Mtume Muhammad: Jamii isipotoshwe; Jua huzama katika Chemchemu ya matope Meusi na Mazito

Mtume Muhammad: Jamii isipotoshwe; Jua huzama katika Chemchemu ya matope Meusi na Mazito

Status
Not open for further replies.
Siyo mimi ninayependa mambo mteremko.

Mungu wako ndiye hana logical consistency.

Ameandikwa kama Mungu mwenye uwezo wote, ujuzi wote na upendo wote.

Hana sababu ya kutowapa viumbe wake mteremko. Asiwape mteremko kwa nini?

Uwezo anao, upendo anao, ujuzi anao.

Sasa kama tunaona maisha hayana mteremko, tukiuliza kwa nini Mungu hajatupa mteremko si kwa sababu tunapenda mteremko.

Ni kwa sababu tunahoji kama huyo Mungu yupo, kama yupo, mbona anajipinga mwenyewe?

Inakuwaje baba mwenye uwezo, ujuzi na upendo anawafanyia uchoyo wanawe anaowapenda?

Hujajibu swali hili.
Ukijibiwa bado utauliza kwanin kawafanya wengine matajiri na wengine maskini badala ya wote kuwa sawa
 
Ukijibiwa bado utauliza kwanin kawafanya wengine matajiri na wengine maskini badala ya wote kuwa sawa
Matajiri na maskini wapo kwa sababu Mungu hayupo.

Angekuwepo Mungu mjuzi wa yote, mwenye uwezo wote na upendo wote, kila mtu angekuwa tajiri na umasikini usingejulikana.
 
Habari kwamba watoto wadogo wanakatishwa maisha yao hata kabla hayajaanza vizuri, mama zao wanasikitika sana kwa kutenganishwa na watoto hawa, inanitesa.

Huyu Mungu imekuwaje akaumba ulimwengu ambao watoto wadogo wanakufa, wengine kikatili sana, wakati aliweza kuumba ulimwengu ambao hauna kifo, na watu wanaopendana hawatenganishwi kwa kifo?

Hujajibu swali hili.
Je sio kwamba kifo kipo kwa ajili ya kubalansi dunia!!!! To create life a life must be taken
 
Hiyo aya mbona imekaa kama 'code' na sio km inamaanisha ivo ulivyo tafsiri wew mtoa uzi. Kwa uelewa wangu " chemchem yenye matope meusi ndipo alipotakiwa kwenda (destination) huyo aliyepewa njia za kila ktu (Dhul Qarnain) na kuzama kwa jua kweny matope meusi ilikuwa ndo km inamwongoza kufika pale alipohitajika. Itakapofikia unaona jua linazama kweny matope meusi basi hapo ndipo unapotakiwa kuwepo. Au sio hivyo!?
Yap atleast ni hvyo ukiwa pwani ya bahari nyeusi muda wa machweo ya jua kwa mtu asiejua rotation anaona kama linazama kwenye hayo maji meusi na ndo lengwa kuitwa matope meusi
images%20(12).jpeg
 
Habari za kisha nikaona farasi mweupe kama saruji,akija mawinguni,na mgogoni amekaa mwana wa Adam,akiwa na upanga,
Ukizitafsiri kwa sasa,haingii akilini farasi kupaa angani,na haileti maana,mwana wa adamu kupambana na upanga zama hizi za makombora ya cruiser.
Lugha iliyotumika ni kwa ajili ya wakati huko,na bahati mbaya mungu hajaleta new version
hahaaa " na kwanini ashike upanga kwani walkuwa wanakwnda vitani ?
 
Je sio kwamba kifo kipo kwa ajili ya kubalansi dunia!!!! To create life a life must be taken
Mungu alishindwa kuumba dunia ambayo haina kifo na haikosi balance?

Tatizo moja ninaloliona hapa ni kwamba watu wanajifunga katika ulimwengu uliopo.

Wakati habari za Mungu zinasema ana uwezo wote.

Sasa kama ana uwezo wote, maana yake aliweza kuumba ulimwengu ambao hauna kifo na una balance.

