Mtu akiandika hivi huwa najisikia hasira

Hamna kitu sipendi kama mwanaume mwenaume mwenzangu kuniita "best".
Aisee siipendi hii kitu basi tu.
 
Hiyo ya kuandika dhamani badala ya thamani nawaona sana watu wa Kilimanjaro wengi ndio wana huo ugonjwa
 
Kiongozi, tena maeneo ya Shinyanga na Tabora kuna changamoto kubwa sana.Wanafunzi wanaongea lugha za makabila yao hadi darasani.
 
Kwahiyo tunafundishwa lugha na uzee huu?😂😂😂😂

Wengi nikiwemo Mimi hii lugha hatujanyooka kivile ila sipendi mtu kunitumia SMS.

Xaxa hivi nakuja.
 
unazungumzia magazeti yapi?
 
2O8 (tuonane, yaani demu akitumia hiyo code kama kichwa panzi hutakaa uelewe)
 
Wakurya

Nirikuambia, nitakura, nitamwereza

Wasukuma wenzangu

Nilikujjaga kipindi cha mavuno, alikwenddaga kwao lakini nililikumbuka kweli...neno sawa atasema xawa

Wachagga

Nillienda ttabora, kulla, haabari gani manggi.


Watu wa dar

Nrikwenda, ujui usemalo, abali gani, ujaniambia kitu, nrisafiri morgoro/arousha


Wamasai


Qwaqweli, happana enda, naomba tafasalli, alienda maalli fulanni kutafuta chakulla.
 
Kuna haya maneno kama;
Mamb, tyu,
Saw, ukuje, pow au pw, xax inakuwaj, jomon, kutokutofautisha R na L, n2mie, kazaa badala ya kadhaa,
aiseee.. huwa yanani turn off sana
 
Tyu, jomoni, vepe, mwaya yaani siyapendi alafu unakuta ni mwanaume ndiyo anaongea huwa nachefukwa.
 
Nitakugea[emoji38][emoji38][emoji38].nikisikia hili neno huwa naondoka kabisa eneo husika.
 
Watu wanaopenda kutumia xx badala ya s,hovyo sana.unakuta mtu anakuandikia p badala ya poa.
 
Sipendi kusikia mtu akisema
MIMI KAMA MIMI
YEYE KAMA YEYE
JUMA KAMA JUMA
MKUU WA MKOA KAMA MKUU WA MKOA
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…