Msimu huu kwa Mpira huu 'mwingi' wa Yanga SC tutawasingizia Wananunua tu

Msimu huu kwa Mpira huu 'mwingi' wa Yanga SC tutawasingizia Wananunua tu

Najua huko ( huku ) Mitaani sasa Gumzo ni Yanga SC 'Kanunua' kwa KMC FC na kwamba Kipa Farouq Shikalo na Beki Vicent Dante Chikupe ndiyo 'wamechomesha' kwa Kuchukua 'Mlungula' Yanga SC kwakuwa walitoka huko.

Nadhani JamiiForums nzima hakuna asiyejua kuwa GENTAMYCINE Mimi ni Simba SC 'lia lia' na kama kuna Timu au Klabu siipendi duniani basi ni Yanga ( japo kwa Ulaya ni Manchester United nayo siipendi pia ) ila leo nataka kusema Ukweli bila kuwa Mnafiki na Mgumu wa Kukubali Uzuri wa Kikosi cha Yanga SC na Mikakati yao ya 'Kiufundi' Uwanjani.

Ufuatao ni Mtizamo wangu GENTAMYCINE wa Jicho la 'Kiufundi' la kwanini Yanga SC inafanya vyema katika NBC Tanzania Premier League na kama Timu zote Pinzani ( ikiwemo yangu ya Simba SC ) zisipojipanga 'Kimkakati' zitafungwa sana tu na kuendelea Kuimba Wimbo wetu wa Kipumbavu ( Kipopoma ) wenye 'Wivu' mwingi kuwa Yanga SC inabebwa au inahonga Timu ( Vilabu ) Pinzani......

1. Yanga SC wamesajili Kiushindani

2. Yanga SC ina Wachezaji wenye Tamaa ya Mafanikio

3. Yanga SC ina Kocha mwenye Kipaji cha Kuwasoma Wapinzani hasa Kiudhaifu wao

4. Yanga SC ina Wachezaji mahiri wa Kigeni wenye kujua Kumaliza Mechi

5. Yanga SC imefanikiwa zaidi Kuwajenga 'Kinguvu' Wachezaji wake na nampa mno Sifa Kocha wao mpya wa Viungo kwani Wachezaji wa Yanga SC wa sasa wana Nguvu na inawasaidia

6. Yanga SC wana Mshikamano mkubwa kuanzia ndani kwa Wachezaji wao husika na hata nje wa Wanachama, Wapenzi na Mashabiki wao

7. Yanga SC ina Wachezaji wenye 'Confidence' ya hali ya Juu kitu ambacho 'Kiufundi' pia huwa kina Faida na kuwa 'Tishio' kwa Timu ( Vilabu ) Pinzani.

Wana Simba SC Wenzangu leo mnisamehe Mwenzenu GENTAMYCINE kwa huu Ukweli na Uwazi wangu bali na Sisi hatujachelewa ama Kuyaaiga baadhi au hata yote haya ya 'Kiufundi' kutoka kwa Wapinzani wetu Yanga SC ili tuendelee kuwa Bora zaidi yao ila tukizembea 'Kimikakati' basi ni dhahiri Msimu huu huenda Yanga SC nao wakajiuliza na hata Kutuvua Ubingwa.

Najua fika kuwa Ligi Kuu ndiyo Kwanza bado Mbichi ila Wahenga zetu hawakukosea walipokuja na hii 'Misemo' isemayo 'Dalili ya Mvua ni Mawingu' na 'Biashara asubuhi Mahesabu jioni' hivyo Simba SC tusibweteke wala tusikariri au tusiishi Kimazoea kwani si kila mwaka Upepo utakuwa upande Wetu tu na tusisahau kuwa hata Bingwa wa Msimu huu hachukui zile Shilingi Milioni 70 au Shilingi Milioni 80 tulizozizoea bali sasa anachukua Shilingi Milioni 500 kutoka Azam.

Hongereni tu Watani zangu mpo vizuri.
Yanga wamesajili kiushindani, hivi wanawakirisha nchi yetu kwenye mashindano yapi vile? Mkuu hata wewe ukicheza na watoto wa vijijini lazima utaonekana unajuwa kucheza mpira tena shinda hata Mbappe na Messi. Wanaume wanawakilisha nchi kimataifa si kucheza vijijini tu na wauza mboga mboga.
 
