Mtu anaechukua mkopo wa milioni 100 kujenga nyumba ya milioni 10, na anaemkopesha ndiye anayejenga (lazima); ana akili timamu kichwani kwake?

FRANCIS DA DON

JF-Expert Member
Joined
Sep 4, 2013
Posts
38,920
Reaction score
44,970
Tuchukulie kwa mfano mtu anakuja kukushawishi akukopeshe pesa kiasi cha milioni 100 ili ujenge nyumba ya kuishi; ila sasa masharti ya huo mkopo ni kwamba lazima ramani za jemgo, vifaa vya kujengea, BOQ, na mafundi wote watoke kwake huyo anaekukopesha.

Halafu huyo anaekukopesha anakuletea ramani ya nyumba ya thamani ya milioni 10, ila kwakuwa QS aliyeandaa BOQ ni wake, anaweka thamani ya jengo ni milioni 100, hivyo pesa yote inaishia kwake katika material na mafundi, hivyo kujihakikishia soko la bidhaa zake na ajira kwa mafundi wake.
Na kwakuwa mkopo huu hauna riba , basi unapachikwa jina la ‘Mkopo wenye masharti nafuu’.

Sasa nauliza tu, huyu mtu anaechukua mkopo wa aina hii, ana akili timamu kweli?
 

Huyo mtu ana akili kwa mambo mengine lakini hana FINANCIAL INTELLIGENCE!!! Umenielewa hapo?
 
Inafanana na kisa kwenye hadithi by truly yours, iitwayo, Nyumba Ya Maskini. Amazon product ASIN B003ELPWI2
 
Akili anazo timamu kabisa hiyo ni indirect business kila upande unanufaika.
 
Inafaa mkopaji atandikwe bakora za shingoni nyingi sana kwa muda wa kila masaa manane kama dozi ya malaria.😂😂😂
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…