Mtazamo wangu kuhusu siasa za Tanzania na Rais Magufuli

Mtazamo wangu kuhusu siasa za Tanzania na Rais Magufuli

Mleta mada umeandika mengi, ila binafsi hebu nitulie hapo kwa Magufuli na Tundu Lissu.

Umesema binafsi hauna chama, good; umeanza kuzungumzia tukio la Tundu Lissu kwa kulaumu uovu ule aliofanyiwa.

Baadae umesogea zaidi ukazumgumzia uhasama uliopo kati ya Lissu na Magufuli ( kwa mtazamo wako).

Halafu ukaja hapo chini kumlaumu Lissu kwa kuichafua Tanzania, hapa sasa ndio nataka unisome vizuri unijibu;

Tanzania kwa mtazamo wako ni nini?

a) Rais Magufuli

b) Eneo la ardhi linalounda nchi yetu.

Kama jibu lako ni (a) iko hivi;

Rais Magufuli akiwa kama kiongozi wa taifa la Tanzania, tukubaliane kwa nafasi yake alikuwa na uwezo wa angalau kuagiza uchunguzi ufanyike juu ya tukio lile la kushambuliwa Tundu Lissu. Lakini hakuwahi kufanya hivyo, huku sio kuichafua Tanzania, ni kusema ukweli juu ya maovu yanayotokea Tanzania chini ya uongozi wa Rais Magufuli.

Sasa unapomshambulia Tundu Lissu anaichafua Tanzania kwenye hili ningependa kujua umetumia vigezo gani, na ningependa pia kujua wewe kwa upande wako ulitaka Lissu afanyaje kama wale wenye mamlaka ya kufanya kitu waliamua kukaa kimya?

Kama jibu lako ni (b) kwamba Tanzania ni eneo la ardhi, binafsi sijaona popote Lissu akilaumu kitu hicho, bali hulaumu yale yafanywayo ndani ya eneo hilo huku viongozi wake wenye mamlaka ya kuzuia hali hiyo wakiwa kimya, na hapa ndipo Lissu hu-base malalamiko yake.

Mara nyingi Lissu hutumia maneno; "Tanzania chini ya Rais Magufuli" akiwa anamaanisha Tanzania kama nchi, chini ya uongozi wa Rais Magufuli, kwamba huyu kiongozi ndie mwenye mamlaka ya kuhakikisha ulinzi na usalama wa raia wake, bila kujali itikadi, rangi, dini, wala kabila.

Sent using Jamii Forums mobile app
Be blessed
 
Kwa mtazamo wangu sio (a) wala (b), kwangu Tanzania ni watu, eneo la ardhi likiwepo bila sisi kuwepo hapa pasingekuwa Tanzania. Kwa mtazamo wangu ukifanya jambo kuhusu Tanzania umelifanya kwa watu wa Tanzania na si kwa ardhi ya Tanzania kama unavyoona wewe. .

Binafsinaomba mnielewe siwezi kushangilia Tundu Lisu kupigwa risasi hata kama sina undugu nae tuna damu ya UTANZANIA kewa hiyo naelewa kushindwa hata mabeberu huko ulaya. .

Ila hapa inavyoonekana hili jambi linapelekwa kisiasa sana kana kwamba Magufuli anajua aliyempiga risasi Tundu Lisu. Hapo ndio naposhindwa ku argue na yeyote yule alafu mtu kufanyiwa uhalifu anaweza kuwa kafanyiwa na yeyote na tukiweka list ya nadharia ya watu wanaoweza kufanya vile ni wengi mno. .

Ila nchi hii ni mamlaka, na mamlaka katika mapana yake kunamamlaka chini yake. Hii nchi ina polisi na hata huko ughaibuni kuna polisi kama interpols si ndiyo? Unaweza kupeleka kesi yako popote pale kama umeona polisi wa Tanzania hawawezi kukusaidia. Tundu Lisu kagoma kutoa ushirikiano wowote kwa polisi wa Tanzania, Hapo Magufuli anafanyaje? Kwamba aamru polisi wafanye kazi yake? Au watu wanachotaka ni kuwaMagufuli acheze wimbo wa Lisu ili mseme kuwa si mnaona anacheza ule wimbo wake? Hana Imani na raisi alafu leo tushangae kuwa kwa nini Magu anaendelea na yake?

