Mtandao wa Jumia wafunga biashara yake nchini Tanzania

Mtandao wa Jumia wafunga biashara yake nchini Tanzania

Ulitegemea kupata huduma nzuri kwenye baa ya Arusha?????!! Shukuru Mungu sana kama huyo mhudumu hakukubandika Tusi moja matata sana
Kama Watumishi ni Wabongo wala sitoshangaa kampuni kukwama.

Mimi huwa napenda sana kufuatilia huduma kila niingiapo Ofisi, Mgahawani, Duka au Usafiri...ninachogundua mara nyingi ukiona huduma ni nzuri na ya kujali Mteja basi anayekuhudumia mara nyingi ndiye mmiliki wa hiyo Ofisi/Duka/Mgahawa n.k.

Ni juzi tu nimeingia Bar moja kubwa tu A town, nikaagiza vinywaji Muhudumu akaleta kisha akakimbilia kuketi meza ya pembeni na kuanza kuchezea simu yake ili hali ile meza ilikuwa chafu..nikamuangalia kwa muda nikiwa nimekasirika sana kisha nikamuita, nikagomba kwamba "hivi huna uwezo wa kuona hii meza ni chafu?" basi akaenda kuchukua kitambaa huku amevuta mdomo utasema nimemtukana tusi la nguoni.

Inashangaza sana Mtu hajui hata kama mimi kuja pale ndio kampuni yake wanapata pesa ya kumlipa mshahara wake.

Ndio ile unakuta Mtu anawekeza kwenye usafirishaji, ananunua Mabasi ya gharama kubwa lakini anaishia kuajiri Wapuuzi watupu kutoa huduma...Wabongo tuwajinga sana.
 
Mimi ni miongoni mwa wateja wazuri sana wa Jumia. Nimeshafanya nao biashara mara nyingi sana kwa kununua bidhaa kwao na zimekuwa zikinifikia kwa uhakika na uaminifu mkubwa sana.

Hata pale nilipopata changamoto walinisaidia sana.

Nimesikitika sana kusikia kuwa kwa sasa wamefunga huduma zao kwa Tanzania nimesikitika sana na sijui wamekumbwa na nini.
 
Hapo wabongo wenzetu (customer care, bodaboda wa kusafirisha bidhaa, wapokeaji wa order, IT, wauzaji wa bidhaa) vibarua vimeshaota nyasi. Wanarudi uraiani.

Poleni JUMIA, Poleni WAAJIRIWA.
 
Hapo wabongo wenzetu (customer care, bodaboda wa kusafirisha bidhaa, wapokeaji wa order, IT, wauzaji wa bidhaa) vibarua vimeshaota nyasi. Wanarudi uraiani.

Poleni JUMIA, Poleni WAAJIRIWA.
Yaani aiseee na wamesha ondoa hadi app yao ya jumia tanzania kule playstore nimesikitika sana aisee coz nilikuwa na mpango wa kuorder hivi karibuni
 
Dah, hawa jamaa nilikuwa nataka nianze kutumia huduma zao lakini kuna kitu kilinistua nikasita,nikawa tu mtazamaji wa ofa zao tu
Mimi kwakweli hawajawahi kuniangusha kabisa hakuna nunuzi nililo fanya kwao likanigharimu chochote kila nilicho nunua kilikuwa sawa kabisa ila ilikuwa vifaa electronics vilifika vizuri na nilipo pata shida walinipa msaada sana mimi niliwapenda kwakweli

Nakumbuka washawahi nirudishia pesa baada ya kununua bidhaa halafu ikawa mbovu walirudisha pesa yote
 
Dah! Kuna mataifa Afrika hii ili utoke inabidi utumie nguvu sana, ni mfupa uliomshinda hata fisi, maana mpaka Jumia 'Amazon of Africa' wanashindwa na kufungasha.