Kwa nini hakuumba ulimwengu huo (ambao hau contradict nature yake ya upendo) akaumba huu ambao una vifo vingi sana, vingine vya kikatili kwa watoto wadogo (hili lina contradict nature yake ya upendo).

Huyo Mungu kwa nini mkatili na anajipinga mwenyewe nature yake hivyo?

Yupo kweli?

Au katungwa na watu tu?
 
Je hujui kuwa sehemu yoyote ambayo hakuna sheria na taratibu ujue hakuna maisha pia
Unaelewa kwamba sikatai sheria. Nakataa Mungu kujipinga nature zake za msingi?

Unaelewa kwamba dhana ya Mungu anayejipinga nature zake za msingi pia inavunja sheria ya logical consistency?

Unaelewa kwamba ukishasema Mungu ana uwezo wote, ujuzi wote na upendo wote hakuna sababu yoyote iliyo na logical consistency na natures zake hizo ya Mungu huyo kuumba dunia anbayo mabaya yoyote yanawezekana?

Unaelewa kwamba kuwezekana kuwepo kwa mabaya yoyote katika ulimwengu huu kunaonesha Mungu huyo hayupo?
 
Wanajukwaa:

Dunia yetu inaendelea kushika kasi katika suala la Sayansi na Tekinolojia.Kwa siku za hivi karibuni,wanasayansi wamegundua kuweza kutengeneza Moyo kwa kutumia stem cells,ikiwa ni hatua katika kuelekea kutengeneza moyo wa binadamu,hali ambayo itasaidia katika kukabiliana na matatizo ya Moyo yanayowakabili wanadamu,kwa kiasi kikubwa, yale ambayo uhusisha mwanadamu kupoteza maisha, kwa sababu tu Moyo wa mgonjwa husika hauna repair au hauwezi kubadilishwa.Miaka kama kumi hivi iliyopita,wanasayansi walikuwa wamefanikiwa kutengeneza Moyo wa panya kwa kutumia hizo stem cells.

Kumbe,kwa tafiti mbalimbali zinazoendelea kufanyika sehemu mbalimbali duniani,ama ardhini au angani,zote zinalenga katika kuboresha maisha ya mwanadamu na hata kuongeza siku za kuishi kwake.Historia inao watu wengi sana ambao wamejihusisha na Sayansi kwa nyakati tofuati tofauti.

Leo,ninataka tumuangalie Mtume Muhammad kwa namna alivyoweza kujihusisha na suala la Sayansi kwa kile kinachosemwa ni kwa msaada wa Mungu.Kurani neno la Mungu;maneno ambayo Mungu akiisha kuyaandika huko Mbinguni, alikuwa anampatia Malaika Gabriel na malaika Gabriel akampatia Mtume Muhammad katika Nyakati tofauti tofauti na Muhammad kuyaweka katika maandishi,lakini kwa namna ya pekee,kwa mara ya kwanza kabisa ikiwa ni katika Pango lililoko katika Mlima Hira, Jabal an-Nour,huko Makka,ambako inadaiwa Mtume Muhammad alipokea ufunuo huo, kwa matatizo sana kwa sababu ya kutojua kwake kusoma na kuandika,Malaika Gabrieli alijikuta anamkaba.

Kwa njia ya ufunuo wa Kurani,tunafunuliwa mambo mengi ya Kisayansi ambamo Muhammad anatujuza jinsi mambo yalivyo.Kwa leo, ninawaletea jambo moja tu.Nalo ni juu ya namna Jua linavyokuchwa na kadri Mungu atakavyotujalia tutayaangazia na mambo mengine.


Kurani kupitia Sura al-Kahf (18: 83-86), inaeleza kwamba Jua huchwea katika chemchemu ya matope meusi mazito(dark Muddy spring):

“83-Na wanakuuliza khabari za Dhul- Qarnaini. Waambie: Nitakusimulieni baadhi ya hadithi yake.84 -Sisi tulimtilia nguvu katika ardhi na tukampa njia za kila kitu.85 - Basi akaifuata njia. 86 - Hata alipo fika machwea-jua aliliona linatua katika chemchem yenye matope meusi. Na hapo akawakuta watu. Tukasema: Ewe Dhul-Qarnaini! Ama uwaadhibu au watwae kwa wema.”

