Mtaalamu wa Dawa na Tiba: Ninakaribisha maswali kuhusu Magonjwa, Tiba na Dawa

Mtaalamu wa Dawa na Tiba: Ninakaribisha maswali kuhusu Magonjwa, Tiba na Dawa

Hilo tatizo linaitwa' "Hypnic Jerk". Hakuna haja kuchukuwa dawa yeyote kwaajili ya tatizo hili. Inabidi ubadilishe mambo machache kwenye maisha yako.

1. Ule chakula saa moja au zaidi kabla yakulala.
2. Usitumie simu, kompyuta, tv au chochote electronic nusu saa kabla ya kulala.
3. Unapolala usikuwe na fikra yeyote. Inabidi uwe umerelax na upo kwenye starehe.
4. Ni vizuri sana upate usingizi wa masaa sita au saba kila siku.

Zote hizi zitasaidia kupunguza tatizo hilo. Asante.
Asante sana sana
 
Dr.mimi ninatatizo la chembe ya moyo ni dawa gani naweza kutumia ili kumaliza tatizo
 
Asante kwa huduma hii;
1. Kuna dawa ya kuongeza sperms count?
2. Kuna dawa ya kurejesha sexual health kwa mtu aliyeathirika na musterbation ya muda mrefu?
3. Musterbation inaweza sababisha infertility in male?
Shukrani.
 
Nauliziza cha kufanya ili kuacha sigara kwa mtu aliyevuta kwa zaidi ya miaka mitano, anayevuta wastani wa sigara tano(5) kwa siku.
 
Dr nilikuuliza tatizo la uzazi nahisi kama umenidharau, umesema tukuombe maaada na ndio maana tunakueleza matatizo yanayotusumbua
 
Dokta mm nina tatizo LA chango ambalo linakimbilia sehemu ya tumboni kushuka mpaka kwenye sehemu ya matakoni.na hii hunisababishia kupata maumivu makali mnoo ninapojisaidia.kuna mda natamani kupiga kelele kwa maumivu.na hii hunitokea Mara kwa Mara..nkupomwambia MTU akaniambia itakuwa chango, Naomba MSAADA wako ni kitu gani kinanisumbua na.Dawa yake ni IPI.Nashukuru
 
ninasumbuliwa na pua kuziba sana baada ya muda ina badili kutoka pua moja na kwenda nyingine na mafua ya Mara kwa Mara yananipata nimeenda hospital tofauti nimeambiwa Nina allerg katika Tiba zao sikufanikiwa kupata nafuu je ninaweza kufanyaje nipate nafuu

Duh,mkuu tatizo lako km langu,nna miaka zaidi ya kumi linanisumbua,,kingine mi nikipata harufu Kali ya petrol au moshi was cigarette au either nguo mpya,nakohoa balaa,unaweza sema nakufa muda simrefu,ili nipate nafuu nikihisi nijiwai kupooza kwa kunywa maji ,msaada. Doctor
 
Dr.Habari
1.Nina dada yangu mguu wa kulia unajaa lakini haumi,amefanya checkup ya sukar,pressure,moyo na figo yupo fine,na pia akifika wakati wa hedhi miguu hujaa sana.Dr alimshauri awe anainua miguu wakati wa kukaa.Sasa anatafuta suluhisho la kudumu,naomba msaada kwa ilo.
2.Baba yangu anatatizo la kisukari,pressure na moyo kuwa mkubwa kwa kipindi cha miaka mitatu,mwaka huu tumbo umeanza amekuwa akisumbuliwa na tumbo ambapo kila atakapo kula anaharisha,na amepima typhoid hana.
3.Nini sababu ya mtoto kila akitaka kucheua analia sana.Ni mara chache kucheu bila kulia
Msaada tafadhali.
 
Hello dokta,
Hongera kwa kazi nzuri ya kusaidia jamii,

Dokta mimi nina matatizo ya miguu,inauma sana pindi ninapofanya mazoezi magumu(kwa mda mrefu),sikua na tatizo hili kabla,limeanza miaka 5 iliyopita,i am athletic nilikua nikicheza mpira vizuri tu bila matatizo then baadae haya maumivu yakaanza(chini ya magoti kwenda chini) sielewi ni maumivu ya mifupa,misuli au ni nini!sifurahii kucheza mpira any more,nisaidie inaweza kua tatizo gani na nitatibu hili tatizo namna gani.
 
Nauliziza cha kufanya ili kuacha sigara kwa mtu aliyevuta kwa zaidi ya miaka mitano, anayevuta wastani wa sigara tano(5) kwa siku.

Tatizo la kuacha sigara linakuja kutokana na chemikali ya Nicotini iliyopo ndani ya tumbaku. Inabidi uache sigara kwa kupunguza pole pole na mbadala ya sigara unaweza kula ubani ya nicotini inayopatikana kwenye duka la dawa. Hizi ubani za nicotini husaidia mtu ache sigara pole pole.
 
habari dr
last time niliuliza swali sijapata jibu hadi leo......narudia huenda leo sitadharauliwa
nilifanya mapenz na mpenz wangu after one wiki nikawa nasikia maumivu makali wakat wa kukojoa na na ute mweupe unatoka sehem ya kukojole....pia muda mwngine nasikia maumivu hata bila kukojoa je nn hyo na ni dawa gan naweza tumia
AHSANTE

Yaonekana umepata infection wakati ya mapenzi. Itabidi utumie antibiotic hizi kama nilivyoeleza. Usikose dozi.

1. Ciprofloxacin 500mg kidonge kimoja.
2. Doxycycline 100mg, kidonge kimoja kutwa mara mbili kwa siku saba.
3. Metronidazole 400mg kidonge kimoja kutwa mara tatu kwa siku saba.
 
Back
Top Bottom