Msimamo wa chama cha ACT-Tanzania na katiba mpya

Msimamo wa chama cha ACT-Tanzania na katiba mpya

Huko nyuma Kitila Mkumbo aliandika sana juu ya jinsi gani taifa linahitaji mbadala wa chama kikuu cha upinzani - yani mbadala wa chadema. Katika suala nyeti Kama hili la mchakato wa katiba mpya, ACT kuja na msimamo Kama wa chadema, hasa juu ya kuwa upande wa wananchi, halafu hapo hapo kutounga mkono UKAWA ni kitendo ambacho kinaacha maswali mengi kuliko majibu huku mitaani. Nazungumza Nikiwa kijiweni nikisikiliza mijadala Hapa. Wanasema mengi lakini in a nutshell, ni hayo hapo juu.


Sent from my iPhone using JamiiForums

Mchambuzi,

Asante sana.Na Kitila Mkumbo, alikua ndani ya kamati kuu ya CHADEMA maoni yaliyopelekwa Tume anayajua na pia ndio yalikua msingi wa maandiko yake kwenye makala.

Hata maoni ya mkwamo wa bunge la katiba Lissu alizungumzia na Dr.Slaa alishawi kutoa msimamo kuwa hakuna haja ya haraka ya katiba mpya na kama haiwezekani iliyopo ifanyiwe marekebisho.

Mara kadhaa ndugu Zitto amekua akikebehi msimamo huu kwenye page yake ya Facebook.

Sasa leo wanakuja na summary zile zile kama vile ni maoni mapya tena yanayopingana na misimamo yao kwa sasa.
 
Last edited by a moderator:
Maoni ya ACT yanatofauti gani na Maoni yaliyotolewa na CHADEMA?Yaani mna-copy na Ku-paste maoni ya CHADEMA?
Tena asilimia kubwa ya maoni hayo ni kwa tume ya katiba.Hilo la kuahirisha Bunge pia ni maoni ya CHADEMA na hata marekebisho ya katiba kuruhusu uundwaji wa tume huru ya uchaguzi na taasisi nyingine za kidemokrasia ni maoni ya CHADEMA

Huu ujanja ujanja wa kudandia hoja ndio uliowapeleka JB Hotel kuitisha Press?
Mbona hata nyie mtindo wa kujilipua mnacopy kwenye mataifa mengine?

Hivi ule uongo wa Lissu na wale madiwani ni mpya?

Kuna tatizo gani mtu akiona jambo zuri akalisema tena? Acha chuki kijana hakuna jipya chini ya jua!
 
Mwl,''kudhaa'' ndio kufanyaje?
Mchakato utadhaa......... !
 
Wamechukua Maoni ya CHADEMA kwa tume ya Katiba na pia maoni juu ya mchakato wa Bunge Maalumu la Katiba.

Huu ushabiki wa Simba na Yanga kwa vyama vya siasa ndio unaofanya hivi vyama kuwa tatizo badala ya solution....

Hivi kuna ubaya gani wa Chama au Taasisi nyingine kuwa na Maoni au msimamo sawa na chama fulani (in this case chadema)
 
Mbona hata nyie mtindo wa kujilipua mnacopy kwenye mataifa mengine?

Hivi ule uongo wa Lissu na wale madiwani ni mpya?

Kuna tatizo gani mtu akiona jambo zuri akalisema tena? Acha chuki kijana hakuna jipya chini ya jua!

Sasa mkuu huoni ni utapeli kwa jinsi headline/title ya thread ilivyokaa?Watasemaje ni maoni ya ACT -Tanzania ?

Headline ilipaswa kuwa ACT-Tanzania yaunga Mkono msimamo na maoni ya CHADEMA
 
Mchambuzi,

Asante sana.Na Kitila Mkumbo, alikua ndani ya kamati kuu ya CHADEMA maoni yaliyopelekwa Tume anayajua na pia ndio yalikua msingi wa maandiko yake kwenye makala.

Hata maoni ya mkwamo wa bunge la katiba Lissu alizungumzia na Dr.Slaa alishawi kutoa msimamo kuwa hakuna haja ya haraka ya katiba mpya na kama haiwezekani iliyopo ifanyiwe marekebisho.

Mara kadhaa ndugu Zitto amekua akikebehi msimamo huu kwenye page yake ya Facebook.

Sasa leo wanakuja na summary zile zile kama vile ni maoni mapya tena yanayopingana na misimamo yao kwa sasa.
Maridhiano ni pamoja na kukubali kupoteza sasa nyie mnataka ushindi na hamtaki kusiikiliza wengine Mnataka nyie ndio msikilizwe tuu!

Sasa Act wameshauri mwende kwenye Maridhiano lakini wewe uoni Kama ni jipya maana umekariri Kuwa maridhiano ni kukubaliwa Hoja zako kumbe hata kukubali hoja za wengine!
 
