Pre GE2025 Mtazamo: Wanamtengenezea mazingira ya kuchukiwa na umma ili 2025, kundi kubwa la CCM lijitenge ili wamuangushe kwenye uchaguzi

Pre GE2025 Mtazamo: Wanamtengenezea mazingira ya kuchukiwa na umma ili 2025, kundi kubwa la CCM lijitenge ili wamuangushe kwenye uchaguzi

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)
Natamani ungemjua vizuri kinara wetu,si hulka zake kabisa mapigo kama haya na simuoga wa malumbano ya fikra.Sina kumbukumbu ya mtawala aliyeridhia watu waandamane kadri wanavyojisikia kwenye nchi yetu,lakini wa sasa aliacha mlango wazi,kuthibitisha haogopi mnyukano wa fikra.Ukimsoma salary slip kadadavua vizuri kabisa.Kawaida ukitaka kumuua mbwa lazima umpe jina baya.
Uongo mtupu.
 
Unawezaje kuteka, kupoteza na kuua watu kwa kiwango hiki tena kwa mfululizo ndani ya muda mfupi kama sio njama?
TLS wametaja List zaidi ya 75, watano ni wakati wa Jpm na 70 ni wakati huu awamu ya Sita.

Wakati huo Huo Mh Mbowe ametanabaisha kuwa waliotekwa na kupoteza ama kuuawa ni zaidi ya 200.

Maswali ya kujiuliza ni juu ya Ujasiri wa kutunga zile sheria za
1. Sheria ya mabadiliko ya Usalama wa Taifa
2. sheria ya Uchaguzi
3. Sheria ya Tume ya Uchaguzi
4. Sheria ya Vyama vya siasa

Na baadhi ya matukio ya kusikitisha kama
1. Bunge kushindwa kutoa msaada na mwongozo kwenye mambo haya.

2. Mahakama kutojali kabisa hisia za Raia.

Haya mambo yanatafakarisha sana
 
Wahafidhina ndani ya CCM na Serikali tangu awali kabisa hawakutaka akalie hicho kigoda, baada ya kushindwa katika kuzuia sasa wamekuja na mkakati mpya wa kumtengenezea ajali ya kisiasa ili litimie lile neno kuwa mgombea wa 2025 ni yeye labda hapa katikati mambo yaharibike sana. Na uzuri ni kuwa hata yeye mwenyewe anafahamu kuwa wabaya wake anao huko huko kwani wakati fulani alisema kuna mstaafu mmoja alimtonya kuwa wabaya wako ni wavaa kijani wenzako,sasa la kujiuliza jee anashindwa kujinasua na hii mitego anayotegewa?
Hizi ni hisia potofu.

Yaani wahafidhina wasideal na Raia au wao kwa wao wahamie kwa wapinzani tu?
 
Nikitazama mwenendo wa mambo, hii ndio picha ninyoipata kutokana na haya matukio hasa kwa jinai yanavyotekelezwa.

Wanafanya ukatili mbaya na wa kutisha halafu wanaacha nafasi ya watu kushuhudia ukatili uliiofanywa kwenye mwili wa muathirika lengo ni kuamsha chuki na hasira na wanajua lawama zote zirakuwa kwake.

Kwa mfano , jiulize, yule mzee walishindwa kumtengeneza ajali, kumpa sumu, n.k?Kulikuwa na ulazima wa kumteka kwa style ile tena huku kelele za watu kutekwa na kupotezwa zikiwa zimepamba moto?

Unawezaje kuteka, kupoteza na kuua watu kwa kiwango hiki tena kwa mfululizo ndani ya muda mfupi kama sio njama?

Unampiga mtu risasi halafu unaenda kumtupa kwenye mbuga ya wanyama lakini katika eneo ambalo ni rahisi watu kumuona. Je, hii sio makusudi?

Unampiga mtu mpaka kumua halafu usoni unamgwagia tindikali eti asitambulike lakini unaacha sehemu zingine za mwili zenye clue inayoweza kufanya watu(ndugu na jamaa) wamtambue marehemu. Ni kukosa umakini kweli? Hii sio hujuma?

We. endelea kuwaaminii hao watu ila kumbuka walitaka hiyo nafasi usipate sema tu yule Mkuu wa Wajeda wa wakati ule ndio alikuokoa. Hata kama umeweka watu wako hizo sehemu nyeti, usidhani ndio uko salama hasa ukizingatia umetoka upande wa pili wa hii nchi na zaid jinsia yako ni tatizo lingine.

