Mtu kama huyu ni binadamu au shetani? Anaombeaje Corona ifike Tanzania. Kuiombea nchi yako majanga, sio zaidi ya uendawazimu? Huu sio ushetani?

[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji119][emoji119][emoji119][emoji119]

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mkku nanukuu maneno ta askofu bagonza "ukimpiga MTU usimyime haki ya kulia"
Watu wengi wamepigwa ndo wanalia hivyo, wengine wanalia vizuri Ila wengine wanalia vibaya, ni haki yao, kulia

ni jukumu lako wewe mwandishi mkongwe kumweleza anayewapiga watu kwa kuwaonea kuwa wanalia vibaya acha kuwapiga
 
PASCHAL ulishawahi kuwaza hata siku moja kwamba muuwaji wa mawazo pale KATORO busanda nanani ulishawahi kujiuliza Azory gwanda yu wapi kangoye Benn saa nane nk ukishapata majibu mazuri nitag hapa unaendekeza ukabila mnoo Kama Mbona wasukuma tupo wengi Sana na hatuamini katika kunyanyasana wewe kama Kuna kitu unakifukuzia fanya hivyo kimya kimyaa Usitake wenzako waumie kisha wewe upate ukitakacho Usitake kutuchokonoa Tunayo mengi ya kusema ila tumekua Kama samaki majini punguza upoyoyo.
 
Mbona Al Kaaba imefungwa! Kweli virus wanafanya Al Kaaba ifungwe?
Naona huelewi hata unachokiandika.

Kaaba siku zote inafungwa haiwachwi wazi, hufunguliwa mara mbili tu kwa mwaka. soma...

The building is opened twice a year for a ceremony known as "the cleaning of the Kaaba." This ceremony takes place approximately thirty days before the start of the month of Ramadan and thirty days before the start of Hajj. The keys to the Kaaba are held by the Banī Shaybah (بني شيبة) tribe. Members of the tribe greet visitors to the inside of the Kaaba on the occasion of the cleaning ceremony. A small number of dignitaries and foreign diplomats are invited to participate in the ceremony. The governor of Mecca leads the guests who ritually clean the structure, using a broom.[82]

Chanzo: Kaaba - Wikipedia.
 
Pascal kwanza usimpe Mchaga hela akutunzie, pili watakao faidika na Corona na wanachekelea ni CCM ambao miaka minne wanafanya kampeni huku wakiwazuia wapinzani wao.

Tanzania tunafundishwa tuishi kwa chuki jambo jipya kwetu na huyo hajasema vibaya alichosema gharama kubwa zinazotumika kupambana na Chadema zielekezwe kwenye Corona na tunashuhudia kutokuwepo maandalizi yoyote kuipokea Corona kama majeshi yalivyokua yakijiandaa wakisikia Chadema itaandamana, huu ndiyo ujumbe wake.

Mgonjwa alazwa Mount Meru Arusha ahamishiwa Mawenzi Moshi vipimo vyapelekwa Dar es Salaam! Tumejipanga kuikabili Corona wataalamu wetu wamesambaa nchi mzima, kauli ya Waziri Mkuu siku ya nne Corona yatua nchini.
 
Mayalla Sikubaliani na huyo mtu anaeliombea taifa janga la Corona. Lakini naomba nikukumbushe Tanzania haiwezi kupata Corona kwa maombi ya mtu na pia haiwezi kujiepusha na Corona kwa maombi.
Kama ilivyokuwa kwenye ukimwi, tutajikinga na Corona ikiwa serikali tu itachukua hatua stahiki na wananchi wakatii na ku support juhudi za serikali

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Pascal Mayalla umeongea vema kwakuwa hilo limekugusa zaidi. Unatuasa sote tusimame kama Taifa moja. Tuwe wazalendo. Kwakuwa Wapinzani wakiteswa wakiumizwa huwezi kuanzisha uzi kama huu.

Naomba nikuilize yafuatayo: Hivi unakumbuka janga la TETEMEKO kule Kagera? Unakumbuka tulisimama kama Taifa kuwasaidia wenzetu lkn cha ajabu Mkuu wa Kaya alijitokeza hadharani akiwatuhumu Waathirika wale kuwa kwanini kila JANGA ni wao tu? Je ulituunganisha kama Taifa kulaani ubaguzi ule wa wazi??

Muanzilishi na Mbaguzi ktk haya yote anajulikana lkn hakuna Uzalendo ktk kulikemea. Tuacheni unafiki wa kujificha nyuma ya uzalendo.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hao ni watu waliokata tamaa na kufilisika kimawazo Pascal,wasamehe bure,corona haiji Tanzania.Watapata wanaokaa na waliokaa Ulaya,Marekani,na East Asia ambako kuna hotspots za 5G.

Pascal sijui Trump naye tumuweke kwenye kundi gani,maana kasema Corona inaweza kuwa jambo jema kwa uchumi wa Marekani.
 
Kwa nini kuna waTanzania wamefika hapo? Kuwakamata na kuwaweka ndani ni sawa, ila tungetafuta chanzo kilichowafikisha hapo, tukashughulika nacho ingekuwa vizuri zaidi
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…