Mtanzania mwingine apigwa risasi Afrika Kusini

Mtanzania mwingine apigwa risasi Afrika Kusini

Tanzania kuna tatizo kubwa la maarifa,hata miradi inayoanzishwa na vijana wengi wa ndani ni ile ya kutaka kutambiana na watu wa mtaani au tuliosoma nao,hatuanzishi vitu kwa ajili ya kuitawala Afrika Mashariki au Kusini mwa Afrika kibiashara au kiubunifu,

Kenya na sasa Rwanda wanafanya vitu si tu kwa ajili ya kutambiana bali kuifanya Afrika kuwajua wao ni watu wanaotumia akili zao vizuri,

Sisi tumebaki kuzungumzia Mpira masaa 24 km wapumbavu,wale wauza uchi wakina Mobeto na Paula ndio tunaona watu wa kuigwa,katika jukwaa la biashara na fursa kaangalieni nyuzi ngapi za maana huwa hazipati wachangiaji lakini ukiweka nyuzi za kisengerema wabongolala wanavyokulupuka kuchangia,

Tubadilikeni wakuu,tuitazame sekta ya madini na kilimo kwa jicho la pili,sekta hizi zinaweza kuwabidilisha vijana wengi wakaishi ndoto zao hapa hapa Bongo bila ya kwenda kuteseka huko ughaibuni km sisi tulivofanya miaka hiyo
 
Watanzania wanaoishi Msumbiji hasa maeneo ya Nampula ni tofauti na wabongo wa Kaburu,hata Malawi na Zambia watu wanajiongeza sana,

Tatizo wengi wanaoingia miaka ya hivi karibuni ni madogo ambao akili na maarifa ya hii dunia bado,pili wanaowapokea na wao akili zimeshakuwa mbovu kutokana mfumo wa maisha wengi wauza madawa au beach boys kwa mitaa ya kule Durban,

Vijana wa sasa wa Tanzania tumelala sana,mitandao imetufanya tumekuwa wapumbavu badala ya kuitumia kuongeza maarifa ya kupata taarifa za kutusaidia maishani,

Kwa sasa maisha bora yanapatikana Africa na hasa Tanzania kwa sababu dunia ya viwanda imehamia China na malighafi zinapatikana kwetu,

Leo nilikuwa na Wanyarwanda wamekuja kuwekeza katika madini ya Kopa,hawa wajamaa wanatushangaa kweli nchi ilivyokuwa na rasilimali juu juu tu lakini watu wanapambana na boda boda au kuja huko Kaburu wakiamini watatoboa,

Tufungue vichwa na tuangalie maisha bora yanapatikanaje,na njia ipi itumike kuboresha maisha yetu kwa sasa na watoto wetu
Mkuu ulichoandika kina ukweli fulani, ndiomaana mimi kuna post hapo juu nimeandika kuwa watanzania tuna laana fulani hivi ambayo wenyewe hatuijui.
Mwezi uliyopita niliona video flani ya mkuu wa polisi mkoa wa Dodoma akiwaasa wazazi wa mkoa huo kuwalea vizuri watoto wao baada ya vijana wengi kujiingiza katika makundi mabovu ya kihalifu. Kamanda huyo alisema kwamba viwanda na mashamba mengi yaliyopo huko yamejaa warundi na wanyarwanda baada ya wazawa kushindwa kufanya kazi katika mashamba na viwanda hivyo.

Kamanda anasema ikitokea baadhi ya wazawa kujitahidi kufanya kazi basi siku akipokea mshahara wake harudi kazini mpaka siku hela zitapoisha 🤣🤣🤣
 
Habari zenu wana JF wenzangu.

Nikiwa natoka zangu kwenye shughuli zangu, nikaamua kupitia maskan fulani ya wabongo huko town. Nika stick kwa masela huku tukipiga story mbili tatu na kukumbushana mambo flan flan ya miaka kadhaa iliyopita (maana ni miaka sasa sifiki town kwa washkaji) ghafla linapita kundi la vijana wanne wakiwa na daftari la michango, na picha ya homeboy wetu flan ambae mimi siimfahamu.

