Mtoto wako alikuwa hana mazoea ya kwenda kwa jirani fulani lakini ghafla habanduki huko, shtuka!

Mtoto wako alikuwa hana mazoea ya kwenda kwa jirani fulani lakini ghafla habanduki huko, shtuka!

Rare Sapphire

JF-Expert Member
Joined
Jul 24, 2021
Posts
590
Reaction score
1,648
Wakuu,

Una jirani, rafiki yako au hata ndugu mnaoishi karibu na mtoto wako alikuwa hana mazoea ya kwenda huko lakini ghafla amekuwa habanduki kwa jirani huyo mzazi shtuka. Na kinyume chake vile vile, mtoto wako alikuwa anapenda kwenda sehemu fulani kucheza lakini ghafla haendi huko na unajua kuna rafiki yake mzuri muda wote hucheza pamoja shtuka pia, kuna uwezekano mkubwa kuwa kuna jambo baya limetokea huko ambalo limefanya awe anaenda au aache kwenda sehemu husika.

Badala ya kufurahia mtoto akienda sehemu fulani unapata muda wa kufanya mambo yako, au sasa mtoto wako ameacha kuzurura na kupenda mchezo kila wakati, fuatilia ujue kuna nini.

Watoto wengi wanapitia unyanyaji wa kingono kwa kwa njia hii kutoka kwa watu wazima au hata watoto wenzao, mpaka mzazi unakuja kushtuka unakuta ameshaharibika au ameshafanyiwa vitendo vibaya muda mrefu.

Ni vizuri pia kuweka utaratibu wa kupiga stori na mwanao kila siku jioni, muulize siku yake ilikuaje, amefanya nini, amecheza na nani, amejifunza nini, kwa kufanya hivi itakuwa rahisi kujua nini kinaendelea kwenye ulimwengu wa mtoto wako na kutambua tatizo mapema pale linapotokea.
 
Wakuu,

Una jirani, rafiki yako au hata ndugu mnaoishi karibu na mtoto wako alikuwa hana mazoea ya kwenda huko lakini ghafla amekuwa habanduki kwa jirani huyo mzazi shtuka...
Ni vizuri pia kuweka utaratibu wa kupiga stori na mwanao kila siku jioni, muulize siku yake ilikuaje, amefanya nini, amecheza na nani, amejifunza nini, kwa kufanya hivi itakuwa rahisi kujua nini kinaendelea kwenye ulimwengu wa mtoto wako na kutambua tatizo mapema pale linapotokea.[emoji419][emoji375]

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Wakuu,

Una jirani, rafiki yako au hata ndugu mnaoishi karibu na mtoto wako alikuwa hana mazoea ya kwenda huko lakini ghafla amekuwa habanduki kwa jirani huyo mzazi shtuka. Na kinyume chake vile vile, mtoto wako alikuwa anapenda kwenda sehemu fulani kucheza lakini ghafla haendi huko na unajua kuna rafiki yake mzuri muda wote hucheza pamoja shtuka pia, kuna uwezekano mkubwa kuwa kuna jambo baya limetokea huko ambalo limefanya awe anaenda au aache kwenda sehemu husika.

Badala ya kufurahia mtoto akienda sehemu fulani unapata muda wa kufanya mambo yako, au sasa mtoto wako ameacha kuzurura na kupenda mchezo kila wakati, fuatilia ujue kuna nini.

Watoto wengi wanapitia unyanyaji wa kingono kwa kwa njia hii kutoka kwa watu wazima au hata watoto wenzao, mpaka mzazi unakuja kushtuka unakuta ameshaharibika au ameshafanyiwa vitendo vibaya muda mrefu.

Ni vizuri pia kuweka utaratibu wa kupiga stori na mwanao kila siku jioni, muulize siku yake ilikuaje, amefanya nini, amecheza na nani, amejifunza nini, kwa kufanya hivi itakuwa rahisi kujua nini kinaendelea kwenye ulimwengu wa mtoto wako na kutambua tatizo mapema pale linapotokea.

Ushauri Mzuri sana Mkuu.
 
Kwanza naona ajabu sana mzazi kuona kawaida mtoto wake kwenda kwa jirani.
Kwajinsi dunia ilivyo badilika, mimi wanangu wana sehem 3 katika mzunguko wao kwa wiki nzima ambazo ni akitoka shuleni ni straight nyumbani na jumapili ni kanisani. Siku nikitaka watoke kwenda sehem tofauti lazima niwapeleke mimi mwenyewe au mama yao wakacheze, waogelee, wabembee then nawarudisha home.
Kama ni mucheza ninaamini shuleni wanapata muda mzuri wa kucheza na kujichanganya na watoto wenzao, lakini pia home wanaendesha baisikeli zao na kucheza mpira ndani ya fensi.
Kwa wale wakubwa ambao wapo vyuoni, wao tuna utaratibu kwamba kila anapotaka kutoka kwenda sehem lazima atoe taarifa na anapokwenda lazima pawe panajulikana, na muda wa kurudi nyumbani mwisho ni kabla ya giza lazima awepo nyumbani.
Pia kama mzazi nimejiwekea utaratibu wa kua nakula pamoja na watoto wote kama wanakuepo hasa kipindi cha likizo, then tunakaa sebleni kwa maongezi ya kawaida wote kwa ujumla tukijadili mambo mbalimbali.
 
Wazazi tujitahidi kuwafundisha watoto wenu kumjua MUNGU pia kufanya maombi pamoja na malezi Bora yatokanayo na mafundisho wanayopata wakiwa kwenye nyumba za ibada
Ni kweli mkuu
Ila huko nyumba za ibada nako kuna mambo ya ovyo pia.
Hapo ni mzazi ku step up hakuna kumuachia mungu wala shemasi be responsible .
 
Back
Top Bottom