Mtazamo: Kuhusu MCC kusitisha msaada wa MCC 2 na shughuli zake Tanzania

Mtazamo: Kuhusu MCC kusitisha msaada wa MCC 2 na shughuli zake Tanzania

Mkuu watu kama PolePole nilisema ni hatari kwa ustawi wa Taifa, wanaishi kwa uongo na ubabaishaji. ......Tumevunja uhusiano kwasababu ya kumweka Shein madarakani.Yaani kundi la Wahafidhiana wasiozidi kumi limeweka nchi ya watu milioni 45 rehani.

Kundi halina uzalendo wakati Jecha anatumbikiza Taifa la watu milioni 4 matatizoni.
Wakati Shein anagomea matokeo kwa kigezo cha demokrasia ya Afrika.

Wanatuaminisha kilichofanyika ZNZ ni demokrasia tuungane nao katika uzalendo wa kihuni. Wanajua watakaposema sisi ni mazezeta tutawaunga wamkono!

Hapana! Wazalendo wa nchi hii tusimame pamoja na kumwambia Magu, ameliweka Taifa rehani kwa interest za Shein na wahafidhina wanaoishi 'peponi kwa sasa''
Masilahi ya watu wasiozidi 10 ni bora kuliko masilahi ya watu milioni 45!!!

Hapana tukatae na kumwambia Magu uzalendo huo ni kundi lake .
Uzalendo wetu ni kwa masikini milioni 40 wa Taifa hili.

Tunasema wazi, hili MCC wapo sahihi, wananchi milioni 45 wapo sahihi.

Waliokosea ni Magufuli akitetea watu wasiozidi 10 kwa gharama ya watu milioni 45

Tuweke siasa kando, tukemee Wazalendo ni milioni 45 wanaoteseka kukosa MCC ni muhimu kuliko watu wasiozidi 10

Hili ni la Magufuli! Hakuna uzalendo isipokuwa wa watu milioni 45!

Milioni 45 ndio wazalendo.

Tusimame na kumwabia Magufuli hapana! hili na wenzake wachache hautukubali
Nguvu3...
Ni kauli ya CCM ,kuulinda "muungano" kwa gharama yoyote iwayo.
Kubaka demokrasia ina gharama zake. Ukipiga mahesabu ya haraka, Magu amepeleka jeshi, askari polisi na vifaa Zanzibar ili kuhakikisha maigizo ya uchaguzi wa marudio yanafanikiwa kwa kiwango kile CCM walijipangia. Shilingi bilioni ngapi zimetumika hapo?
Igizo lenyewe kwa mujibu wa ZEC limegharimu shilingi bilioni 5+, kuchapisha "vikaratasi" huku CCM ikiamini serikali/ nchi haitolewi kwa "vikaratasi"/ kura. Ukichanganya na Trilioni za MCC.

Gharama hazitoishia hapo. Tunaelekea kuisoma namba vile inavyotakiwa isomeke. Hapana kazi tu.
"Maisha bora" waliyotupatia CCM wakati wa mtembeza bakuli ili tusife njaa, yanageuzwa jipu na bora kuishi katika zama za utumbuaji majipu. Huku mtaani maisha yanatishia uhai na kwa kukosa lishe majipu yameanza mwilini na majipu yanatishia uhai. Naiona Tanzania mpya ile inakuja, Tanzania ya viwanda. Viwanda vya majipu.

Kung'ang'ania madaraka ina gharama zake bana.

Tanzania Mpya ya utumbuaji majipu inaua nafasi za kazi hapo kwa miradi ya MCC kusitishwa. Ni wafanyakazi wangapi( walalahoi) watalazimika kuingia katika mbinu mpya za kupunguza ujambazi?

Magufuli ni CCM na CCM imejipa "haki miliki" ya nchi ya "wadanganyika". Hivi kati ya 45 milioni waccm ni wangapi?
Ukiondoa hao wasisiemu kati ya 45 milioni,waliobaki ni majipu. Majipu ni lazima yatumbuliwe na maumivu hayaepukiki.
Hapana kazi tu!

Ukapa unajirudia? Kila zama na mambo yake- Ali Mwinyi( Mzee ruksa)

Link US pulls Tanzanian aid worth $470m over Zanzibar vote - BBC News

Link2. Uchaguzi Zanzibar wazuia mabilioni

Fedha hizo za MCC awamu ya pili ni kwa ajili ya kuiwezesha Tanzania kusambaza umeme na kuwaunganisha wananchi wengi katika Gridi ya Taifa na uimarishaji wa taasisi zinazohusika na na sekta ya nishati.

Mambo ambayo Serikali ya Marekani iliitaka Tanzania kumaliza haraka ni suala mgogoro wa kisiasa wa Zanzibar pamoja na kupata ufafanuzi wa watuhumiwa waliokamatwa kwa makosa ya mtandaoni, wakati wa Uchaguzi Mkuu Oktoba 25, mwaka huu.

Akizungumza na Nipashe, Katibu Mkuu Kiongozi, Balozi Ombeni Sefue, alisema suala hilo haliisumbui serikali na ni tatizo dogo ambalo linatatuliwa.

Alisema serikali ina uhakika wa kumaliza masuala hayo kabla ya kikao hicho cha Bodi ya MCC kukaa ambao masuala hayo yatakuwa yameshatatuliwa na kupatiwa ufumbuzi.

Alisema Bodi ya MCC ilikaa kikao chake cha kwanza Septemba, mwaka huu na inatarajia kukaa tena kikao chake Desemba, mwaka huu.

Alisema serikali ina uhakika Bodi ya MCC ikikaa kikao cha Desemba, mwaka huu itapitisha pasipo na shaka yoyote. link Serikali yazungumzia tishio la Marekani




Kura laki 2 na elfu 99 alizobuni Jecha/ CCM kumpatia Urais Dr. Shein zinagharimu zaidi ya shs. trilioni 1 kwa mwaka. Hili nalo ni jipu.
 
Msikilize mtu anasema hataki msaada wakati hata matangazo ya siku ya choo yanafadhiliwa na watu wa Marekani
Je makusanyo ya Magu yatanunua dawa za ARV wanazopewa waathirika nchi nzima bure kwa msaada wa wahisani,wakati malaria inaua watu wengi kuliko ukimwi na hakuna dawa ya bure
Aah!...yako mengi mengine
 
MTIZAMO WANGU KUHUSU BODI YA MCC KUSITISHA

MSAADA WA MCC 2 KWA SERIKALI YA TANZANIA


C:\Users\toshiba\AppData\Local\Temp\msohtmlclip1\01\clip_image001.gif


Na Alexander Mhando

Utangulizi;

Tukianza na nukuu ya Baba wa Taifa alisema “…….Inapotokea taifa kuuza uhuru wake kwa ajili ya misaada ya kiuchumi au kukubali kukaliwa na majeshi ya nje, taifa hilo linakuwa limepotea na litanyonywa na watu wake watakuwa wanakandimizwa popote pale……” alisema Mwalimu.

Katika swala la msaada wa pesa za Millenium Challenge Corporation’s (MCC) ambazo huwa tunapewa nchi zinazoendelea kama msaada kwa ajili ya Maswala ya maendeleo kwa Nchi zetu, Pesa hizi hutolewa na Bodi ya Shirika la changamoto za Milenium (MCC) ambayo inamilikiwa na serikali ya marekani ili kusaidia nchi zinazoendelea.

Katika kikao cha Bodi ya MCC kilichokaliwa jana tar 28/3/2016 kimefikia uamuzi wa kutishia kusitisha pesa za msaada za MCC kwa Tanzania kwa sababu walizozitoa wao ambazo ni swala la uchaguzi wa Zanzibar na swala la sheria za makosa ya matumizi mabaya ya mitandao ya kijamii katika uchaguzi wa Zanzibar na wa mwaka jana.

Tukikumbuka Katika kikao cha tar 16 December mwaka jana cha Bodi ya MCC, Bodi ya MCC katika kikao chake ilijadili pendekekezo la mkataba mpya na serikali ya Tanzania wenye thamani za Dola za Kimarekani Millioni 472.8 na kuamua pesa hizo zitolewe baada ya Tanzania kutimiza kigezo cha kuzuia Rushwa. Msaada huo ulikuwa ni maalumu kwa ajili ya kuimarisha secta ya umeme nchini, likiwa lengo ni kuwawezesha watanzania wengi zaidi kupata nishati hiyo kwa uhakika na kwa bei nafuu. Lakini pia kuimarisha taasisi zinazohusika na usambazaji wa nishati ya umeme na usimamizi wake.

Katika hali ya kushangaza swala la Rushwa limeshafanyiwa kazi na serikali ya awamu ya Tano kwa kasi kubwa kupambana na Rushwa na Ufisadi lakini bado Bodi ya MCC wanakuja na hoja nyingine nakuaacha ile ya kwanza ya Swala la Rushwa na ufisadi. Sasa swali la kujiuliza je, MCC wanataka tuuze uhuru wetu na utu wetu kwa pesa za msaada??



Mtizamo wangu;

Hatutakiwi tudharau misaada yoyote tunayopewa lakini tusikubali katu kuuza uhuru wetu au mali zetu kwa sababu ya msaada, tukikumbuka mwalimu Nyerere mwaka 1964 alikubali kuvunja uhusiano na Ujerumani Magharibi pale walipotaka kuingilia umoja wetu na Muungano wetu wa Tanganyika na Zanzibar. Lazima tujue kuwa MCC ni sehemu tu ya Bodi inayojitegemea na sio serikali ya Marekani japo inasimamiwa na serikali ya Marekani, kwa hiyo kukosa msaada wa MCC hautatuathiri chochote katika uhusiano wetu na Taifa la Marekani kwani kauli ya MCC sio Kauli ya Serikali ya Marekani. Uhusiano wetu na Taifa la Marekani bado uko palepale na hautatetereka kwa sababu ya pesa za MCC.

Tukikumbuka AZIMIO LA ARUSHA la mwaka 1967 chini ya TANU lilikuwa na maudhui mbalimbali, moja lilikuwa ni swala la Pembe tatu za ukombozi ambapo lilitambua kwamba uhuru wanchi hautakuwa na maana wala hatutakuwa salama kama tukiendelea kuwa tegemezi , yaani kutegemea misaada , mikopo na uwekezaji kutoka nje. Kwa sababu mikopo haitapatikana ya kutosha na hiyo kidogo itakayopatikana itaambatana na masharti yatakayodidimiza nchi zaidi. Isitotoshe hata kama tungepata misaada, mikopo na uwekezaji kwa ajili ya maendeleo vitahatarisha uhuru wetu. Mwalimu Nyerere katika kitabu cha Azimio la Arusha amesema, “Kujitawala ni kujitegemea, kujitawala kwa kweli hakuwezekani ikiwa Taifa moja linategemea misaada na mikopo kutoka Taifa jingine kwa maendeleo yake” mwisho wa kunukuu.

Pia tuambue kuwa Serikali ya Tanzania kwa awamu hii ya Tano chini ya Raisi Dr John Pombe Magufuli, imejipanga kikamilifu katika kukusanya kodi na kutafuta pesa kwa ajili ya kuendesha serikali bila hata kutegemea misaada ya wahisani ambayo ina masharti magumu na yenye ukandamizaji na unyonyaji ndani yake. Katika Pesa hizi za MCC lazima tujiandae kisaikolojia na sio kupotosha kwani Tukipatiwa pesa hizi au Tusipopatiwa pesa hizi bado tunaamini tutaweza endesha serikali yetu na maisha yetu kama kawaida. Tukumbuke kuwa pesa hizi zilianza kutolewa mwaka 2008 , Je, kabla ya hapo serikali ilikuwa inajiendesha vipi? Kama Tuliweza kujiendesha maisha yetu na serikali kwa kipindi hicho , hata sasa tutaweza. Hatudharau pesa za msaada na za wahisani lakini tusitumie kama kigezo cha kuondoa uhuru wetu na utanzania wetu kisa pesa za misaada. Lakini pia tutambue kuwa pesa za MCC sio marekani pekee anayechangia zipo nchi nyingine .

Lakini pia Vyama vyetu vya siasa nchini vijifunze utaifa na uzalendo, Ni aibu kuona chama cha Siasa cha Tanzania kinaungana na maadui wakutoka nje wasioitakia mema nchi yetu kwa kushabikia kila nia yao ovu juu ya maendeleo ya nchi yetu, tutambue kuwa si kila nchi kwa sasa inafurahia mafanikio ya Tanzania mfano uwepo wa Gesi, Madini yakutosha aridhini, wanyama pori wa kila aina, mlima Kilimanjaro,samaki wakutosha ziwani na baharini, ardhi ya kutosha, Bandal, misitu mikubwa, n.k hivi vyote tutambue si kila taifa litafurahia sisi kuwa navyo wanatamani tuvunje amani yetu ili waje wachukue mali zetu.

Rai yangu kwa Vyama vya upinzani nchini jaribuni kuweka utaifa kwanza na siasa baadae, swala la kukaa kushabikia vibaraka weupe wenye lengo la kutukandamiza sio jambo zuri hata kidogo na huo sio uzalendo. Katika Tamko lililotolewa na CHADEMA lenye kichwa cha Ujumbe “Hatma ya msaada wa Fedha za MCC kwa serikali ya Tanzania” ni tamko linaloonesha kushabikia swala la MCC kuikandamiza Tanzania. Tusilete siasa kwenye maswala ya kitaifa na maendeleo ya wananchi. Na hii inaonesha kuwa vyama hivi kama vitapewa dora vitaongoza nchi kwa kutegemea kuombaomba kwa wazungu na mwishowe vinaweza hata kuuza mali za nchi ili kutafuta msaada nje, kwa hili upinzani badilikeni wekeni utaifa mbele na sio tamaa ya uongozi.

Mwisho;

Lazima tujue kuwa msaada mtu anahiyari yake akusaidie au la. Vile vile misaada ni silaha kubwa kwa nchi za magharibi kulidumaza bara la afrika na kuhakikisha haliwezi kujitegemea bali liwategemee wao kwani misaada mingi inayotolewa na nchi hizi hailengi sehemu za maendeleo ya nchi na wananchi wake, na siku zote riba zake huishia kuwa kubwa kuliko misaada yenyewe na kwa kweli nchi yenye kujitambua haiwezi kujiendesha kwa kutegemea misaada hasa kutoka nchi kama marekani utanynyasika tu.


COPIED AND PASTED

Ni mtizamo wako juu ya MCC , binasfi namuunga mkono aliyeandika huu waraka kiukweli sio muda wa kumbembeleza msaada , bora tupambane tujitegemee.
Mkuu hushawahi kaa area Q? Sorry lakin!!!!
 
mlipokuwa mnachezea demokrasia hamkujua kuna MCC? kuna mtu humu namuunga mkono anaposema kwenye hili la mcc hawezi kuvaa uzalendo wa kinafiki. mleta uzi unaandika upuuzi wa karne eti sijui madini, mapori tele, haya yote sio mageni hapa nchini, kilitushinda nini kuendelea mpaka rais wetu aliyepita akawa anasafiri kaila siku kwenda kutuombea kibaba? propaganda kwwnye huu upuuzi wa ccm huku mkijifanya nchi kwanza kumbe pembeni ni ccm kw
 
tufike sehemu tujikubali,,ipo siku watatuonea wivu,,ndipo misaada yao haitakuwa na mashart makali,,mcc safar njema natambua ipo siku mtarud kwa jina lingine namsipe nafas kirahis kama mlivyo ingia.
 
Mkuu ile imani kali ya mwalimu enzi za ukoministi ulioshindwa unaigizwa kimagumashi na miCCM iliyomfuata kwa kuchanganyikiwa (yaani hayana dira wala mwelekeo). Wanajifaragua kwenye vyombo vya habari walivyopora na kuwadhibiti wengine wasitumie vyombo mbadala. Hawaheshimu maamuzi ya wapiga kura iwe bara au visiwani. Hawana dhamira ya kutafuta muafaka uwe wa kisiasa au wa kiutawala.

Hawa wababe tuwaiteje sasa? Wanapanda migongoni mwetu kutuumiza na kutunyima misaada toka nje kwa maslahi yao. Angalau humu JF tunaweza kuweka maoni mbadala. Wamejazana humu kuhoroja kwa maslahi ya watawala wababe na kujiita wana akili ya kuielewa dunia. Hili LA MCC ni racking ya kijeshi tusubiri shambulizi halizi
 
Mimi Niliweke wazi Jambo hili bila kupepesa Macho, japo mimi siungi Mkono Misaada ya wageni. Maana nchi hii ni Tajiri sana.

Tusi jifichie Maovu yetu kuwatukana hawa mabeberu, bali Msema kweli ni Mpenzi wa Mungu. Tanzania na viongozi wa Chama Cha Mapinduzi watende Haki waache Michezo michezo yao ya ujanja ujanja, Taifa lisimame kwenye misingi ya Ukweli na haki "HAKI UINUA TAIFA"

Tuache Michezo, maana siyo mizuri isije ikatugharimu kutuondolea Amani yetu jamani, maana ugumu wa maisha unavyozidi mitaani inapelekea chuki na kuzalisha makundi ya ualifu.

Mwisho. Tujenge nchi yetu kwenye misingi ya taifa linalojitegemea jamani, Hembu tujiulize hao wamarekani na wachina wao wanakopeshwa na waisani gani?

Mbona Kanali muhamar gadaffy aliweza kuiendesha libya bila kutembeza bakuli kwa wazungu na wachina? Sisi katuroga nani?

Hembu turudi kwenye misingi ya haki tuache uroho wa madaraka, kama ccm kimeshindwa kuwaletea watanzania maendeleo kwa miaka 50 basi kwa moya mweupe wawape na wenzao nao waendeleze gurudumu.

Tuige basi mazuri ya wenzetu, democrat na republcan vyama shindani vya marekani, vinabadilishana madaraka kwa demokracy kabisa, umeshindwa kaa pembeni baada ya miaka 4 wananchi wataamua, wenzetu wameondokana na ujima wa kutaka wewetu ndiyo utawale hata kama uwezo wako wa kuleta mabadiliko ya kiuchumi umefikia ukomo.

Wenzetu wanathamini sana Maendeleo, ndiyo maana hata wafuasi wa vyama vyao hawashabikii chama kama vilabu vya soka. Bali upima hoja na uwezo wa chama na mtu husika.
 
Yani polepole anaona kidonda kimetokana na kung'atwa na nyoka aitwaye moma halafu anasema hakkiwezi kufanya mguu ukatwe kwasababu mguu umeungana na tako na kiuno hivyo kidonda cha Kansa ya nyoka kitaondoka kiuache mguu hata kama hakitibiwi. Sijui anajua kule kwao kondoa ule umeme utaongezwa bili?sijui hajui kama yale maji ya 50 yatakuwa 2000 kwa ndoo kule kijijini?sijui anawazaje kuhusu elimu vijijini ambayo serikali ilitegemea miradi hii ili ijiendeshe?Ukiwa na uwezo wa kufikiri kasha ukaamuungaa mkono polepole lazima utakuwa umelaaniwa kwa kumchungulia mzazi wako akiwa anaoga
 
Mtizamo wangu pia nikuwa, Tanzania siyo kisiwa, kiasi cha kujifanya tunaweza kujitegemea. Tuwe wakweli juu ya hili. Tusidhani ni hili tu bali litakwenda kutuharibia hata mahusiano yetu mengine. Mimi ninaamini Tanzania tukiingia wenyewe mkataba huo na sasa tumeshindwa masharti hivyo tunastahiki kufanyiwa hivyo wala yusijifari kwa kunakili maneno ya mwakimu ili kutupa public support. Miradi mingi itasimama na sisi hatuna ujanja wa kuiendeleza. Mimi ninamuomba Mh. Rais Magufuli asidanganyike na washauri wasioitakia mema nchi hii . Ajitajihidi kushughulkia suala hili kwa hekima kwakuwa ninajuaana hekima hiyo. Fedha hizo za MCC tunazihitaji sana kipindi hiki kuliko wakati mwingine wowote ule, ukizingatia chama chetu kimeahidi mambo mengi kuwafanyia wananchi. Mwalimu pamoja na kauli zake lakini aliizita nchi hizi ni giant kama hatutashikana nazo sisi wadogo tuta umia. Hivyo huo ndy wito wangu. Tuache kupotosha ukwelu
 
Hadi standard VII wanajifanya wataalamu wa uchumi, wanabeza misaada ya nje kwamba hatuihitaji...eti tuna uwezo wa kujitegemea.

Endeleeni kijidanganya, maana mnaongea msichokijua.
 
yaani nilivyo ona haraka haraka ndo mchambuzi nimeishia hapohapo....
 
Eti MCC naomba mh rais mstaafu jk atoe mtizamo wake juu ya hli I hope itasaidia
 
ukitaka kuona ujinga wa watanzania soma Uzi kama huu...eti Wao ndio wanajiita wazalendo.....
 
Kama Taifa tutasonga mbele mcc na madudu yake weka pembeni. We are great natiö. Hawatuwezi wala kamwe hawato tuweza. Mungu yupo upande wetu.
 
Umeenda mbali huko kwenye matangazo ya vyoo kutegemea wahisani halafu watu humu wakijidai kuwa tutaweza kwa kutegemea wanyamapori, madini n.k, huu ni Uzuzu kwani hata vita tu ya kupambana na majangili kwa wanyama wetu tunategemea Wahisani, madini waamuzi wa bei ni hao hao wanaoitwa wahisani wakati mwingine watz tuacheni mbwembwe...
 
Back
Top Bottom