GENTAMYCINE
JF-Expert Member
- Jul 13, 2013
- 60,660
- 121,325
Najua huko ( huku ) Mitaani sasa Gumzo ni Yanga SC 'Kanunua' kwa KMC FC na kwamba Kipa Farouq Shikalo na Beki Vicent Dante Chikupe ndiyo 'wamechomesha' kwa Kuchukua 'Mlungula' Yanga SC kwakuwa walitoka huko.
Nadhani JamiiForums nzima hakuna asiyejua kuwa GENTAMYCINE Mimi ni Simba SC 'lia lia' na kama kuna Timu au Klabu siipendi duniani basi ni Yanga ( japo kwa Ulaya ni Manchester United nayo siipendi pia ) ila leo nataka kusema Ukweli bila kuwa Mnafiki na Mgumu wa Kukubali Uzuri wa Kikosi cha Yanga SC na Mikakati yao ya 'Kiufundi' Uwanjani.
Ufuatao ni Mtizamo wangu GENTAMYCINE wa Jicho la 'Kiufundi' la kwanini Yanga SC inafanya vyema katika NBC Tanzania Premier League na kama Timu zote Pinzani ( ikiwemo yangu ya Simba SC ) zisipojipanga 'Kimkakati' zitafungwa sana tu na kuendelea Kuimba Wimbo wetu wa Kipumbavu ( Kipopoma ) wenye 'Wivu' mwingi kuwa Yanga SC inabebwa au inahonga Timu ( Vilabu ) Pinzani......
1. Yanga SC wamesajili Kiushindani
2. Yanga SC ina Wachezaji wenye Tamaa ya Mafanikio
3. Yanga SC ina Kocha mwenye Kipaji cha Kuwasoma Wapinzani hasa Kiudhaifu wao
4. Yanga SC ina Wachezaji mahiri wa Kigeni wenye kujua Kumaliza Mechi
5. Yanga SC imefanikiwa zaidi Kuwajenga 'Kinguvu' Wachezaji wake na nampa mno Sifa Kocha wao mpya wa Viungo kwani Wachezaji wa Yanga SC wa sasa wana Nguvu na inawasaidia
6. Yanga SC wana Mshikamano mkubwa kuanzia ndani kwa Wachezaji wao husika na hata nje wa Wanachama, Wapenzi na Mashabiki wao
7. Yanga SC ina Wachezaji wenye 'Confidence' ya hali ya Juu kitu ambacho 'Kiufundi' pia huwa kina Faida na kuwa 'Tishio' kwa Timu (Vilabu) Pinzani.
Wana Simba SC Wenzangu leo mnisamehe Mwenzenu GENTAMYCINE kwa huu Ukweli na Uwazi wangu bali na Sisi hatujachelewa ama Kuyaiga baadhi au hata yote haya ya 'Kiufundi' kutoka kwa Wapinzani wetu Yanga SC ili tuendelee kuwa Bora zaidi yao ila tukizembea 'Kimikakati' basi ni dhahiri Msimu huu huenda Yanga SC nao wakajiuliza na hata Kutuvua Ubingwa.
Najua fika kuwa Ligi Kuu ndiyo Kwanza bado Mbichi ila Wahenga zetu hawakukosea walipokuja na hii 'Misemo' isemayo 'Dalili ya Mvua ni Mawingu' na 'Biashara asubuhi Mahesabu jioni' hivyo Simba SC tusibweteke wala tusikariri au tusiishi Kimazoea kwani si kila mwaka Upepo utakuwa upande Wetu tu na tusisahau kuwa hata Bingwa wa Msimu huu hachukui zile Shilingi Milioni 70 au Shilingi Milioni 80 tulizozizoea bali sasa anachukua Shilingi Milioni 500 kutoka Azam.
Hongereni tu Watani zangu mpo vizuri.
Nadhani JamiiForums nzima hakuna asiyejua kuwa GENTAMYCINE Mimi ni Simba SC 'lia lia' na kama kuna Timu au Klabu siipendi duniani basi ni Yanga ( japo kwa Ulaya ni Manchester United nayo siipendi pia ) ila leo nataka kusema Ukweli bila kuwa Mnafiki na Mgumu wa Kukubali Uzuri wa Kikosi cha Yanga SC na Mikakati yao ya 'Kiufundi' Uwanjani.
Ufuatao ni Mtizamo wangu GENTAMYCINE wa Jicho la 'Kiufundi' la kwanini Yanga SC inafanya vyema katika NBC Tanzania Premier League na kama Timu zote Pinzani ( ikiwemo yangu ya Simba SC ) zisipojipanga 'Kimkakati' zitafungwa sana tu na kuendelea Kuimba Wimbo wetu wa Kipumbavu ( Kipopoma ) wenye 'Wivu' mwingi kuwa Yanga SC inabebwa au inahonga Timu ( Vilabu ) Pinzani......
1. Yanga SC wamesajili Kiushindani
2. Yanga SC ina Wachezaji wenye Tamaa ya Mafanikio
3. Yanga SC ina Kocha mwenye Kipaji cha Kuwasoma Wapinzani hasa Kiudhaifu wao
4. Yanga SC ina Wachezaji mahiri wa Kigeni wenye kujua Kumaliza Mechi
5. Yanga SC imefanikiwa zaidi Kuwajenga 'Kinguvu' Wachezaji wake na nampa mno Sifa Kocha wao mpya wa Viungo kwani Wachezaji wa Yanga SC wa sasa wana Nguvu na inawasaidia
6. Yanga SC wana Mshikamano mkubwa kuanzia ndani kwa Wachezaji wao husika na hata nje wa Wanachama, Wapenzi na Mashabiki wao
7. Yanga SC ina Wachezaji wenye 'Confidence' ya hali ya Juu kitu ambacho 'Kiufundi' pia huwa kina Faida na kuwa 'Tishio' kwa Timu (Vilabu) Pinzani.
Wana Simba SC Wenzangu leo mnisamehe Mwenzenu GENTAMYCINE kwa huu Ukweli na Uwazi wangu bali na Sisi hatujachelewa ama Kuyaiga baadhi au hata yote haya ya 'Kiufundi' kutoka kwa Wapinzani wetu Yanga SC ili tuendelee kuwa Bora zaidi yao ila tukizembea 'Kimikakati' basi ni dhahiri Msimu huu huenda Yanga SC nao wakajiuliza na hata Kutuvua Ubingwa.
Najua fika kuwa Ligi Kuu ndiyo Kwanza bado Mbichi ila Wahenga zetu hawakukosea walipokuja na hii 'Misemo' isemayo 'Dalili ya Mvua ni Mawingu' na 'Biashara asubuhi Mahesabu jioni' hivyo Simba SC tusibweteke wala tusikariri au tusiishi Kimazoea kwani si kila mwaka Upepo utakuwa upande Wetu tu na tusisahau kuwa hata Bingwa wa Msimu huu hachukui zile Shilingi Milioni 70 au Shilingi Milioni 80 tulizozizoea bali sasa anachukua Shilingi Milioni 500 kutoka Azam.
Hongereni tu Watani zangu mpo vizuri.