Mti mzuri wa kivuli usiochafua na majani

mikungu pia inatoa majanii mengi tu.

Ni kawaida ya miti kipindi cha kiangazi kupukutisha majani, sidhani kama kuna mti ambao haufanyi hivi.

Ila huo mti mharadari ni kweli unatoa majani mengi na vimatunda vyekundu ambavyo vinachafua sana.
Ni kweli dear halafu hii haina msimu.
Inazaa vitunda na kumwaga majani kila wakati.
Ukijumlisha na uchafuzi wa kinyesi cha popo ni kero sana
 
Aysee! Hicho kivuli tu,sijui real itakuwaje!
Kuna mada flani aliieta sijui ni Mshana Jr sijui nani inahusu mambo ya miti miti,miti inayotakiwa kupandwa majumbani na mingine isiyotakiwa kupandwa majumbani kwamba ina nuksi na maniaje niaje mengine kibao!! Ukiipata ile utakutana na mengi! Watu walifunguka sana kuhusu mambo ya miti mule! Kama vipi ngoja tumuombe Mshana Jr aje ailete achungulie na kivuli kidogo😎
 
Huyu bonge kwenye picha anayezoa uchafu ndiyo wewe? Unaonekana uko m-cute sana! Hiyo miti kwenye picha ndiyo miharadali? Kuna mtu alinishauri na mimi nipande hiyo hiyo! Lakini kama unayosema kama inapukutisha majani sana basi ni hatari. Huku kwetu kuna miti wanaita Midodoma inakaa mwaka mzima iko green ina kivuli kuzuri sana! Sijawahi kuona majani yake yaliyodondoka!
 
Asante mkuu.
Hata mie niliwaza muembe au mpera ila sikua na uhakika.
Mpera achana nao ule unadondosha majani sana! Kwa mwembe sawa kabisa hata ukidondosha majani unaweza kuyaokota tu!
 
Sijui unaitwaje ila sidhani kama miti yote inamwaga majani mengi kama hii.Kuna picha nimeweka hapo juu,hayo mafungu ya majani yamejikisanya masaa mawili baada ya eneo kufagiliwa.Upepo ukivuma yanasambaa kila sehemu.
Majani ya miti yaliyoanguka pia ni urembo kwenye nyumba. Yanaonyesha uhai kwenye mazingira yako.

Cha msingi panda nyasi nzuri chini ya miti yako. Hapo cha kushughulika nacho ni hao popo tu, kama aina ya mti ndio unawavutia badilisha aina
 
Haha anajua kufanya makusudi sana huyu. Hiyo picha sidhani kama amepiga kimakosa...
 
Sawa.
Thanks🙏
 
Usipande hii utajuta.
Picha ya mdodoma please🙏
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…