Mie sitaki kubishana kuhusu Lisu ila chukiyake ilikuwa kabla ya kupigwa risasi, kinachotokea hapa ni public sympathy. Nakumbuka siku Lisu anapigwa risasi nilisali sana kwa Yesu amtie nguvu na nimalaani sana kitendo hicho. Lakini haimpi sababu ya kufanya anayoyafanya na kuyaeleza huko ughaibuni huku akilenga kuharibu Tanzania (nikimanisha sisi ndio tunaoumia sio Magufuli) kwa chuki binafsi dhidi ya Magufuli. .
Hivi nikuulize mkuu, mfano Dr. Sengondo Mvungi (Mungu amrehemu huko aliko) Alivamiwa akapigwa na kuporwa vitu vyake kama 💻 na vingine, Je yeye ni marehemu ni ushirikiano upi aliouonyesha hadi watesi wake wakapatikana na sheria ikachukua mkondo wake au marehemu RPC BALO wa Mwanza? We vp?
 
Hujasoma nilichokiandika vizuri naomba ukasome tena

Nimeandika Upinzani kwa juhudi za kukusanya michango au kuwaleta wananchi pamoja wangeweza kuleta maendeleo mengi sana. Mfano wangeweza wakakusanya hela halafu wakanunua madawati, serikali ingekataa tu wananchi wangejua Upinzani unafanya kazi nyingi za kuleta maendeleo huku utawala unapinga huoni ingeleta tija kwa upinzani bila kutumia nguvu nyingi kushidana kwa kelele ambazo hazina msingi


Navyozungumza hivi naomba msininukuu vibaya mie napinga CCM kwa kuwa ni mbovu mno, hata viongozi wengi wanaochaguliwa ndani ya CCM na Magufuli wameonyesha udhaifu wa hali ya juu mbali na usomi wao .Ila vile vile napinga upinzani Pia kwa kunionyesha kuwa bado wanashindwa kuleta mabadiliko, hoja zao hata humu ndani ni matusi na kelele tu. .
Hukumuona yule mbunge viti maalum alipeleka msaada shuleni wakamkatalia kisa mpinzani? We vp?
 
Mimi binafsi sina chama, si kwa sababu nataka iwe ivyo, ni kwa sababu sijaona chama Tanzania chenye misimamo nayotaka mimi.

Rais Magufuli na Bunge:
Kwa mtazamo wangu nadhani si kwamba raisi Magufuli anapinga mhimili wa bunge, hili limedhihirishwa na mkataba alioingia Muheshimiwa Kangi Lugola. Kwa kauli yake kupinga mkataba ule Kwa kuwa haukushirikisha bunge wala serikali yake wala wizara nyingine husika Kama Wizara Ya Fedha. Nafikiri tu kwa raisi magufuli kukubali kupeleka mambo mengi ambayo anafanya sasa bungeni basi hayo mambo yangebaki kwenye ubishani yasingefanyika.

Kupeleka majadiliano bungeni inakuwa Kama mbwa ukimshika mkia hata afanye vipi atafanya unavyotaka wewe. Serikali yetu ingekuwa imeshikiliwa mkia ingebweka tu ila bunge lingekuwa linapoteza mda mwingi kwenye mabishano ya kisiasa yasiyo zaa matunda na mambo mengi yangesimama kama tulivyoona serikali zilizopita. Hapa tuna kubwa la kujifunza, kutokuwa Na uwiano mzuri kati ya serikali Na bunge.

Raisi Magufuli na Misimamo Yake Kisiasa:
Nakumbuka raisi Magufuli alivyoingia madarakani katika mambo aliyoyafanya mwanzo Ni kupinga siasa zisifanyike wakati uchaguzi umepita. Kwa wapinzani waliona Kama wananyimwa kuwa huru kisiasa kiasi cha kumwita Magufuli Ni ditekta. Upande wa pili kwa raisi Magufuli alipinga hili ili kupisha maendeleo yafanywe na wale viongozi waliochaguliwa, akisisitizia, siasa za majukwaa zimepita sasa waliochaguliwa wafanye siasa za ktekeleza yale waliyoyaimba kwenye majukwaa. Lakini kitu ambacho nakiwaza tu Ni kuwa raisi Magufuli aliruhusu waliochaguliwa wawe wapinzani au awe CCM anaruhusiwa kufanya siasa kwenye jimbo lake hususani madiwani Na wabunge.

