Mtazamo wangu: Yanga ndiye bingwa wa CAFCC 2023

Mtazamo wangu: Yanga ndiye bingwa wa CAFCC 2023

Chariton003

JF-Expert Member
Joined
Jul 18, 2022
Posts
333
Reaction score
905
Naanza kwa kuipongeza timu ya Yanga kwa hatua kubwa waliyoifikia kimpira!

IMG_7440.jpeg


Japo hawakushinda kwa mujibu wa sheria na taratibu zilizowekwa na CAF binafsi naamini Yanga ndiye bingwa wa michuano ya CAFCC 2023. Wamecheza soka safi na la kisomi, hongera kwako Nabi na timu yako ya benchi la ufundi, uongozi wa Yanga na mashabiki wote wa Yanga!

Binafsi naamini kushindwa kwa Yanga kuleta kombe nyumbani ni kutokana na stile ya ushabiki wa mpira hapa nchini almaarufu Kama utani wa jadi unaofanywa na Simba na Yanga! Nafikiri umefikia pabaya na kama serikali haitaingilia kati sioni tukifanikiwa kimichezo! Aina hii ya ushabiki imehusisha mpaka wivu wa "kike", uchawi na inaua uzalendo wetu! Hapana lazima viongozi ngazi ya taifa waingilie kati!

Kama si Simba kuisaidia USM kwa namna ilivyoisaidia (sina ushahidi, ni mawazo yangu) hakuna namna yoyote USM angesinda mechi ya fainali ya kwanza iliyochezwa Dar achilia mbali kuchukua kombe hili!

Nilipokuwa natazama mechi ya mchezo wa fainali ya kwanza iliyochezwa Dar es Salaam, mashabiki wa Simba walifurahi kuliko hata USM wenyewe Yanga walipofungwa goli la kwanza! Lakini Kama haitoshi, mashabiki hao hao wa Simba waliumia kiasi cha kutokwa machozi pale Yanga ilipofunga goli na huwezi amini walifurahi furaha kuu ajabu pale USM walipofunga goli la pili! Haipaswi kuwa hivi! Chonde sana serikali, ingilieni kati suala hili!

Natamani sana kuona michezo ikileta na kukuza umoja, uzalendo, amani, upendo, furaha nk.

Tusipoangalia, tutashindwa kuishangilia timu yetu ya taifa vizuri kwa kuwa tu mfungaji ni wa Simba au Yanga!

Ni jambo la kushangaza watu wa Kenya, Rwanda na mataifa ya jirani walikuwa wakiishangilia Yanga jana kwa kigezo cha timu yetu inayoiwakilisha Afrika Mashariki eti kuna mitanzania ilikuwa inaiombea mabaya!!! Huu ni ushabiki wa kilofa!

Nimemaliza!
 
Mwishowe utasema serikali iingilie kati watu wanaooa single Mothers, huwa ni hiyari kijana
Nahisi kama hujanielewa! Sisemi serikali iingilie kati kutuamulia cha kushabikia ninachosema iingilie kati kutujengea uzalendo na kuitanguliza nchi badala ya umimi!
 
Nahisi kama hujanielewa! Sisemi serikali iingilie kati kutuamulia cha kushabikia ninachosema iingilie kati kutujengea uzalendo na kuitanguliza nchi badala ya umimi!

Hakuna mtu anaweza kujengea mtu uzalengo duniani, uzalendo ni tunda la haki na fairness, Ni ujinga sana kitu simba wamefanya, ila wametumia uhuru wao.

Nina over 50 years, mpaka hapa nilipo sijawahi kuona mzalendo kweli wa hii ncbi, Lissu na Mbowe are trying, ila bado, neno uzalendo linatumika vibaya na sio kwa maana halisi.
 
KARMA ipo and is real mbwa nyie yooote mliyowafanyia SIMBA SC Mpaka kufikia kwenda kupokea timu Pinzani Airport kwa maturumbeta, Mpaka kuwapa mabasi mpaka kuitisha Press Conference mkawaamboa waje na Maji yao, wasitumie vyumba vya nguo, nk nk mpaka CAF ikaleta wachunguzi mechi sa Simba kisa Uongo uongo wenu. Hatimaye yamewarudi! Hamtakaa mfanikiwe kamweeee.

Halafu vile inawaumaa kukosa KOMBE KWA FAIDA YA GOLI LA UGENINI ndivyo hivyo hivyo inawauma Watanzania KATIBA ILICHOWAFANYA BAADA YA MSIBA WA JPM pambaneni na hali yenu Kima nyie!
 
Hakuna mtu anaweza kujengea mtu uzalengo duniani, uzalendo ni tunda la haki na fairness...
Mimi nadhani inawezekana mkuu! Kama tukiamua kuanzia level ya primary kuwajenga watoto kuipenda nchi yao kwa moyo tunaweza tukajenga uzalendo kwa wananchi wetu!

Kuna somo linaitwa Uraia na Maadili linazungumzia uzalendo lakini si kwa undani!
 
Tatizo lipo TFF, walianza kuisigina Yanga mapema sana kabla hata haijafika hatua hii.

Ndio maana Yanga waliamua kuweka nguvu kubwa mechi za ugenini Kwa sababu nyumbani hakueleweki.
 
KARMA ipo and is real mbwa nyie yooote mliyowafanyia SIMBA SC Mpaka kufikia kwenda kupokea !
Na ndiyo maana nikasema tukiendelea na uyanga na usimba hakuna namna soka la Tanzania linaweza kutoboa!

Si Simba peke yao wanakosea, hata Yanga kuna mahali tunakosea! Lakini haipaswi kuwa hivi!
 
Nahisi kama hujanielewa! Sisemi serikali iingilie kati kutuamulia cha kushabikia ninachosema iingilie kati kutujengea uzalendo na kuitanguliza nchi badala ya umimi!
Mkuu,kama mashabiki wa Yanga waliwapania mashabiki wa Simba endapo wangechukua kombe wangewadhihaki sana,sasa hapo unataka mashabiki wa Simba waiombee mema Yanga?

Halafu team pinzani ndio zilivyo, huwezi kukuta shabiki wa Barcelona akaiombea mema Madrid au shabiki wa Real madrid aiombee ushindi Barcelona.

Relax, ndio ushabiki ulivyo, Anyway Yanga imejitahidi sana, hope next time watachukua kombe.
 
Back
Top Bottom