELEZEA UMMA KUHUSU UTATA HUU.​

Msemaji wa JWTZ ni Kanali Ngemela Lubinga.

Katibu Mteule wa NEC ya CCM Siasa na Uhusiano wa Kimataifa ni Kanali Ngemela Eslom Lubinga.

Katiba ya Jamhuri 1977 inasema :-

SURA YA TISA
MAJESHI YA ULINZI

Ibara ya 147.

Ibara ndogo ya (3),
Itakuwa ni marufuku kwa mwanajeshi yeyote kujiunga na chama chohote cha siasa, isipokuwa tu kama atakuwa na haki ya kupiga kura iliyotajwa katika ibara ya 5 ya Katiba hii.

Ibara ndogo ya (4),
Kwa madhumuni ya ibara hii, "mwanajeshi" maana yake ni askari aliyeajiriwa kwa masharti ya muda au ya kudumu katika Jeshi la Ulinzi, Jeshi la Polisi, Jeshi la Magereza au Jeshi la Kujenga Taifa.
duuuuuuuh......na mtemi kapita
 
Back
Top Bottom