Mimi binafsi niko wilaya ya Ubungo Na nimepita sana Pwani huko na hata mkoani Kilimanjaro ambapo ni nyumbani, lakini sijaona madiwani au wabunge walioita mikutano kujadili lipi lifanyike kuleta maendeleo (nimeuliza maeneo mengi ila hiki ndicho kinachoendelea). Nani kaenda kufanya mikutano ya hadhara kakataliwa kwenye jimbo lake?

Magufuli na Tundu Lisu:
Kwanza kabisa nasikitika Sana kwa mheshimiwa Tundu Lisu kupigwa risasi mchana kweupe na jambo hili kupelekwa kisiasa. Ila nimeona jambo ndani ya Mheshimiwa Tundu Lisu na chuki yake dhidi ya raisi Magufuli. Binafsi wanasiasa wanachukiana ila chuki zao ni za kisiasa wakiwa kwenye mziki wanacheza pamoja, binafsi sijui chuki hizi zililetwa na nini ila wao binafsi wanaelewa kindaki ndaki sio tunashabikia tu. Ila nasikitika sana kitendo cha mheshimiwa Tundu Lisu kwenda kuichafua Tanzania ili tusipewe misaada kwa chuki yake binafsi dhidi ya raisi, bila kujali anachikiomba anawaathiri vipi wa Tanzania.

Mheshimiwa Tundu Lissu anazunguka sehemu nyingi duniani kutaka wajitenge Na Tanzania wakati familia yake, ndugu zake Na ukoo wake wapo Tanzania. Amezunguka akiomba mabeberu watunyime misaada kitu ambacho hajui kingemuathiri kila mTanzania. Amediriki kukubaliana Na mabeberu tena nimesikitika Sana kusikia mheshimiwa Tundu Lisu akisapoti ushoga kabisa kwa mdomo wake mwenyewe na kuikandia serikali ya Tanzania ka kukataa ushiga ilihali anajua tamaduni hizi kwetu hazipo. Mbali na kuichafua Tanzania hao mabeberu bado wamekuwa mstari wa mbele kuleta misaada na kuikopesha Tanzania.

Mheshimiwa Tundu Lisu amekosa uzalendo kuhusu Tanzania juu ya chuki yake dhidi ya Magufuli. Kama alikuwa na mashtaka binafsi juu ya Magufuli sikatai ila hana ulazima wa kuichafua Tanzania na kuchinganisha na nchi rafiki, hata Magufuli akitoka madarakani uhusiano uliopo kati ya Tanzania na nchi nyingine utabaki, anapotaka kuuvuruga hata aje raisi mwingine lile doa litakuwepo tu ..

Raisi Magufuli hata Kama anayoyafanya analazimisha Kwa wananchi wa Tanzania na yatabaki kwa wananchi wa Tanzania. Hizo ndege si zake Ni za waTanzania, Na juhudi hizi zinaonekana ni za kujenga Tanzanua; huku Tundu Lisu anabomoa kile kinachojengwa kwa wa Tanzania. Tanzania inasonga mbele Kwa shida kwa raha ila inasonga mbele.

Siasa na Taaluma:
Kwa mtazamo wangu tu nchi yetu imeshindwa kutofautisha siasa na taaluma, hapo mwanzo tulikuwa tuko kwenye shimo dogo tu ila kwa sasa tuko kwenye shimo kubwa sana. Raisi Magufuli kwa kuchagua viongozi wenye taaluma zao kwa asilimia kubwa ameua nguvu nzito kwenye taaluma yetu. Kila m Tanzania sasa amekuwa mwanasiasa kitu ambacho kimekuwa sana katika utawala huu wa awamu ya tano. Ukienda chuoni, mashuleni, jeshini na maofisini watu wengi wamekuwa wanaacha taaluma zao na kuingia kwenye siasa. Baadhi ya viongozi au taaluma (mfano maprofesa, madokta, wanajeshi) ambao wamechaguliwa na raisi wetu wangeweza kuwa walimu wazuri wazalishe wanasiasa wazuri ila wameacha kuzalisha wanasiasa na wamekuwa ndio wanasiasa wakubwa. Sasa kumekuwa na taaluma mbovu kwa sababu ya siasa za kupita, ila manufaa ya taaluma si ya kupita.

