Mtanzania kwafukuta, Absalom Kibanda kupewa likizo ya lazima kupisha uchaguzi Mkuu

Mtanzania kwafukuta, Absalom Kibanda kupewa likizo ya lazima kupisha uchaguzi Mkuu

Nimepata taarifa za ndani kuwa mambo si shwari pale New Habari tangu gazeti la Mtanzania liliporipoti habari yenye kichwa cha habari cha Madudu ya Serikali.

Habari hiyo ilikuwa na ripoti za ufujaji wa pesa za umma na utendaji mbovu wa serikali inayomaliza muda wake, huku Wizara ya Ujenzi ikivurunda zaidi.

Kwa mara ya kwanza habari hiyo ilichapishwa kwenye Mtanzania lakini gazeti likadhibitiwa ili kutosambaa, lakini kwa kuwa Mtanzania huchapishwa katika mitambo ya Mwanza, gazeti hilo lilisambaa kanda ya ziwa.

Kutokana na hilo, wahariri wa Mtanzania wakakubaliana kuirudia habari hiyo siku iliyofuata, lakini taarifa zikafika kwa JK kabla gazeti kuingia mtamboni.

JK akaamua kuwasiliana na RA na kumuuliza hiyo ya gazeti la kesho ndio zawadi ya birthday? Kwani kesho yake ilikuwa ni birthday ya JK.

Kutokana na hilo ikabidi RA avute waya na kuongea na wahariri wake kwa kuwaagiza kuiacha habari hiyo na kupunguza kumuandika vizuri EL na kumpa nafasi JM.

Wahariri walikubali kuitoa habari hiyo, na katika kikao chao wakaamua kutoandika kabisa habari za kampeni za uchaguzi, kwani walipinga kuingiliwa kazi yao.

Baada uamuzi huo gazeti la Mtanzania likaporomoka sana kimauzo, hali iliyofanya kuwe na mvutano juu ya kurejea katika habari za kampeni, mwishowe kuna mhariri mmoja akasimamishwa na kupitishwa agizo toka juu kuwa lazima waandike kampeni na watoe nafasi kubwa kwa JM. Agizo hilo likafanyiwa kazi pamoja na kuwekwa mabango katika gazeti la Dimba.

Kwa bahati mbaya mauzo yakashuka sana ikilinganishwa na wakati ambao picha za EL zilikuwa zinapata nafasi kubwa ukurasa wa mbele, hivyo uongozi wa juu ukaamini jopo la wahariri linahujumu ili kushusha mauzo.

Wakati ukweli ni kwamba habari za kumpamba JM zimekuwa hazifanyi vizuri kimauzo.

Sasa wakati huu nimepata taarifa kuwa Absalom Kibanda, Kulwa Kaledia na Arodia Peter wamesimamishwa.

Ova

PIA, SOMA:

- Absalom Kibanda (Mwenyekiti wa Jukwa la Wahariri) avamiwa na watu wasiojulikana na kujeruhiwa

 
Mtanzania walifafanua vilivyo kuhusu huo ufisadi.
 

Attachments

  • attachment-46.jpeg
    attachment-46.jpeg
    8.6 KB · Views: 3,136
Waende Tanzania Daima waendelee kutulisha nuz bin nuz
 
Tatizo ninaloona linasumbua nchi na litakalosumbua nchi ni mwenyekit wa ccm.
 
'Uhuru wa vyombo vya habari umeongeza wigo wa demokrasia ambapo sasa vyombo vya habari vipo huru kupita wakati wowote' - Jakaya Kikwete

Cc: Kaka PASKO
 
Last edited by a moderator:
Halafu kwa unafiki mkuu huyo huyo kikwete anathubutu kusimama jukwaani na kuwataka eti waandishi wafuate maadili ya uandishi!! Ulofa tu
 
Mtu mzima ukishakuwa mdaku hata akili zinakuruka, haya tumesikia kachukue hivyo viroba vyako upoze koo

ukiona mtu mzima anashabikia ana ccm ujue akizeeka atakua fundi baiskeli,muuza kahawa,mchawi,mpiga ramli au mpiga pembe la msibani.
tulia sindano ikuingie.
 
'Uhuru wa vyombo vya habari umeongeza wigo wa demokrasia ambapo sasa vyombo vya habari vipo huru kupita wakati wowote' - Jakaya Kikwete

Cc: Kaka PASKO

Kama huamini hilo tutajie kipindi gani kulikuwa na Uhuru zaid ya uliopo sasa?
 
Last edited by a moderator:
Na kweli,hakuna mwandishi makini kama kibanda na kubenea,hawa wengine ni waimba taarabu tu.

Hamjui maana ya uandishi wa habari mnashabikia tu. Kubenea huyuhuyu aliyekuwa bize kuandika makala kusemea ufisadi wa Lowassa na kudai ana ushahidi leo anamlamba miguu na anagombea ubunge?
Huyo Kibanda zaidi ya kuwa vuvuzela wa Lowassa ameandika story zipi kubwa? Hebu tuache ushabiki!
 
Hamjui maana ya uandishi wa habari mnashabikia tu. Kubenea huyuhuyu aliyekuwa bize kuandika makala kusemea ufisadi wa Lowassa na kudai ana ushahidi leo anamlamba miguu na anagombea ubunge?
Huyo Kibanda zaidi ya kuwa vuvuzela wa Lowassa ameandika story zipi kubwa? Hebu tuache ushabiki!
kaandike wewe basi mwenye story za mantiki
 
Back
Top Bottom