Mtazamo: Kuhusu MCC kusitisha msaada wa MCC 2 na shughuli zake Tanzania

Kuwa kama msomi umeulizwa specific question wewe unatoa jibu la jumla. Tafadhali jibu specific tena kwa details and supportive data.
Taja msaada na masharti yake then conclude kuwa ni wakistaarabu au sio wakistaarabu.
 
PolePole Unapozungumzia kupewa Pesa ili ikusaidie siasa haziusini hapo!. Kila kitu duniani kina Masharti. Na Mashariti yanabadilika kutegemea vipaumbele vya mtoa Masharti. Unapozungumzia Marekani kutoa ela Misri au Israel bila Masharti ivyo ni vipaumbele vyao kwa hao na sisi tuna vya kwetu. Mbona China anatoa Msaada Korea Kasikazini wakati Mataifa mengine hayatoi, au Urusi anazisaidia kinyume cha Sheria ya kimataifa Ossetia ya Kasikazini, Abkhazia pesa nyingi yajitenge zidi ya Georgia? Yote kwa sababu wana vipaumbele kwa hao. Kipaumbele cha Tanzania ni Maendeleo, kiwe kidogo au kikubwa tunakiitaji either kutoka Uchina au USA. Labda uniambie kwa sasa tumefanikiwa tayari, kama Sivyo unachoongea hapa ni Sizitaki mbichi hizi uku tunachechemea. Tumepoteza na tutaumia!!!!.
 
Kumbe fedha za kigeni zinaletwa na MCC tu au ndio pesa yetu ingeongezeka thamani maradufu mkuu
 
Binafsi nimefurahi sana kwa kunyimwa huu msaada.

Ni wakati muafaka wa kufanya yetu bila kutegemea misaada.
Kuipa cuf zanzibar ni kukaribisha ugaidi wa waislam wenye madevu..by Samuel Six....ahahaaa..faizaaaaaaaaaa...
 
Vyandarua, Dawa ya Mseto(maleria),ARV/HIV, Condoms, Utafit, Barabara(namtumbo,Mbinga, Sumbawanga, Iringa etc), symbion Ubungo, Vyuo(Dodoma), Umeme(REA) na Power Africa, Kutupunguzia Madeni, Kutulinda dhidi ya Magaidi(FBI) Yooote hayo na Mengine mengi ni kwa hisani ya watu wa Marekani. Umoja wa Ulaya (EU) nao Umesema anakuja na ya kwao. Mtu bora duniani ni yule anaesoma nyakati, je hizi nyakati ndo za kukataa misaada??. Je ni kweli sisi ni tajiri(Kuwa na Mali nyingi ardhini ndo inamaanisha utajiri au Vinginevyo)(Japan aina malighafi yoyote ya maana ardhin lakini inaitwa tajiri na ukiingalia ni Matajiri).
 
Mi nadhani tujitafakari kama taifa, tusiwe watu wakuwa tunakurupuka tu nakutoa nukuu mbali mbali wakati ukweli ukowazi.

Nchi inalaumiwa kwakukiuka misingi ya Demokrasia, tena wazi wazi kabisa hata mtoto mdogo ambaye hata shule hajaanza hili ukimuuliza stakupatia jibu. Tusijidanganye, tutakaoumia nisisi wenyewe. Walichofanya Ccm kinapaswa kulaaniwa nakila mtanzania anayeitakia mema nchi yake.

Kujipa Moyo huku hakutatufikisha popote nisawa na kuota umejenga ghorofa naumehamia ndani tayari, lakini ujue utakapozinduka usingizini Tembe hilo ndo lililo lako.
 
Watanzania tumekuwa watu wa kulalamika kila wakati hasa panapotokea tatizo libalogusa mstakabali wa taifa letu. Lakini tunasahau kuwa kulalamika tu bila kuchukua uamuzi tatuzi haisaidi hata chembe. Hii nisawa namethali ya wa zee wetu kuwa dua la kuku halimpati mwewe. Ni wakati muafaka kutafakari kwa kina tuliweza vipi kupata mamilioni ya Mcc hapo nyuma na tumeshindwa vipi kupata mamilioni hayo na kitu gani kifanyike.

Siku zote wazee wetu wanatuasa kuwa sikio likikua halizidi kichwa. Tanzania tunaweza kuwa namaendeleo yetu na mipango yetu mizuri lakini haiwezi kutuletea maendeleo bila kushirikiana na nchi zilizoendelea.

Mwanzo wa ngoma ni lele. Akumulikae mchana usiku atakuchoma. Muungwana akivuliwa nguo huchutama.

