Muhimbili, kulikuwa na haja gani ya upasuaji kutenganisha watoto mapacha?

Ila tukubaliane tu hata hao mabeberu nao walianza hivi hivi. Hivyo wakati mwingine tuwaunge mkono madktari wetu kwa jitihada zao.

Sidhani kama walidhamiria kutokea kwa hayo mauti ya mabinti zetu wapendwa.
Hao hao madaktari Waziri mwenye dhamana aliyejionea mwenyewe pasi na cheng's wanaombana Rushwa! Unatarajia upasuaji wa hali ya juu hivyo waweze wapi.
Bado tuna safari ndefu.
Kuna mwingine alikuja hapa JF anadainfudia ya Mil. 500 Daktaribwa TMJ kumfanyianupaduaji na KUTOA teuzi na mwishowe kudai ana Kansa! Alipoenda India akakuta Kuna makosa yalifanyika na hakuwa na kansa. Wakati walimpeleka ocean road akaanze mionzi akagomea hapo.? [emoji89]Ni shida hospitali zetu. Dr anaamua yeye mwenyewe bila kushirikisha wengine kwanza.
 
Inavyoonyesha walikuwa wameungana tumbo tu, na hilo pia limetushinda?
 
Ile wametangaza kufanya operation hiyo nikajua tu wameamua kuwauwa Kisima...never trust tz Doctors tena mloganzila wale wanafunzi? Hell no.
Acha kukurupuka mkuu, unamzungumzia swala nyeti afu unapotosha, tuwekee hapa jopo la madaktari walofanya ile kazi afu utuoneshe miungoni mwao yupi mwanafunzi, pathetic...
 
Nadhani ilikuwa hatua nzuri sana. Ingawa tumewapoteza, lakini kama kuna makosa yamefanyika kesho tutawaokoa wengi.
 
Dah! Hapa sasa umechanganya vitu vingi kwa wakati mmoja. Hoja iliyopo mezani ni ya mapacha wawili walio ungana kufariki kwa nyakati tofauti baada ya kufanyiwa upasuaji uliofanikiwa katika Hospitali ya Taifa Muhimbili.

Hizo kesi nyingine, sina uwezo wa kuzijibia, au kuzitolea maelezo kwa kweli.
 
Ukishaingia ICU theater una mambo mawili tu, kufanikiwa kupona ama kufa, hata hivyo madaktari walijitahidi kadri walipoweza na hakuna namna unaweza kuwalaumu kwa sababu walifanikisha zoezi,na patients wanaendelea kusurvive. Mengine mwachie Mungu.
Muhimbili walichokosea ni kuanza na mbwembwe nyingi, Ila bado nasema ni mwanzo mzuri. Wapunguze maneno udaktari ni vitendo
 
Kwa kweli tz bado sana.Hivi kama huyo mama wa watoto hao angekuwa ndugu wa kiongozi mkubwa kama rais wangekubali kweli kufanyiwa operation hapo muhimbili?Naamini wangepelekwa ubeberuni.Maana inasemekana kunakiongozi mkubwa hapa tz aliwahi kufanyiwa operation ya tezi dume ulaya ambayo hata kwenye kituo chochote cha afya ingewezekana

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Huwezi pata 100 kama hujawahi pata 90 na huwezi pata 90 kama hujawahi kupata 70 na huwezi pata 50 kama hujawahi pata 30 kutoka katika uwezo wa akili yako katika kufanya jambo lolote ili kuweza kutatua matatizo yake hayo mambo lazima yatokee ili kuweza kujifunza kadri watakavyokuwa wanafanya sana ndio wataweza kufika juu tunaomba waje wengine walioungana na wawatenganishe tena mwisho wataweza

Kumbuka hata aliyegundua unknown rays[x rays] alikufa kwa kuwa alikuwa anajipiga kila mara yeye anavyojipiga anaona raha kumbe anaua seli zake pumzika kwa amani Rontegen je yeye bila kufanya hivyo labda asingekufa na leo tusingekuwa na x rays
 
Ni unfortunate.
Unachokisema ni sawasawa na kusema kwamba kwanini dereve wa gari aliruhusu safari kama angeenda kugongana uso kwa uso na fuso.

Kitakachotokea kitatokea na hakuna kitu utafafanya hasa baada ya kutokea.
 
Hatukutakiwa kufanya majaribio kwenye uhai wa watu Kwa kifupi walikuwa wanatafuta publicity
 
Sawa, ila ndo uandike jina la Mungu kwa kuanza na herufi ndogo.?
 
Kwani kulikuwa na ulazima gani wa kuwatenganisha. Wangeachwa hivyo hivyo waendelee na maisha yao ingekuwaje. Two in one is allowed. Msitafutie ujuzi kwenye maisha ya watu enyi watu.


YESU KRISTO NI BWANA NA MWOKOZI
 
Kwani hawa watoto ndio wa.kwanza kufanyiwa Operation ya kutenganishwa?

Sent from my Nokia 3.2 using JamiiForums mobile app
 
Ila tukubaliane tu hata hao mabeberu nao walianza hivi hivi. Hivyo wakati mwingine tuwaunge mkono madktari wetu kwa jitihada zao.

Sidhani kama walidhamiria kutokea kwa hayo mauti ya mabinti zetu wapendwa.
Upo sahihi, tuwe na imani na wataalamu wetu
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…