Mtu kama huyu ni binadamu au shetani? Anaombeaje Corona ifike Tanzania. Kuiombea nchi yako majanga, sio zaidi ya uendawazimu? Huu sio ushetani?

Mtu kama huyu ni binadamu au shetani? Anaombeaje Corona ifike Tanzania. Kuiombea nchi yako majanga, sio zaidi ya uendawazimu? Huu sio ushetani?

Jana kuna mtu aliuliza kwa mshangao JF imekuwaje?
Mbona mijadala yenye tija kwa watu kujibu hoja kwa hoja haipo??

Kwa mada hii ya Mkuu Pasco watu wanatoka nje ya mada na matusi juu yake.

Iko haja JF admin ikaja na mfumo mpya wa usajili hasa jukwaa hili la siasa.

Hoja ya maana inapotolewa kama watu hawana mchango hata kama ni kuipinga kwa facts bora wakae kimya kuliko kuitana majina ya ajabu ajabu.
Bila shaka Melo na wenzio japo.l mnafanyia kazi nyumbani, tutazingatia hoja kuirejesha JF kuwa great thinkers site.

Nie uendawazimu kuwaombea mabaya Watanzania kwa kuwa na shauku magonjwa kama Corona yatuvamie. Sio sawa hata kama tuna utofauti wa kiitikadi.

Tanzania, Tanzania, nakupenda kwa Moyo wote

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Shida yetu ni ujinga na umaskini unaokatisha watu tamaa ya maisha na utu kupotea.
Kunamjinga mwingine anasema tuchkue tahadhari ya korona ili tumsaidie rahis jon pombe!!
 
Hapa nadhani umehamisha magoli. Mtoa mada anasema kuna mtu anaombea ugonjwa uje. Kinyume cha sayansi. Hakuna mahali mtoa mada kasema kuwa kuna mtu anausambaza kwa makusudi ili awaambukize wengine.
Wapi mleta mada kasema mtu anaombea ugonjwa uje kinyume cha sayansi?

Ugonjwa unaweza vipi kuja kinyume cha sayansi?

Kuombea ugonjwa uje kinyume na sayansi kukoje na kuombea ugonjwa uje kisayansi kukoje?

Sent from my typewriter using Tapatalk
 
Nilikuambia jana, umetumwa humu jukwaani kutetea ccm/serekali, lakini una tatizo kubwa la kiuandishi hasa matumizi ya herufi H. Sio vibaya hao wanaokutuma wakupige msasa wa kuandika, au umtumie Polepole ahakiki propaganda yako mfu kabla ya kuitapika humu ndani. Pia kama huoni aibu rudi shule ukajifunze kuandika, tena uzuri sasa hivi hamna kisingizio maana elimu ni bure.
Hakiri

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Pasco umeona watu walivyo kosa uzalendo??? Hii yote ni kwasababu ya viongozi wetu wanayoyafanya kukandamiza/kuumiza/kuua/kuteka/kutesa kwa kisingizio Cha uzalendo.

Chuki imefika pakubwa umoja na mshikamano kwa Tanzania unazidi kufifi toka awamu ya tano imeingia madarakani.
 
kama siyo wewe, wajukuu wako watakuta madhara ya huyu mtu. Tpambane na wewe uwemo pia...
Hivi ushafikiria madhara watakayoyakuta wajukuu zetu kwa aina ya silaha tunazotaka kutumia kupambana na adui zetu?

Hivi kweli wajukuu zetu wanastahili kukuta athari za corona,vita au ugaidi kama mambo ambayo babu zao tulikuwa tukiyaomba yaje ili kupambana na mbaya wetu?
 
Sahihi kabisa,
Nashangaa kwa mtu kama Pasco kuandika thread ndeeefu kwa ajili ya hiyo comment moja,
Halafu anapaswa ajue humu jf kuna watoto wengi sana wameingia kupitia facebook, utawajua kwa mada zao na comments zao, ikifanyika censor ya umri humu utachoka.
Hata watu wazima wapo pia ila ni 'watu wazima kiyambo' utawajua kwa mada zao na comments zao.
hakuna mtu mzima anashabikia CCM wengne afya zao za akili ni goi goi

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Wapi mleta mada kasema mtu anaombea ugonjwa uje kinyume cha sayansi?

Ugonjwa unaweza vipi kuja kinyume cha sayansi?

Kuombea ugonjwa uje kinyume na sayansi kukoje na kuombea ugonjwa uje kisayansi kukoje?

Sent from my typewriter using Tapatalk

Kinyume cha sayansi ni kuutaka ugonjwa uje kwa kuposti JF. Hapo ni sawa na kujaribu kuikausha bahari.
 
Hapo anaonyesha hisia zake za kuchoshwa na namna Serikali inavyowaumiza na kuwapa vilema vya maisha wapinzani as if ni watu toka Congo ama Rwanda na si Watanzania wenzetu.

Serikali inawawinda kuwatafutia makosa kila sehemu, Bungeni, Mitaaani, Magelezani - Yaani popote alipo mpinzani ni mtuhumiwa tayari. hapa ndipo tatizo lilipo

Geleza hilo hilo walilovujiwa mikono na migongo wapinzani ndiyo hilo hilo jamaa mmoja wa CCM alifika kwa mbwembwe na makamera ya video na waandishi kawabeba as if yeye ni mwalikwa!! au mfanyakazi wa Geleza - hakuguswa -- sasa kumbe Kunya ni kwa kuku tu ...ila bata hapana......||


Kweli jamaa kachoshwa mno namna mambo yanavyoendeshwa katika nchi hii.
 
Mdau Ana Hoja. Hatuhitaji Corona Hatuihitaji Hali Iliyopo. Corona Ije Au Isije Cha Moto Tunakiona Na, Tutaendelea Kukiona.

Bora Ije Ili Hiki Cha Moto Tukione Wote, Sio Cha Moto Tukuine Sisi Tu Kila Siku.
Ahsante.

Kwa Maslahi Ya Walio Wengi.
 
Kinyume cha sayansi ni kuutaka ugonjwa uje kwa kuposti JF. Hapo ni sawa na kujaribu kuikausha bahari.
Unaelewa kwamba mtu anaweza kuwa Ulaya akawahabarisha wenzake waupeleke ugonjwa Tanzania kwa kupost JF, na wenzake wakasoma na kuupeleka ugonjwa Tanzania?

Na hivyo, mtu anaweza kusambaza ugonjwa kwa kupost JF?

Kisayansi kabisa.

Sent from my typewriter using Tapatalk
 
Back
Top Bottom