Bufa
JF-Expert Member
- Mar 31, 2012
- 12,599
- 26,263
Ataendesha usiku
Hata akiendesha mchana hilo ni kosa lingine that's not my concern, for now, kaadhibiwa kwa mujibu wa sheria kwa kosa allilotenda hapo awali.
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Ataendesha usiku
duh... Bima ya chombo ina gharama kuliko faini yake, Nashukuru kwa kulifahamu hilo🙏View attachment 2333685
Mfanyabiashara, James Simbachawene (24) ambaye ni mtoto wa Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge na Uratibu), George Simbachawene, amehukumiwa kulipa faini ya Sh250, 000 na kufungiwa leseni yake ya udereva kwa miezi sita baada ya kukiri makossa matatu.
Mtoto huyo amefikishwa mahakamani hapo leo Jumatano Agosti 24, 2022 jioni na kusomewa mashtaka yake na wakili wa Serikali, Daisy Makakala, mbele ya Hakimu Mkazi Aron Lyamuya.
Mashitaka hayo ni pamoja na kuendesha gari kwa hatari, kuendesha gari akiwa amelewa na kuendesha gari bila kuwa na bima.
Baada ya kusomewa mashitaka hayo, Simbachawene alikiri na ndipo hakimu Lyamuya alipoahirisha kesi ili kumwandikia hukumu.
Baada ya muda mfupi, ndipo hakimu Lyamuya alimhukumu Simbachawene kulipa faini ya Sh100,000 kwa kosa la kuendesha gari kwa hatari, Sh100,000 kwa kosa la kuendesha gari akiwa amelewa na Sh50,000 kwa kosa la kuendesha gari bila kuwa na bima.
Pamoja na faini hiyo, leseni ya Simbachawene imefungiwa kwa miezi sita.
Credit; Mwananchi News Paper
Huyo Mwendawazimu hajauona Ndugu.Soma mstari wa mwisho.
Kuonesha hasira acha hio kazi uliyonayo mkuu ili iwe kama mfanoningekuwa mimi pamoja na yote hayo, ningejiuzulu nafasi yangu niliyo teuliwa ili kuonyesha uwajibikaji kwa kitendo alicho fanya mtoto wangu haswa pale alipo tumia cheo cha Baba yake kujigamba kuwa yupo juu ya sheria na anaweza fanya makosa bila kuchukuliwa hatua kwa kutegemea wadhifa wa Baba yake.
viongozi wetu kuweni na utamaduni wa kuwajibika nyinyi wenyewe kwa makosa mbalimbali yanayo jitokeza, sio mpaka unyofolewe.
Hivi,hatukukubaliana kwamba kila mtu ni sawa mbele ya sheria?Ingekuwa adhabu ya 25m na kifungo cha miezi sita jela ndo ingekuwa sawa
Wana bima? Wamfungulie mashitaka ya uharibifu wa mali zao.Vipi kuhusu wale walioharibiwa magari yao na huyo dogo? Au wao ndio imeisha hiyo?
Sent using Jamii Forums mobile app
Hata yeye kwa jinsi alivyorekodiwa, alidai ana pesa, naona kulipia bima ya gari aliona sio kipaumbele.TZS 250,000/= kwa mtoto wa Waziri ni issue ndogo tu. Ni swala tu la Chawene Mkubwa kupiga simu moja tu hela ikaletwa fasta.
Mbona hata mim nna mwaka sasa sna bima wala sija update lesen. Hahah. Bonho raha sana.. natoka asubuh sa 12 hamna askar narud sa 12 jion hamna askar.. hahahUnadhani ndo hataonekana road na gari? Labda sio Tz...ataendesha vizuri tu
Ndio maana babaake kasema achukuliwe hatua kwa mujibu wa sheria.Traffic case ni kesi za kawaida sana hata angegonga akaua watu 10 bado adhabu yake ingekua siyo kubwa kesi za barabarani hazina mambo mengi labda uwe hauna lesen ndo inakuaga ngumu kidogo hata makosa aliyo yafanya huyo jamaa ni makosa ya kawaida tu ila kwakua ni mtoto wa kiongozi ndo maana imechukuliwa tofauti ila Sheria ni 1 tu
Vile virungu sijui vimetengenezwa na nini kwa ule mdundo wake katika ugoko na kwenye maungio ya mkono😭Utapewa kesi ya Kutukana matusi, utapewa kesi ya kumzuia askari kufanya majukumu yake, na jinai zingine kadhaa tu hivi. Hiyo miezi anayofungiwa kuendesha gari lakin anakua uraiani, kama ndio wewe utakua uko mahabusu ukiwa ushakula virungu vya kutosha tu.
Siku zote nawambiaga watu, ukiwa unavuka barabara fanya chap usilinge. Sheria za makosa barabarani adhabu zake ni ndogo sana. Jamaa-angu aligonga na kuua Kimara, akakili kosa mahakamani alilipa 186k tu, eti gari ndo iliyoua sio yeye kwa kuendeshwa kwa uzembe.250K , hela ya kifurushi cha DStv?
Katukana na kudharau mamlaka, huyu ilibidi apewe hata miaka 15 jela na faini si chini ya milioni 10. Kamdhalilisha sana babake na familia yake.View attachment 2333685
Mfanyabiashara, James Simbachawene (24) ambaye ni mtoto wa Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge na Uratibu), George Simbachawene, amehukumiwa kulipa faini ya sh. 250,000 na kufungiwa leseni yake ya udereva kwa miezi sita baada ya kukiri makosa matatu.
Mtoto huyo amefikishwa mahakamani hapo leo Jumatano Agosti 24, 2022 jioni na kusomewa mashtaka yake na wakili wa serikali, Daisy Makakala, mbele ya Hakimu Mkazi Aron Lyamuya.
Mashitaka hayo ni pamoja na kuendesha gari kwa hatari, kuendesha gari akiwa amelewa na kuendesha gari bila kuwa na bima.
Baada ya kusomewa mashitaka hayo, Simbachawene alikiri na ndipo hakimu Lyamuya alipoahirisha kesi ili kumwandikia hukumu.
Baada ya muda mfupi, ndipo hakimu Lyamuya alimhukumu Simbachawene kulipa faini ya Sh100,000 kwa kosa la kuendesha gari kwa hatari, Sh100,000 kwa kosa la kuendesha gari akiwa amelewa na Sh50,000 kwa kosa la kuendesha gari bila kuwa na bima.
Pamoja na faini hiyo, leseni ya Simbachawene imefungiwa kwa miezi sita.
Chanzo: Mwananchi News Paper
Tupo wengi😃Mbona hata mim nna mwaka sasa sna bima wala sija update lesen. Hahah. Bonho raha sana.. natoka asubuh sa 12 hamna askar narud sa 12 jion hamna askar.. hahah
Ukitaka kamatwa toka saa nne asubuh au tembea mida ya mchana lazima askar akusimamishe
Hakuna sheria hiyo???Katukana na kudharau mamlaka, huyu ilibidi apewe hata miaka 15 jela na faini si chini ya milioni 10. Kamdhalilisha sana babake na familia yake.