Mufindi: Afungwa Jela miaka 20 kwa kukutwa na kilo 32 za nyama ya Tandala

Mufindi: Afungwa Jela miaka 20 kwa kukutwa na kilo 32 za nyama ya Tandala

Mahakama ya Wilaya ya Mufindi, imemhukumu Mbogo Tinda (45), Mkazi wa Kijiji cha Ihoanza Tarafa ya Malangali, wilayani hapa, kutumia kifungo cha miaka 20 gerezani, baada ya kumtia hatiani kwa makosa mawili.

Makosa hayo ni lile la kukutwa na nyara za Serikali (nyama ya Tandala – Kudu, yenye uzito wa kilo 32), lakini pia kujihusisha nyara za Serikali bila kuwa na kibali.

Hukumu hiyo imetolewa jana September 4, 2023; na Hakimu Mkazi Mwandamizi wa Mahakama hiyo, Benedict Nkomola, ambapo imedaiwa mshtakiwa huyo alipatikana na nyama ya Tandala yenye thamani ya Sh7, 859, 136 milioni.

Akisoma shtaka hilo, hakimu huyo amesema mnamo August 26, 2023 katika Kijiji cha Idope, Kata ya Ihoanza, wilayani hapa, mshtakiwa huyo alikutwa na nyama ya Tandala ambayo alikuwa anaiuza bila kuwa na uhalali wa kufanya shughuli hiyo.

Inadaiwa kuwa mshtakiwa alinunua na kuuza nyama ya Tandala kilo 32, yenye thamani ya kiasi hicho cha fedha ambayo ni mali Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania bila kuwa na vibali au leseni ya kuuza nyama hiyo.

Pia hakimu huyo amesema kosa hilo ni kinyume na kifungu namba 86(1) (2) (a) na kifungu (3) cha sheria ya uhifadhi wa wanyapori sura 283 rejeo la Mwaka 2022, ikisomwa pamoja na aya ya 14 Jedwari la kwanza la vifungu vya 57(1), na 60 (1) (2) vya sheria ya makosa ya uhujumu uchumi na makosa ya kupangwa, sura 200 rejeo la Mwaka 2022.

Aidha katika kesi hiyo ya uhujumu uchumi namba 11, 2023; mshtakiwa alikiri kutenda makosa hayo, ndipo mahakama ikamtia hatiani na kumhukumu kwenda jela miaka 20 kwa kosa la kwanza na pili ambapo adhabu hizo zitaenda sambamba.

Awali akizungumza kabla ya kutolewa hukumu hiyo, Mwendesha Mashtaka wa Serikali, Ahmad Magenda, aliiomba mahakama itoe adhabu kali kwa mshtakiwa.

"Niombe mahakama yako itoe adhabu kali kwa washtakiwa wote ambao wanafanya makosa kama haya ya kuhujumu wanyapori ambao ni vivutio kwa watalii, sanjari na kukuza pato la mtu mmoja mmoja na Taifa kwa ujumla," amesema Magenda.

MWANANCHI
Mkuu Kwa wale hatujui nyama ya tandala tuwekee japo picha😂😂😂😂😂😂😂🤣🤣🤣🤣🤣
 
Yaani wanyama wanapigwa risasi na watalii na kuacha mizoga ila masikini akibeba anahukumiwa jela why?

Yaani kama hakima anaweza kumfunga mtuhumiwa kwa kukutwa na nyama pori basi hana huruma kabisa huyo

Kuna majizi yameiba hela zetu na yameporomosha majengo ila bado wanapigiwa salute 🫡 kutwa
 
Sijajua tandala ndo mnyama gani, lakini hukumu ni ya hivyo sana.

Mnyama akiua binadamu fidia milioni moja.

Binadamu akiua mnyama fidia milioni 20.

Tuendelee kuwaheshimu wanyama. [emoji23]
 
Mimi Niko hapa kunyoosha ukweli, nothing but the truth.

Rostam Ana kampuni ya uwindaji inaitwa miombo Safari ipo Masaki, kwa kampuni za uwindaji store zao huwezi kukosa nyala na bunduki nyingi tu na vyote ni halali.

Zile zilikuwa ni siasa chafu za Magufuli kupora pesa wafanyabiashara hakuna kingine.