Kwa vile mimi sio mgeni na mambo haya nikawa nimeshaelewa nini kinachoendelea kupitia daftari lile, ila kwa ku confirm ikabidi niulize kuhusu mchango ule kwamba ni wa kifo au ugonjwa. Jamaa wakanijibu kwamba ni kifo cha homeboy wetu alieuwawa kwa kupigwa risasi siku kadhaa zilizopita.

Basi mimi sikutaka maelezo marefu kwa sababu naelewa mazingira ya vifo vyetu, nikaingiza mkono mfukoni na kutoa nilichojaaliwa kuchangia nikawapa jamaa (bila kujali kama kifo kile ni cha kweli au vijana wametengeneza mazingira ya kupiga pesa) maana dunia ishaharibika. Mnaweza kujikuta mnachangishwa mchango wa mtu aliekufa na kuzikwa tayari miaka miwili au mmoja uliyopita, au pengine picha ya mtu ambe alisharudi bongo kitambo ikatumiwa tu na vijana wasela mavi kujipatia hela za kulewea.

Sikitiko langu kubwa ni kwa hawa ndugu zangu au zetu ambao wameshindwa kuelewa uhalisia wa maisha ya nchi hii. Hii nchi ni kaburi na jahanam kwa watu waliozoea maisha ya kipanya road panya road kule bongo, na ni peponi au mahali pazuri kupata mafanikio kwa watu waliozoea maisha ya kutafuta kwa kupitia mikono yao na akili zao.

Nchii hii ina mchanganyiko wa watu kutoka maeneo mbali mbali ya dunia hii, na kila raia wanaishi kulingana na mazingira ya maisha waliyozoea kutoka nchini kwao. Kwa mfano Warundi wengi kazi zao hapa ni salon na gereji. Wakenya ni walimu, manesi, madaktari na wa wafanya biashara wa vinyago, maua nk. Waganda nao wamejitupa kwenye uganga wa kienyeji na wanapiga hela kweli kweli (sababu nchi hii watu wengi wanahitaji mafanikio ya haraka haraka kupitia njia za giza) Wakongo wao ni kazi za ulinzi, salon, wachungaji makanisani nk. Na nchi zote nilizotaja hapo juu huwa zina utamaduni au utaratibu wa kuletana huku kwa lengo la kuendelea na hayo wanayofanya wenzao na wanatusua.

Sasa ndugu zetu wabongo wengi wakija huku wanakuwa hawajui wanakuja kufanya nini. Wengi hawana elimu au ujuzi wa kuandika na kusoma hata kiswahili chetu wenyewe (achilia mbali English, Zulu na Afrikans) ambazo ni lugha muhimu zinazoongelewa hapa. Wabongo wengi hawana ujuzi wa kazi, biashara wala elimu, kwahiyo wakifika nchi hii lazima wafeli na kujiingiza katika mambo ambayo mwisho wa siku uhatarisha maisha yao.

Mtu unaweza kujiuliza inakuaje nchi yenye raia wa mataifa zaidi ya 50, ni wabongo tu ndio wawe wanauwawa, wanafungwa, wanateswa na kupigwa na polisi au makundi mengine ya kihalifu kila siku. Yan haipiti mwezi bila kusikia kuna mbongo kajeruhiwa, au kuuwawa aidha na polisi au mtu au kundi fulani la wahalifu. Ni muda sasa wa wabongo kuwa tunaambiana ukweli ili kupunguza haya matukio kuendelea upande wetu.

