Mtaturu: Gharama za ATCL ndani ya Tanzania ni kubwa kuliko zile za Dubai

Mtaturu: Gharama za ATCL ndani ya Tanzania ni kubwa kuliko zile za Dubai

Hao wabunge wangeomba mchanganuo wa gharama za uendeshaji ili waishauri vizuri Serikali sio tu kupiga porojo bila kujua kuan nini humo ndani ya bei za ndege. Afrika yote ndege ni ghali sana kutokana na gharama kubwa za uendeshaji maana bima ziko juu, hakuna viwanda vya spare na mrundikano wa kodi za serikali.

Wabunge waache unafiki wajiongeze watueleze ni sababu gani ATCL wanakuwa na nauli za juu na pia watupe mlinganisho na Precision maana nauli ziko mtandaoni. ATCL fanyeni biashara acheni siasa za majukwaani. Seriakli ikitaka isiwatoze kodi na tozo nyingine lukuki zilizopo.
ATCL, kama yalivyo mashirika mengine ya Serikali, hakuna watu wenye uwezo wa kuendesha shirika kibiashara.

Sijui kodi, vipuli ni sababu zisizo na msingi. Fastjet walipokuwa wanatoa ticket kwa sh 80,000toka Mwanza to Dar, walikuwa wanatengeneza vipuli nchini?

Hakuja biashara ambayo Serikali ya Tanzania imewahi kufanya kwa ufanisi.
 
Hata wakiwachukua hao CEOs, bado hawataweza kutengeneza faida
Ndege tulizonunua ki sifa sifa , hazifai kwa biashara ya budget airline
Fastjet wakati wanafunga biashara walikuwa wantumie embraer e90 one of the most efficient airline for budget business, sasa unaponunua dreamliner 787 ambazo ni gas guzzles huwezi kuwa na nauli nafuu
Uko sahihi kabisa ndugu yangu. Yaani mimi hapa nilipo muda huu natamani angalau hata kwa muujiza fulani, hivi ningekuwa mmojawapo wa washauri wakuu kabla ndege hizi hazijanunuliwa. Unajua hili tatizo la kuwa tunahujumu mtu binafsi kwa kudhani kuwa tunamhujumu yeye wakati tunawahujumu wa-Tanzania!
 
Emirates ilianza na ndege mbili za mtumba walizonunua kutoka ‘Air India’ mwaka 1985.

Mtawala wa Dubai alikuwa ana idea na business plan ya kuitangaza na kuikuza Dubai kupitia shirika la ndege (jamaa ni business man mzuri sana duniani); the rest is history.

Sisi tunalilia ndege Kwanza kwa sababu Rwanda na Kenya wanazo; kabla ya kuwa na business plan na mkurugenzi mwenyewe alikuwa air traffic controller Ghana. Hana experience ya kufanya kazi kwenye shirika la ndege wala hana background ya business studies.

With that info unapata ideas the chances ya ilo shirika kuendeshwa kwa ufasaha ni ndogo sana; litabaki kuwa kupe siku zote linalotegemea ruzuku.
 

Mbunge Miraji Mataturu alia na bei za ATCL

MTATURU PIC
===
Mbunge wa Singida Mashariki (CCM), Miraji Mtaturu ameitaka Serikali kutafuta suluhisho la bei kubwa ya usafiri katika ndege za Shirika la Ndege Nchini (ATCL) ambapo amezifananisha gharama hizo na gharama za kwenda Dubai.

Mtaturu ameyasema hayo jana Jumanne Februari 15, 2022 wakati akichangia taarifa ya shughuli za Kamati ya Bunge ya Miundombinu kwa kipindi cha Januari 2021 hadi Februari 2022.

Amesema Shirika la ATCL limekuwa likifanya vizuri baada ya Serikali kulinunua ndege lakini limekuwa likikabiliwa na changamoto mbalimbali.

Amesema bei ya tiketi ya ndege kutoka Dar es Salaam kwenda Dodoma inafikia Sh400,000 hadi Sh700,000, gharama ambayo ukiangalia ni kama abiria anakwenda Dubai.

“Tumekuwa na changamoto kubwa kwa maana ya bei za tiketi. Ukiangalia tiketi ya kutoka Dar es Salaam kuja Dodoma ni Sh400,000 hadi Sh700,000 ukiangalia wengine ni kama umeenda Dubai kumbe uko Tanzania hapa kumekuwa na changamoto lakini hakuna majibu,”amesema.

