Mtungie shairi lenye ubeti mmoja au zaidi mwanadada umpendaye hapa JF

Mtungie shairi lenye ubeti mmoja au zaidi mwanadada umpendaye hapa JF

Naam,

The heading above is concerned!

Tunga shairi lenye ubeti mmoja au zaidi kwa mwanamke yeyote ambaye unampenda hapa jf.

Shairi linaweza kuwa la kimapokeo yaani lenye vina na mizani au la kisasa lisilozingatia urari wa vina na mizani...

Mimi ninamtungia Hajar, mwanamke wa ndoto zangu hapa JF.

"Nampenda msichana, Mnyange mrembo sana
Hajar ndo lake jina, hakuna wa kumfanana
Kichwani ushungi sana, nywele hutoziona
Mwanamke wa ndoto zangu, ni Hajar hakyanani "

Haya.. Tuendelee kuwatungia mashairi.. Yaani wasipoelewa kwa mashahiri haya, basi hatuna namna ingine..

==========================

Ona shairi la Psych Counselor kwa Demiss

" Demiss my love, nimekupenda siku nyingi.
Pembe langu la ndovu, lanitesa nikiona lako wigi.
Umati jf wanishangaa, napoandika shairi hili.
Uko wapi Demiss wangu, njoo ua la moyo wangu."
Hahaha hili sio shairi itakuwa verse kwenye bongo flavor!!!!
 
Mmh Jamii Forum, ni uwanja mpana usifikiri ni column
Hapa tunaelimika, na pia kuburudika
Cha msingi kutulia, madharau achia Tulia
Muhimu kuheshimiana, hata kama mtajamiiana
Kuna wengi wasichana, ila wengine kina mama
Usihadaike na avatar, kuna wengine hawapo Dar
Ila mapenzi hayana formula, ukimpata we fumua
Tunayasoma muda mwingi, watu wakishaingizwa kingi
Wanakuja na threads mia, tena wakilia lia
JF nakuzimia, nitakuheshimu na kukuvumilia.
 
Back
Top Bottom