Wabongo mababu zetu kupitia serikali yetu (chini ya Nyerere) walipambana kuleta uhuru katika nchi hizi. Na zamani wakati tunafika fika katika nchi hii tulipewa heshima kubwa na raia wa nchi hii wakiwemo viongozi, lakini kwa kutokujitambua kwetu tukashindwa kuitumia fursa hiyo kujiendeleza na matokeo yake wenzetu kutoka Afrika Magharibi haswa Nigeria wakaja kuitumia fursa hiyo na kupata mafanikio makubwa. Maeneo mengi ya maduka ya nje yalikuwa yanamilikiwa na wabongo, ila kwa kuendekeza viuno na kukosa elimu na maarifa sehemu hizo tukaziuza kwa wingi kwa Wanigeria. Matokeo yake sasa wabongo wengi wanahangaika kwa kukosa kazi au sehemu za kufanyia biashara na mwisho wa siku wanafanya yale wasiotakiwa kufanya ili mkono uende kinywani. Namaanisha mbongo anaamua kuuza chochote hata kile ambacho si halali kuuzwa mtaani na kupelekea migogoro kati yao na serikali (polisi).

Wasomali na Waethiopia wanakuja nchi hii wakiwa hawajui lolote, hata kumsalimia mtu asubuhi "Good morning" wanashindwa. Lakini kwa vile wanakuwa wanajua malengo na sababu ya kilichowaleta hapa basi baada ya mwaka au miaka kadhaa wanatusua na kuwa na maisha mazuri kuliko raia wa nchi nyingi za Afrika.

Kwahiyo ndugu zangu wabongo na watanzania kwa ujumla, ni muda wa kujitafakari zaidi pindi tunapokuwa hapa au kabla ya kuja hapa kwamba tumekuja kufanya nini na tutarudi nyumbani na nini. Swala la viuno, tungi na mihadarati mingine haina tija kwa dunia ya leo. Tutaisha nchi hii.

Karibu tuchangie ndugu zangu.
Watanzania walioko South Africa ni watu walio tofauti Sana ki matabaka, Kuna Ma Professor wanafundisha vyuo vikuu...UWC, UCT nk,Kuna watu wameajiriwa katika makampuni makubwa,Ma Engineer,Kuna watu wataalamu WA kuchimba Mafuta kwenye ma Oil rigs baharini,Kuna ma manager WA SuperMarkets,Na Mameneja was Mahotel Na Restaurants halafu Kuna walio wengi Zaidi hawana ujuzi wowote,wakiulizwa Sasa umekuja kufanya nini,majibu....nasubiri Meli,Kazi yoyote hawawezi kufanya,wanaishia kutafuta opportunities Za kufanya uhalifu wowote wakimbie hapo ndipo matatizo yanapoanza.....Sasa haiwezekani watanzania wote walioko South Africa,wakajumuika pamoja eti wakajadili mambo ya maendeleo,Maprofessional niliowataja hapo wanajumuika pamoja Na kujadili mambo Kadha WA kadhaa ya maendeleo, mikutano mingi ikifanyika University of Western Cape, UCT ni ambapo vijana Walala nje,Ma beach boy wanaogopa Hata kufika....
Sasa Ushauri Tu ni kwamba kabla hujasafiri lazima ujue unakuja kufanya nini....
 
Watanzania walioko South Africa ni watu walio tofauti Sana ki matabaka, Kuna Ma Professor wanafundisha vyuo vikuu...UWC, UCT nk,Kuna watu wameajiriwa katika makampuni makubwa,Ma Engineer,Kuna watu wataalamu WA kuchimba Mafuta kwenye ma Oil rigs baharini,Kuna ma manager WA SuperMarkets,Na Mameneja was Mahotel Na Restaurants halafu Kuna walio wengi Zaidi hawana ujuzi wowote,wakiulizwa Sasa umekuja kufanya nini,majibu....nasubiri Meli,Kazi yoyote hawawezi kufanya,wanaishia kutafuta opportunities Za kufanya uhalifu wowote wakimbie hapo ndipo matatizo yanapoanza.....Sasa haiwezekani watanzania wote walioko South Africa,wakajumuika pamoja eti wakajadili mambo ya maendeleo,Maprofessional niliowataja hapo wanajumuika pamoja Na kujadili mambo Kadha WA kadhaa ya maendeleo, mikutano mingi ikifanyika University of Western Cape, UCT ni ambapo vijana Walala nje,Ma beach boy wanaogopa Hata kufika....
Sasa Ushauri Tu ni kwamba kabla hujasafiri lazima ujue unakuja kufanya nini....
Asante mkuu kwa ushauri. Najua ni vigumu kwa watanzania wengi kutuelewa, lakini sio mbaya tukitoa angalizo kama hili ili wale wenye akili waweze kufuata ushauri wetu kabla ya kuchukua maamuzi.
 