Mtaturu ameiomba Serikali kuangalia changamoto hiyo ya bei ya usafiri wa ndege.

Aidha, kumekuwa na malalamiko makubwa katika masuala ya mabando na kwamba mara nyingi wamewaeleza Mamlaka ya Udhibiti wa Mawasiliano (TCRA) waweze kuwasimamia watoa huduma kuhusu changamoto hiyo lakini haijafanyiwa kazi.

“Leo unaweka bado la wiki moja ikiisha fedha zinaondoka wakati ulilipia mwenyewe. Wananchi wanalalamika, tunaiomba Serikali iwasaidie wananchi waweze kuwa na haki yao ya msingi katika wanapoweka bando,”amesema.

Amesema licha ya kuwasilisha changamoto hiyo TCRA limekuwa ni tatizo isiyokuwa na majibu hata wanapoulizwa watu wahuduma kwa wateja wamekuwa hawana majibu ya moja kwa moja.

Ameiomba Serikali kulifanyia kazi ili kuwapa haki wateja.
Effects of monopoly
 
Siyo yeye anayefanya ni serikali wakati wa Lissu serikali ilikuwa haipeleki maendeleo ili kummaliza kisiasa Lissu
Huyu jamaa ni mzalendo zaidi kuliko Lissu,

Tangu amechukua lile jimbo limepiga hatua kubwa sana kimaendeleo,

Mtaturu Chapa kazi,
 
ATCL, kama yalivyo mashirika mengine ya Serikali, hakuna watu wenye uwezo wa kuendesha shirika kibiashara.

Sijui kodi, vipuli ni sababu zisizo na msingi. Fastjet walipokuwa wanatoa ticket kwa sh 80,000toka Mwanza to Dar, walikuwa wanatengeneza vipuli nchini?

Hakuja biashara ambayo Serikali ya Tanzania imewahi kufanya kwa ufanisi.
Mkuu ebu visit hapa kisha wasaidie wabunge na ATCL kuhusu hiyo nauli unayosema: Cheap flights to Zimbabwe, South Africa and Botswana
 
Huyu jamaa ni mzalendo zaidi kuliko Lissu,

Tangu amechukua lile jimbo limepiga hatua kubwa sana kimaendeleo,

Mtaturu Chapa kazi,
Sasa Lisu anaingia vp hapo? Jamaa ameanza kuwasumbua hata hajafika🤣🤣
 

Mbunge Miraji Mataturu alia na bei za ATCL

MTATURU PIC
===
Mbunge wa Singida Mashariki (CCM), Miraji Mtaturu ameitaka Serikali kutafuta suluhisho la bei kubwa ya usafiri katika ndege za Shirika la Ndege Nchini (ATCL) ambapo amezifananisha gharama hizo na gharama za kwenda Dubai.

Mtaturu ameyasema hayo jana Jumanne Februari 15, 2022 wakati akichangia taarifa ya shughuli za Kamati ya Bunge ya Miundombinu kwa kipindi cha Januari 2021 hadi Februari 2022.

Amesema Shirika la ATCL limekuwa likifanya vizuri baada ya Serikali kulinunua ndege lakini limekuwa likikabiliwa na changamoto mbalimbali.

Amesema bei ya tiketi ya ndege kutoka Dar es Salaam kwenda Dodoma inafikia Sh400,000 hadi Sh700,000, gharama ambayo ukiangalia ni kama abiria anakwenda Dubai.

“Tumekuwa na changamoto kubwa kwa maana ya bei za tiketi. Ukiangalia tiketi ya kutoka Dar es Salaam kuja Dodoma ni Sh400,000 hadi Sh700,000 ukiangalia wengine ni kama umeenda Dubai kumbe uko Tanzania hapa kumekuwa na changamoto lakini hakuna majibu,”amesema.

Mtaturu ameiomba Serikali kuangalia changamoto hiyo ya bei ya usafiri wa ndege.

Aidha, kumekuwa na malalamiko makubwa katika masuala ya mabando na kwamba mara nyingi wamewaeleza Mamlaka ya Udhibiti wa Mawasiliano (TCRA) waweze kuwasimamia watoa huduma kuhusu changamoto hiyo lakini haijafanyiwa kazi.