Je sisi tuchukue uelekeo upi kama nchi na tukishupaa shingo a.k.a kukomaa na maamuzi ya MCC au tuchutame na kufikia muafaka? Unasemaje???
 
Well said mkuu!! [emoji106]
 
Swala la kujitegemea ni swala la heri na zuri sana, na hili lazima kama nchi tulipiganie na tujitahidi ili ndoto yetu itimie.
Kuhusu suala la pesa za MCC, hizi pesa kwa hali hii tuliyonayo nahisi tunazihitaji, kwani zilisaidia sana kujenga miundo mbini ya nishati na barabara, sehemu kubwa ya Tanzania vijijini ilipata umeme, mie nimefika vijijini ndani ndani kule watu wananiambia huu ni umeme wa REA, hivyo ulikuwa na manufaa sana.
Kuhusu masharti yake nahisi sio magumu kivile, hata kabla ya kupewa na kusign huu mkataba nahisi serikali ya Tz iliyapitia masharti yote na ikakubali, moja ya mambo hayo ni pamoja na kudumisha democrasia nchini, ambalo pia ni jambo la heri, kama mkataba ungelikuwa na mambo ya udhalilishaji wa utu wa MTZ au uavunja unachochea kuvunjika kwa muungano wetu au mapigano, machafuko au mambo ya ndoa ya jinsia moja basi nina uhakika tusingekubali mkataba wa aina hiyo, sasa kwa leo hii tukija tukasema eti waende tu misaada yenyewe ina masharti kama hiyo tunakuwa hatueleweki, kwa nini hatukataa mapema? tungewaambia sisi tuna mpango wa kujitegema hivyo misaada kama hii hatuhitaji.Tujifunze ku implement kitu ambacho tuna kisign au tunakisema, wachina wanasema PRACTICE WHAT U SAY. Kama tuliamua twende na democracia basi tukifanye kitu kwa umahili zaidi, democrasia maana yake ni haki, haki inapofuatwa basi hiyo ndo democrasia, nahisi tukibadilika na tukaacha kuwa tunachukulia vitu juujuu na kuangalia chanzo cha tatizo bila kuoneana haya wala kuleta issue za vyama tutafika mbali.
Issue ya maendeleo pasipo misaada ya USA , inawezekana sana, lakini sio kwa kipindi hiki, bado tunahitaji kujipanga, mapato mengi tunayokusanya ndg zangu hayatoshi, hivi leo hii tunauza nini katika soko la dunia? hiyo china yenyewe ambayo ni largest export in the world soko lao kubwa lipo USA, haya mambo yalitokea enzi za china , wakajidanganya kuwa hii nchi bila wawekezaji, donors toka USA na europe tutaweza, lakini walishindwa, hivyo mwaka 1978 raisi wa china DENG XIAOPING akaanzisha issue za economy restructure na akamkaribisha raisi wa USA, NIXON kwenda china , na wakatenga maeneo ya uwekezaji china kutoka nchi za magharibi, at the same time china ilianza kudebate issue za human rights na comparison between ujamaa na ubepari ili kupunguza makali ya USA aweze kuingia china kuwekeza na pia kuendelea kutoa misaada wanapjipanga. Hivyo binafsi naona tuangalie mahali tulipojikwaa rujirekebishe tunapojipanga, hatuwezi kujietegema kwa staili ya kuongea kwenye TV ,radio ,wala magazetini tukiwa hatuna hata kiwanda cha maana Tanzania.
 
*
 
wamekazana kutamba eti hatutishiki wakae na hela zao. nafananisha tukio hili na baba mwenye familia ambae aliambiwa alime shamba lake kama sharti la kupewa mbolea ya msaada badala ya kulima yeye akaendekeza na uroho wa anasa na uvivu akashndwa kulima lile shamba hivyo kupoteza sifa ya kupewa mbolea ya msaada badala ya kujionea aibu kwa uvivu wake anaanza kujitutumua na kujifanya hana haja na hiyo mbolea huku akijua fika kua hakuna namna hayo mazao yatasitawi bila mbolea pia akijua fika hiyo familia inaingia kuishi maisha magumu si kwa sababu ya ubabe wa mtoa mbolea bali uroho uvivu na uzembe wake ndivyo vinaiingiza familia kwenye dhiki. nadhani ni busara sasa huyu baba avae uhusika aone jinsi gani watoto watakavyoteseka na njaa kwani ni ukweli ulio wazi kua hata huyu baba hatapungukiwa chochote nadhani ndio msingi wa jeuri yake
 
Polepole inaelekea unapotea kwa mwendo wa Polepole. Na kazi liyokabidhiwa inakupozeza na kufuta Ujasiri na umahiri uliokuwa nao ktk uchambuzi wa masuala mbalimbali.