Wakati Muhammad akiwa ametupasha ukweli huo ambao aliandikiwa na Mungu, Ukweli wa kisayansi umebainisha kwamba Jua ni kubwa zaidi na lenye joto kali kuliko dunia.Na ikitokea kwamba Dunia inakaribiana na Jua,basi dunia itayeyuka kutokana na joto kubwa la Jua.

Ukweli mwingine,ambao pia Sayansi imetupatia ni kwamba Jua halitembei bali sayari mbalimbali ndio hulizunguka,ikiwemo Sayari yetu ya Dunia. Historia inaonyesha kwamba mtu wa kwanza kugusagusa habari za kuwa Jua lilikuwa halizunguki alikuwa ni Aristarchus (310-230KK).

Aristarchus alikuwa ni mwana-Astronomia wa Kigriki.
Yeye aliamini dunia ilikuwa katikati ya Mfumo wa Jua(Solar system) na sayari zingine (ikijumuishwa na nyota ambazo zilikuwa zimefungwa katika nafasi fulani) ndio zilizokuwa zikilizunguka Jua.

Hata hivyo, baadaye mwanasayansi,Aristarchus, alikuja kugundua kuwa sio dunia iliyokuwa katikati ya Mfumo wa Jua, bali ni Jua na hivi kwamba ni Dunia na sayari zingine ndizo zilikuwa zikilizunguka Jua.Ugunduzi wa namna hii ulipatikana miaka mingi sana (takribani karne tatu hivi) kabla hata ya Yesu Kristu kuzaliwa na karne tisa kabla ya Muhammad kuzaliwa.

Mwanasayansi mwingine pia aliyekuja na mtizamo tofuati na wa Muhammad (kwa kadri ya ufunuo kutoka kwa Mungu) ni Jean Buridan (1300-1359/61). Huyu) anafahamika kama Mwanafalsafa Mashuhuri sana katika Ufaransa.Buridan alikuwa Mwalimu katika Kitivo cha Sanaa cha Chuo Kikuu cha Paris kwa kupindi chote cha maisha yake ya kitaaluma akimakinika hasa hasa katika masuala ya Logiki (Logic) na kazi za mwanafalsafa Aristotle.

Ni Bridan aliyeanzisha wazo juu ya kiitwacho Copernican Revolution katika Ulaya.Hili ni fundisho lililoleta mwangaza kutoka kuamini kwamba dunia ilikuwa imesimama sehemu moja katika ulimwengu na kwamba Jua ndio lilikuwa linaizunguka dunia (Geocentrism) hadi kueleweka kwamba kumbe Jua ndilo limesimama wakati dunia na sayari zingine zikilizunguka (Heliocentrism).

Kumbe, sasa kwa uchache,kwa mawazo ya hao wanasayansi wawili,tunapata picha kwamba Muenendo wa Jua kuchomoza na kutua sio jambo lililoanza wakati wa Muhammad.Na kama suala la Sayansi ya Mfumo wa Jua lilianza mapema kabla ya Yesu na Muhammad kuzaliwa, yeye Muhammad alipopewa ufunuo na Mungu, hakuweza kujiuliza iwapo ufunuo huo wa Mungu inakuwaje unapingana na ukweli wa mambo?Katika kutafakari ufunuo huu wa Mungu kwa Muhammad, nimejikuta nina maswali yafuatayo,ambayo naomba yatuongoze katika kujadili suala hili.Ni muhimu kujadili kwa sababu pengine Dunia inatufundisha vitu ambavyo havipo.Hivi kweli Mungu anaweza kumueleza Muhammad mambo ya uongo?Maswali mengine ambayo bila shaka hata wewe unaweza kujiuliza ni haya:

1. Hiyo Chemchemi ya matope mazito na meusi iko hapa duniani?Na kama haipo hapa duniani iko angani? Na kama iko angani iko sehemu gani?