Magufuli na Wananchi Wake:
Kwa mtazamo wangu kuna wananchi wanakubali Sana kazi na mwenendo wa serikali ya raisi Magufuli. Ila pia kuna wananchi wanachukia sana mwenendo wa serikali hii ya awamu ya tano kwa mitazamo yao mingi tu. La kusikitisha kipindi hiki cha miaka mitano wananchi wamepandikizwa chuki mbaya ambazo Ni kinyume Na utamaduni wetu Kama waTanzania. Chuki hizi zinaonekana mpaka baina ya ndugu Na ndugu huku watu wakiwa wamesahau siasa si chuki. Mfano tu humu ndani ya JF nimesoma nyuzi nyingi humu ndani watu wameshindwa kabisa kubishana kwa hoja majibu yao yanakuwa mfano “nenda kachukue buku saba lumbumba”, huku jukwaa hili la siasa likikosa sifa kabisa kwa kuwa na matusi mengi ambayo nashindwa kuyaandika hapa kwa maadili yangu yalivyo. Nahimiza tu watu wawe CCM, CHADEMA, au chama chochote kile siasa sio ‘Matusi’ “Hoja Hupingwa Kwa Hoja”

Siasa za Upinzani:

Kwa mtazamo wangu tu siasa zimebadilika Sana Kwa wapinzania Kwa sasa zile siasa za kusema tutajenga mashule, hospitali, barabara, tutaleta maji nk Kwa sasa hazisikiki. Nimekuwa najiuliza Sana Kwa nini hazisikiki? Nimegundua kuwa Kwa sasa vitu vingi vimejengwa au kuboreshwa Na serikali hii ya awamu ya Tano. Wapinzani wa raisi Magufuli kwa asilimia kubwa kazi zao zimekuwa ni kuponda tu huku huku hawawi mbele kusema kipi kifanyike. Kwa akili ya kawaida tu huwezi kuwa mmekaa kibarazani aje mwenye nyumba awaulize ‘mmekula nataka kuwaletea chakula’ alafu mmoja wenu ajibu “sie tumeshiba” huku mnakuta wengine wana njaa kali amewasemea bila kuwauliza kama wanahitaji kula. Kwa sasa siasa zimekita kwenye udikteta wa raisi Magufuli na kuponda yale anayofanya huku wakiwa hawasemi nini kifanyike tusonge mbele..

Kwa mtazamo wangu tu Wapinzani kuleta maendeleo si lazima wawe wamechaguliwa: Kwa jinsi nilivyoona wapinzani wakiwa msatri wa mbele kuomba michango ya kuwatoa wenzao gerezani au kuomba hela za hospitali za mheshimiwa Tundu Lisu basi wangeweza kutumia njia hizo hizo kukusanya michango kwa waTanzania ili kuleta maendeleo. Hata Kama hili lingepingwa wapinzani hawa wangeweza kuanzisha utaratibu Kwa viongozi waliowachaguliwa ndani ya upinzani kuleta maendeleo Kwa michango ya wananchi wenyewe ILA zingeonekana Ni juhudi zao ndio zimeleta maendeleo. Wapinzani wanaonekana kuwa wamesahau kabisa kuwa ‘Maendeleo Hayana Chama”

La mwisho ningependa sana kuona siku moja upinzani umeshika madaraka Tanzania ila si kwa upinzani huu naouona sasa. Na ningependa sana kuona CCM inavunjwa Na kuanzishwa chama kipya chenye wanasiasa mahiri wanaoweza kuleta mabadiliko ya kweli Tanzania Kwa wananchi wake. Ningependelea sana kuona siasa zenye tija na maendeleo kwa waTanzania wote bila kujali wametokea vyama gani vya siasa. .
Mpaka hpo tumejua upande wako
 
Unaandika sana, too wordy!!

