Majura Magafu licha ya utaalamu wake lakini kama Ushahidi umenyooka huwa anagonga mwamba,nadhani alikuwepo kwenye kuwatetea wale waliomuua Bilionea Msuya na wote walihukumiwa KUNYONGWA japo kwenye Rufaa akachomoka mmoja huku Master mwenyewe aliyefadhili Pesa ili mpango ukamilike akibaki ndani mpaka leo kusubiria Hukumu licha ya utajili wake wote. Kwa hiyo kwa kifupi Kesi hii ni ngumu kwa ndugu yangu Gilbert Kalanje. Inafanana na ile Kesi ya Zombe lakini hii ni ngumu maana Mtekelezaji wa Mauaji ndie mshtakiwa wa kwanza(Gilbert Kalanje). Ile Kesi ya Zombe Mtekelezaji wa Mauaji ya wale Wafanyabiashara na Dreva Tax (Koplo Saad)hakuwahi kukamatwa mpaka leo ndio maana Jaji aliwaachia huru kina Zombe na akawaambia Upande wa Mashtaka wamlete Muuaji Mahakamani yaani Koplo Saad