Mtanzania mwingine apigwa risasi Afrika Kusini

Mtanzania mwingine apigwa risasi Afrika Kusini

Habari zenu wana JF wenzangu.

Nikiwa natoka zangu kwenye shughuli zangu, nikaamua kupitia maskan fulani ya wabongo huko town. Nika stick kwa masela huku tukipiga story mbili tatu na kukumbushana...
Watanzania sijui nini kinaturoga, malezi, elimu au aina ya maisha yetu?
 
Bila shaka ni huyu mwamba ,kafariki juzi Jo'berg, sababu kupigwa risasi.
FB_IMG_16783783186931099.jpg
 
Bora wawapunguze punguze huko huko,maana wakishafeli maisha wanarudi huku na itikadi zao za 26,27 wanatusumbua.
Yan wakija mikuki inakua mingi kwenu🤣🤣🤣
 
Nimezika washkaji wanne tena wawili madogo kwangu wamepigwa shaba yaani kweupe hakuna kesi wala nn tumezika ...Kingine hebu nendeni kule Facebook Kuna group linaitwa sailors then angalieni watu wanavyokufa daily nyie jiungeni then muone watu wanavyokufa .

Tuacheni ushabiki nchi za watu ni hatar sana sio waarabu , wazungu wala waafrica wenzetu
Screenshot_20230309-192819.png
 
Kuna Jamaa yangu anafanya Ubalozi wetu huko, aliniambia hakuna Ubalozi unaopata Changamoto kama Ubalozi Wetu Afrika Kusini.

Watu wengi sana wanauwawa na idadi kubwa sana wanafungwa jela. Wanazamia bila passport na kujiingiza kwenye maswala ya Unyang'anyi na Madawa ya kulevya. Wengi mno wanapigwa risasi.

Jamaa anasema acha wafe. Kwa sababu Kuna 'mentality' ilijengeka kuwa Jozi maisha mteremko. Kutoboa ni fasta. Ikawavutia vijana kujiingiza kiholela. Lakini kwa matukio yanayoendelea, watu watakoma kujiingiza na kufanya mambo haramu.
 
Yeah na tunazidi kuharibu passport yetu, nipo hapa lingusenguse nasoma news24.com, mtanzania na jina limetajwa kakamatwa mpumalanga na gari ya moto...
Maisha wanayoishi ndugu zetu wabongo wengi ni aibu hata kusimulia. Ndo maana nashauri wawe wanajifikiria mara mbili kabla ya kuja au baada ya kuja, kwamba wako hapa kushindana kupiga bao nne hadi tano kwa kina Thuli na Nomtando au kutafuta na kurudi nyumban kujenga na kuwekeza.
 
Kuna Jamaa yangu anafanya Ubalozi wetu huko, aliniambia hakuna Ubalozi unaopata Changamoto kama Ubalozi Wetu Afrika Kusini.

Watu wengi sana wanauwawa na idadi kubwa sana wanafungwa jela...
Inafika kipindi mtu unashindwa hata kujitambulisha kama ni mtanzania kutokana na aina ya maisha wanayoishi watanzania wenzetu hapa Kaburu.
 
Back
Top Bottom