Last edited by a moderator:
Huu ushabiki wa Simba na Yanga kwa vyama vya siasa ndio unaofanya hivi vyama kuwa tatizo badala ya solution....

Hivi kuna ubaya gani wa Chama au Taasisi nyingine kuwa na Maoni au msimamo sawa na chama fulani (in this case chadema)

Jaribio la kutaka kuaminisha watu kuwa huo ni msimamo wao huku wakipingana kivitendo na waliotoa msimamo huo ni utapeli wa kisiasa na kijamii.Tena unaweka signature chini kuwa umetolewa na katibu mkuu wa ACT wakati hayo ni maoni ambayo yalishatolewa huoni kuwa kuna athari juu ya matumizi ya raslimali muda na fedha kwa jamii?
 
Umeshawahi kuona ccm ikawa na wazo jipya? Sana sana ni kuteka hoja za CDM na kuzifanya zakwao na ndiyo maana wanaishia kuumbuka kwa kukosa ufahamu juu ya agenda wanazoziteka. Mfano agenda ya Katiba mpya sasa inawaumbua!.

Wameumba ACT kama kitengo cha kutafuta nguvu machoni pa wananchi kwa kutoa matamko yanayofunika aibu zao, kuhamasisha watu kukubaliana na misimamo ya ccm, na kuhujumu upinzani. It is known. Angalia na utaona kuanzia sasa, kila watakapochemka, ACT itakuja na aina fulani ya kurekebisha lakini kwa kuiba ideas za CDM.

Lakini, Democrasia Makini (kama sikosei) ilianzishwa ccm Zanzibar ili kupunguza nguvu ya CUF. Na viongozi walichukuliwa kutoka vyama mbali mbali chini ya ufadhili wa serikali ya ccm lakini mwisho wake uko wapi?

CCM haina namna namna kwa CDM.

Copy and Paste..! Hakuna kitu hapo
 
Maridhiano ni pamoja na kukubali kupoteza sasa nyie mnataka ushindi na hamtaki kusiikiliza wengine Mnataka nyie ndio msikilizwe tuu!

Sasa A-Ct wameshauri mwende kwenye Maridhiano lakini wewe uoni Kama ni jipya maana umekariri Kuwa maridhiano ni kukubaliwa Hoja zako kumbe hata kukubali hoja za wengine!

Viongozi wetu walikua kwenye vikao.Kunahitaji maridhiano gani zaidi ya kujadili Maoni ya Rasimu ya Tume yaliyotolewa na Wananchi?Maridhiano ya kukubali kupunguza People's Sovereignity katika utungaji wa katiba ni hujuma kwa Taifa na watu wake
 
Sasa mkuu huoni ni utapeli kwa jinsi headline/title ya thread ilivyokaa?Watasemaje ni maoni ya ACT -Tanzania ?

Headline ilipaswa kuwa ACT-Tanzania yaunga Mkono msimamo na maoni ya CHADEMA
hawajaunga mkono kila jambo na hoja zenu wasome utaona!

Nyie hamtaki Maridhiano bali mnahitaji ushindi wao wana washauri mwende kwenye maridhiano na maana yake muwe tayari kupoteza na kupata. Tatizo la chadema ni ujuaji mwingi!
 
Wamechukua Maoni ya CHADEMA kwa tume ya Katiba na pia maoni juu ya mchakato wa Bunge Maalumu la Katiba.

Mbona haya haya ndiyo aliyoyaandika Zitto kwenye wall yake ya FB? Hiki chama kina uhusiano gani na MM2?
 
ACT ni kati ya wale Prof. Kabudi anawaita walioshupaa

Hamna mpya zaidi ya kuripoti na kuwa centre,chagueni upande
 
Viongozi wetu walikua kwenye vikao.Kunahitaji maridhiano gani zaidi ya kujadili Maoni ya Rasimu ya Tume yaliyotolewa na Wananchi?Maridhiano ya kukubali kupunguza People's Sovereignity katika utungaji wa katiba ni hujuma kwa Taifa na watu wake
Kinacho jadiliwa ni maoni ya wananchi kutoka kwenye Rasimu na hata kabla ya nyie kususa wote mlikuwa mnajadili hayo hayo maoni na hata leo ndio yanayo jadiliwa na kuchambuliwa! Au kabla ya nyie kutoka mlikuwa mnajadili nini bungeni na kwenye kamati!

Umeona Rasimu mpya pale!
 
hawajaunga mkono kila jambo na hoja zenu wasome utaona!

Nyie hamtaki Maridhiano bali mnahitaji ushindi wao wana washauri mwende kwenye maridhiano na maana yake muwe tayari kupoteza na kupata. Tatizo la chadema ni ujuaji mwingi!