Siwapendi kabisa hawa kina Rostam lakini ukweli halisi ndio huu lazima tuuweke wazi.
Kumbe ilikuwa figisu? Mbona Polisi walitangaza kuwa ana milki siraha na nyara kinyume cha Sheria
 
Kweli mkuu kama yule Mchina juzikati hapo alipigwa Fine ya Laki mbili tu. Huu ni uonevu.
Zipo kesi nyingi tu,tena wanakutwa na maliasili za kutosha.....tukisema RUSHWA ipo mahakamani Kwa hili hawawezi kukataa
 
Mahakama ya Wilaya ya Mufindi, imemhukumu Mbogo Tinda (45), Mkazi wa Kijiji cha Ihoanza Tarafa ya Malangali, wilayani hapa, kutumia kifungo cha miaka 20 gerezani, baada ya kumtia hatiani kwa makosa mawili.

Makosa hayo ni lile la kukutwa na nyara za Serikali (nyama ya Tandala – Kudu, yenye uzito wa kilo 32), lakini pia kujihusisha nyara za Serikali bila kuwa na kibali.

Hukumu hiyo imetolewa jana September 4, 2023; na Hakimu Mkazi Mwandamizi wa Mahakama hiyo, Benedict Nkomola, ambapo imedaiwa mshtakiwa huyo alipatikana na nyama ya Tandala yenye thamani ya Sh7, 859, 136 milioni.

Akisoma shtaka hilo, hakimu huyo amesema mnamo August 26, 2023 katika Kijiji cha Idope, Kata ya Ihoanza, wilayani hapa, mshtakiwa huyo alikutwa na nyama ya Tandala ambayo alikuwa anaiuza bila kuwa na uhalali wa kufanya shughuli hiyo.

Inadaiwa kuwa mshtakiwa alinunua na kuuza nyama ya Tandala kilo 32, yenye thamani ya kiasi hicho cha fedha ambayo ni mali Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania bila kuwa na vibali au leseni ya kuuza nyama hiyo.

Pia hakimu huyo amesema kosa hilo ni kinyume na kifungu namba 86(1) (2) (a) na kifungu (3) cha sheria ya uhifadhi wa wanyapori sura 283 rejeo la Mwaka 2022, ikisomwa pamoja na aya ya 14 Jedwari la kwanza la vifungu vya 57(1), na 60 (1) (2) vya sheria ya makosa ya uhujumu uchumi na makosa ya kupangwa, sura 200 rejeo la Mwaka 2022.

Aidha katika kesi hiyo ya uhujumu uchumi namba 11, 2023; mshtakiwa alikiri kutenda makosa hayo, ndipo mahakama ikamtia hatiani na kumhukumu kwenda jela miaka 20 kwa kosa la kwanza na pili ambapo adhabu hizo zitaenda sambamba.

Awali akizungumza kabla ya kutolewa hukumu hiyo, Mwendesha Mashtaka wa Serikali, Ahmad Magenda, aliiomba mahakama itoe adhabu kali kwa mshtakiwa.

"Niombe mahakama yako itoe adhabu kali kwa washtakiwa wote ambao wanafanya makosa kama haya ya kuhujumu wanyapori ambao ni vivutio kwa watalii, sanjari na kukuza pato la mtu mmoja mmoja na Taifa kwa ujumla," amesema Magenda.

MWANANCHI
Siwezi kushangaa sababu kuna uwezekano aliyetoa hukumu hajawahi kuingia hata selo ya polisi

Lakini kama watoaji hukumu wangekuwa wameshaingia jela au walau selo jpo kwa week hakika hizi hukumu za miaka 20+ kwa kesi kama hii zisingekuwepogo

Maana jela kunatisha sidhani kama kuna mtu anaeujua msoto wa jela akawa anatamani mwenzake akamalizie maisha kule
 
So what if caught? But others get caught and released
Hapo ndiyo mnapofeli,eti umekamatwa na Jinai, utetezi wako ni eti mbona kuna wengine wanafanya Jinai lakini hawa kamatwi,na hata wakikamatwa wanaweza achiwa police au Mahakamani,utafungwa mapema sana! Wwe jiteteee wwe Kama wwe na Jinai yako!! Jinai maana yake halisi ni kua Umekinzana na Sheria!!

Sent from my TECNO KC8 using JamiiForums mobile app
 
Ndiyo nani huyo Tandala?
1693935357468.png
 
Back
Top Bottom