Unajaribu kuwa neutral ili uuze hoja yako umeshindwa!!

Be brief and to the point!!

Mwenzio mwanaharakati huru alianza hivi hivi sasa hivi hata hajielewi!!

Amekuwa kichekesho cha taifa


Sent from my iPhone using JamiiForums
 
Kwani huduma bora kwa hao watu wa vijijini zinaletwa na ccm au ni kutokana na kodi za wananchi? Siasa za majukwaani hazijawahi kupitwa na wakati maana ndio siasa zenyewe. Labda kama hujui siasa ni nini. Siasa za kwenye vyombo vya habari na mitandaoni ni kutokana na nyakati, hizi ni nyakati digital, taarifa nyingi hupatikana mitandaoni.

Acha upotoshaji, wapinzani hawataki tume huru ya uchaguzi ili kuwapeleka ikulu, wapinzani wanahitaji tume huru ya uchaguzi ili mshindi apatikane kwa uhalali. Huenda unabishana kuhusu uwepo wa tume huru bila kujua hata wanaoidai wanamaanisha nini. Tatizo lililopo sio kuwa hamshindi baadhi ya sehemu kihalali, bali huwa sehemu kubwa ya ushindi wenu ni kupitia udhaifu wa tume mnayolazimisha iendelee kuwepo.

Hongera kwa kukiri kuwa Serikali iliyoko madarakani inatumia vizuri kodi za wananchi kuboresha huduma za kijamii pale upouliza Kwani huduma bora kwa hao watu wa vijijini zinaletwa na ccm au ni kutokana na kodi za wananchi?.

Je, upinzani unajivunia nini, katika miaka 4 ya utawala wa Serikali iliyoko madarakani, cha kuwaambia wananchi, wapiga kura. Au wataendeleza ngonjera zao za madai ya Demokrasia, Tume Huru ya Uchaguzi, Haki bila kuwajibika, na Uhuru usio na mipaka. Naamini hawatawaambia wapiga kura, kwenye majukwaa ya siasa, ukweli kuwa wamekuwa wakitumia Demokrasia, Haki na Uhuru uliopo kufikisha madai hayo ndani na nje ya mipaka ya nchi hii.
 
Hongera kwa kukiri kuwa Serikali iliyoko madarakani inatumia vizuri kodi za wananchi kuboresha huduma za kijamii pale upouliza Kwani huduma bora kwa hao watu wa vijijini zinaletwa na ccm au ni kutokana na kodi za wananchi?.

Je, upinzani unajivunia nini, katika miaka 4 ya utawala wa Serikali iliyoko madarakani, cha kuwaambia wananchi, wapiga kura. Au wataendeleza ngonjera zao za madai ya Demokrasia, Tume Huru ya Uchaguzi, Haki bila kuwajibika, na Uhuru usio na mipaka. Naamini hawatawaambia wapiga kura, kwenye majukwaa ya siasa, ukweli kuwa wamekuwa wakitumia Demokrasia, Haki na Uhuru uliopo kufikisha madai hayo ndani na nje ya mipaka ya nchi hii.

Acha kunilisha maneno, wapi nimesema serikali inatumia vizuri kodi za wananchi? Kuna kutoa huduma za jamii kutokana na kodi za wananchi, lakini kutumia vizuri kodi za wananchi kutoa huduma ni jambo jingine.

Kwani Nyerere alipoenda kudai uhuru huko UNO alikuwa amejenga madaraja mangapi, na barabara ngapi za kuwaonyesha wananchi hadi atake kupewa uhuru? Huna ujualo zaidi ya kupiga siasa mfu hapa jukwaani.
 
Acha kunilisha maneno, wapi nimesema serikali inatumia vizuri kodi za wananchi? Kuna kutoa huduma za jamii kutokana na kodi za wananchi, lakini kutumia vizuri kodi za wananchi kutoa huduma ni jambo jingine.