Kwamba tukubali rasimu nyingine ijadiliwe bungeni?Kama hayo ndio maridhiano basi maridhiano ni adui wa haki ,demokrasia na ni adui wa katiba ya wananchi
 
ACT Wanatafuta Kiki tu. Kijiwe cha wasaliti hufuata upepo tu wa kusaka umaarufu.
Ova.
 
Tumia akili yako kujenga hoja sio ubishi usio na msingi.
 
Alliance for Change and Transparency-Tanzania Maoni ya ACT-Tanzania kuhusu namna ya kutoka katika mkwamo uliopo katika mchakato wa Katiba Mpya.

1. Nchi yetu iliingia katika mchakato wa Katiba kwa kushirikisha wananchi wote ili kupata Katiba bora yenye kuakisi matakwa ya nchi kwa sasa na baadaye. Ili kupata Katiba bora na inayokubalika na wananchi wengi iwezekanavyo, ni lazima mchakato wa kutunga Katiba uwe wazi, shirikishi na wenye kuzaa mwafaka na maridhiano miongoni mwa makundi mbalimbali ya wananchi

2. Chama cha ACT-Tanzania kinaipongeza sana Tume ya Mabadiliko ya Katiba iliyofanya kazi yake kwa bidii, umakini na weledi mkubwa kwa kuwashirikisha wananchi kwa upana wake na kwa kuzingatia maoni ya wananchi na matakwa ya nchi ya sasa na baadaye katika kuandika Rasimu ya Katiba.

3. Chama cha ACT-Tanzania kilitarajia kwamba Bunge Maalumu la Katiba lingeiga na kuendeleza utamaduni wa iliyokuwa Tume ya Mabadiliko ya Katiba katika kuhakikisha kwamba mwafaka na maridhiano yanapewa nafasi katika kila hatua ya mjadala badala ya kuzingatia misimano ya vyama vya siasa na wingi wa wajumbe wanaounga mkono hoja fulani katika mijadala. Bahati mbaya Bunge Maalumu la Katiba limeshindwa kuzingatia utamaduni wa maridhiano uliojengwa na wajumbe wa iliyokuwa Tume ya Mabadiliko ya Katiba.

4. Chama cha ACT-Tanzania kimesikitishwa sana na viongozi wa vyama vya siasa wa CCM na vile vinavyounda kundi la UKAWA kwa kushindwa kwao kupata mwafaka na maridhiano kuhusu muundo wa muungano wa nchi yetu na hata kusababisha kuvurugika kwa mchakato wa Katiba. Ni aibu kwamba mchakato mzima wa Katiba katika Bunge Maalumu umetekwa na sera za vyama vya siasa kuhusu muundo wa serikali ya Muungano badala ya kutafakari na kujadaili Rasimu ya Katiba kwa upana wake na kwa maslahi ya nchi na wananchi kwa ujumla.

5. Chama cha ACT-Tanzania kinasikitika kwamba Bunge Maalumu la Katiba linaendelea na ratiba yake ilihali kundi kubwa la wajumbe likiwa nje ya mchakato. Bila kujali sababu za kundi la UKAWA kuwa nje ya Bunge Maalumu la Katiba, ACT- Tanzania haiamini kwamba mchakato huu utadhaa Katiba bora na yenye kukubalika kwa upana bila makundi yote muhimu kushiriki katika mchakato huu kwa ukamilifu wake mwanzo hadi mwisho. Ni maoni ya ACT-Tanzania kuwa tukiendelea na mchakato kama ulivyo sasa inawezekana tukapata katiba mpya yenye uhalali kisheria. Lakini itakuwa ni katiba isiyo na uhalali wa kisiasa wala kijamii, na kwa maana hiyo itakuwa haina tofauti ya maana na katiba ya sasa na hivyo kuifanya nchi kuingia kwenye hasara kubwa ya fedha za umma.

6. ACT-Tanzania haioni uwezekano wa kupatikana katiba mpya iliyo bora katika kipindi hiki, hasa kwa kuzingatia mkwamo uliomo baada ya wajumbe kujikita katika misimamo ya vyama vyao badala kujadili rasimu ya katiba mpya kwa uhuru, umakini na weledi.

7. Kutokana na mazingira ya mchakato wa Katiba tuliyoeleza hapo juu, ACT-Tanzania inapendekeza hatua zifuatazo zichukuliwe mapema iwezekanavyo ili kunusuru mchakato wa Katiba na kurudisha hali ya kuelewana katika jamii yetu:

a. Bunge Maalumu la Katiba lisimamishwe ili kuendelea kutoa fursa ya mazungumzo ya kutafuta mwafaka na maridhiano.

b. Mchakato wa kuandika katiba mpya uahirishwe hadi baada ya uchaguzi mkuu.

c. Katika kipindi hiki kuelekea uchaguzi mkuu, Bunge la Jamhuri ya Muungano lifanye marekebisho katika katiba ya sasa ili kutengeneza mazingira ya uchaguzi ulio huru na haki.