====
JOHANNESBURG – Online retailer Jumia Technologies, often called “the Amazon of Africa,” has closed its e-commerce business in Tanzania, it said in a statement on Thursday, less than two weeks after shutting down in Cameroon.

“As part of our ongoing portfolio optimisation effort, Jumia has come to the difficult decision to cease our operations in Tanzania effective on November 27,” the company said in a statement.

Source: Reuters
 
Kampuni nyingi za nje zinazoshindwa kufanya biashara Tanzania na hata kwenye nchi nyingine zinatakiwa kujua zaidi ya uwepo wa soko kuna vitu vingine muhimu wanatakiwa kuvizingatia...... kati ya hivyo Culture ya watu ni kitu kikubwa na muhimu.

Unapowaza uendeshaji wa biashara S.A. uwe sawasawa na Tanzania utaharibu tu, ukweli ni kwamba biashara inaweza kuwa moja na malengo yakafanana,,, ila mfumo wa uendeshaji sio lazima uwe sawasawa na unapolazimisha utatoa huduma isiyoridhisha na kuutaishia kupata hasara
 
Kampuni nyingi za nje zinazoshindwa kufanya biashara Tanzania na hata kwenye nchi nyingine zinatakiwa kujua zaidi ya uwepo wa soko kuna vitu vingine muhimu wanatakiwa kuvizingatia...... kati ya hivyo Culture ya watu ni kitu kikubwa na muhimu.

Unapowaza uendeshaji wa biashara S.A. uwe sawasawa na Tanzania utaharibu tu, ukweli ni kwamba biashara inaweza kuwa moja na malengo yakafanana,,, ila mfumo wa uendeshaji sio lazima uwe sawasawa na unapolazimisha utatoa huduma isiyoridhisha na kuutaishia kupata hasara
Aliyeanzisha kauli ya "Think globally act locally" mimi namuelewa sana alimaanisha nn.

Shukrani kwa maelezo.mazuri mamaD
 
Kampuni nyingi za nje zinazoshindwa kufanya biashara Tanzania na hata kwenye nchi nyingine zinatakiwa kujua zaidi ya uwepo wa soko kuna vitu vingine muhimu wanatakiwa kuvizingatia...... kati ya hivyo Culture ya watu ni kitu kikubwa na muhimu.

Unapowaza uendeshaji wa biashara S.A. uwe sawasawa na Tanzania utaharibu tu, ukweli ni kwamba biashara inaweza kuwa moja na malengo yakafanana,,, ila mfumo wa uendeshaji sio lazima uwe sawasawa na unapolazimisha utatoa huduma isiyoridhisha na kuutaishia kupata hasara

Yaani hapo ulipo unakaa na kufikiria kampuni ije iwekeze mamilioni ya hela Bongo bila kufanya utafiti wowote, kwamba walikuja kichwa kichwa tu na kufungua milango ya maduka yao.

Multi-nationals siku zote hutumia hela nyingi na nguvu nyingi kwenye utafiti, wanashirikisha wazawa na kukagua kila hali, sema baadhi ya haya mataifa ili utoke au ufaulu kibiashara lazima uhangaike sana, haswa kwa Tanzania huwa vigumu sana kufaulu maana wengi hampo kwenye uchumi wa kati, na wachache waliopo ni wabahili kupita maelezo.
Ndio maana biashara za shopping malls huko huwa hazifaulu, utawekeza jengo kubwa lenye maduka lakini ubaki na wahudumu wako kila siku miayo tu, Mtanzania na hela yake hata taxi hataki kutumia, bora abanane kwenye daladala na wamama wanaokwenda kuuza samaki Kivukoni, hajali shombo.

Leo hii hata hayo mabasi ya mwendo kasi yanaendeshwa kwa hasara maana mligoma nauli isizidi mia sita na kuwa elfu, ndio maana mengi yameegeshwa hayatumiki, hakuna operator anayeweza kuendesha huo mradi na akapata faida yoyote.
 
