Mtoto wa Rais Samia, Abdul ana cheo gani Serikalini/Wizara ya Nishati hadi akutane na Rais Museveni?

Mtoto wa Rais Samia, Abdul ana cheo gani Serikalini/Wizara ya Nishati hadi akutane na Rais Museveni?

Inaelekea ameenda kupiga deal zake za kampuni binafsi kuwekeza kwenye solar energy Uganda.

🤫 Sitoshangaa kusikia kwa upande wa Tanzania hii miradi TANESCO inayoingia ya kununua umeme wa renewables kuna kampuni moja, yeye na mama yake ni wabia (kama sio wamiliki 100%).
Sioni shida akifanya biashara halali
 
Sioni shida akifanya biashara halali
Majuzi Rostam Aziz katangaza anawekeza $100m Zambia kwenye LPG umeona kazua mjadala wowote, si kila mtu anaelewa ni mfanyabiashara ata kama alianza kama fisadi.

Sana sana kilichozua mjadala siku hiyo aliposema majaji watanzania ni wakupigiwa simu, lakini hakuna aliezungumzia uwekezaji wake.

Same Bakhresa, Sawaya, Mo Dewji na matajiri wengine tukisikia wana mpango wa kuwekeza $25m million sehemu hiyo wala sio habari; wanajulikana ni wafanyabiashara matajiri, shughuli zao rasmi zinajulikana na wanakopesheka ata bank zilizopo nje ya Tanzania.

Shida sio mtoto wa raisi kuwekeza, shida ni hizo hela anatoa wapi; hawana historia ya utajiri kwenye familia yao.
 
Tulisema lengo la kuuza Bandari ni biashara haramu. Aliye jirani na Museveni amshitue tutakuwa kama Kenya kuleeee karibu na mpaka wa wapenda vita…
East Africa inatengeneza bomu la nuklia kupitia Tanganyika
Umeandika upuuzi mtupu. Unaweza kuweka ushahidi wowote wa maandishi unaoonyesha bandari kuwa imeuzwa?.
 
Rais Mseven wa Uganda amekutana na ujumbe wa serikali ya Tanzania ambao umeongozwa na mtoto wa wa kiume wa Rais Samia.

Uzuri wa taarifa hii imethibitishwa rasmi na ofisi ya Mseveni mwenyewe kupitia akaunti ya raisi.

Swali- mtoto huyu wa rais wetu,ana cheo gani serikalini?!!

Kama taarifa hii isingetolewa na Mseveni,tungetangaziwa na ofisi gani huku Tanzannia?!!

Swali la kujiuliza pia,mambo mangapi mtoto huyu amekua ameyafanya kwa kutumia kodi za Taifa na pasi na taarifa kuwekwa wazi kwa umma?!!

Ni wazi kua mtoto huyu anafanya haya kwa ruksa ya Rais Samia ambae ni mzazi wake,je huu sio uvunjaji wa katiba?!!

NB- imewahi kuandikwa tetesi kua kijana fulani amefungua ofisi Dubai kwenye kasri mojawapo na kua hata DP WORLD ni moja wapo ya mradi wake/wao na waarabu!!.

Kuhoji haya ni kwa nia njema,kama kijana ana kampuni zake za biashara iwekwe wazi Ila pia na wahusika wapime kama yanayofanywa yanatoa taswira hasi ama kua familia imekaa kibiashara tu?!!

View attachment 2715337View attachment 2715338View attachment 2715339
Tumerudi kulekule, wahuni wameanza kuhuni nchi
 
Tutamkumbuka mpka akili zitukae sawa,kila nafsi itataja jina lake. Ngojea tuwekwe sawa kwanza.
 
Huyu mtoto wa rais ni kwamba anafundishwa kazi za biashara za kimataifa baina ya Tanzania na mataifa mengine na mwalimu wake ni Rastam.
Hata hii DP world watakuwa wana shea ya kifamilia na ndio maana mkataba ulikuwa wa kimya kimya bila kumhusisha mwana sheria wa serikali.
Mwana sheria wa serikali hakuwa na habari ya kile kilichokua kinaendelea bungeni wakati wa kipitisha mkataba maana tuliona hakutoa mchango wowote.
Bahati mbaya nchi ina usalama wa watawala na sii usalama wa taifa.
 
Majuzi Rostam Aziz katangaza anawekeza $100m Zambia kwenye LPG umeona kazua mjadala wowote, si kila mtu anaelewa ni mfanyabiashara ata kama alianza kama fisadi.

Sana sana kilichozua mjadala siku hiyo aliposema majaji watanzania ni wakupigiwa simu, lakini hakuna aliezungumzia uwekezaji wake.

Same Bakhresa, Sawaya, Mo Dewji na matajiri wengine tukisikia wana mpango wa kuwekeza $25m million sehemu hiyo wala sio habari; wanajulikana ni wafanyabiashara matajiri, shughuli zao rasmi zinajulikana na wanakopesheka ata bank zilizopo nje ya Tanzania.

Shida sio mtoto wa raisi kuwekeza, shida ni hizo hela anatoa wapi; hawana historia ya utajiri kwenye familia yao.
Hela za kuwekeza lazima zitoke mfukoni kwake? Hakuna benki zinakopesha? Hakuna partnership anaweza fanya na watu wenye mitaji?

Maswali yako hayana msingi. We unataka kujua watu hela wanapata wapi watafute binafsi wakueleze sio unatuletea maswali ya kimaskini hapa. Au nikuulize wewe hapa hela zako unapata wapi?
 
Huyu mtoto wa rais ni kwamba anafundishwa kazi za biashara za kimataifa baina ya Tanzania na mataifa mengine na mwalimu wake ni Rastam.
Hata hii DP world watakuwa wana shea ya kifamilia na ndio maana mkataba ulikuwa wa kimya kimya bila kumhusisha mwana sheria wa serikali.
Mwana sheria wa serikali hakuwa na habari ya kile kilichokua kinaendelea bungeni wakati wa kipitisha mkataba maana tuliona hakutoa mchango wowote.
Bahati mbaya nchi ina usalama wa watawala na sii usalama wa taifa.
Wapi imesemwa mwanasheria wa serikali hakushirikishwa mkataba wa DP World?
 
Mnajisumbua!

Nchi hii siku hizi uongozi ni wa kurithi. Ni mwendo wa ufalme na umalkia tu! Mfumo ushabadilishwa kitambo! Na ndomana wakaibuka (walamba asali)

Endeleeni kupiga kelele.
 
Majuzi Rostam Aziz katangaza anawekeza $100m Zambia kwenye LPG umeona kazua mjadala wowote, si kila mtu anaelewa ni mfanyabiashara ata kama alianza kama fisadi.

Sana sana kilichozua mjadala siku hiyo aliposema majaji watanzania ni wakupigiwa simu, lakini hakuna aliezungumzia uwekezaji wake.

Same Bakhresa, Sawaya, Mo Dewji na matajiri wengine tukisikia wana mpango wa kuwekeza $25m million sehemu hiyo wala sio habari; wanajulikana ni wafanyabiashara matajiri, shughuli zao rasmi zinajulikana na wanakopesheka ata bank zilizopo nje ya Tanzania.

Shida sio mtoto wa raisi kuwekeza, shida ni hizo hela anatoa wapi; hawana historia ya utajiri kwenye familia yao.
Wewe una historia ya kuingia JF kwenye familia yako?
 
Kwa hicho lingine Magu alisema ni kichaa tu anayeweza kufanya mambo ya hovyo akiwa ikulu
 
Watanganyika tusipisimama hizo familia zimeshaganya cartel ndani ya nchi
 
Back
Top Bottom