Tunapendekeza marekebisho ya katiba ya sasa katika maeneo kumi (10) yafuatayo:

i) Tume ya Uchaguzi iwe huru na ionekane kuwa huru,

ii) Kuruhusu mgombea binafsi na wabunge ‘kukatisha kapeti’ bila kupoteza ubunge wao ili kudhibiti ubabe wa vyama vya siasa

iii) Kushusha umri wa mgombea urais ili kuwapa vijana haki na fursa ya kugombea katika nafasi hii muhimu, hasa ukizingatia kwamba karibu theluthi mbili (65%) ya wapiga kura wote Tanzania wapo chini wa umri wa miaka 40, na ukweli kwamba takwimu za Tume ya Marekebisho ya Katiba zinaonyesha kuwa wananchi walio wengi (53.7%) waliotoa maoni kuhusu umri wa mgombea urais walitaka umri huo ushushwe.

iv) Kuweka sharti kwamba ili mgombea atangazwe kuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano lazima apate angalau asilimia 50 ya kura zilizo halali.

v) Kuweka msingi wa kikatiba kwamba wagombea Urais lazima wawe na angalau midahalo mitatu katika kipindi cha kampeni.

vi) Kuondoa suala la Mafuta na Gesi katika mambo ya Muungano ili kuruhusu Zanzibar kuendelea na utafutaji wa Mafuta na Gesi asilia kwa uhuru na bila kuingiliwa na Tanzania bara

vii) Kuruhusu Zanzibar kuwa na mahusiano na ushirikiano wa kimataifa (International Cooperation) kwa faida za maendeleo yake.

viii) Kuweka mipaka ya Mashtaka ya Kesi za Rushwa ili kuruhusu TAKUKURU kufanya uchunguzi na kuendesha kesi hususani kwa kesi ufisadi wa mali umma bila kupita kwa Mkurugenzi wa Mashtaka.

ix) Kuweka msingi wa kisheria wa Tangazo la Mali na Madeni ya Viongozi kuwa wazi kwa Umma na uthibitisho wa uhalali wa mali ambazo mtu anamiliki uwe upande wa mtuhumiwa (reverse of burden of proof).

x) Kuweka msingi wa Kikatiba wa Uhuru wa kupata habari kwa wananchi (Freedom to access information) na kupiga marufuku vyombo vya habari kufungiwa isipokuwa kwa amri ya mahakama.

8 Chama cha ACT-Tanzania kinatoa wito kwa wadau wote wa Katiba kuungana katika kushinikiza mchakato wa Katiba unaoendelea kusimamishwa na kuruhusu mabadiliko hayo machache ya Katiba ya sasa ili kupisha uchaguzi na kuhakikisha Taifa linapata muda wa kutosha wa kuandika Katiba bila shinikizo na katika hali ya utulivu.

8 ACT-Tanzania inawataka mahasimu katika mchakato wa Katiba kutoa fursa kwa majadiliano na kujenga mwafaka na maridhiano ya nchi katika maeneo hayo. Tunasisitiza kwamba tusichoke kuzungumza katika masuala ya nchi yetu kwani mbadala wa mazungumzo ni fujo na upotevu wa amani.

Asanteni kwa kunisikiliza
Ndugu Samson Mwigamba
Katibu Mkuu, ACT-Tanzania.

Hizi ni sera na misimamo ya zito ubinafsi, eti kushusha umri wa mgombea urais na na mgombea binafsi ili zito agombee urais. Tumewashutukia. Hamna pakutokea hapo mmekwisha
 
Sasa mkuu huoni ni utapeli kwa jinsi headline/title ya thread ilivyokaa?Watasemaje ni maoni ya ACT -Tanzania ?

Headline ilipaswa kuwa ACT-Tanzania yaunga Mkono msimamo na maoni ya CHADEMA

Taratibu kidogo...

Ni wapi Chadema wameshauri kama hatua ya dharura wakati huu baada ya kuharishwa mchakato wa katiba basi

1. Umri wa mgombea urais ushushwe?

2. Chadema wameshauri wapi mshindi wa urais awe na 50%?hiyo 52% ya Dr Slaa sijui kaiona nchi gani, unless hajui maana ya kuvuka nusu.

3. Chadema wameshauri wapi suala la mafuta na gesi litolewe kwenye masuala ya muungano?

4. Chadema wameshauri wapi mgombea Ubunge aweze kuhama chama bila kupoteza ubunge??

5. Je Chadema na Dr Slaa hapo ameshauri kipengele cha mgombea binafsi kiwekwe SASA??


Kama haya hayapo kwenye taarifa ya Chadema basi hiyo sio copy na kupaste, unless hujui maana ya kucopy na kupaste.
 
Back
Top Bottom