2. Huyo Dhul-Qarnaini alikuwa ni kiumbe wa namna gani huyo aliyepewa uwezo wa kuona Jua linavyotumbukia katika matope?


3. Pamoja na kwamba wakati wakati wa Muhammad, labda Sayansi ya kwamba Jua halizunguki, isipokuwa dunia ndio hulizunguka Jua, ilikuwa haijafika katika maeneo ya ardhi ya Arabia, bado hata vizazi vya zamani sana havikupata kuwa na uelewa kama huo wa Muhammad kuwa Jua lilikuwa linatua matope meusi! Je,ilikuwaje katika Vizazi vyote hivyo hapo katikati(ikiwemo na Yesu mwenyewe ambaye Muhammad anamuelezea kama aliyekuwa na uwezo wa kufinyanga wanasesere na kuwapulizia uhai na wakawa ndege kamili), kabla ya Muhammad, akakosekana mtu mwenye uelewa wa kuliona Jua likizama katika matope meusi tofauti? Hivi wewe kwa sayansi hii ya Muhamma juu ya Jua kuchwea katika matope meusi haikupelekei kujiuliza yafuatayo:

· Je, Muhammad kusema mambo ambayo hakuwa nayo uthibitisho ilikuwa ni kutafuta tu kuonekana kwamba Mungu amempa ufunuo wa kipekee juu ya ulimwengu?


· Je, vizazi ya Kiarabu na dunia kwa ujumla baada ya kugundua kwa tafiti za kisayansi, ambazo zimethibitisha kuwa Jua huzungukwa na sayari mbalimbali, ikiwemo Sayari yetu ya dunia, vimuoneje, Muhammad na Uislamu kwa ujumla?


· Je,wanadamu wa vizazi vyote vinavyofahamu kuwa Jua halijawahi kuzama katika matope ama meusi,bluu au meupe, visimuamini Muhammad katika mambo mengine aliyoyasema au vimuchukulie kama mtu aliyekuwa anajaribu kupiga ramli ya jinsi mambo yalivyo?

Lakini swali la mwisho kabisa ambalo nitaomba ujiulize ni hili:Je,Ni kwa nini hadi leo baada ya kugundulika kuwa Jua halizami na wala halizunguki,ni kwa nini hadi sasa aya hiyo iko imesalia katika Kurani?Je,ni nani anasema uongo kati ya Mungu na wanasayansi juu ya suala la Jua?

Karibu kwa mjadala ili tupate kujua ukweli kwa faida ya maendeleo ya Dunia yetu.
Umeandika maneno mengi lakin pumba....kinachokusumbua wewe na wengine wengi ni tafsiri kaa ukijua kiswahili ni lugha ambayo hajajitosheleza kwa maneno kuna vitu vingi hajitafsiriwa inavyotakikana kutokana na uchache wa kisamiati sio Quran tu hata kwenye bible...sasa kilichopo kwenye hiyo sura Allah ametumia neno maghirib...maghrib linamaana ya kuchwea, au kuelekea mwisho wa kitu au kureflect....maana zote zinafit kwa alichokisema Allah kuwa Dhur alifika eneo muda jua kutuama likiwa lina reflect miale yake kwenye tope sio jua kuzama kwenye tope maana ya hapa Allah alizungumzia nyakati...halafu ni mtu tu umeamua kujitoa akili ni Aya ngapi Quran imezu gumzia jua na muzunguko yake had ambayo sayans mwanzo ilituambja jua halizunguki zinazunguka sayari zingine(kama.ambavyo wewe bado unaamini sababu hutafuti unapenda kulishwa maneno ya upotoshaji) ila Quran imesema jua linazunguka na baada ya sayans kupiga hatua wakagundua jua huchukua siku 26 kumaliza mzunguko wake kuna kitu wanaita black dot kwenye mzunguko wa jua ambayo jua huchukua siku 26 kuifikia ile dot Quran imesema hayo, Quran imezungumzia The big bang kwenye surah ambiya, Quran inazunguzia embriology ambayo hatua za ukuwahi wa binadamu ambazo huwez kuziona kwa macho ya kawaida had microscope ambayo by the time haikuwepo..na ndio maana Allaha kasema mara nyingi hichi ni kitabu kwa watu wenye akili wenye kufikiri...unatakiwa usome sana wengi wenu mnatatizwa na tafsri na mnafata vitabu vya wazungu na wao walivhemka tafsiri au wanapotosha makusud sababu ukiandika kitabu against islam kinapata biashara kubwa sana haswa kwa ulaya na america.!

