Black Sniper
JF-Expert Member
- Dec 10, 2013
- 32,406
- 55,148
Ndio ngono za utotoni zinaanza hapoHii mambo ya mtoto mtaa mzima kila mtu uncle uncle uncle uncle uncle uncle uncle uncle ni kumuweka mtoto mazingira hatari kwa usalama wake
Mkuu sio kutekwa tu hata matusi wanafundishana njeAisee ilo ni fundisho kubwa sana mambo ya mtoto kuchekacheka na mtu ambae hamfahamu ni mbaya sana mwisho wa siku mtoto wanamlaghai na kutekwa mazima nimepata funzo hapa wacha niwafundishe watoto wangu mazoea na watu hapana hii itanisaidia sana mana hali ni tete sana
MhuuuHabari za usiku wakuu!
Jamani juzi kati hapa kuna mtu alipost uzi fulani kuhusiana na tatizo la utekaji wa watoto baadhi ya maeneo ya dar es salaam. Leo almanusura tumpoteze mtoto wa ndugu yetu, tukio lilitaka kutokea maeneo ya kimara matosa, mtoto aliitwa na watu wasiojulikana walikuwa kwenye noa nyeusi tinted mtoto aliambiwa akachukue pipi lakini mtoto alisita akakimbia, ivyo ndio ikawa pona pona yake.
Ivyo naomba niwaombe wazazi na walezi tuwe makini sana na watoto wetu.
Niwatakie usiku mwema.
Hili ni muhimu sana. Unakuta watoto wanaambiwa eti wawe watii kwa wakubwa na kusalimia kila mtu. Maweee!Zamani nilikuwa nawashangaa wazungu wanawafundisha watoto wao wasiongee wala kuwajibu strangers
Baadae nikajua umuhimu wake
Na mimi nikawafundisha watoto
Hata umuitaje kama hakujui imekula kwako
Wazazi na hata mliomo humu bila watoto jaribuni kuwafundisha watoto wasiongee wala kuwaitikia wasiowajua hata wapepe box la pipi
Watoto huku hawapewi kitu
Kama ni sumu au ana allergy
Kweli sisi tuko tofauti kwa sababu ya upendo lakini mambo yamebadilika sana siku hizi
Hakuna kumuaminia mtu mtoto na ajue hakuna cha anti wala anko
Huku Mikoan ni kawaida kuona mtoto anatembea km 15 kufuata shule.Daah Mungu anasaidia TU maana leo nimekutana na mtoto wa darasa la kwanza kanapita porini peke yake umbali wa kilomita tano hv
Eneo ni hatari kuna Nyati na tembo smtms hakuna makazi ya watu wala wapitanjia!
Nilikapa lift, niliwaza mbali sana kwa jinsi dunia watu wamekuwa wanyama.... Kufika kakashuka na kusema "asante Mungu akubariki"
Wazazi tulinde watoto wetu, hasa pia mida ya kutuma dukani usiku ni hatari, bora uende mwenyewe tu
Bora mkoani kuna usalama kdg, binadamu wakatili siyo wengi, japo ni hatari kwa watoto.Huku Mikoan ni kawaida kuona mtoto anatembea km 15 kufuata shule.
Nimecheka utafikiri mazuri, sema mkuu unaweza ukawa na mtoto mmoja alafu ukashangaa janga limempata mtoto wako ni vile tu mazingira kwa sasa ni hatar sanaKwann mtu asizae watoto ambao ataweza kuwahudumia na kuwaweka mazingira salama!!
Mtu anazaa km sungura, serekali inabidi hiamishie nguvu ktk elimu ya uzazi wa mpango
Wanakata Mkono wa kulia alafu wanachomoa sehemu za SiriSerikali ipo bize na misafaraaa..........
Kiukweli dunia imekwisha jamani mambo yamebadilika sana juzi juzi vitoto vya majirani cha kike kidogo na cha kiume kikubwa kidogo vimekutwa vinakulana aisee sio powa mambo ovyo kabisa suhala la kuchunga watoto ni muhimu sanaMkuu sio kutekwa tu hata matusi wanafundishana nje
Mazoea na watu kataza kabisa mana ngono pia huwa zinaanzia huko wanakoenda
Kuwa rafiki na watoto waambie madhara ya kuwa nje na hatari zake
Mkuu hamuoni watu wasio waswahili watoto wao hawaonekani wakicheza hovyo nje?Kiukweli dunia imekwisha jamani mambo yamebadilika sana juzi juzi vitoto vya majirani cha kike kidogo na cha kiume kikubwa kidogo vimekutwa vinakulana aisee sio powa mambo ovyo kabisa suhala la kuchunga watoto ni muhimu sana
Huku mtu unayemuamini ndio anayedhuru, si umeona mtoto aliyeuwawa ni mpango wa baba yake na watu wa karibu wa kiroho.!!
Tena hiyo tabia ndio siipendi na kina mama ndio wanaona ni heshima halafu jitu kubwa linampaka mtoto wa kike hao ni mbwa kabisaHili ni muhimu sana. Unakuta watoto wanaambiwa eti wawe watii kwa wakubwa na kusalimia kila mtu. Maweee!
Hapo unachanganya mazingira ya uswahili na ushuani, vipato havifanani mkuu.!!Mkuu hamuoni watu wasio waswahili watoto wao hawaonekani wakicheza hovyo nje?
Tunasema ni wabaguzi kumbe wao ndio wako sahihi kila wakati
Wangewaacha mngeona damu changanyikeni kila mahali
Tuwafunze maadili watoto la sivyo mtaendelea kuona mtoto wa miaka 12 yuko na jamaa gesti
Unaweza kuwa karibu na wanao na kuwafundisha mazuri na kuwakataza mabayaHapo unachanganya mazingira ya uswahili na ushuani, vipato havifanani mkuu.!!
Kwahiyo unataka wote tuwe matajiri tufungie watoto kwenye mageti??
Huku uswahilini ndio matukio ya utekaji mengi, na yanasababishwa na hali ngumu ya kimaisha.!!
Hapa tunajadili utekaji sio malezi, hayo malezi hayahusiani na utekaji.!!Unaweza kuwa karibu na wanao na kuwafundisha mazuri na kuwakataza mabaya
Watoto bila kuwaonya hawajui na kipigo hakisaidii
Bora kuwaambia
Sikatai watoto kucheza pamoja ila wawe na mda na pia wanaonba ruhusa na wewe unawa monitor
Kuhusu ushuani na changanyikeni sawa
Lakini hata masikini awe na mda wa kuwa nje na watoto wake sio lazima kuwapeleka mahoteli makubwa au beach lakini onyesha upendo kwa kutembea nao hata mitaa miwili mitatu
Be close to them wajue unawajali hata kama huna gari mama
Nayajua maisha yote pande mbili ila wazazi tuwe waangalifu hakuna cha anko wala anti