Msikilize Mzungu akitoa sababu za Sub-Saharan Africa kuwa Masikini

Mkuu ulichoandika ili nihalalishe nilichosema ni hapana, ila nilichoandika kina jambo la juu zaidi either uelewa wako ni mdogo.

Mambo ya kodi nk ni mambo madogo mno kwa mataifa beberu, eavy issues zao zikiguswa ndipo huwa wanatoka vitini ila hayo mambo ya mmeibiana na kurogana ni utoto wenu.


Mfano, nini sababu ya kumuua Gaddaf..?
 
Kuna issues ndani ya hii dunia kama huzijui unaandika as you wrote.
Unahitaji uweze kuona vitu katika all dimension na ukiwa open minded kuona uhalisia.
maafisa wa CIA huwa wanasema mengi siku zao za kuondoka zikifika.
 
Jiwe ni Corona bana
 
Uzi ni mzuri sana ningetamani kusoma kila comment…

Ila ukweli ni kwamba kuna mabeberu wanaotegemea raw materials/resources kutoka Afrika watafanya kila njia wasiingiliwe kwenye anga hizo…they are so powerful and well organized…

Ukitaka ujikomboe lazima ufunge mkanda kweli kweli mkanda sio wakitoto…hili hakuna mtanzania ambae yuko tayari utapigwa vita kila kona…dikteta muuwaji sijui nani majina yote utapewa..sijui Mao kwa wachina walimuita nani…

Kuhusu viongozi wa Afrika na waafrika kwa ujumla kuna mzungu mmoja aliwahi kusema shetani hana haja ya kuja kuhangaika kuwadanganya waafrika..umaskini, ujinga na njaa tu zinawafanya mtende dhambi…shetani ana kazi Vegas uko watu wanapesa hawajui wazifanyie nini….kwa maana hio hata watumiminie mabilioni zitaenda mifukoni kwa wenye madaraka na hilo wazungu wanalijua….

Kwahio pamoja na kuwacontrolled na super powers “the elite” tuna upungufu wa watu wenye guts na uzalendo na kujitoa muhanga kwa ajili ya kujenga nchi…tunaweza kuwa nao ila supporting system yote imeshakuaa corrupt au km sio brain washed na elimu za wazungu…ndio maana JPM alipoona gurudumu ni gumu kulizungusha mwenyewe na ni sababu ya upofu wa waliomzunguka akaomba somo la historia lifanyiwe marekebisho mashuleni labda kuna mbegu fulani itapandwa itakuwa na manufaa baadae…
 
Bahati mbaya sana somo lenyewe limetupiliwa mbali huko!
 
hili hakuna mtanzania ambae yuko tayari utapigwa vita kila kona
YES.
Afrika ni bado sana, Mao alijitoa na akaamua kama anavyoamua yule wa north Korea vinginevyo beberu hakupi nafasi.

Gaddaf alikuwa kwenye traki nzuri ila ndiyo hivyo.
 
Hicho kiatu kilitengenezwa kiwanda cha mitaa gani hapo memorial.maana usikute ulikutana na wazungu wajinga mkaanza kujadili ujinga.

Sent from my SM-A107F using JamiiForums mobile app
Ujinga ni pale wewe unayezani maimoria wanakiwanda cha viatu wakati pale wanauza mitumba inayotoka ulaya na marekani! Nisawa na uniulize nimepataje VX Toyota hapa Tanzania wakati hakuna kiwanda ilihali kila ukigeza macho unakutana na yard inauza used cars from Japan!
Hebu nisaidie MJINGA hapa ni nani!
 
Mshiriki umefanya jambo zuri sana.

Ukweli washiriki humu JF tusidhalilishe jukwaa. Mtu hata kama humkubali kwa kiwango chochote, jaribu kujielekeza kwa hoja zenye staha.

Tusaidiane wote kukemea tabia hiyo. Tunajenga familia na jamii ya hovyo kabisa.
 
Changamoto kubwa ya AFRICA ni ubongo mbovu wa mtu mmoja mmoja.Hata kama hutaki ukweli ndo huo
Tujiulize huo ubongo mbovu unasababishwa na nini? Ni kuumbwa kwetu? Ni mazingira? Au ni nini?
 
Bwana Peter the rock shusha madini yako humu. Haya ndio mambo ya kujadili humu.
Kidogo kidogo tuelimishane hadharani.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…