Allah amezungumza kuchomoza na kuchwea kwa jua ili tuekewa kwasababu ndivyo tynavyozungumza sisi wanadamu ikiwe hata wana sayansi wanatumia neno sun set and sun rise lakin je jua huchomoza?? Jua linaonekana na kupotea kulingana na mzunguko wa dunia.. ALLAH amesema ni yeye ndio analiwezesha hilo mchana ku overlap kiza na kiza ku overlap mchana na akase hii ni kwa watu wenye akili..!

Hich ni kitabu kisicho na shaka ndani na Allah amema "mnasema kitabu hichi kaandika Muhammad basi leten japo mfano wake" pia akajitamba leten japo mfano wa sura moja na kisha akasema leten mfano wa aya kumi na baadae akasema leten mfano wa aya moja...sababu structure ya Quran hajazaliwa mwanadamu wa kuiweka vile ilivyo nikipata muda nitawaletea mada ya muujiza wa Quran kinamba.!
 
Pangoni Hira, Muhammad alikuwa peke yake, unafikiria kutakuwa na shahidi gani tena mkuu? Ukilazimisha sana jambo hilo utaletewa Mijusi,Buibui,kenge na Nge tu.
hahaaa halafu akajiwekea defense mechanism kwamba mtu yeyote atakaye mpinga mtume basi amelaaniwa " means hata ukiona amekwambia uwongo uukubali tu '' Kama huo uwongo wa jua kuzama kwenye matope
 
Kama hakuna Mungu, hao watoto kufa si kitu cha ajabu.

Wanakufa kwa sababu Mungu mjuzi wa yote, mwenye uwezo wote na upendo wote ambaye angeweza kuzuia wasife hayupo.

Hili jambo halina contradiction, halikosi logical consistency.

Ukisema Mungu huyo yupo, halafu kaumba ulimwengu huo unaoachia watoto wafe hivyo, hapo ndipo contradiction inapokuja.

Watu popote tulipotokea (na sijifanyi kwamba najua jibu) naweza kusema hatujatoka kwa Mungu huyo.

Tungetoka kwa Mungu huyo, dunia isingekuwa na mabaya kama ilivyo nayo sasa.

Ni lazima tufe kwa sababu Mungu mwenye ujuzi wote, uwezo wote na upendo wote ambaye angetunusuru na kifo hayupo.

Kifo kinaonesha Mungu hayupo, hakioneshi Mungu yupo.

Mungu angekuwepo, mwenye uwezo wote, ujuzi wote na upendo wote, angetunusuru na kifo.

Hayupo.

Ndiyo maana hatunusuriki na kifo.
mate unauwezo mkubwa Sana wakujibu na kujenga hoja aiseee
 
Mpaka sasa watu wanasema mengi sana kuhusu Mungu.

Lakini hakuna hata mtu mmoja anayeweza kuthibitisha kwa namna isiyojipinga kimantiki kwamba Mungu yupo.

Kwa sababu hayupo.

Kama unabisha, thibitisha Mungu yupo.
Thibitisha wew kwamba hayupo
 
Quran inasema Mungu kawafunga watu fulani macho na masikio na kawafanya mioyo yao iwe migumu wasimjue.

Hata msisumbuke nao hao.

Halafu atawahukumu kwa kuwa hawajamjua.

Sasa huyu Allah Mungu gani anazuia watu kumjua, halafu anawahukumu kwa sababu hawajamjua?

Hili jambo linaingiaje akilini?
Hujamalizia....hapo hapo bado pia Mungu ni mwingi wa kusamehe
 