Mimi naongea na wewe Mzee. Pambana na mimi. Usiwaingize watu ambao hawapo hapa. Hizo ni dalili za ufinyu kichwani.

Usitumie kichwa kufugia nywele pekee, jaribu kuweka akili ndani yake. Itakusaidia katika maisha yako.

Yaani kati ya mechi 30 tatu zimechezwa umekuwa mchambuzi. Jifunze kwangu dogo.
Tangia lini Vitani Maadui huchaguliana Silaha na jinsi ya Kupambana? Nina Uzoefu mkubwa wa Kupambana na Maadui ( Wapumbavu ) kama Wewe na nimeiga 'Characters' zote za Kiyahudi kuanzia kutumia Akili nyingi na Kumkabili Adui mpaka nimmalize na sijaiweka hapo hiyo Avatar ya Former Israel Premier Benjamin 'BIBI' Netanyahu bure au Kimakosa tu.
 
Yanga wamesajili kiushindani, hivi wanawakirisha nchi yetu kwenye mashindano yapi vile? Mkuu hata wewe ukicheza na watoto wa vijijini lazima utaonekana unajuwa kucheza mpira tena shinda hata Mbappe na Messi. Wanaume wanawakilisha nchi kimataifa si kucheza vijijini tu na wauza mboga mboga.
What a Foolish response from you Fool.
 
Yaani Mpumbavu kama Wewe unapata wapi Uhalali wa Kunipangia 'Brainiac' na 'All Rounder' kama cha Kufanya na Kuandika hapa JamiiForums?

Na kwa Kukusaidia tu sasa siishii tu kufanya Analysis za Mpira bali hata katika Masuala ya Siasa, Ulinzi, Usalama, Diplomasia, Jamii, Elimu na Taaluma kote huko nipo vyema ( nondo ) ile mbaya.

Sasa kama tu ID yangu hii ya GENTAMYCINE inasomwa na Kufuatiliwa kutwa na Marais wako wa sasa ( tokea akiwa Makamu ) n Hayati Mwendazake na Mstaafu Kikwete, Mkuu wako wa Majeshi CDF Jenerali Mabeyo ( na anaikubali hii ID hakuna mfano ) Viongozi, Waandishi wa Habari, Wadau wa Michezo, Taasisi ya Ikulu, Usalama wa Taifa na Wana Taaluma na Wanafunzi wa Vyuo Vikuu huku kila Kukicha tu nikiongeza idadi ya 'Followers' hapa Mpumbavu Mmoja kama Wewe utaweza Kujilinganisha na Mimi?

au hujui ( hujajua ) tu kuwa 85% ya Threads zangu hapa JamiiForums Watu wa Mitandao mingine ( siyo JamiiForums ) hupenda Kuzitumia ili Kuvutia Mijadala katika Blogs na Websites zao?

Kipawa ( Kipaji ) nilichonacho si cha Kawaida na ni Tunu ( Shani ) pekee kutoka kwa Mwenyezi Mungu na ndiyo maana nikabarikiwa na kuwa 'Purely Talented, Charismatic Fella, Game Changer and Entertainer' hivi kiasi kwamba hata Wewe pamoja na Kuvutiwa nami umeamua Kuufungua huu Uzi wangu, Kuusoma Wote na mpaka kupata muda wa Kujibizana hivi nami.
Hizi takataka ndio unajiita mchambuzi.
Nimekuuliza swali.
Yanga wecheza mechi 3 kati ya 30 formula gani umetumia kuweka uchambuzi wako huu.

UNAANZA KUANDIKA INSHA.
JIBU SWALI NILILOKUULIZA
 
Mpira mzuri dhidi ya akina nani?
Rivers utd wamewapiga nje ndani na kuwasepesha virago mapema.
(Usizungumzie derby, derby inabaki kuwa derby kokote duniani)
 
Hizi takataka ndio unajiita mchambuzi.
Nimekuuliza swali.
Yanga wecheza mechi 3 kati ya 30 formula gani umetumia kuweka uchambuzi wako huu.

