Mtangazaji Maulid Kitenge ahamia WASAFI FM akitokea EFM

Mtangazaji Maulid Kitenge ahamia WASAFI FM akitokea EFM

GENTAMYCINE

JF-Expert Member
Joined
Jul 13, 2013
Posts
60,660
Reaction score
121,325
56823BF8-4428-45B5-8FD8-DD68787032B8.jpeg


"Kuanzia Jumatatu ya wiki ijayo nitakuwa nafanya Kipindi cha Sports Arena ambacho kitakuwa hewani kuanzia saa mbili hadi saa tano asubuhi, lakini pia nitakuwa nasoma magazeti kwenye kipindi cha asubuhi saa moja na nusu" Maulid Kitenge, @mshambuliaji Akitangaza kuhamia Wasafi FM

Chanzo Taarifa: Mtandao wa Darmpya

GENTAMYCINE namtakia Kila la Kheri huko japo naona wazi ' Anguko ' la Efm hasa katika Vipindi vyake vya Michezo na najua kuwa Wachambuzi ' mahiri ' wa Michezo nchini kama mwana Simba mwenzangu Oscar Oscar nae atamfuata huko na huenda hata Mwanadada mwana Simba na mwana Liverpool mwenzangu Tunu Hassan Shemkome nae akaungana nae na wengineo.

Ukiachia mbali kuwa Maulid Kitenge huwa ananikera kwa Mahaba yake Kupitiliza kwa Yanga SC yake ila Kiutendaji ni Mtangazaji wa Michezo bora kabisa na mwenye Kipaji cha hali ya Juu na Mvuto wa Kipekee kabisa ambao unamfanya kila awapo awavutie Wasikilizaji wengi.
 
Daaah bye bye EFM.

Na ni ' bai bai ' kweli Mkuu kwani Maulid Kitenge huwa ana ' Nyota ' kali sana ya ' Kimvuto ' na Utangazaji wa ' Kiushawishi ' kuliko Watangazaji wote wa Michezo nchini Tanzania. Kwa tunaoijua vyema hii ' Tasnia ' na tukiwa ' tumetukuka ' nayo pia vile vile tunasema rasmi kuwa Maulid Kitenge ameacha Msiba wa Kiutangazaji Habari za Michezo hapo Efm na sijaona bado mbadala wake japo najua kuwa Mtangazaji mwenzie na mwana Simba mwenzangu Ibrahim Masoud ' Maestro ' ndiyo sasa atakuwa ' Boss ' wa Dawati la Michezo Efm ila hana ' Ushawishi ' na ' Mvuto ' kama aliokuwa nao Maulid Baraka Kitenge na hicho Kipindi chao cha ' Sports Headquarters ' na kile cha ' E Sports ' kitaanza Kukosa Mvuto labda Efm na ' Maestro ' waje na ' Strategy ' mpya. Ngoja nami GENTAMYCINE nianze sasa Kujilazimisha na Kuzoea Kusikiliza Wasafi fm Radio ili hadi Jumatatu ijayo niwe nimeizoea na Maulid Kitenge akianza Kutangaza nitiririke na niserereke nae kama ambavyo ilivyokuwa akiwa na Efm.
 
Bila Shaka wasafi FM wata heshimu Trip za nje ya nchi za kila wiki za Edo na Kitenge.Kule mavingu FM aka Wafu FM hali Ina zidi kuwa mbaya baada ya wasafi kutikisa EFM sasa itakuwa zamu ya Wafu FM.
 
Na edo Kumwembe atakuwa pembeni kwa uchambuzi wa soka, bila shaka huu ni usajili wa gharama zaidi toka kuanzishwa kwa Wasafi FM.

Uko sahihi Mkuu kwani nasikia Kumtoa pale Efm hawa Wasafi fm ' wamekamulika ' vilivyo na kwa Kipaji cha Kipekee kabisa alichonacho Kitenge nina uhakika hicho Kipindi chake huko kitapata Wadhamini wengi na Pesa yao itaanza kurudi taratibu.Kwakuwa Edo Kumwembe nae ni mwana Simba mwenzangu nitakuwa ni mwenye furaha nikisikia ameungana nae hapo.
 
Huyu Kitenge mbona anahamahama sana vituo vya kazi?. Mwisho wa siku atajikuta anarudi Redio one. Ila namtakia mema huko alipohamia. Hajaacha pengo kubwa kwa kuwa Efm kwa sasa inajimudu imeifunika sana Clouds na kiuchambuzi wapo vizuri.
 
Naona wasafi wanazidi kujiimarisha nimeona upande wa wasafi tv washaanza kuweka vipindi nafikiri after 5 year watakuwa juu zaidi.
 
Pesa pesa pesa..ila si mbaya pia
Huyu Kitenge mbona anahamahama sana vituo vya kazi?. Mwisho wa siku atajikuta anarudi Redio one. Ila namtakia mema huko alipohamia. Hajaacha pengo kubwa kwa kuwa Efm kwa sasa inajimudu imeifunika sana Clouds na kiuchambuzi wapo vizuri.
 
Back
Top Bottom