Inasikitisha sana Bwana Polepole kujifanya hamnazo kwa kushabikia kubakwa kwa Demokrasia ktk Taifa Jirani la Zanzibar. Hivi wale Wasimamizi wa Uchaguzi wa Wilaya waliowapa vyeti vya ushindi Wawakilishi kutoka CUF walioshinda uchaguzi wa Mwezi Octoba 2015 walikuwa Majuha ?.

Leo wakiamua kwenda kutafuta haki yao Mahakama kwa kunyanganywa Uwakilishi wao na ushahidi mkubwa ukiwa ni vyeti vya ushindi, utakuja na hoja kuwa wanatumiwa na watu wa nje ?.

Hapa hakuna haja ya kupepesa macho, ukweli ni kuwa waliokupa kazi ya kupiga Chapuo ujinga wao "Magamba" ndio wanaotaka kutulaza na njaa ya maendeleo huku wakihubiri kauli tata "HAPA KAZI TU".

Kazi zina mahusiano makubwa na Utawala Bora wenye misingi imara ya Demokrasia.
 
Alafu wanajinasibu eti tuna raslimali za kutosha kama madini,gesi,samaki,mbuga za wanyama,bandari,mlima k/njaro n.k mfano mdogo tu, leo unaweza mueleza mwananchi wa kawaida toka tugundue madini yeye kanufaika vipi?au kama Taifa tunanufaika vipi ,Bandari tunayo tumeona hujuma zilizokuwa zinafanyika kuhujumu mapato ya ndani na yote haya yanafanyika chini ya serikali ya CCM,kuhusu mbuga za wanyama nako si haba tunashuhudia wanyama kila leo wakisafirishwa tena kwa baraka za wakubwa toka serikali ya CCM,sababu ndio wako madarakani na madudu mengi ambayo yameibuliwa hivi karibuni yote hayo yamefanyika chini ya utawala wa CCM,angalia mikataba yote mibovu ya raslimali zetu ni serikali ya CCM ndio imeingia na hao wawekezaji linapokuja suala la utaifa kila mtu ni mtaifa mbona haya madudu yote yaliyotekelezwa na serikali ya CCM utaifa ulikaa kando mkabariki raslimali zetu kutwaliwa kwa mikataba ya ovyo ambayo inamuumiza Mwananchi, kwa mfano huu wa IPTL ni mkataba uliopata baraka za serikali ya CCM,wakati wa mfumo wa chama kimoja tuliamini katika Ujamaa na Kujitegemea na kweli tulijitegemea kwa mambo mengi hatuungi mkono taifa kuwa tegemezi kutokana na raslimali tulizonazo, lakini tujiulize waliotufikisha hapa na kuwa omba omba nini akina nani?
 
Nilidhani unasema tuachane na misaada yote kumbe umejitutumua na MCC tu, kama tutaendelea kupokea misaada mingine tutakwepa vipi masharti??????

CCM mmebaka demokrasia Zanzibar halafu mnataka mkinge mikono kupokea misaada ya watu shame on you ccm!!!!!
 
Unapotaka missada ya kistaarabu nawe fanya ustaarabu kwa wananchi wako. Swali rahisi kwanini wazanzibari wanadhulumiwa chaguo lao kwa mtutu?!
 
Nimekuambia usiseme "watanzania"! Mimi na wengine kama milioni 30 hatuna mawazo kama ya kwako! Semea NAFSI yako na siyo kujumuisha watanzania wengine!
Jaribu kupitia magazeti na vyanzo vya habari uone maoni ya watanzania wenzako kuhusu Jecha na sheria ya makosa ya mitandao
 
Unapotaka missada ya kistaarabu nawe fanya ustaarabu kwa wananchi wako. Swali rahisi kwanini wazanzibari wanadhulumiwa chaguo lao kwa mtutu?!
Haya maneno ya kuweka UWINGI ndiyo yanaleta ukakasi. Nani amekuambia "Wazanzibari wote"? Sema BAADHI yao!
 
Jaribu kupitia magazeti na vyanzo vya habari uone maoni ya watanzania wenzako kuhusu Jecha na sheria ya makosa ya mitandao
Mimi ninachokataa ni kuweka UWINGI kwa kitu kinachofanywa na watu wachache! Kati ya Watanzania milioni 45 ni wangapi wamechangia katika hayo magazeti? Sana sana hawazidi hata laki moja ukijumlisha CUF na UKAWA Bara!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…