“Leo unaweka bado la wiki moja ikiisha fedha zinaondoka wakati ulilipia mwenyewe. Wananchi wanalalamika, tunaiomba Serikali iwasaidie wananchi waweze kuwa na haki yao ya msingi katika wanapoweka bando,”amesema.

Amesema licha ya kuwasilisha changamoto hiyo TCRA limekuwa ni tatizo isiyokuwa na majibu hata wanapoulizwa watu wahuduma kwa wateja wamekuwa hawana majibu ya moja kwa moja.

Ameiomba Serikali kulifanyia kazi ili kuwapa haki wateja.
Mbunge Miraji Mataturu singida kuna uwanja wa ndege?
Nimeuliza tu
 

Mbunge Miraji Mataturu alia na bei za ATCL

MTATURU PIC
===
Mbunge wa Singida Mashariki (CCM), Miraji Mtaturu ameitaka Serikali kutafuta suluhisho la bei kubwa ya usafiri katika ndege za Shirika la Ndege Nchini (ATCL) ambapo amezifananisha gharama hizo na gharama za kwenda Dubai.

Mtaturu ameyasema hayo jana Jumanne Februari 15, 2022 wakati akichangia taarifa ya shughuli za Kamati ya Bunge ya Miundombinu kwa kipindi cha Januari 2021 hadi Februari 2022.

Amesema Shirika la ATCL limekuwa likifanya vizuri baada ya Serikali kulinunua ndege lakini limekuwa likikabiliwa na changamoto mbalimbali.

Amesema bei ya tiketi ya ndege kutoka Dar es Salaam kwenda Dodoma inafikia Sh400,000 hadi Sh700,000, gharama ambayo ukiangalia ni kama abiria anakwenda Dubai.

“Tumekuwa na changamoto kubwa kwa maana ya bei za tiketi. Ukiangalia tiketi ya kutoka Dar es Salaam kuja Dodoma ni Sh400,000 hadi Sh700,000 ukiangalia wengine ni kama umeenda Dubai kumbe uko Tanzania hapa kumekuwa na changamoto lakini hakuna majibu,”amesema.

Mtaturu ameiomba Serikali kuangalia changamoto hiyo ya bei ya usafiri wa ndege.

Aidha, kumekuwa na malalamiko makubwa katika masuala ya mabando na kwamba mara nyingi wamewaeleza Mamlaka ya Udhibiti wa Mawasiliano (TCRA) waweze kuwasimamia watoa huduma kuhusu changamoto hiyo lakini haijafanyiwa kazi.

“Leo unaweka bado la wiki moja ikiisha fedha zinaondoka wakati ulilipia mwenyewe. Wananchi wanalalamika, tunaiomba Serikali iwasaidie wananchi waweze kuwa na haki yao ya msingi katika wanapoweka bando,”amesema.

Amesema licha ya kuwasilisha changamoto hiyo TCRA limekuwa ni tatizo isiyokuwa na majibu hata wanapoulizwa watu wahuduma kwa wateja wamekuwa hawana majibu ya moja kwa moja.

Ameiomba Serikali kulifanyia kazi ili kuwapa haki wateja.
Hawa Wabunge wetu ni aibu tu hawajui uchumi wetu tuliamua uendeshweje au hawasomi. Tanzania tuliamua kuwa sehemu kubwa ya uchumi wetu itaendeshwa kwa ushindani kwa maana kuwa watoa huduma wawe wengi na watashindana kutoa huduma kwa wananchi. Kufikia somo hili tulijifunza baada ya Shirika la Ndege wakati wa Ujamaa kuwa na ukiritimba: wakati huo kupata nafasi ya ndege kutoka Mwanza-Dar ulikuwa uhonge. Serikali ikaamua tuwashindanishe watoa usafiri wa ndege chini ya uangalizi wa Mdhibiti. Wameshindana na nafuu tumeiona. Watanzania wengi wameweza kusafiri kwa ndege kwa sababu nauli zilikuwa zinafikika. Serikali imerejesha ukiritimba wa ATCL kwa kupunguza ushindani pia kufifisha nafasi/ uhuru/ uteuzi wa Mdhibiti. Bunge lipo na wachache wanalalamika bila kufanya utafiti wa kina. Ndiyo maana nchi zetu zinaitwa majina mabaya. Maneno mengi yasiyo na tija wala mantiki! Tunapenda kurudi kwenye matope kuliko kujikwamua.
 
Back
Top Bottom