Angalia wamekaa kimya, hata mitandaoni hawasemii chochote hawataki kujiharibia. Hao machawa wadogo wadogo hawatakusaidia lolote na matamko yao.

Jiwe alikuwa mkatili na alifanya ukatili mkubwa sana lakini wakubwa hawa walikuwa nae bega kwa bega kumtetea kila mahali kuanzia mitandaoni, kwenye vyombo vya habari, n.k.

Jiulize leo hiii ni wakubwa wangapi wanasimama na wewe kukutetea unaposhambuliwa na kulaumiwa?Hujiulizi ni kwanini?

Hivyo, kwa mtazamo wangu, inawzekana kabisa wanasubiri tu muda ufike waungane kisha wakuhujumu hata kama hawataondoka wote. Unaweza kujikuta huna wabunge wa kutosha na Bunge likatawaliwa na wapinzani wako na huo ndio ukawa mwanzo wa anguko lako kamli hapo baaadae wakishibdwa kukuondoa hiyo 2025.

Nimalizie kwa kusema, akili ya kuambiwa, .........
Duh!
Bandiko lako nimelielewa sana.
Naanza kuhisi ukweli ndani yake.
Lkn je ht JK swahiba wake kashindwa kumbumbulua!?
 
Wanamtia kiwewe ili ajiuzulu mwenyewe au akigoma wazee wachama watatumia haya matukio kama ushahidi na kumlazimisha aachie ngazi kwa usalama wa chama maana... Na wanatumia njia hii ya kumtia kiwewe ili ajiuzulu mwenyewe kwasababu ya kuulinda muungano wanajua wakitumia nguvu za kumtoa Wanzanzibar wataleta mushkeli kwamba ndugu yao anaonewa.
Katuni ya masudi inaujumbe mzito maza keshajua mchezo wao kwa hiyo nae kakaza kama vipi tukose wote.
 
Kwa mfano , jiulize, yule mzee walishindwa kumtengeneza ajali, kumpa sumu, n.k?Kulikuwa na ulazima wa kumteka kwa style ile tena huku kelele za watu kutekwa na kupotezwa zikiwa zimepamba moto?

Unawezaje kuteka, kupoteza na kuua watu kwa kiwango hiki tena kwa mfululizo ndani ya muda mfupi kama sio njama?

Unampiga mtu risasi halafu unaenda kumtupa kwenye mbuga ya wanyama lakini katika eneo ambalo ni rahisi watu kumuona. Je, hii sio makusudi?

Unampiga mtu mpaka kumua halafu usoni unamgwagia tindikali eti asitambulike lakini unaacha sehemu zingine za mwili zenye clue inayoweza kufanya watu(ndugu na jamaa) wamtambue marehemu. Ni kukosa umakini kweli? Hii sio
Mimi ninakushangaa wewe mwenye fikra potofu kiasi hiki.

Unashindwa vipi kujua kwa nini hiyo mifano uliyoonyesha hapo inafanyika hivyo?

Kama kusudio lako ni kumdharau Samia kwa kiwango chake kidogo kabisa cha uelewa na uhafifu wa uongozi; kuna mifano mingi sahihi inayo elezea sifa zake hizo.
Kuja hapa na kudai "anahujumiwa"? Utakuwa umekosa kazi nyingine ya maana ya kuelekezea akili yako huko.
 
Huo ni mtazamo wako ni sawa pia. Ila mimi nawewe hatujui kinachoendelea. Naomba kuuliza swali, Tanzania hii nayoijua kikundi tu cha watu kijitokeze, kuteka mtu na silaha nzito, tena barabarani jua linawaka Je inawezekana? Jaribu kufanya hivyo, utuletee mrejesho.

Upande wangu naona ni namna ya kuogopesha watu, kunyamazisha uhuru wa habari tukielekea Uchaguzi mkuu mwakani. Nina amini, baada ya uchaguzi, haya ya kuteka yatapungua kama si kuisha kabisa.
Kill one, terrify thousand
Kauli mbiu ya government sponsored terrorism nchini Tanzania.

Hata hili lilitokea Kenya linaiogopesha serikali. Hivyo wanaogopesha raia.
 
endeleeni kumtetea na kumtafutia visingizio kwamba hahusiki. akija kuwamaliza wote ndio mtajua alikuwa mtu sio..
 