Kwani Nyerere alipoenda kudai uhuru huko UNO alikuwa amejenga madaraja mangapi, na barabara ngapi za kuwaonyesha wananchi hadi atake kupewa uhuru? Huna ujualo zaidi ya kupiga siasa mfu hapa jukwaani.

Nimekuelewa sasa kuwa viongozi wa upinzani, siyo wanachama wao, wanadai/tafuta uhuru wa kutawala na siyo maendeleo ya watu!
 
Why not!

Kama tutaendelea kuwa na uhuru wetu na haki yetu ya kuwaondoa tukiona hawatufai baada ya kuwaweka hapo, si ni bora kuliko anayetafuta njia za kutuzuia hata tusiweze kumwondoa; bali yeye ndie awe mwamuzi wa kutuondoa sisi tuliomweka kwenye madaraka kwa kutojua tabia zake!
Uongozi wa nchi hauna majaribio. Hata vile, kwa maneno na matendo ya viongozi wa upinzani, ni dhahiri hawajawa tayari kuongoza nchi. Japo wanaongoza katika baadhi ya Halmashauri na Majimbo ya uchaguzi, hawajaonesha utofauti wa mabadiliko, zaidi ya hali kuendelea kuwa mbaya.
 
Umeandika makala ndefu yenye maudhui mbili tu.
Yakwanza kumsifia Bw Yule. Hata kwa maovu ya wazi aliowatendea Wapinzani wake ndani ya chama na nje ya chama chake.
Pili ni kujaribu kumchafua Mh Lissu aliyekwenda nje kupigania uhai wake uliokuwa uondolewe na eti wasiojulikana ingawa hata ww mwenyewe unawajua fika.

Kwasasa Watz sio wale uliokuwa ukiwafikiria enzi zile za zidumu fikra za mwenyekiti. Wana muomko mkubwa na pia wanajitambua. Usihangaike kutumia propaganda zako mfu ktk kujenga hoja kwenye mioyo ya Watz wa sasa. Usuwafanye Watz majuha kwakuwa unaemsujudia kakamata mpini. Wakati wowote huo mpini unaweza kuvunjika au kumponyoka.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kwa mtazamo wangu sio (a) wala (b), kwangu Tanzania ni watu, eneo la ardhi likiwepo bila sisi kuwepo hapa pasingekuwa Tanzania. Kwa mtazamo wangu ukifanya jambo kuhusu Tanzania umelifanya kwa watu wa Tanzania na si kwa ardhi ya Tanzania kama unavyoona wewe. .

Binafsinaomba mnielewe siwezi kushangilia Tundu Lisu kupigwa risasi hata kama sina undugu nae tuna damu ya UTANZANIA kewa hiyo naelewa kushindwa hata mabeberu huko ulaya. .

Ila hapa inavyoonekana hili jambi linapelekwa kisiasa sana kana kwamba Magufuli anajua aliyempiga risasi Tundu Lisu. Hapo ndio naposhindwa ku argue na yeyote yule alafu mtu kufanyiwa uhalifu anaweza kuwa kafanyiwa na yeyote na tukiweka list ya nadharia ya watu wanaoweza kufanya vile ni wengi mno. .

Ila nchi hii ni mamlaka, na mamlaka katika mapana yake kunamamlaka chini yake. Hii nchi ina polisi na hata huko ughaibuni kuna polisi kama interpols si ndiyo? Unaweza kupeleka kesi yako popote pale kama umeona polisi wa Tanzania hawawezi kukusaidia. Tundu Lisu kagoma kutoa ushirikiano wowote kwa polisi wa Tanzania, Hapo Magufuli anafanyaje? Kwamba aamru polisi wafanye kazi yake? Au watu wanachotaka ni kuwaMagufuli acheze wimbo wa Lisu ili mseme kuwa si mnaona anacheza ule wimbo wake? Hana Imani na raisi alafu leo tushangae kuwa kwa nini Magu anaendelea na yake?