Binafsi elimu dunia nimeisoma na kuilinganisha na elimu ya Mungu. Elimu ya Mungu iko pure na hapana chembe ya uongo. Suala la jua kutozunguka hiyo ni uongo wa kisayansi, kwani kiuhalisia hata kwa kulitazama jua lina Move.
Kwamba dunia ni elliptical sphere, pamoja kung'ang'anizwa nikariri hivyo mpaka leo hii nimekataa na naona kwa macho yangu dunia ni flat, Jua, Mwezi na Nyota zote zinazunguka juu ya uso wa dunia, Jua na mwezi zikiwa na ukubwa sawa na kiwango cha mwanga tofauti lakini Nyota zikiwa ni ndogo kuliko jua na mwezi.
By the way, Jua sio Nyota na wala Nyota sio jua kama sayansi inavyolazimisha.
Zaidi ya hapo vitu vinavyoitwa sayari is just "sci-fi" tu but in reality hakuna kitu kinaitwa sayari angani but kuna Mwezi, Jua, na Nyota.
Drama za NASA hasa ni za kupinga ukweli halisi (ambao hata wao wa Naujua) na kule launch uongo mkuu kwa malengo maalumu kabisa.
Bila Shaka Dunia sio sayari na haijawahi kuwa, tena ni kweli Antarctica sio bara la saba kwa ukubwa bali ni Sio bara kabisa ndio maana hata kwenye bendera ya UN naya USGS halijaoneshwa kwa kwa kuwa sio bara.
Kwa kumalizia ni kwamba sio wanasayansi wote wanaothibisha kuwa jua ni Immovable objects lipo kundi kubwa tu la wanasayansi wa kale na wa kisasa wanaothibisha pasipo chembe ya shaka kuwa dunia ni immovable, na jua, mwezi na Nyota ni movable objects.
So neno la Mungu always linabaki sahihi na la binadamu (hao wanasayansi) uongo wa makusudi wenye nia ovu!!
Mkuu umenifanya nikufollow bila kutarajia...you're truly a great thinker...mie napenda kusoma na kufuatilia watu wenye mawazo kama hayo and not otherwise...usiniangushe next tym mkuu...big up sana
 
Muhammad hakuwahi kusema uongo na wala haitatokea aya iwe kwenye Qur'an au Bible itakayoonesha kwamba hapa alisema uongo na ukatafutwa mbadala wake ukaonekana ukweli ni huu!. Au kama wewe una sehemu tuoneshe ili tukuamini wewe badala ya Muhammad kuanzia sasa.
wewe unaushahidi gani " kuwa muhhamad " hakuwahi kusema uwongo " Kama unahuo ushahidi leta hapa "
 
Hujamalizia....hapo hapo bado pia Mungu ni mwingi wa kusamehe
Contradiction.

Atamsamehe vipi mtu ambaye kamfunga macho na masikio na kamfanya moyo wake uwe mgumu na kakataza watu wasishughulike naye?

Swali langu la msingi hujalijibu.

Kwa nini Mungu wa rehema anawafunga watu mioyo wasimjue badala ya kuwasaidia wamjue?
 
Picha ya kwanza na ya tano nikiwa namsimulia mtu jinsI nilivyoliona jua linazama nikamiambia nimeliona jua linazama kwenye maji nitakua namaanisha linazama kwenye maji kweli au ndivyo nilivyoona kwa muono wangu? VipI kuhusu picha ya pili Jua si naliona linazama ardhini? Na picha ya tatu utamuelezeaje mtu kwamba unaliona jua linazama vipi? Nikisema nyuma ya mlima nitakosea? Picha ya nne nikisema jua limezama kwenye mawingu meusi je?

Nadhani hata huyo anaesimuliwa katika Qur an anasema aliliona jua linazama katika matope meusi kwa muono kama huo hapo juu.View attachment 814741View attachment 814742View attachment 814743View attachment 814744View attachment 814745
[emoji106] [emoji106]
 
Soma ujihakikishie mwenyewe tujadili hapa.

Ukiniuliza mimi halafu nikakudanganya, kama hujasoma utajuaje?

Au kama nimeelewa vibaya nikakupotosha, utajuaje?

Soma na wewe utoe chako kutokana na ulivyosoma.

Usisubiri kutafuniwa na mtu.
Mimi huwezi kunidanganya kwani siwezi amini bila my own proof. Na wala sihitaji wewe uniambie. Unachotakiwa uwe na proof yako mwenyewe sio ya kuendelea kushikiwa akili na ngozi nyeupe. PROVE BIG BANG THEORY TOFAUTI NA HAPO HUNA TOFAUTI NA WAFUASI WA MUHAMMAD AU YESU
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom