Mstaafu wa Jeshi atuhumiwa kuua kwa risasi kisa mgogoro wa mipaka

Mstaafu wa Jeshi atuhumiwa kuua kwa risasi kisa mgogoro wa mipaka

Roving Journalist

JF Roving Journalist
Joined
Apr 18, 2017
Posts
3,984
Reaction score
13,760
Jonas Ziganyige (71) mstaafu wa Jeshi la Wananchi, Mkazi wa Mbezi Juu kwa tuhuma za kumpiga risasi na kumuua Patient Romwadi (48) mfanyabiashara, Mkazi wa Wazo Mivumoni, Kinondoni katika mgogoro wa mipaka.

Mtuhumiwa anadaiwa kufanya tukio hilo Julai 9, 2022 ambapo marehemu alifika eneo akiongozana na Recy Renso (52) kwa lengo la kuangalia mipaka ya kiwanja chake, ndipo mtuhumiwa akatoka ndani akiwa na hasira akampiga risasi Romward na baada ya tukio alikimbia kabla ya kukamatwa Julai 10, 2022 akiwa Kibaha Maili Moja, Pwani alikokuwa amejificha.

Jeshi la Polisi Kanda Maalum Muliro Jumanne amesema wameipata silaha aliyotumia ambayo ni Mark IV ikiwa na risasi 4, atafikishwa Mahakamani kujibu mashtaka yanayo mkabili.

Wakati huohuo, Jeshi la Polisi Kanda Maalum linaendelea pia na jitihada za kuzuia vitendo vya kihalifu kwa kufanya Oparesheni kali inayoongozwa na taarifa fiche dhidi ya Uhalifu na Wahalifu katika maeneo mbalimbali ya Jiji la Dar es Salaam.

Watuhumiwa 8 sugu wa uvunjaji nyumba na kuiba vifaa vya magari akiwemo Jumanne Omary (28) Mkazi wa Mikwambe na wenzake 7 wamekamatwa wakiwa na Tv flat screen za aina ya mbalimbali 4, laptop mbili, sab ufa moja, simu aina mbalimbali tano pamoja na vifaa vya kutendea uhalifu vikiwemo mikasi miwili mikubwa ya kuvunjia, panga moja, kisu kimoja, Prize na Bisibisi, Tochi na Nyaraka mbalimbali.

Pia gari lenye namba za usajili T.787 DGW aina ya Toyota Gaia limekamatwa kwa kuhusishwa na kutumiwa kwenye vitendo vya kihalifu.

Jeshi la Polisi Kanda Maaluma ya Dar es Salaam linatoa wito kwa wananchi kuacha kujihusisha na vitendo vya kihalifu kwani kwa kufanya vitendo hivyo watakamatwa na watajikuta wakiwa katika msuguano mkali wa kiseria na vyombo vya dola.
 
Nimepakana na askari wawili kwenye eneo langu wote tuliuziwa na mtu mmoja aliyeamua kuuza eneo lake vipandevipande, mmoja alinikuta nimeshanunua na mwingine nilimkuta. viwanja vyote vilikuwa vimepimwa. tuliamua kupitia mipaka kwa pamoja ukaibuka mgogoro wa mipaka.

Nilijaribu kutafuta suluhu bila mafanikio, mmoja alikubaliana na bikoni zilizowekwa mwingine alikataa nikaamua kumwachia kijisehemu anakong'ang'ania.

lakini wote 2 walikuwa wababe. Ingawa mmoja alikuwa muelewa na alivitambua vipimo na bikoni za wataalamu.

Itakuwa ni shule na shughuli za jeshi zinawaathiri kwa kiasi fulani baadhi yao hawa wenzetu.

tunawaomba wenzetu mjitahidi kuishi vyema na jamii. Matumizi ya nguvu sio mara zote huleta suluhu.
 
Ukubwa wa eneo sasa linalogombewa
Utakuta vihatua 3,4 tu
Na siku zote ugomvi wa ardhi huwa mmbaya sana,kama watu hamuelewani iko siku ardhi hiyo hiyo
Itammeza mtu

Ova
Kuna ndugu yangu mmoja anasemaga hawez kugombania inshu za mipaka kama jirani atasogeza atamwambia kistarabu kama asipoelewa basi anamwachia
 
Nimepakana na askari wawili kwenye eneo langu wote tuliuziwa na mtu mmoja aliyeamua kuuza eneo lake vipandevipande, mmoja alinikuta nimeshanunua na mwingine nilimkuta. viwanja vyote vilikuwa vimepimwa. tuliamua kupitia mipaka kwa pamoja ukaibuka mgogoro wa mipaka.

Nilijaribu kutafuta suluhu bila mafanikio, mmoja alikubaliana na bikoni zilizowekwa mwingine alikataa nikaamua kumwachia kijisehemu anakong'ang'ania.

lakini wote 2 walikuwa wababe. Ingawa mmoja alikuwa muelewa na alivitambua vipimo na bikoni za wataalamu.

Itakuwa ni shule na shughuli za jeshi zinawaathiri kwa kiasi fulani baadhi yao hawa wenzetu.

tunawaomba wenzetu mjitahidi kuishi vyema na jamii. Matumizi ya nguvu sio mara zote huleta suluhu.
Tatizo wanavuta mibangi
 
Ukubwa wa eneo sasa linalogombewa
Utakuta vihatua 3,4 tu
Na siku zote ugomvi wa ardhi huwa mmbaya sana,kama watu hamuelewani iko siku ardhi hiyo hiyo
Itammeza mtu

Ova
ukweli mtupu[emoji115]
 
Nimepakana na jamaa mmoja (mhirack) pasua kichwa! Kichwani mweupe haelewi kila siku ugomvi! Uzuri natenganishwa naye na barabara. Anatamani ahamishe/achepushe barabara ije kwangu! Ukiwa na jirani kama huyu na ukawa mpole, uwe na uhakika atakunyanganya eneo lako! Wakati mwingine inabidi ukomalie mali yako na ya watoto wako no matter what!
 
Jirani yangu huyu ni Askari wa Jeshi la Wananchi, nilimsimamisha ujenzi maana ameingia kwenye eneo langu. Kula juu kajenga kama alivyoweka msingi huku,hajaacha nafasi, mabati yananing’inia kwenye eneo langu. Nataka siku nimwambie atoe mabati yake kwa kuyakata au nitajenga mabada ya kuku alafu yatamwaga maji kwenye madirisha yake. Kuna watu ni wa ajabu sana hapa Duniani, unaweza kuua mtu kirahisi tu.
IMG_2038.jpg
 
Back
Top Bottom