Mambo makuu kadhaa yanawaunganisha na kuwatenganisha watanzania nyakati zote na itafika wakati wanaweza chagua kuukataa utanzania wao ni vile tu hajatokea Wa kuwahoji kiuhuru. Ukitaka kuujua unafiki wetu upo kwenye haya mambo na hatuangalii facts tunaangalia mahaba yetu kwenye yanayotujenga kwa mgawanyo ufuatao;
1. DINI, hapa watanzania wako tayari kuungana wakitetea lolote linalohusu dini zao na hakika wanasahau kabisa tofauti zao za kichama, itikadi na makabila na mapenzi ya mpira. Hapa utawajua waislam na wakristo hata kama kwenye siasa hupishana ila wakiwa dini moja lazima watetee lililo jema au baya kuilinda dini yao husika. Hapa napo wanagawanyika ikija mijadala ya kimadhehebu lazima wapoteane hata kama wote wanatumia kitabu kimoja kisha mengine hufuata
2. SIASA.. hapa wanasahau dini zao wanakomalia vyama vyao kwa umoja kabisa hata uovu wa hivyo vyama hutetewa kwa nguvu zote. Ulitaka kuwapoteza lete hoja za kidini hiyo siku chama tawala na upinzani wataungana kwenye hoja. U great thinker na fikra huru haupo tena kikubwa chama cha siasa na viongozi wake..
3. SOKA
Ushabiki Wa soka la ndani pia huwagawanya kwa misingi ya simba na yanga
Hapa ni rahisi sana kumkuta tundu lissu na magufuli jukwaa moja wakishangilia yanga timu yao mathalani.
Watasahau yote ya dini na siasa.
4. UKANDA NA UKABILA SPECIAL
Hapa kuna kanda na makabila yale special yanayojiona ni cream ya taifa yaani yakianzisha ligi humu utadhani makabila mengine na kanda zingine za nchi ni wakimbizi.
NOTE: UKITAFAKARI KWA KINA KABISA KWA NAFSI HURU BILA UNAFIKI SINA HAKIKA KAMA CHANGAMOTO ZA NCHI HII ZINATATULIKA KWA KUKOMALIA HAYO BADALA YA UHURU WA FIKRA ZA UTAIFA WA KWELI. CHANGAMOTO ZA TAIFA HILI HUWAPATA WATU WOTE BILA KUJALI ITIKADI ZAO ZA KICHAMA, KIDINI, KIKABILA NA KISOKA, HIVYO BASI NAFSI HURU ZENYE KUTAFAKARI KWA KINA ZINGEZINGATIWA KATIKA KILA HOJA ZINAZOJENGWA KULIKOMBOA TAIFA.
SINA HAKIKA KAMA IDADI KUBWA YA WATU WALIOPATA MANUFAA MAKUBWA KWA NYANJA ZOTE KWAKUWA WAMEKUWA WA DINI FULANI BALI MAJANGA YALIYOPO YANAWAATHIRI WANANCHI WOTE KWA NAFASI ZAO UKIWATOA WALA KEKI YA TAIFA KWA RAHA ZAO WAKIJITAPA HADHARANI WAKINA BASHITE..
Sent using
Jamii Forums mobile app