Mie sitaki kubishana kuhusu Lisu ila chukiyake ilikuwa kabla ya kupigwa risasi, kinachotokea hapa ni public sympathy. Nakumbuka siku Lisu anapigwa risasi nilisali sana kwa Yesu amtie nguvu na nimalaani sana kitendo hicho. Lakini haimpi sababu ya kufanya anayoyafanya na kuyaeleza huko ughaibuni huku akilenga kuharibu Tanzania (nikimanisha sisi ndio tunaoumia sio Magufuli) kwa chuki binafsi dhidi ya Magufuli. .
Unasema Rais Magufuli hawajui waliompiga Mh Lissu risasi. Unasema ni Mh Lissu ndiye aliyekataa kutoa ushirikiano kwa Polisi. Je Lissu alipokuwa Hosp Nairobi nchini Kenye kuna Polisi waliokwenda kumuona kwa lengo la kumhoji?? Je nini kiliwapata Wabunge wenzake toka chama tawala??
Nani alizuia fedha za matibabu kwa Mh Lissu??

Unaetaka kumsafisha hasafishiki kwa propaganda zako hizi. Usikimbilie kupindisha ukweli juu ya shambulio lile kwani hata unaejaribu kumsafisha alishakiri mwenyewe kuwa Watz sio Wajinga.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
Kitendo cha Chadema kumkubali kwa mikono miwili Lowassa waliokuwa wakimsema kuwa ni fisadi kwa miaka mingi lilinichekesha mpaka leo.
Aisee siasa za Tanzania ni za kuchekesha sana.
Halafu Lowassa aliporudi CCM wakaanza tena kumshushia mvua ya matusi. [emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
Nahisi Magufuli akihamia UPINZANI watamshangilia BALAA na WATAMSAFISHA KWELIKWELI [emoji23][emoji23][emoji23]
Hivi wakati Lowasa alipotimkia Chadema ninyi mlikaa kimya? Je unayakumbuka maneno ya Polepole?? Lowasa hivi sasa yuko huko kwenu kama kweli ni fisadi mtimueni.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Nimekuelewa sasa kuwa viongozi wa upinzani, siyo wanachama wao, wanadai/tafuta uhuru wa kutawala na siyo maendeleo ya watu!

Unaongea utoto gani mwengeso, ni nani atatawala bila kuleta maendeleo yoyote? Hata wakoloni walitutawala lakini kuna maendeleo walileta.
 
Uongozi wa nchi hauna majaribio. Hata vile, kwa maneno na matendo ya viongozi wa upinzani, ni dhahiri hawajawa tayari kuongoza nchi. Japo wanaongoza katika baadhi ya Halmashauri na Majimbo ya uchaguzi, hawajaonesha utofauti wa mabadiliko, zaidi ya hali kuendelea kuwa mbaya.
Kwa hiyo nchi nzima tufuate tu hisia za watu kama hizi zako?

Tulipopata uhuru Tanganyika tulikuwa nao viongozi wenye uzoefu wa kuendesha serikali; mbali hata ya kutokuwa na watumishi wenye sifa za kufanya kazi maofisini?
 
Nimepitia hoja za wachangiaji pamoja na majibu ya mleta mada katika hoja hizo,nimegundua yafuatayo!
1.Michango yote ambayo mleta mada ameweka alama ya "like" ni zile zinazoshambulia upinzani au kumtetea JPM!
2.Kuna hoja moja ambayo mleta mada ameiweka ambayo ni Tundu Lissu kuichafua Tanzania!Lakini hajaeleza ni kwa vipi Tundu Lissu anaichafua nchi,lakini pia sioni uhusiano waowote kati ya hoja ya ushoga aliyoishikia bango na kuchafua nchi!Hakuna alipoonesha Tundu Lissu anachafua nchi zaidi ya kurejea ushoga!
3.Mleta mada anajaribu kujificha kwenye kivuli cha kutokuwa na Chama ili kujenga hoja zake,lakini ukisoma hoja zake anashindwa kuficha mahaba yake kwa serikali ya JPM!Anasifu hatua ya JPM katika sakata la akina Lugola kuwa linaonesha JPM anavyoheshimu mamlaka ya bunge kwenye maamuzi!Lakini anasahau mambo ambayo JPM anafanya bila kulishirikisha Bunge!JPM amelaumiwa sana kwa kutumia fedha kinyume na bajeti,ndio kisa hata cha 1.5 trilion CAG alizosema hajui ziliko maana CAG hukagua miradi kulingana na bajeti ilivyopitishwa na bunge,sasa kama kuna miradi nje ya bajeti hiyo CAG hana mkono wa kuikagua!Hapa ndiko kulizaa bunge kuitwa dhaifu baada ya kuonekana halina meno!
Sasa kisa tu cha kesi ya kina Lugola,mleta mada kajitia boriti kwenye macho yake!Hii inadhihirisha mahaba ya wazi kwa JPM!
4.Mleta mada kashindwa kueleza nini chanzo cha chuki!Katika zama kama hizi ambacho watawala wanaona upinzani ni kama Corona na unapaswa kutokomezwa,kweli anashindwa kujua chanzo cha chuki!Manyanyaso wanayopitia wapinzani,mleta mada kashindwa kuona ndio chanzo cha chuki iliyopo!

Nawasilisha!
 
Unaongea utoto gani mwengeso, ni nani atatawala bila kuleta maendeleo yoyote? Hata wakoloni walitutawala lakini kuna maendeleo walileta.
Yaani nawashangaa wapinzani kwa tafsiri yao ya maendeleo kuwa ni wao kuwa madarakani! Du!

Kama viongozi wa upinzani wameshindwa kuonesha umma wa wapiga kura matumizi mazuri ya ruzuku, demokrasia ndani ya vyama vyao, na udhibiti wa lugha wanayotumia kufikisha ujumbe wao, hakika bado ni wanasiasa uchwara.
 
Yaani nawashangaa wapinzani kwa tafsiri yao ya maendeleo kuwa ni wao kuwa madarakani! Du!

Kama viongozi wa upinzani wameshindwa kuonesha umma wa wapiga kura matumizi mazuri ya ruzuku, demokrasia ndani ya vyama vyao, na udhibiti wa lugha wanayotumia kufikisha ujumbe wao, hakika bado ni wanasiasa uchwara.
Wakuamua nani apewe ridhaa ni wananchi wapiga kura,so wakati wa uchaguzi wataenda kuuza sera zao ni nini watafanya na wakiaminiwa wanachaguliwa!Huo mtazamo ni wako wewe kada wa lumumba!
 
Kwahyo unataka kusema kwmb Tanzania inahitaji Rais mwenye siasa nyingi kuliko kutenda, ckia nikwambie mnyonge tumnyonge ila haki yake tumpe, mm cjampigia kura Rais Magufuli lkn pia hata maisha yng co mazuri kivile but haitoshi kuwa mbinafsi kwa kutoona juhudi anazofanya Magu, japo ni kweli ana mapungufu yake lkn kwa hali tuliyokuwa nayo ilitupasa kuwa na rais huyu, umeongelea kuhusu siasa kubanwa, cjui uhuru wa habari, je watu wanakula uhuru wa habari?, watu wanatembea juu ya uhuru wa habari? Watu wanakunywa uhuru wa habari? Nikukumbushe tu kwmb tangu tupate uhuru nchi hii hatujawahi kujenga reli zaidi ya kuhangaika na reli ya mkoloni, je hilo hulioni unaona uhuru wa habari, ni kweli uhuru wa habari kwa ss umebanwa, je unaonaje uhuru wa habari kubanwa kwa miaka 10 lkn kupata reli kwa vizazi na vizazi au kukosa reli, miundombinu bora, maji safi na salama, vituo vya afya lkn kuwa huo uhuru wa habari ambao kila cku tulijiongopea kuwa nao ilihali watu wana EPA nchi, wana ESCROW nchi kila cku.

Watanzania tuache unafki na ubinafsi, tusimame pamoja kujenga nchi, siasa hazijawahi kutupeleka popote zaidi ya kutuumiza tu.

Sent using Jamii Forums mobile app
CCm ndio chama cha magufuli na ndio sababu ya uharo wote huu Tanzania na kwa taarifa yako ccm imejengwa kwa misingi ya rushwa wizi na uuwaji hii ndio CCM sasa kama wataka kumsifu msifu tu na pia CCM ujuwe huu ni mwaka wa 60 kutawala Tanzania
 
Back
Top Bottom