UNAANZA KUANDIKA INSHA.
JIBU SWALI NILILOKUULIZA
Usinipotezee muda rejea post yangu #45 niliyokuandikia sawa? Eti umeniuliza Swali hivi Mpumbavu nae huwa anajua hata Kuuliza Swali? Yaani ndiyo nazidi tu Kukudharau.
 
Dalili za kutokuwa na akili kichwani. Unakimbilia kutoa maneno machafu.
Jikite kwenye mada yako Mzee. Tunakuuliza maswali yajibu kiume. Acha kutoa mipasho.

JE, WEWE NI HADIJA KOPPA!?
Mpumbavu nae huwa anajua Kuuliza Maswali? Umeanza kuwa na Akili lini hapa JamiiForums?
 
Ajabu kweli, eti mpira mzuri😂😂😂
Mpira mzuri dhidi ya team zipi. Wakati juzi tu wamecheza utopolo na wanigeria🚮🚮
Umeanza lini labda Kufuatilia Michezo?
 
Mimi siyo Mwana Simba SC tu pekee kama ulivyo bali ni Mwana Simba SC lakini pia ni Mwanamichezo na Mdau mkubwa wa Mpira halafu sina Utamaduni wa Unafiki, Ushamba na Upumbavu kama mlionao wengi Wenu.

ANGALIZO / ONYO

Tafadhali kama unajijua Wewe ni Mwana Simba SC ambaye hupendi Kusikia Yanga SC ikisifiwa Kimpira ( Kimchezo ) na Mimi GENTAMYCINE nakuomba uwe unaacha ama Kufungua au hata Kusoma tu Threads na Posts zangu hapa JamiiForums.

Sijajiunga JamiiForums ili niwe tu nawafurahisha Wana Simba SC au wana CCM Wenzangu bali GENTAMYCINE nipo hapa kama Mtu Huru na mwenye Mtazamo na Mawazo yangu ambayo hayafungamani na upande Wowote ule. Yanga SC na CHADEMA ( Wapinzani ) wakipatia sitoacha Kuwasifia na acheni kutaka Kunipangia cha Kuandika hapa kwani Uhalali huo hamna na Wala hamtoupata.

Nimemaliza.
Kama kawaida chizi kalogwa tena
 
Mpira mzuri dhidi ya akina nani?
Rivers utd wamewapiga nje ndani na kuwasepesha virago mapema.
(Usizungumzie darby, darby inabaki kuwa darby kokote duniani)
Sasa kama tu Wewe Mwana Simba SC Mwenzangu kuandika tu vyema na Kiufasaha neno 'Derby' umeshindwa na umeandika Kimakosa 'Darby' kwanini Watu wa Yanga SC wasitudharau, wasitucheke na watuite Makolo?
 
Mpumbavu nae huwa anajua Kuuliza Maswali? Umeanza kuwa na Akili lini hapa JamiiForums?
Acha mipasho Mzee.
Kama uzi umekushinda. Sepa.
Mechi za lingi yanga alizocheza.
1. Kagera
2. Geita Gold
3. KMC

Sasa uchambuzi wako huu wa kitoto umeegemea wapi!?
Yanga anatakiwa kucheza na team 15 mara mbili so far amecheza na team 3.

Uchambuzi wako ni wa taarabu. Nenda kaongee na ZUCHU.
🤣🤣🤣
 
Ajabu kweli, eti mpira mzuri😂😂😂
Mpira mzuri dhidi ya team zipi. Wakati juzi tu wamecheza utopolo na wanigeria🚮🚮
Huyu jamaa dish limeyumba. TV inaonesha chenga chenga.
 
Kama kawaida chizi kalogwa tena
Hivi BAKITA wanajua neno lako la 'Kalogwa' au lao la 'Karogwa' tu? Sasa kwa Kukosea huku neno hili tu jepesi na la Kawaida Mimi na Wewe Nani ameshajulikana na Kujianika kuwa ni Chizi 'aliyerogwa' tena?

Huwa nikiwadharau hapa siwakosei.
 
Back
Top Bottom