Muda wa kuanza safari za mabasi uangaliwe upya

Muda wa kuanza safari za mabasi uangaliwe upya

Mparee2

JF-Expert Member
Joined
Sep 2, 2012
Posts
3,092
Reaction score
5,386
Nafikiri sheria tunayotumia kwa sasa ya kuanza safari saa kumi na mbili (06h00) asubuhi ni sheria ya miaka ya nyuma na hivyo inaweza kuboreshwa kwani mambo yamebadilika sana

Fikiria safari za Morogoro to Dar unalazimisha basi liondoke saa 12 asubuhi hivi kweli hicho kipande kina hatari gani hadi mabasi yazuiwe kuondoka labda saa kumi ya alfajiri?

Watu wanahitaji kuwahi kazini au biashara kariakoo na jioni warudi , tunadumaza uchumi.

Safari za kutoka Arusha au Moshi kwenda Dar/Moro una lazimisha basi liondoke saa kumi na mbili wakati hiyo miji karibia imeungana (kuna hatari gani?)

Natamani tufikie mahali tuwe na mabasi yanayosafiri usiku kwa vile vipande salama. Mf basi litoke Arusha 12 jioni lifike Dar saa 11 alfajiri hapo ndio tutakuza uchumi na sio watu kwa mamia kushinda kutwa nzima barabarani badala ya kuzalisha

Kuruhusu mabasi yote saa kumi na mbili kunafanya kuwe na mabasi mengi sana barabarani kwa wakati mmoja na hivyo kusababisha mashindano yanayoweza kuepukika au kupunguzwa.

TUngeweza kuanza na miji michache inayoonekana kutokuwa na hatari; Namaanisha mabasi yaruhusiwe kuondoka kuanzia saa kumi ya Alfajiri
 
Barabara zetu ni nyembamba sana
Ukisema barabara nyembaba unamaanisha hazina viwango vya kupitisha magari mawili kwa usalama?

Au pengine ungetoa vipimo standard vya kimataifa vya upana wa barabara za kupitisha magari ili tuone huo wembamba.

Nijuavyo barabara zimejengwa kwa kuzimezingatia upana wa barabara wa kimataifa (standard); Highway haijengwi kama barabara ya kuelekea nyumbani kwa mtu
 
Namjua. Hata wewe nikiamua nikufaham nakufaham ndan ya dakika kadhaa.
Thubutu Alishindwa lazaro alex mpelelezi wa kimataifa akahaidiwa kupewa pesa kibao labda utumie majini 150 kidogo utafanikiwa kupata jina langu labda kama unaweza picha yangu ndio hy kwenye avatar ila sio kunijua mm Mkuu[emoji24][emoji24][emoji24][emoji24]
 
Uhusiano mbona upo wazi.

Usiku generally ni hatari wewe, Ongeza na wembamba wa barabara hatari mara mbili.
Tumia akili dogo.


Tangu miaka ya 1980's/1990's mabasi yalikuwa yakisafiri usiku! Je, kipindi hicho barabara zilikuwa pana?

Haya ndiyo matatizo ya watoto waliozaliwa kwenye karne ya 21! Upeo wenu wa kufikiri uko chini sana.
 
Nafikiri sheria tunayotumia kwa sasa ya kuanza safari saa kumi na mbili (06h00) asubuhi ni sheria ya miaka ya nyuma na hivyo inaweza kuboreshwa kwani mambo yamebadilika sana

1. Fikiria safari za Morogoro to Dar unalazimisha basi liondoke 06h00; hivi kweli hicho kipande kina hatari gani hadi mabasi yazuiwe kuondoka labda saa kumi ya Alfajiri?
watu wanahitaji kuwahi kazini au biashara kariakoo na jioni warudi , tunadumaza uchumi!
2. Safari za kutoka Arusha au Moshi kwenda Dar/Moro una lazimisha basi liondoke saa kumi na mbili wakati hiyo miji karibia imeungana (kuna hatari gani?)
3. Natamani tufikie mahali tuwe na mabasi yanayosafiri usiku kwa vile vipande salama. Mf basi litoke Arusha 18h00 kufika dar 05h00) hapo ndio tutakuza uchumi na sio watu kwa mamia kushinda kutwa nzima barabarani badala ya kuzalisha
4. Kuruhusu mabasi yote saa kumi na mbili (06h00) kunafanya kuwe na mabasi mengi sana barabarani kwa wakati mmoja na hivyo kusababisha mashindano yanayoweza kuepukika au kupunguzwa.

TUngeweza kuanza na miji michache inayoonekana kutokuwa na hatari; Namaanisha mabasi yaruhusiwe kuondoka kuanzia saa kumi (04h00) ya Alfajiri
Watoto wa hakuna kulala Mbeya to Dsm wameliona hilo,last time nimeanza safari saa nne usiku Dsm kuja Mikumi ili niende Kilombero kiroho safi,nadhani ratiba hiyo ni polisi warafi wanapenda,ili kubabaisha watu na vijisenti vya kupaka dawa za viatu
 
Utakuwa ni mtoto wa jingalao bila shaka! Umeamua umuunge mkono baba yako kwenye hoja ya kijinga!

Tangu miaka ya 1980's/1990's mabasi yalikuwa yakisafiri usiku! Je, kipindi hicho barabara zilikuwa pana? Haya ndiyo matatizo ya watoto waliozaliwa kwenye karne ya 21! Upeo wenu wa kufikiri uko chini sana.
Sawa Mr Chopeko!
 
Saa 12 kamili ni kama sheria, hata Flight nyingi zinaruka muda huo
 
Back
Top Bottom