Mtu msomi ni nani?

Mtu msomi ni nani?

Jamaa mbona unawadharau wenye degree zao wakati ndio wanaohudumu kwenye maofisi na sekta nyingi ambazo wewe unapata huduma,?

Au wewe usomi ni mpaka mtu agundue kitu,??
Kama ni matatizo ya jamii wasomi wengi tu wenye degree wanayatatua.
Tatizo waafrika wengi hawataki kuambiwa ukweli, ukitaka usonge mbele, kubali tatizo na weka mikakati ya kusonga mbele
 
Msomi ni mtu ambaye akili yake haijaharibiwa na shule anajifunza kulingana n mazingira na anaishi kulingana na mazingira ukienda shule tu wewe ni mjinga wazungu wanafuta maarifa ya asili tuliyopewa na mungu na kukariri Elimu ambayo Haina msaada Zaid ya makaratasi ndio maana utasikia wazee wa zaman walikuwa Wana akili japo hawakusoma

Tafakari: Mungu aliumba akili sio Elimu tumia akili yako katika mazingira sahihi na uwe msomi
Wazee wa zamani waliokuwa wanavaa viraka ndo waliokuwa na akili??..
 
Ahaa.... Unamaanisha mbwa ukimfindisha kukaa juu ya kiti na akafanikiwa, tutasema mbwa ana akili na siyo mbwa kaenda shule siyo.. au nimekuelewa vibaya
Namaanisha kabla ya kumfundisha mbwa kukaa tayari anajua kukaa ila unapo mfundisha kukaa kwenye kiti siku nyingine usije ukamkuta amekaa kwenye meza au kitandani ukafoka maana umesha mtoa maarifa yake ya asili ya mazingira yake nakujua sehemu yake sahihi kulingana na mazingira yake
 
Namaanisha kabla ya kumfundisha mbwa kukaa tayari anajua kukaa ila unapo mfundisha kukaa kwenye kiti siku nyingine usije ukamkuta amekaa kwenye meza au kitandani ukafoka maana umesha mtoa maarifa yake ya asili ya mazingira yake nakujua sehemu yake sahihi kulingana na mazingira yake
Ahaa... Ndio maana wanazuia kuwapa chakula wanyama hasa maeneo ya hifadhi Kwa kuhofia wanyama hao watabadili tabia zao za asili na kuanza kumtegemea bin Adam Kwa chakula.. sawa nimekuelewa
 
Tatizo waafrika wengi hawataki kuambiwa ukweli, ukitaka usonge mbele, kubali tatizo na weka mikakati ya kusonga mbele
Tatizo liko wapi??
Mkuu hivi huoni impact ya wasomi nchini?
Japo ni ndogo lakini huwezi kusema hakuna impact ya wasomi na uko serious kabisa.

Ch kushangaza upo jf kwenye platform ya Maxence Melo ambaye ni msomi wa tz. Uko serious kweli kijana??
Punguza dhihaka.
 
Mada utakuwa umeielewa vizuri sasa
Nimeielewa nachotaka mimi ni facts. Nataka uniambie ni asilimia ngapi ya waTz waliofanikiwa kufika hiyo elimu na asilimia ngap hawajafanikiwa. Ukifanikisha hilo unayo nafasi ya kuiita elimu ya degree ya kawaida
 
Mtu msomi ni kile kitu anachobaki nacho baada ya kupewa maarifa, nina maana kwamba kile kinachobaki kichwani baada ya kupata mafunzo flan au taaluma yoyote ile ingawa kuna watu wanasema Degree ndio usomi lkn hapana nimechunguza kuna watu hawana degree wala diploma lkn wako vizuri sana...
 
Back
Top Bottom