Dunia ya leo ambapo kuna VETA NA SIDO, kijana jnatakiwa uchangamkie fani kwanza upewe kijicheti chako, kwanza ujifunze kupaka rangi magari na ujue kweli, ukajifunze kushona nguo kama una nia miaka miwili ushajua kabisa, ujenzi wa majumba na decoration tena kisasa kabisa, ufundi wa magari hapa nenda garage za mtaani piga spana za kutosha veta katafute cheti tu, ukiwa na fani amini utakakoenda lazima utapata sehemu ya kuanzia, hasa unaenda nchi za watu hauna ujuzi wowote unawaza ukauze drugs mimi nakuona ni mwehu tu hata ukiuliwa naandika RIP napita kushoto
 
Small fish kwenye small pond......
Anataka kuonekana mkubwa baharini.

Kama Bongo hii huwezi kumudu maisha yako ( hujui hata ukiamka kesho unaenda wapi kufanya nini).
Usiende Kwenye Nchi za kibepari, utaishia kula shaba tu.
Waoga wa maisha nyinyi wabongo, mmeshazoea, kesho nitaponea kwa shemeji, kesho kutwa kwa mjomba
Mkishakula mmeshiba tumbo ndiii, mnaridhika na ratiba, saa ngapi utafikiria kujikomboa
Hao wacha wafe, ni mabingwa wamejikomboa kwenye ratiba yako, ya kusarandia ndugu na washkaji upone siku iende
 
Mkuu kwa aina hii ya maisha wanayoishi watanzania wenzetu hata waende Marekani hawawezi kutoboa. Kama ulivyosema kwamba wabongo wengi wanapenda maisha ya short cut, ila hawawezi kujishughulisha na kazi za mikono yao. Wengi wamefeli kwa sababu ya kutokujua au kujishughulisha na kazi.

Ndomaana mimi leo sishangai kusikia kuwa wizara ya mambo ya ndani kupitia uhamiaji wameamua kutoa vibali maalum na uraia wa muda kwa wageni watakaotaka kuja kufanyakazi za kilimo na uvuvi kwani wazawa wengi ni wavivu na kazi zinaelekea kuwashinda.

Pia mwezi uliyopita nilimsikia kamanda wa polisi mkoa wa Dodoma akiwaasa watanzania waache uvivu na kufanyakazi, hii ni baada ya kamanda huyo kugundua kwamba maeneo mengi ya viwandani na mashambani wameajiri vijana kutoka Burundi, Rwanda na Congo baada ya wazawa wenyewe kushindwa kufanya kazi hizo.
Ila ukweli wangu broh siwezi kwenda SA kufanya kibarua cha mashambani au kuvua fish......

I rather be a misheni town ila siyo kuuza ngada na vitu vya wizi....kwani nikiuza nguo na viatu siwezi toboa, jibu ni kuwa nitatoboa chap tu.
Tatizo vijana wa bongo wanataka kuwa mabeach boy na usuper star wa kishamba...wakati kwao bongo mama analia njaa.
 
Waoga wa maisha nyinyi wabongo, mmeshazoea, kesho nitaponea kwa shemeji, kesho kutwa kwa mjomba
Mkishakula mmeshiba tumbo ndiii, mnaridhika na ratiba, saa ngapi utafikiria kujikomboa
Hao wacha wafe, ni mabingwa wamejikomboa kwenye ratiba yako, ya kusarandia ndugu na washkaji upone siku iende
Elimu huna....
Ujuzi huna.....
Huna ramani yoyote.
Unadhani hivi vyote vitapatikana ukifika south?
 
Back
Top Bottom