Mtikila: Hili bunge la katiba limejaa wahuni na washenzi sijawahi kuona toka tupate uhuru

Mtikila: Hili bunge la katiba limejaa wahuni na washenzi sijawahi kuona toka tupate uhuru

Yeye awezi kusema kitu bila uchunguzi, ukiona ameongea hivyo ujue amefanya uchunguzi wa kina, na ukitaka kujua kwanini amewaita washenzi muulize atakufafanulia, kumbuka huyu ni mtu wa mungu hivyo basi he thinks beyond!
 
Bunge la kutaka tu potsho kubwa badala ya kuangalia kilichowapeleka kujadili. Huyo mbunge aliyetoa hoja hafai kabisa kuwa mbunge wa nchi hii. Nasema kwa sababu yeye anataka kubomoa badala ya kujenga.Hizo 300000 kwa siku kwa mda wa siku 30 ni millionaire 18,000,000. Hii ni sawa na mshahara wa mtu wa sh.300,000 kwa mwezi kwa mda wa miaka 5. KAMA MSHA
HARA WA MTU MMOJA KWA MIAKA MITANO ANAPEWA MBUNGE POSHO KWA MIEZI MIWILI TU AMBAYO NI MILIONI 90 KWA MWEZI HALAFU BADO ANALALAMIKA KUWA NI KIDOGO. JE, HUYU NI WA KUJENGA AMA KUBOMOA? HAFAI KUWA MBUNGE KABISA.

we mwalimu wako wa hesabu alikuwa nani?
 
Mtikila ndiyo mhuni namba moja, anafanya siasa za maigizo, ana chama cha siasa ambacho hakijuikani kipo kwa maslahi ya nani, yeye siasa zake ni mahakamani, kama angekuwa mwema, angeungana na wanamapinduzi wa kweli, lakini cha ajabu, mara kadhaa amekuwa akitumika na ccm kutoa kauli zenye utata kwa wanamapinduzi, rejea kauli aliyotoa kuhusiana na bomu lililorushwa kwenye kufunga kampeni za Chadema pale Arusha, waganga njaa tu hawa.
 
Kwa hiyo na yeye ni mmojawapo maana naye yumo miongoni...
 
Mtikila ni zaidi ya CHADEMA!

Mtanisamehe kwani kwenye posho,hakuna tofauti ya wapinzani na chama tawala!

ukiongelea posho usitaje vyama,sema wabunge wote ktk swala la posho wanakuwa mbogo.wakitoka nje wanajifanya ni wapiga kelele kweli
 
hujamalizia usemi WA Mtikila kua
"Haiwezekani 95% ya bunge la katiba liundwe na wanasiasa ambao Tanzania hii hawazidi hata milion Tano. halafu Watanzania walio wengi wawe na 5% tu ya uwakilishi. watanzania wamenyimwa uwakilishi wa kutosha
HIVYO TUTAENDA MAHAKAMANI NA TUTASHIDA! !!"
 
Namkumbuka huyu REV. MTIKILA katika miaka ya tisini alikuwa anadai KATIBA na TANGANYIKA irudishwe, watu wengi walidhania ni chizi kutokana na lugha yake. Leo yale mawazo yake ndiyo yanapiganiwa na wengi. Huyu jamaa huwa ni MTAIFA sana, ila bahati mbaya watu wengi hawamuelewi. nakumbuka alishaipeleka serikali mahakamani akidai mgombea binafsi, alivyoshinda ile kesi PINDA akampotezea. Leo hii tunapigania mgombea BINAFSI.
ungeanza kabisa na Abdu Jumbe, maana yeye alianza kudai Tanganyika irudi tangu mwanzoni mwa miaka ya 80's.
 
Walau Mtikila amethubutu kuyasema yote. Hilo ni bunge la kihuni na hakuna kitu pale wala maamuzi yenye afya kwa taifa yatakayofikiwa. Kwa tunaojua tunajua maamuzi yatakuwa ni viini macho tu.

Prof Shivji na wasomi wengi tu wasionunulika walishalibaisnisha hili. Bunge hili halipaswi kutokana na vyama bali wajumbe wake wawe ni WaTanzania tu. Leo bunge lile lina sura ya vyama na wengi wakiwa ni watu kutoka chama tawala.

Ukweli tumeshindwa hata kujifunza kwa wenzetu kutoka nchi jirani ya Kenya kwani walau wao wamethubutu. Pamoja na vurugu zao zilizotokea na kupoteza maisha ya watu lakini walau wametufundisha somo ambalo sisi bado tunasua sua kujitendea haki pasipo kutanguliza hila na ubinafsi.

Hivi umeona wapi mtu mmoja akaamka asubuhi akateuwa watu zaidi ya 600 kwa utashi wake na jinsi alivyojisikia mwenyewe na wakawapa haki watanzania zaidi ya 45 millioni?

Wabunge wa BLK walipaswa kuchaguliwa na wananchi wenyewe bila sura ya vyama na si kuteuliwa kihuni na mtu mhuni mwenye nia kuwatendea watu uhuni.

Mkuu umefunga thread.
 
Katika watu ambao nawaamini ni Mtikila, huyo ni muasisi wa Tanganyika
na naamini wakimsikiliza atatoa mchango sahihi hao wengine ni macho fedha tu

hana lolote hao
 
Kikwete ni mnafiki ndiyo maana hata Lowasa ana hasira naye ni mtu gani anayeshindwa kuheshimu
wananchi? unateua wabunge wa bunge la katiba ambao ni watu wako kwani hakuna walimu nchi hii

mimi naamini angeteu walimu waganga na wakulima bunge lingekuwa halina malalamiko ya wananchi
kikwete ni lazima atapata matatizo baada ya muda wake mtu gani anakuwa na mipango ya chini chini
 
Kama unamkubali Mtikila mwenye chama chenye usajili wa kudumu ingawa wanachama wote alionao hawafiki 150, basi unamatatizo makubwa.

Wengi wetu tunampenda Rev. Mtikila kama mwanaharakati na mpigania haki za binadamu na sio mwanasiasa...ndugu sio wote wanapenda mtu kwa sababu ya mvuto kisiasa kama wewe..
Hivi unajua kama isingekuwa juhudi zake Rev. Mtikila leo hii watanganyika tungekua tunaingia Zanzibar kwa passport...!!
Hivi unajua kama sio Rev. Mtikila leo hii swala la mgombea binafsi lisingekuwepo kwenye rasimu ya katiba...??
Hivi unajua kama sio Rev. Mtikila kupaza sauti ya utanganyika wetu swala la Tanganyika na utanganyika wetu lilikua linaenda kupotea wakati Zanzibar na uzanzibari unaendelea kushamili kwa kasi..
Yapo mengi na mengi Rev. Mtikila ameyapigania for public interest na sio political interest..
Nadhani we humjui vizuri Rev. Mtikila
 
Back
Top Bottom