Nani nakwambia mabasi ya mwendo kasi yanaendeshwa kwa hasara, unadhani brt ni KQ
 
Watu wanakuja kichwa kichwa. Nakumati waliangukia pua, Uchumi supermarket nao waliangukia pua.
Wanakuja kichwa kichwa bika kufanya research.

Just imagin, unauza maembe online Tsh 1500 wakati maembe safi mtaa yanauzwa kila kona Tsh 800.

Unataka uuze Unga wa ugali online wakati jirani na home kuna duka la mangi unga na soda za kumwaga.

Kwa upande wa chakula online business haiwezi kuwezekana TZ.

Online business unaweza fanya:
1. Nguo
2. Car spear parts.
3. Nyumba za kupanga
4. Hotel
nk.

Lakini kwenye chakula lazima utaangukia pua.
Take it or leave it.
 
Mkuu, hivyo vyote ulivyoorodhesha mbona nchi nyingi zipo tu na online shopping business bado inanoga!
Tena Jumia Mall hufanya kazi vipi?
 
Venus Star,
Mkuu, hivyo vyote ulivyoorodhesha mbona nchi nyingi zipo tu na online shopping business bado inanoga!

Tena Jumia Mall hufanya kazi vipi?
 
Mkuu, hivyo vyote ulivyoorodhesha mbona nchi nyingi zipo tu na online shopping business bado inanoga!
Tena Jumia Mall hufanya kazi vipi?

Wewe unaweza enda kununua Nyanya Supermarket?
Huo ni utamaduni mzee, Wabongo hawana utamaduni wa kununua Mchicha au vitunguu online Over Mambanda ya Mangi mitaani.
Soma umuelewe huyo uliyemquote.
 
Wewe unaweza enda kununua Nyanya Supermarket?
Huo ni utamaduni mzee, Wabongo hawana utamaduni wa kununua Mchicha au vitunguu online Over Mambanda ya Mangi mitaani.
Soma umuelewe huyo uliyemquote.
There is so much more to get in the Supermarket apart from groceries ambazo naona tu ndio mnaquote. Maduka yote Tz hufungwa kwa kuwa watu hawanunui nyanya na vitunguu?
Vifaa ya electronic, furniture, kitchen n.k je? Utavipata kwa Mabanda ya Mangi?
 
There is so much more to get in the Supermarket apart from groceries ambazo naona tu ndio mnaquote. Maduka yote Tz hufungwa kwa kuwa watu hawanunui nyanya na vitunguu?
Vifaa ya electronic, furniture, kitchen n.k je? Utavipata kwa Mabanda ya Mangi?
Usilazimishe tufanane mzee.
Unatakiwa ufanye research kwanza kabla ya kuanza businesses.

Kuna vifaa vinauzwa kila kona. Unatakiwa ufa utafiti kwanza kabla ya kuingia biashara.
Biashara zinazofaa online:-
1. Nguo
2. Spear parts
3. Hotel and apartment
Biashara ya chakula TZ utaangukia pua.
Huwezi ukauzwa biscuit, soda, juice, unga, sukari, nyama nk onlie. Uta fail tu.
 
Mkuu hata ulichoandika hapa kuhusu MABASI YA MWENDOKASI, SHOPPING MALLS na TAX inaonyesha kuna udhaifu mkubwa kwenye tafiti zako, kwa sababu hakuna ukweli hapo. Na kwa maana hiyo kunaweza kuwa na mapungufu pia kwenye hizo tafiti za makampuni ya nje unayoongelea

Tahadhari - usikosee kutumia majibu ya tafiti zilizofanyika Uganda kufanya maamuzi au utelezaji wa miradi Kenya au Tanzania ukidhadhi itakua sawa sababu ya kuwa zote ni nchi za Afrika mashariki. Kila nchi ina tofauti kubwa sana kihistoria na hilo linajenga jamii yenye tofauti flaniflani.....
 
Back
Top Bottom