Mtoto miaka 4 apasua kioo cha basi la Shabiby kwa manati

Mtoto miaka 4 apasua kioo cha basi la Shabiby kwa manati

Hii chai, 4 years anawezaje vuta manati na kurusha jiwe kwa umbali kuleta madhara hayo.. Labda kama miaka sio sahihi.
 
Siku moja tulikuwa tunasafiri kuelekea wilaya ya Kwimba, basi njiani kijana mdogo alirusha dongo kubwa kwenye kioo. Bahati nzuri mimi nilikuwa seat ya mbele nilifunga kioo kwa hivyo liligonga kioo. Tuliposimamisha gari yule kijana na wenzake wawili walikimbia. Wenzangu walishuka na kuwafukuza mpaka kwao, na wakakuta akina mama wamekaa wanasukana nywele. Waliuliza nani mwenye mtoto wao wakakataa kujibu, wenzangu wakawaambia tunampeleka polisi kama hamutaki kujibu, na hapo siyo chini ya kilomita 60 kutoka hapo kijijini. Mama yake ilibidi alijibu haraka maana aliogopa ni gari ya serikali.

Yule mama aliambiwa kama anataka mwanawe asipelekwe kituoni basi akate fimbo amchape mpaka bakora zimkolee. Masikini yule mama alikata fimbo na kumchapa kisawasawa yule mtoto wake, lakini nadhani ilkuwa adabu stahiki kwa yule kijana.
Safiiii sana
 
watu wa mbeya sikuhizi wapuuzi sana, sasa hapo mhempelekea makofi bibi yake tu. kuna dc kasulu aliwalamba mboko familia nzima kisa mtoto kuponda gari yake, ila ukikna mtu anatumia jiwe kushambulia mwingine hiyo ni dalili ya umasikini
 
watu wa mbeya sikuhizi wapuuzi sana, sasa hapo mhempelekea makofi bibi yake tu. kuna dc kasulu aliwalamba mboko familia nzima kisa mtoto kuponda gari yake, ila ukikna mtu anatumia jiwe kushambulia mwingine hiyo ni dalili ya umasikini
Safi familia nzima kula fimbo hadharani
 
chai.jpg
 
Mtoto wa miaka 4 avunja kioo cha Shabiby kwa manati

Basi la Shabiby Line lililokuwa likitokea Mbeya kwenda Dodoma lilichelewa kwa takriban saa moja na nusu Agosti 14, 2024, baada ya mtoto wa miaka minne wa Kijiji cha Ndolela, Iringa, kuvunja dirisha la basi kwa manati kutokea upande wa pili wa barabara.

Mtoto huyo ambaye pia alisababisha kisa kama hicho hapo awali, alikimbilia kwa bibi yake baada ya usumbufu huo.

Abiria walishuka kumtafuta mtoto huyo ambaye hatimaye alipatikana amejificha. Katika tukio la awali, bibi wa mtoto huyo alilipa Sh170,000 kufidia uharibifu huo.

Basi hilo ambalo awali lilitakiwa kuwasili Dodoma saa 2:30 usiku, lilifika saa 4:15 lilipoelekea.

Ingawa hakuna abiria aliyejeruhiwa, mmoja alikwepa chupuchupu kupigwa na jiwe hilo.

Kuna wasiwasi unaoongezeka kuhusu tabia hatari ya mvulana huyo, ambayo inaweza kusababisha ajali mbaya katika siku zijazo

Credit: DJ Fetty kwa msaada wa The Citizen Tanzania

USSR
Huyo mtoto ni bonge la asset , ya nini kumlipisha bibi yake hela kwa tukio la mtoto wa mika minne?
Yaani Shabib wanaenda kumdai mtoto wa miaka minne?
 
Dogo awe poti ana kipaji baadae aje acharaze viboko kina Mnyika na Sugu
 
Mnazaa Zara hovyo Kama Mbuzi, mnawapeleka watoto kijijini mnabaki Sinza kufanya umalaya!!!!
 
Bibi CCM mtoto akikua mkubwa Ccm na mmiliki wa mabasi pia Ccm so watajuana wao bana
 
Back
Top Bottom