Mtungie shairi lenye ubeti mmoja au zaidi mwanadada umpendaye hapa JF

Beti maridhawa, zenye maana sawia,
Zenye mizani sawa, mpaka ujumbe ukanifikia,
Moyo ni kawa, mengi hufunikia,
Nasema shukriya, machache umefungikia.

Ujasiri umejizazia, binti usiye na ria,
Jambo kulifikishia, pasipo udhia,
Walimwengu wakisikia, bila kukukasirikia,
Nasema shukriya, machache umefungukia.

Sina zaidi ya asante, kwa nilopokea,
Baraka nazo upate, mema yatakuneemea,
Kwa yako machache, uliyonighania,
Nasema shukriya, Demiss kwa uloniambia,

Nashindwa kuendelea, nina hofu,
Mganga ananiangalia, atanipa upofu,
Mali yake kuighania, litamtoka povu,
Nasema shukriya, Demiss kwa uloniambia
 
Hakika nakusalimu, mlimbwende Preta ,
Wewe ndiwe mahamumu, mtima nimekupakata,
Penzi lako adhimu, kwingine sitolipata,
Preta wangu tulia, baru baru uwaepuke
 
Jicho lako ni kama kobe,mgongo wako mithili ya mamba mtoa roho!
E mupenzi nikujutiae,uhali gani huko jehanam..?
figure yako namba tasa,ni kama nafungua kurasa
uangaliapo mboga huchacha,kwa tabasam swadakta!.
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23] mkuu hebu mtaje.

Ukikaa naye kula si vinachacha kabla ya kula sasa
 
[emoji2] [emoji2] [emoji2] [emoji2] mnanifurahisha sana leo.
 
Naangalia mpira nitakujibu
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…