Natamani ungemjua vizuri kinara wetu,si hulka zake kabisa mapigo kama haya na simuoga wa malumbano ya fikra.Sina kumbukumbu ya mtawala aliyeridhia watu waandamane kadri wanavyojisikia kwenye nchi yetu,lakini wa sasa aliacha mlango wazi,kuthibitisha haogopi mnyukano wa fikra.Ukimsoma salary slip kadadavua vizuri kabisa.Kawaida ukitaka kumuua mbwa lazima umpe jina baya.
Unajichanganya mwenyewe humo humo kwenye andiko lako fupi hili mkuu 'Uthman'!

Hizo sifa unazo zielezea yeye kuwa nazo; halafu wakati huo huo asijue lipi la kufanya na kundi linalo semekana kumhujumu?
Watu mnazo njia za kuchanganya akili za watu mkifikiri watu hao ni wapumbavu!
 
Kill one, terrify thousand
Kauli mbiu ya government sponsored terrorism nchini Tanzania.

Hata hili lilitokea Kenya linaiogopesha serikali. Hivyo wanaogopesha raia.
Hakuna la ziada ya hili ulilo elezea hapa.
Hawa wanao okoteza visababu pembeni wanazo sababu zao wenyewe.
 
Nikitazama mwenendo wa mambo, hii ndio picha ninyoipata kutokana na haya matukio hasa kwa jinai yanavyotekelezwa.

Wanafanya ukatili mbaya na wa kutisha halafu wanaacha nafasi ya watu kushuhudia ukatili uliiofanywa kwenye mwili wa muathirika lengo ni kuamsha chuki na hasira na wanajua lawama zote zirakuwa kwake.

Kwa mfano , jiulize, yule mzee walishindwa kumtengeneza ajali, kumpa sumu, n.k?Kulikuwa na ulazima wa kumteka kwa style ile tena huku kelele za watu kutekwa na kupotezwa zikiwa zimepamba moto?

Unawezaje kuteka, kupoteza na kuua watu kwa kiwango hiki tena kwa mfululizo ndani ya muda mfupi kama sio njama?

Unampiga mtu risasi halafu unaenda kumtupa kwenye mbuga ya wanyama lakini katika eneo ambalo ni rahisi watu kumuona. Je, hii sio makusudi?

Unampiga mtu mpaka kumua halafu usoni unamgwagia tindikali eti asitambulike lakini unaacha sehemu zingine za mwili zenye clue inayoweza kufanya watu(ndugu na jamaa) wamtambue marehemu. Ni kukosa umakini kweli? Hii sio hujuma?

We. endelea kuwaaminii hao watu ila kumbuka walitaka hiyo nafasi usipate sema tu yule Mkuu wa Wajeda wa wakati ule ndio alikuokoa. Hata kama umeweka watu wako hizo sehemu nyeti, usidhani ndio uko salama hasa ukizingatia umetoka upande wa pili wa hii nchi na zaid jinsia yako ni tatizo lingine.

Angalia wamekaa kimya, hata mitandaoni hawasemii chochote hawataki kujiharibia. Hao machawa wadogo wadogo hawatakusaidia lolote na matamko yao.

Jiwe alikuwa mkatili na alifanya ukatili mkubwa sana lakini wakubwa hawa walikuwa nae bega kwa bega kumtetea kila mahali kuanzia mitandaoni, kwenye vyombo vya habari, n.k.

Jiulize leo hiii ni wakubwa wangapi wanasimama na wewe kukutetea unaposhambuliwa na kulaumiwa?Hujiulizi ni kwanini?

Hivyo, kwa mtazamo wangu, inawzekana kabisa wanasubiri tu muda ufike waungane kisha wakuhujumu hata kama hawataondoka wote. Unaweza kujikuta huna wabunge wa kutosha na Bunge likatawaliwa na wapinzani wako na huo ndio ukawa mwanzo wa anguko lako kamli hapo baaadae wakishibdwa kukuondoa hiyo 2025.

Nimalizie kwa kusema, akili ya kuambiwa, .........
Na yeye asivyo na akili ya utambuzi yupo yupo tu.
 
Unajichanganya mwenyewe humo humo kwenye andiko lako fupi hili mkuu 'Uthman'!

Hizo sifa unazo zielezea yeye kuwa nazo; halafu wakati huo huo asijue lipi la kufanya na kundi linalo semekana kumhujumu?
Watu mnazo njia za kuchanganya akili za watu mkifikiri watu hao ni wapumbavu!
KALAMU,
Sipendelei kuzungumzia political game wakati watu wanapoteza maisha.Lakini kuna wenzetu michezo yao inahusisha maisha yetu na wala hawahisi chochote yanapopotea.Analysis yangu inanipelekea kuamini tuko kati kati ya game of chase.Wahusika wa mchezo wanatizama mbali.Moja ya matarajio yao ndio kupata watu wa mtazamo wako wanaohusisha matukio haya na kushindwa kazi kwa kinara.Kama akishindwa kusukuma kete yake vizuri,basi ukisemacho wewe kitabaki kuwa sahihi.Ila kinara wetu nae siku hizi ni mbobezi kwenye hizi gemu.Tuwe na subra tu maana chase yataka hesabu nyingi kabla ya kusukuma kete.
"HOUSE OF CARDS"
 
Kwa mfano , jiulize, yule mzee walishindwa kumtengeneza ajali, kumpa sumu, n.k?Kulikuwa na ulazima wa kumteka kwa style ile tena huku kelele za watu kutekwa na kupotezwa zikiwa zimepamba moto?
Kwa nini isiwe kwa lengo la "kuogopesha raia, kuwatia woga ili yeye na kundi lake waendelee kufanya wanavyo taka bila ya kupingwa?
Toka mwanzo ni huyu huyu kahimiza matumizi ya "lugha ya staha". Hana uvumilivu wa kusikia lugha ngumu ikielekezwa kwake na kwa serikali yake.

Kwa hiyo, nadharia yako inaanza kuharibikia hapa.
We. endelea kuwaaminii hao watu ila kumbuka walitaka hiyo nafasi usipate sema tu yule Mkuu wa Wajeda wa wakati ule ndio alikuokoa. Hata kama umeweka watu wako hizo sehemu nyeti, usidhani ndio uko salama hasa ukizingatia umetoka upande wa pili wa hii nchi na zaid jinsia yako ni tatizo lingine.
Huu nao ni upotezaji lengo wa maksudi kabisa.
Huyu huyu ameteua wakuu wote wa vitengo vinavyo husika na kuhakikisha usalama wa raia upo; au wanaoweza kutumia nafasi hiyo kufanya anavyotaka yeye vyombo hivyo vifanye.
Kiongozi anaye ona usalama wa raia wake unatiwa doa na akakana mbele ya vyombo vya habari kwa kuyaita maswala hayo kuwa ni "DRAMA", kwako bado haikupi sababu ya kujuwa kwamba huyu kiongozi anao utashi wa kuamua kuzuia au kuruhusu yanayo endelea?

Hao watu/kundi hilo linalo mhujumu huko ndani ya CCM litakuwa na watu wa aina gani ambao Mwenyekiti wa Chama kamwe hawezi kulishughulikia? Tutajie hata mmoja tu kati ya watu hao ndani ya hiyo CCM anayo iongoza Samia sasa hivi.

Wajumbe wa Kammati Kuu ya chama, wote wanajulikana. Tueleze wewe, hili kundi linafanya kazi zake za kumhujumu Samia likiwa wapi?
Toa mfano, angalao mmoja tu, hata kama siyo kwa kutaja majina, uonyeshe kuunga hoja mkono wa nadharia yako hii! Mbona huyo huyo Samia mwenyewe kafanya juhudi kubwa za kuwasambaratisha hata hao ambao wangedhaniwa kuwa mahasimu wake; akina Makonda..., nani mwingine? Ally Bashiru? Atafanya nini huyu nje ya CCM inayo ongozwa na Samia mwenyewe!
Akina Lukuvi, Kalamaganda na wengineo, si ndio hao unawaona wanachezewa akili kama watoto wadogo na huyo huyo Samia?

Hakuna kundi lolote linalo fanya hujuma dhidi ya Samia kwa maksudi ya kutaka kumvurugia asiendelee kuwepo kwenye uongozi hapo 2025.
Kilicho wazi katika haya yanayo endelea sasa ni kundi ambalo linapigana juu chini kuhakikisha Samia anabaki madarakani, hata ikilazimu kuondoa roho za waTanzania; na Samia ni mhusika mkuu katika mpango huo.

Acha kueneza fikra potofu kwa maksudi mazima.
 
Kuna mzee moja mashuhuri maeneo ya magomeni mikumi aliwahi kutabiri na katika tabiri zake naona imebaki moja tu na hiyo kama itatokea 2025 basi yasemwayo yapo ……
Hatukuwa nawe na mzee wako katika tabiri zenu,uweke hapa urabiri wenu.
 
Back
Top Bottom