Mtaalamu wa Dawa na Tiba: Ninakaribisha maswali kuhusu Magonjwa, Tiba na Dawa

Mtaalamu wa Dawa na Tiba: Ninakaribisha maswali kuhusu Magonjwa, Tiba na Dawa

Dr mi nauliza tatizo la mimba, mke wangu anateseka sana na hili tatizo, na tulishajaaliwa kupata watoto bila shida, ila kwa sasa tangu mimba ya mwisho ilipoharibika ukiwa na Miezi 3 akacheleweshwa kisafishwa tangu hapo sasa ni zaidi ya miaka 4 hatujafanikiwa tena, na utra sound akipimwa majibu ni kizungumkuti, kwingine unaambiwa kizazi na mirija safi, kwingine unaambiwa mirija imeziba madawa amekunywa ya kufungua mirija karibu nafungua famasi, mimi nimepima mbegu zimejaa, nisaidie la kufanya maana umri nao unatukimbia sasa hivi mke wangu Ana 42 age lakini bado anableed

Mkuu tafadhali kamuone Gynecologist. Hilo tatizo inaonekana kuwa ya kizazi chake mkewe. Dawa haiwezi kusaidia. Lazima Daktari bingwa wa wanawake na mambo ya kizazi afanye vipimo na akupe ushauri juu ya swala hili. Bila vipimo haiwezekani. Tafadhali mtafute daktari bingwa wa wanawake.
 
Nasumbuliwa na maumivu kwenye korodani kwa Muda mrefu cjui tatizo ni nini

Yaonyesha una infection kwenye korodani. Chukua dawa hizi:

Ciprofloxacin 500mg kidonge kimoja.
Doxycycline 100mg, kidonge kimoja kutwa mara mbili kwa siku saba.
Metronidazole 400mg kidonge kimoja kutwa mara tatu kwa siku saba.

Nipe mrejesho.
 
Dr. Mke Wangu alijufungua mwezi wa pili, baada ya kujifungua ameanza tatizo la kuumwa kiuno mara mara je tatizo ni nini.

Hii tatizo ili anza pale pale baada ya kujifungua au ulianza wiki moja au mbili baada ya kujifungua?
 
Nina tatizo la miguu hasa ktk goti inalia km vijiti vinavyovunjwa hivi ...lkn pia ute ni kama haupo ...pia mifupa huniuma na miguu kuchemka au kuwa ya moto sana na maumivu makali sana...na pia nikisimama muda mrefu nashindwa kabisa ...japo sina unene wowote ...naomba unisaidie

Nimeelewa tatizo lako. Kunywa dawa hizi:

1. Neuroton, Kidonge kimoja kila siku kwa muda wa mwezi mmoja.
2. Gabapentin 300mg, Kidonge kimoja kila siku kwa muda wa mwezi mmoja.
3. Ukiwa na maumivu kwenye goti, kunywa Aceclofenac kidonge kimoja kwa siku.

Asante.
 
Natatizo mmoja.napokuwa na lala kabla sijapata usingizi Wa jumla au nikiwa naelekea kuchukulia na usingizi.nashutuka kwa nguvu sana na hapo ndio napata usingizi nalala moja kwa moja naomba msaada nini tatizo

Hilo tatizo linaitwa' "Hypnic Jerk". Hakuna haja kuchukuwa dawa yeyote kwaajili ya tatizo hili. Inabidi ubadilishe mambo machache kwenye maisha yako.

1. Ule chakula saa moja au zaidi kabla yakulala.
2. Usitumie simu, kompyuta, tv au chochote electronic nusu saa kabla ya kulala.
3. Unapolala usikuwe na fikra yeyote. Inabidi uwe umerelax na upo kwenye starehe.
4. Ni vizuri sana upate usingizi wa masaa sita au saba kila siku.

Zote hizi zitasaidia kupunguza tatizo hilo. Asante.
 
Ninalotatizo la miaka mingi nikisumbuliwa na sub-mandibular salivary glands kwa pande zote mbili. Zinapata blockage na kuzuia mate kutoka. Niliambiwa inaweza kuwa ni stones lakini uchunguzi wangu siyo stones, tatizo ni salivary inakuwa very thick na kushindwa kutoka. nikilazimisha kwa kubonyeza glands, salivary inatoka ikiwa ngumu na wakati mwingine kama uzi.

Nitumie dawa gani?

Mkuu, Unakunywa maji kwa idadi gani kila siku?
Rangi ya mkojo wako ni gani?
 
Dr habari yako, mimi nina tatizo la kupata choo, naweza pita siku tatu sijapata choo, ila nikinywa pombe napata choo kama kawaida nimecheki hospt wnasema hawaoni tatizo,

Niambie unakula chakula cha aina gani na unakunywa maji ya idadi gani?
 
Daktari nahitaji kujua ni vidonge gani huwa vinatumika katika kupunguza stress na pia kupunguza depression??

Kawaida watu waliokuwa wanadepression wanapewa Citalopram 20mg kila siku kwa muda wa wiki mbili.
Lakini kama mtu anatatizo hili lazima amuone daktari.
 
Sikio limekuwa likiwasha kwa ndani likiambatana na madonda karibu na koo na nikitumia dawa ya sikio (drops) madonda yanaongezeka, nikianza kutumia ile ya madonda sikio linawasha zaidi na nikitumia zote ugonjwa unaweza egemea kwenye sikio au madonda. Naomba msaada wa ushauri na dawa Dr.

Natumai nimejibu swala hili. Kama sijajibu tafdhali niambie.
 
Tatizo la meno kuwa na ukakasi kiasi cha kushindwa perasi, nanasi

Piga mswaki kutwa mara mbili na tumia mouth wash ya Listerine kutwa mara mbili. Pamoja na hilo kunywa kidonge kimoja cha Calcivita kila siku kwa muda wa mwezi mmoja. Asante.
 
Unaposema matundu unamanisha vidonda vidogodogo? na hiyo majimaji ni rangi gani?
matundu ambayo mtu anazaliwa nayo,yapo kwa baadhi ya watu mtu akikasirika hutoa majimaji wengine huita vitundu vya hasira
 

Attachments

  • index.jpg
    index.jpg
    4.6 KB · Views: 129
Habari wakuu,

Nakaribisha maswali yoyote kuhusu magonjwa, dawa, tiba na afya kwa ujumla. Kama una maswali kuhusu ugonjwa wowote, vipi kuishi na magonjwa, kufanya mabadiliko kwenye maisha baada yakupata ugonjwa, matibabu, matumizi ya dawa, matumizi ya dawa pamoja na dawa nyingine au athari zake.

Karibuni sana.

View attachment 361607

Kama umejibiwa maswali na mtu mwingine na haijakufaa ni kosa lako.
Mimi nitajibu maswali zote mwenyewe kama Daktari.







habari dr
last time niliuliza swali sijapata jibu hadi leo......narudia huenda leo sitadharauliwa
nilifanya mapenz na mpenz wangu after one wiki nikawa nasikia maumivu makali wakat wa kukojoa na na ute mweupe unatoka sehem ya kukojole....pia muda mwngine nasikia maumivu hata bila kukojoa je nn hyo na ni dawa gan naweza tumia
AHSANTE
 
Back
Top Bottom